Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi-10)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 23, 202528 Comments14 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Kumi 

    “Veronica najua unanisikia, usifanye jaribio la kuondoka  tafadhari” Aliongea Joji akiwa anapanda atokee kwenye lile  dirisha, nikasema liwalo na liwe pembeni kulikuwa na kipande  cha mti uliokauka niliuchukua na kukaa makini nikitazama pale  ambapo angetokea, Honi ilipigwa zaidi ya mara saba hatimaye  ukimya ulitawala. 

    Joji alipotokeza kichwa chake nilimpiga na kile kipande cha  Mti, nilimpiga tena na tena akiwa hawezi hata kurudi nyuma,  nilihakikisha nampiga hadi azimie na ndicho kilichotokea  nilimpiga hadi nikamuaribu ile sura yake, damu zikawa  zinamtoka kama bomba la maji lililo pasuka, kwakuwa ilikuwa  ni nyuma ya nyumba hakukuwa na shida yoyote, nilimuacha akiwa  juu ananing’inia.  Endelea

    SEHEMU YA KUMI NA MOJA

    Nilipochungulia niliona geti likisukumwa, Anko Sanga ndiye  aliyekuwa akisukuma lile geti, nilimtazama kwa makini sana,  kuruka ukuta ilikuwa ni shida nyingine ambayo kwa vyovyote  nisingeiweza kwasababu alikuwa ameweka wavu maalumu wenye  ulinzi wa umeme, Nilimuona sasa akielekea ndani haraka baada  ya kuona Joji hayupo pale kwenye kibanda chake. Nilikaa  makini kusikiliza milio ya funguo hadi alipomaliza na  kufungua geti, kisha akafungua mlango. 

    Bahati nzuri kwangu alikuwa ameacha geti wazi, nilikimbia  kuelekea getini nikafanikiwa kutoka nje kabisa lakini ilikuwa  msituni sana na barabara ilikuwa ya vumbi tena isiyopitisha  magari, mvua zilizokuwa zikinyesha zilisababisha madimbwi ya  maji, nilianza kukimbia kuifuata ile barabara nikakumbuka  kuwa Joji alisema hadi kufika Kwenye makazi ya Watu  ingenichukua Kilomita 90 au zaidi. 

    Nikiwa naendelea kukimbia huku maumivu ya mguu yakiwa juu,  nilisikia gari ya Anko Sanga ikija kwa nyuma, ilinibidi  niongeze mwendo, nilipofika mbele nilijificha, gari ikapita,  nikaona sio salama tena kuendelea kutumia ile barabara  nikazama msituni na kuanza kukata nyika. 

    Nilikimbia na kutembea huku njaa ikianza kunishika,  nilikunywa maji yaliyotuama ili niendelee na safari,  nilikatiza milima na mabonde kwa tabu sana hadi giza lilipo  ingia, nilikuwa naona mwanga wa gari na nilisikia mlio,  nilijua tu Anko Sanga alikuwa akiendelea kunitafuta baada ya  kugundua kuwa nilikuwa nimetoroka. 

    Nilitembea usiku kucha ili tu nifike kwenye makazi ya Watu  niweze kupata msaada, mwendo ulikuwa mrefu hadi kulipo  pambazuka nilijikuta nikiwa juu ya kilele kidogo cha Mlima,  niliona jinsi gari ya Anko Sanga ilivyokuwa ikipiga misele  yake ya kunitafuta Usiku na Mchana. 

    Nilisubiria jua litoke ili nipate nguvu kidogo ya kutembea,  ule mguu ulio na maumivu ulikuwa ukiendelea kunipa shida  sana. Kwa mbali niliona Moshi ukifuka nikajua tu ni lazima  kutakuwa na makazi ya Watu, nguvu ikanijia hata kabla jua  halijatoka nikawa na nguvu ya kusonga mbele. Kila  nilipoitazama picha ya Mtoto wangu nilijikuta napata nguvu ya  kwenda mbele. 

    Nilitembea hadi jua lilipoanza kuwa kali nilikutana na  barabara kubwa, ikiwa na mchepuo mdogo ambayo ndio barabara  iliyoenda kwenye nyumba ya Anko Sanga, mbele kabisa niliona  kibao kikiwa kimeandikwa UNAKARIBIA MPAKA WA KENYA, upande  mwingine ulikuwa ukisema UNAKARIBIA MPAKA WA TANZANIA, hivyo 

    nilikuwa pale katikati, nikaongoza upande wa Tanzania nikiwa  ninakimbia. Nilikimbia kwa spidi sana licha ya kuendelea  kusikia maumivu ya Mguu hadi nilipokaribia kwenye uzio wenye  Askari, nilipogeuka nyuma nililiona gari la Anko Sanga  likija, niliongeza mwendo hadi nilipofika walipo Askari. 

    Wale Askari waliniweka chini ya Ulinzi wakinitaka nitoe  maelezo wakati huo Anko Sanga alikuwa ameshafika pale,  nilijielezea kidogo nikataja namba za kitambulisho changu cha  Taifa, wakakagua na kuthibitisha kuwa ni Mtanzania, Wakati  wote huu Anko Sanga alikuwa kwenye gari lake akinifwatilia  kwa makini, kila nilipogeuka nilikutana nae. 

    Wakamuuliza Anko Sanga alikuwa akielekea wapi akawaambia kuwa  anaenda mjini, nami nilishawaambia naenda mjini wakamwambia  anipe lifti ya kuelekea Mjini, hakukuwa na gari nyingine  zaidi ya ile ya Anko Sanga, wale Askari wakanitaka nifanye  haraka niingie kwenye gari, sikuwa na jinsi bali kuelekea  kwenye lile gari. Nilijua nilikuwa nikiingia tena kwenye  mikono ya Mtu katili, 

    Sikutaka kusema kuwa alikuwa mbaya mbele ya wale polisi  nikihofia zaidi mambo yangekuwa mengi pale, nilichotaka ni  kumpata binti yangu tu. 

    Nilipoingia kwenye gari niliketi siti ya nyuma ya gari yake,  nilipomtazama nilimuona alitoa tabasamu la Furaha kuonesha  kuwa ilikuwa ni ngumu kuruka mitego yake, ikabidi aanze  kuliondoa lile gari, kabla hata hajaondoka wale Askari  walimsimamisha. 

    Kulikuwa na Watu wengine wawili waliotakiwa kupewa Lifti  akiwemo Polisi mmoja na Mama mmoja ambaye alikuwa akiuza  Chakula pale Mpakani, yule polisi alienda kukaa mbele wakati  mimi na Yule Mama tulikaa nyuma, nilimuuliza alikuwa akishuka  wapi akaniambia Mjini kabisa nikaona hawezi kuwa msaada hivyo  nikasubiria atakaposhuka yule polisi ndio nami nishuke. 

    Anko Sanga alinitazama kwa sura ya hasira, yule Mama alikuwa  akiniuliza maswali kadhaa maana nilikuwa kama nimedhohofu  hivi, akanipatia chakula huku safari ikiwa inaendelea.  Tulienda kwa mwendo mrefu hadi jioni ilipoingia, Yule polisi  alishuka kilomita kadhaa kabla ya kufika Mjini, nilikuwa  nikiyafahamu yale mazingira nami nilishuka. 

    “Nilijua unashuka Mjini?” aliniuliza yule Polisi “Hapana natakiwa nishuke hapa mara moja ili nionane na Mtu

    “Haya ndugu una abiria mmoja tu mfikishe salama” aliongea  Polisi kisha Anko Sanga aliondoa lile gari, nilijua hawezi  kumfikisha yule Mama Mjini ni lazima tu atanirudia hivyo  nilikatiza haraka na kuvuka barabara kisha niliingia mtaani,  nilitembea kwa haraka kulekea mjini lakini kwa kutumia Njia  za mtaani, usiku ulipoingia nami nilikuwa naingia Mjini  Arusha ambako nilikuwa nikiishi na Mama yangu siku za nyuma. 

    Ilipata kama saa 4 kasoro, nilipata wazo la kwenda kule  tulikokuwa tunakaa zamani, nilimkumbuka yule jirani aliyenipa  tahadhari kuhusu Mama yangu Mzazi, niligonga mlango nikiwa  nimechoka sana, alinifungulia kisha alifunga mlango 

    “Veronica umepatwa na nini?” aliniuliza, nikamwambia ni stori  ndefu ningependa nipumzike, nilimtoa hofu sababu nilikuwa  nimekonda sana niko hovyo hovyo kama tahira fulani hivi. 

    Aliniacha nipimzike ili nikitulia ndipo nimpe hadithi ya  kilichonikuta, majira ya saa 5 usiku Anko Sanga alikuja pale  kwa jirani, akaniuliza kama nilikuwa nimefika pale, sasa yule  jirani kwa jinsi alivyoyasoma yale mazingira akajua tu huenda  kuna shida akamwambia Anko Sanga kuwa hajaniona kwa zaidi ya  miaka miwili, tena akawa anahoji kuna nini kimetokea?  ikamfanya Anko Sanga aamini kuwa sikuwepo pale, wakati huo  nilikuwa nimelala. 

    Jirani hakulala hadi kulipo pambazuka, nilipoamka ndipo  akaniambia kuwa Anko Sanga alikuwa akiniulizia, nilimsimulia  jinsi ilivyokuwa, kuanzia mwanzo hadi mwisho alisikitika  sana, 

    “Lakini nilikwambia Veronica kuwa Mama yako na Kaka yake  wanaskendo ya ushirikina, wamevuma sana hadi Mama yako  akahama hapa” 

    “Imeshatokea Jirani, namuwaza Mtoto wangu na Mume wangu sijui  wako wapi, sijui Mama anaishi wapi” 

    “Kwasasa Veronica unatakiwa utulize akili kwanza, ukitumia  haraka unaweza ukajikuta umepoteza kila kitu kwenye Maisha  yako, cha msingi uko hai hilo ndio jambo muhimu kuliko yote,  kwanza jiimarishe kiafya, unaonekana una Umwa kabisa” 

    “Nashukuru kwa kunijali Jirani, kila nikikumbuka jinsi  nilivyopona kutoka kifo najikuta nalia tuu” Nilisema 

    “Nakushauri kwa sasa rudi Dar kwanza kisha Afya yako ikikaa  vizuri ndio urudi hapa Arusha, kule ni salama zaidi lakini  hapa watakuwa wanakutafuta, hili jambo linahitaji ushahidi hata kama utaenda polisi, je unao? Nilitafakari alichokisema  niliona kina busara ndani yake nilimuomba anipe nauli ili  niweze kuondoka Arusha. 

    Alinipatia nauli kisha niliondoka siku iliyofuata Alfajiri,  nilipofika Dar nilienda hadi tulikokuwa tunaishi, nyumba  ilikuwa imekaa bila Mtu kwa miaka miwili, ilikuwa ya hovyo  tuu. Nilimtafuta Mama Sofia, aliponiona alinishangaa sana. 

    “Umepatwa na nini Veronica?” ilinibidi nimsimulie kila kitu,  alinipa pole kwa kila kilichotokea. Alimtafuta fundi akavunja  mlango na kuutengeneza kisha alimtafuta Mtu wa usafi  akasafisha nyumba. 

    “Asante Mama Sofia” 

    “Usijali Veronica, kilichobakia na Afya yako, Mara ya mwisho  Jonas aliniambia anaenda Arusha kumchukua Mtoto ndio hajarudi  tena” 

    “Ndio hivyo Mama Sofia” Mama Huyu alihakikisha naenda  hospitali kupimwa maradhi yote, nilikutwa na virusi vya  Ukimwi, nililia sana. 

    “Usilie Sofia ndio Maisha, cha msingi unatakiwa kuimarisha  Afya yako kwanza” alinitia moyo mno maana nilikuwa katika  dimbwi la mawazo, kukutwa na virusi vya Ukimwi kuliniumiza na  nilijua ni Anko Sanga ndiye aliyenipa Ugonjwa. 

    “Sijui kama Mtoto wangu Moyo atakuwa mzima Mama Sofia,  ameniharibia Maisha yangu. Mama yangu nimemkosea nini Mimi?”  nililia kwa uchungu lakini sikuwa na cha kufanya zaidi ya  kupokea matibabu ya magonjwa mengine, nilianza dozi ya ARV 

    Nilirudi nyumbani, nikawa nakula vizuri nafanya mazoezi kila  siku hadi hali yangu ilipoanza kutengemaa. 

    Wema wa Mama Sofia utabaki kwenye kumbukumbu za Maisha yangu,  alihakikisha Maisha yangu yanarudi, alinitia moyo  nilipoonekana kukata tamaa, alinifanya nijihisi sina tatizo  lolote 

    “Veronica, sasa unaweza kwenda kutafuta haki yako ilipo. Afya  yako sasa iko sawa” Alisema Mama Sofia baada ya miezi mitatu  ya kuishi Dar, ni kweli hata nilipojitazama niliona  nimeimarika kiakili na Kiafya 

    “Asante Mama Sofia, sijui bila wewe ingekuwaje kwa haya yote  niliyoyapitia. Nakushukuru sana kwa ukarimu na wema wako!  Mungu akujaze tumaini” Nilimwambia

    “Mpaka sasa nashangaa ni kwanini Mama yako ameamua kuwa hivyo  alivyo, nenda kamchukue Mtoto wako na Mume wako Jonas, mrudi  kuishi Maisha yenu. Naamini umejifunza katika haya  uliyoyapitia” 

    “Nitajaribu kuhakikisha Mama yangu haingii matatizoni, pamoja  na yote alinitendea bado atabaki kuwa Mama pekee kwangu!” 

    “Uungwana ni kulipa mabaya kwa mazuri Veronica, usishawishike  wala usijaribu kuupoteza utu wako. Dunia tunapita tu Mungu  ndio mlipaji wa kila jambo” Maneno ya Mama Sofia yalichangia  kwa kiasi kikubwa nijione kama nimezaliwa upya, tulienda  benki akanipatia pesa kwa ajili ya safari ya kurudi Arusha  Kumtafuta binti yangu Moyo 

    Nilisafiri kurudi Arusha siku iliyofuata, niliwasiliana na  yule jirani yetu tukakutana hotelini ili anisaidie zoezi la  kumpata Mtoto wangu Moyo. 

    “Eeh Veronica umebadirika, umerudi kuwa Veronica yule wa  miaka mingi, ninayemfahamu mimi” Alisema baada ya kuniona 

    “Ha!ha! Jirani unajua kila jambo lina wakati wake, kama  nilivyo kwambia nahitaji unisaidie kufahamu anapoishi Mama  maana ndiye mwenye Mtoto wangu” 

    “Anhaa! sasa itabidi tumpate aliyenunua nyumba yenu atupatie  mawasiliano ya Mama yako!” 

    “Kabla ya yote nahitaji kwanza kwenda kanisani, nguvu ya  Mungu ni kubwa kuliko nguvu wanazozitumia” Tuliongozana hadi  kanisani, Baba Mchungaji alishangaa kuniona 

    “Eeeh! Veronica za miaka mingi?” 

    “Salama Baba Mchungaji” 

    “Mama yako nae hajaonekana kwa zaidi ya miezi mitano sasa,  lakini tunashukuru kwa nguvu ya Yesu iliyomo ndani yake  amesaidia ujenzi wa kabisa hili na baadhi ya miundo mbinu”  Alisema, sikutaka kumharibia Mama mbele ya Watu wa Mungu 

    “Anhaa!! yupo na safari zake za kibiashara” 

    “Basi Mungu aendelee kumtia nguvu popote alipo” “Amina Baba Mchungaji”

    Tulizungumza tukiwa tunatembea tembea kwenye viunga vya  kanisa, nikamwambia nahitaji maombi yenye nguvu 

    “Kwanini Veronica?” 

    “Naona kama napoteza imani iliyo ndani yangu Baba Mchungaji” “Oooh! sawa hilo halina shida, vipi ndoa yako?” 

    “Namshukuru Mungu Baba Mchungaji” Siku hiyo aliniombea  akanipa na mafuta ya baraka, nilihitaji sana nguvu ya Mungu  katika kufanikisha jambo lililo mbele yetu, baada ya maombi  tulirudi hotelini. 

    “Sasa niko tayari Jirani” 

    “Haya Veronica” 

    Siku iliyofuata tulienda kwenye nyumba tuliyokuwa tukiishi  zamani, tulikutana na aliyeinunua akatupatia namba ya Mama  yangu Mzazi, nikajaribu kupiga, akapokea lakini niliposikia  sauti ya Mama yangu nilishindwa kujizuia nilijikuta nikilia  kwa uchungu sana. 

    Jirani alinisaidia kuongea nae, akajifanya ni mfanya  biashara, Mama akampatia anuani ya alipo tukafanikiwa kujua  anapoishi. Tukamtafuta Mtu mwingine ambaye alijifanya ni  Mfanyabiashara maana Mama alikuwa akimfahamu jirani huyo,  yule Mtu akaenda kule kwa lengo la kuangalia vitu viwili,  kwanza uwepo wa Jonas na Mtoto. 

    Nilimpatia pesa kisha akaenda zake, alipofika pale alimuona  Jonas lakini akiwa kwenye kiti cha walemavu na jinsi  alivyoelezea alikuwa kama amepooza viungo vyake, alimuona pia  Mtoto mdogo ambaye ni Moyo. 

    “Asante kwa msaada wako” Nilimpatia ujira wake kwa kazi  aliyoifanya kisha tukapanga jinsi ya kuingia na kuwakomboa  wale wote, Jirani alinishauri twende polisi lakini sikutaka  kumtia matatizoni Mama yangu 

    “Tukienda huko Mama yangu atapotea, ninachotaka ni kuichukua  familia yangu tuu” Kutokana na ramani tuliyopewa tulifika  hadi pale Mchana, tukamkuta msichana wa kazi tu. 

    Hakunipa presha hata kidogo, nilimchukua binti yangu, Jirani  akanisaidia kumkokota Jonas, tukaingia kwenye gari tukaelekea  Hotelini. Ilikuwa ni siku yenye faraja kwangu lakini Jonas  alikuwa kama zuzu tu, yaani hajielewi wala hajitambui,  alikuwa akivuja udenda.

    Nilimkumbatia Moyo wangu, aliyekuwa akilia, hata jirani nae  alikuwa akilia, Kilio cha Moyo kilinishangaza sana 

    “Mbona kama Mtoto anaumia Veronica?” aliniuliza jirani, kwa  jinsi ambavyo Moyo alikuwa akilia alikuwa kama vile anaumizwa  na jambo fulani ndani ya mwili wake. 

    Ikabidi nimtoe nguo zote, Masikini ya Mungu Moyo alikuwa na  vidonda kwenye Papa yake, alikuwa kama amekatwa hivi, nilitoa  bandeji ili niangalie nilijikuta moyo wangu ukiuma hadi  mchozi ulinitoka, alikuwa amekatwa mashavu ya Papa yake yote  mawili 

    “Masikini ya Mungu! hivi Mama yako ni Binadamu kweli?”  aliniuliza yule jirani nikiwa namtazama binti yangu, ikabidi  niende Hospitali nilimuacha Jirani akiwa anamuangalia Jonas,  nilipata wazo la kumpima Ukimwi Mwanangu! 

    “Amepatwa na nini huyu?” aliuliza Daktari baada ya kumuona “Nilisafiri nilimuacha na dada wa kazi sijui hata amekuwaje” “Itabidi kwanza uende polisi ndipo atibiwe” 

    “Daktari, naomba atibiwe tu kwasababu kwenda huko kote  kutachukua muda mrefu wakati Mtoto wangu anateseka tu” 

    “Ok! nitakusaidia sababu ni Mtoto” 

    “Naomba pia apimwe Ukimwi” 

    “sawa!” 

    Nilikaa kusubiria majibu ya Moyo, Mtoto alikutwa na  maambukizi ya Ukimwi, alianza dozi akiwa mdogo kabisa jambo  hili liliniumiza sana sikuweza kuvumilia nilijikuta nikitokwa  na machozi, Moyo alitibiwa tukarudi Hotelini, kwa mara ya  kwanza nililala na binti yangu na mume wangu usiku tukiwa na  amani, japo wao walikuwa na maumivu lakini kuwa hai ilinipa  moyo sana. 

    Nilimwambia jirani arudi tu nyumbani, asubuhi aje  anisindikize Uwanja wa ndege ili niondoke na familia yangu. 

    “Ubaki salama Veronica” Aliondoka zake, Tulilala pale nikiwa  nimewakumbatia bila kujali kuwa Jonas alikuwa zuzu kama  tahira hawezi kuongea wala kujua chochote kile.

    Usiku Majira ya saa 7, nilianza kuota ndoto mbaya sana,  niliota Mama na Anko Sanga wamekuja pale Hotelini wakiwa  katika mazingira ya kichawi, wakawa wanalazimisha kumchukua  Jonas, nilijitabidi sana kumng’ang’ania ili wasimchukue,  nilipiga na maombi ya nguvu nikiwa ndotoni, niliposhtuka  nilimkuta Jonas akiwa anatetemeka sana. 

    Nilijitahidi kumuita Jonas, alikuwa ametoa macho yake, povu  lilianza kumtoka nikamsikia akiniita jina langu, nilipoitika  ndio ikawa mazima. Jonas akatulia kabisaa nilipomuangalia  vizuri niligundua alikuwa akipoteza joto la Mwili wake. 

    Nilichukua simu yangu na kumpigia Mama usiku ule ule, baada  ya kupokea aliniuliza mimi ni nani 

    “Mimi ni Veronica, binti uliyemzaa na kumlea kwa shida, binti  uliyemtesa na kumnyima uhuru, binti uliyemsababishia maumivu  ndani ya Moyo wake! nipo Arusha kwa ajili ya Binti yangu,  nipo na Moyo lakini Jonas Umeshamchukua tena kutoka kwangu!  Naomba MAMA NIACHIE MUME WANGU” yalikuwa ni maneno mazito  niliyoyaongea nikiwa ninalia kwa uchungu sana 

    Hakujibu kitu alikata simu, nilimtazama Moyo nilimuona akiwa  amelala, nilipigia simu jirani aje Hotelini, baada ya  kumaliza kuongea nae nilitoka usiku ule ule. Sikuwa na woga  wa aina yoyote ile nilienda hadi nyumbani kwa Mama yangu,  bahati nzuri wakati nafika ndio geti lilikuwa lilifunguliwa,  niliingia mazima. 

    “Veronica!” Mama aliita baada ya kuniona 

    “Kimekuleta nini hapa?” aliongea tena akiwa anafungua furushi  alilolishika mkononi, nilimfuata nikamsukuma lile furushi  likaangukia pembeni, nilimkamata na kuanza kumgongesha kwenye  kioo cha gari, nilimgongesha kichwa chake hadi damu  zilipoanza kumtoka. 

    Msichana wake wa kazi akaanza kupiga kelele akiomba msaada  ndipo alipokuja mlinzi akiwa amebeba begi kutokea ndani,  alipomulika tochi alimkuta Mama akiwa amechanika sehemu ya  kichwa chake, dimbwi la damu likiwa limejaa chini  alipoangukia 

    Akanifuata na kunikamata, kisha wakapiga simu polisi, Muda  ule ule polisi walifika na kumichukua. 

    Tukio lile lilizua tahamaki kubwa sana, waliotufahamu  walisema Mtoto amemuuwa Mama yake, ikawa ndio stori kubwa,  kesi ikawa na mlolongo mzito, walinitesa nikamtaja Anko  Sanga, walimtafuta na kumkamata.

    Kesi iligubikwa na mambo ya kushangaza sana ambayo yalifanya  kesi ihamishiwe Mahakama ya Kisutu Jiji Dar, Mama Sofia  alipokuja kuniona nilimwambia amlee Mtoto wangu, aliwasiliana  na yule jirani akamchukua Sofia, mwili wa Jonas ulizikwa  Arusha. 

    Nilikuwa namalizia kuwasimulia wale Mawakili wa ile kesi,  wote walikuwa wakitokwa na machozi! 

    Nilirudishwa tena Mahakamani, Mawakili wakaelezea tukio zima  lilivyo, Wakati huo Anko Sanga alikuwa akisumbuliwa na  maradhi mbalimbali hasa Ukimwi alikuwa Hospitali. 

    Hakimu aliamuru nifungwe kifungo cha miaka 10 jela huku  ikitajwa kuwa nimeua bila kukusudia, lakini ripoti ya Afya  yangu ilifanya kifungo kipungue hadi miaka 5. 

    Hii ilikuwa ndio Haki pekee niliyokuwa nikiisubiria kwenye  ile kesi! 

    •••Mwisho•••••

     INAFUATA YA KIJASUSI COMMENTS ZIKIFIKA 100 Naachia Kesho MAPEMA SANA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia

    28 Comments

    1. Warda on May 23, 2025 1:09 pm

      Vero bye byee🥲

      Reply
      • Roda on May 23, 2025 8:25 pm

        Oyyy uwiiiii mm ningeanza na huyo anko sanga aseeee sijui mm jmn ila hyo hadithi is too much kali knm yaan

        Reply
    2. Rachel Richard on May 23, 2025 1:41 pm

      Duh ama kwel dunia ina mengi ya ajabu kikubwa kumuomba mungu tu bas

      Reply
    3. Adam on May 23, 2025 1:46 pm

      Ahsante Saana Story Ni Tamu Saana Ila Daaah inatufundisha Mengi Saana Kwenye Maisha

      Reply
      • Joseph on May 24, 2025 1:45 pm

        Nmeipenda sanaaa hii story hakika mtunz unahitaj pongez🙌

        Reply
    4. Josephat on May 23, 2025 3:07 pm

      Jaman Jonas😭😭😭😭

      Reply
      • Muharram on May 23, 2025 3:26 pm

        Asante

        Reply
      • Yusuf on May 24, 2025 10:16 am

        Duuuu ataliii

        Reply
    5. Muharram on May 23, 2025 3:26 pm

      Asante Sana story Ina mengi ya kuj8funza

      Reply
    6. Vanny on May 23, 2025 4:43 pm

      Story nzuri Asante sana

      Reply
    7. Samwel on May 23, 2025 5:47 pm

      Daaah

      Reply
    8. Maestro05 on May 23, 2025 6:09 pm

      Stori ilikuwa ya Moto Admin apewe maua yake

      Reply
      • Roda on May 23, 2025 8:25 pm

        Oyyy uwiiiii mm ningeanza na huyo anko sanga aseeee sijui mm jmn ila hyo hadithi is too much kali knm yaan

        Reply
    9. Jesca on May 23, 2025 7:30 pm

      Duuuuuuu

      Reply
    10. Hermione3544 on May 23, 2025 9:30 pm

      Super https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    11. Octavian on May 23, 2025 11:06 pm

      Ila mbona veronica ameteseka sana ata kisas chake kama ni kidogo

      Reply
    12. Gervas on May 24, 2025 1:45 am

      Pole Veronica kwa uliyopitia Mungu akutie wepesi mambo yako yaende sawa naww uwe sawa kabisa ,,,, admin hongera kwa kazi nzuri

      Reply
    13. Gervase on May 24, 2025 1:45 am

      Pole Veronica kwa uliyopitia Mungu akutie wepesi mambo yako yaende sawa naww uwe sawa kabisa ,,,, admin hongera kwa kazi nzuri

      Reply
    14. Lorenzo4713 on May 24, 2025 2:35 am

      Cool partnership https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    15. Darwin1361 on May 24, 2025 3:32 am

      Very good https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    16. Emily140 on May 24, 2025 8:34 am

      Very good https://shorturl.fm/bODKa

      Reply
    17. Ava2392 on May 24, 2025 9:16 am

      Cool partnership https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    18. Justin Peter on May 24, 2025 9:17 am

      Duuh

      Reply
    19. Justin Peter on May 24, 2025 9:18 am

      Hatari sana

      Reply
    20. Cleo1354 on May 24, 2025 10:22 am

      Cool partnership https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    21. Peter4639 on May 24, 2025 12:53 pm

      Top https://shorturl.fm/YvSxU

      Reply
    22. Cyrus4135 on May 24, 2025 1:56 pm

      Awesome https://shorturl.fm/oYjg5

      Reply
    23. Ada4906 on May 25, 2025 9:12 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi May 23, 2025

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi Na Moja-11)

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Kumi  “Veronica najua unanisikia, usifanye jaribio la kuondoka …

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kumi-10)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Nane-08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.