Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi 06
Nilikua nikihema, Wazazi wangu walikua wamesimama vile vile kama Watu wasiojitambua.ย Yule Bibi aliendelea kunisogelea huku mguu wake mmoja akiwa anauburuza. Ulikua kama unaย dosari ya ukilema hivi, nilikua kwenye butwaa ambayo ilihitaji Mtu anitingishe ndiyo nitokeย katika ile hali tata.ย
Fumba na kufumbua Macho yule Bibi Kizee alikua amejaa machoni pangu akinimulika naย macho yake makali, nilishtuka na kutoka katika ile hali ya Butwaa. Nilipohitaji kukimbiaย alinishika mkono na kunivuta kwake lakini alipigwa na shoti kali, niliona moto mkaliย uliomsukuma na kumtupa chini.ย Endelea
SEHEMU YA SABA
Alinitazama kwa Mshangao kisha aliniuliza kwa sauti yake kali.ย
โWewe ni Nani?โ aliongea huku akitokwa na moshi mdomoni, bado mvua ilikua ikichapa.ย Niliuangalia mkono wangu, niliiuona ule ushanga, ndio ulionisaidia. Sasa kilichobakia kwanguย kilikua ni kuokoa Uhai wangu, nilirudi nyuma nyuma tayari kukimbia, yule Jini aliwaamrishaย Wazazi wangu wanifukuze.ย
Niliipa miguu yangu mamlaka ya kukimbia, lakini sikufikiria kwenda mbali isipokua kurudiย nyumbani mara moja, nilijigonga getini eneo la mguu lakini halikuninyima mwendo, nilijivutaย haraka na kukimbilia ndani kisha nilifunga mlango.ย ย
Nilifika ndani nikiwa nimechoka, nimelowa na pia nimetawaliwa na hofu. Haikua hali yaย kawaida niwakimbie Wazazi wangu niliowapenda, radi zilikua zikipasua anga halafu sauti yaย kucheka ya yule jini ilikua ikisambaa kila kona.ย
Nilisimama nikiwa nina bubujikwa na machozi, Wazazi wangu walikua kama mazombiย yasiyoelewa Mimi ni Nani kwao, sijui aliwafanyia nini hadi wakaanza kuniwinda kiasi hiki. Basiย nilikua nikiwaona Wazazi wangu kupitia kioo cha mlangoni jinsi walivyokua wamebadilika.
Macho yao yalikuwa hayana kiini cheusi, meupe kama karatasi, walikua wakitokwa na udenda. Niliumia ndani ya moyo wangu kuwaona Wazazi wangu katika hali ile ya ajabu, walikua naย nguvu za ajabu kiasi kwamba walikua wakivunja kioo waingie ndani.ย
Nilitamani sana kuwasihi Wazazi wangu wanitambue lakini niliona isingelikua rahisi,ย nikapandisha ngazi huku nikisikia namna walivyokua wakivunja kioo, nilikimbia kwa spidi sanaย hadi chumbani kwangu, nikawa naitafuta simu yangu ili niombe Msaada nje.ย
Sijui simu nilikua nimeiweka wapi, niliitafuta kila kona. Nilianza kusikia sauti ya kusukumwaย kwa mlango wangu kwa nguvu, walikua wameshafika mlangoni kwangu.ย
Nilikua natetemeka sana maana nafsi yangu ilikosa utetezi tena. Kwa bahati nzuri niliisikia simuย yangu ikiita. Sijui ni saa ngapi iliingia uvunguni mwa kitanda, niliinama, ilikua mbali kidogoย hivyo ni lazima nikivute kitanda kwanza, nilijivuta nikakisukuma kitanda nikaipata simu yangu.ย ย
Nilikua natetemeka sana, mwili ulikua ukichuruzika maji. Mapigo yangu ya moyo yalikuaย yakienda sambamba na pumzi zangu. Mate yalinikauka, kutoa nywira ya simu yangu ilinichukuaย dakika nyingi kutokana na wasiwasi uliokua umenivaa. Nilishindwa hata kuifungua simu yangu,ย mlango ulikua katika nyakati za mwisho kufunguka.ย
Nilidondosha simu yangu huku nikiwa nimeutolea macho mlango ukiwa unatikiswa haswa,ย nilihisi harufu ya kifo. Taratibu nilianza kurudi nyuma nikitamani nipate msaada usiotarajiwa.ย Hamadโผ! Mlango ulifunguka, Baba na Mama yangu walikua mbele yanguย ย
Walikua katika fahamu zisizo zao, walisimama wakinitazama. Niliona huo ni muda waย kuzungumza nao pengine ningeweza kuwashawishi wakarudi katika hali zao, chozi lilinitoka.ย Sikuwahi kuwaza wala kuota kua siku moja Baba na Mama yangu wangekuwa katika hali kamaย hiyo, hali ambayo wasingeliweza kunitambua Mimi binti yao wa pekee Celin.ย
โMamaโผ Babaaโผโ nilianza kwa sauti ya kilio cha maumivu sana, niliishiwa nguvu hata manenoย niliyohitaji kuyatoa yalikua mazito kutoka mdomoni mwangu. Nilikua na maumivu makali sanaย ndani yangu, udenda ulikua ukiwatoka Wazazi wangu.ย
โNi Mimi Celin, najua hamnitambui kama ambavyo ninyi hamjitambui Wazazi wangu. Mimi niย Binti yenu, hampaswi kunidhuruโ walikua wametulia kimya wakati naongea, nilihisi walikuaย wanaanza kunisikiliza.ย
โOna, furaha yenu ni Mimi hapa, furaha yangu ni ninyi hapo. Hayo siyo Maisha yenu, sijawahiย kuwaona mkiwa hivyo naomba wazazi wangu rudini katika halo zenu. Mna mengi ya kuyajuwaย kuhusu hii nyumbaโ Nilisema, hapa sasa ndipo nilipoiona dhamira ya yule jini kwangu,ย alichotaka ni kuhakikisha Wazazi wangu wananimaliza.ย
Walinifuata kwa spidi ya ajabu ili wanishambulie lakini kwa bahati nzuri niliweza kuwakwepaย nikajigonga ukutani, Mama alikua kama Mbogo kwa jinsi alivyokua akitoa sauti ya hasira kamaย Mnyama vile.
โMama ni Mimi Celinโ nilisema, angalau Baba yangu alikua hana hasira kama ambayo Mamaย yangu alikua nayo, alinivamia tena kunishambulia. Alinijeruhi kwa kucha ndefu, kishaย nilimsukuma nikapata nafasi ya kuondoka pale chumbani, nikashusha ngazi haraka huku Mamaย akiendelea kunikimbiza.ย
Nilifika hadi chini, nilipogeuka Mama yangu alinirukia mithiri ya Ndege tai, alinidondosha chiniย kama mzigo halafu akawa ananishambulia vibaya sana usoni kwa kucha, nilijitahidi sanaย kupambana naye ili niinuke, nilifanikiwa kumsukuma lakini alikua amenikwaruza usoni vyaย kutosha.ย ย
Nilisimama huku Mama akijiandaa tena kunishambulia, nilishaona kua kama sitakua ngangaliย basi Mama angeweza kunimaliza, maana alinishambulia usoni bila huruma halafu alinikwanguaย shingoni na kuniacha na maumivu makali sana. Nilipaswa kupambana naye bila kujali kuaย hayupo katika fahamu zake.ย
Alikua akiunguruma kama Simba mwenye njaa, nilikimbilia jikoni lakini kabla hata sijafungaย mlango aliusukuma kwa nguvu, alikua akinifuata taratibu baada ya kuingia jikoni, nilirudiย nyuma nyuma nikifikiria nifanye jambo gani. Mama alinisogelea bila haraka, alijuaย nisingeliweza kukimbilia popote tena. Nilifika mwisho wa jiko, nikakutakana na meza na ukutaย nyuma yangu.ย
Upande wa kushoto palikua na kisu, nilisogea taratibu huku nikiiambia nafsi yangu kuwaย nisipojiokoa sitaweza kupona, nilimpenda Mama yangu lakini aligeuka kua adui yangu. Nilipaswa kumshambulia kama alivyokua akinishambuliaย
Nilipapasa na kukishika kisu.ย
โMama, ni Mimi Celin, Mwanao hupaswi kunitendea hiviโ nilisema kwa mara ya mwisho, kamaย atanisikia na kuacha kunishambulia kwa maelekezo ya yule jini mbaya. Haikusaidia, Mamaย alikuja tena mithiri ya ndege tai ili anishambulieย
Sikujiuliza mara mbili nilipaswa kufanya nini, nilimkita kisu Cha shingo Mama yangu. Kilizamaย upande mmoja na kutokea upande mwingine. Mama aligugumia kwa mumivu mkali, ile hali yaย ushetani ilimtoka ghafla tu akawa Yule Mama niliyempenda kisha alidondoka chini akihema kwaย shida.ย
โMamaaโผโ nilimwita kwa sauti iliyojaa mashaka, kisha nilikaa chini na kukipakata kichwaย chake. Mama alikua akitapatapa kwa maumivu, alikua hawezi kusema chochote kutokana na kileย kisu nilicho mchoma nacho.ย
Alianza kukosa hewa, nilikua ninalia na kumwomba msamaha Mama yangu. Baba alikuja jikoniย akiwa katika hali ya kujitambua kabisa, alikua ameloa nguo zake. Alipotuona alishangaa sanaย kisha alikuja haraka pale chini na kuniuliza kilichompata Mama.
Niliishia kulia nikimtazama Mama, Baba akaniambia tumpeleke Hospitali Mama akapateย huduma ya kwanza, sikuwa na chaguo isipokua kumsikiliza, sote tulikua tumechanganikiwa ilaย Baba alichanganikiwa zaidi maana alionekana kutojua chochote kilichotokea. Muda huo mvuaย ilikua imeacha kunyesha, palikua tulivu na wala hapakua na hali yoyote yenye kutia wasiwasi.ย
Baba alimbeba Mama hadi nje, bahati nzuri palikua na Taxi moja iliyokua ikipita.ย Tuliisimamisha kisha tulimpakiza Mama, tulianza safari ya kuelekea Hospitali. Tulipofika,ย Mama alipokelewa kama mgonjwa mahututi anayehitaji huduma haraka sana bila maelezoย yoyote yale, aliingizwa chumba cha Upasuaji mara moja.ย
Mimi na Baba tulikaa kwenye Benchi, uso wa Baba yangu uliniambia vingi, kimojaย kilichotawala zaidi ni swali la nini kilichotokea hadi Mama akawa katika hali ile, Mimi ndiyeย niliyepaswa kumpa majibu Baba lakini atanielewa?ย ย
โCelinโ Baba aliniita, alikua amevalia shati la Mistari myeupe na suruali nyeusi na kiatu cheusiย chini. Niligeuka kumtazama maana nilikua nimejiinamia nikilia, chochote kitakachotokea basiย Mimi ndiye niliyesababisha. Chozi lilikua linanivujaย
Baba alipepesa macho yake akanitazama mara moja kisha akaangalia chini na kuniuliza kwaย sauti ya taratibu sana.ย
โMama yako amefikwa na nini, kile kisu Nani amemchoma?โ aliuliza Baba, nilibana midomoย yangu. Kila jibu nililo lifikiria kua lingekua jibu kwa Baba lingezua maswali zaidi, nilimtazamaย Baba ili kusoma sura yake alikua akifikiria nini.ย
Kisha nilimwambia Baba โSijui Baba, sijui nini kimetokea. Nimemkuta Mama katika hali ileโย Nililazimika kusema uwongo, Baba alishusha pumzi ndefu. Mtu mzima yeye, alihitaji ushawishiย zaidi kuamini nilikua sijui chochote kuhusu Mama.ย
โPolisi watakuja, tutawajibu hatujui?โ aliniuliza. Nilizidi kudondosha chozi.ย
โBaba, niamini sijui chochote. Nilimkuta akiwa katika hali ile Mimiโ nikizidi kujitetea mbele yaย Baba. Chozi lilikua likinibubujika huku nafsi yangu ikinisuta. Chochote kitakachomkuta Mama,ย wa kulaumiwa ni Mimi hapa Celin.ย
Basi Baba aliniegemeza kwenye bega lake ili kunipa faraja, niliendelea kulia huku tukisubiriaย taarifa kutoka chumba cha Upasuaji. Tulikaa kwa zaidi ya masaa mawili, jua lilikua likikimbiaย kwa kasi kuelekea kuzama, jioni ilikua imeshaingia, taa ziliwashwa kuonesha kua giza lilikuaย linajiandaa kuingia.ย
Nilikua na uchovu wa kukimbizana huku na kule, mwili ulikua na maumivu pia nilikua naย majeraha kadhaa ya kucha za Mama. Baada ya dakika kumi kupita, Daktari mmoja alitokaย chumba cha Upasuaji, tulikua tunasubiria kwa muda mrefu, tuliposikia mlango ukifunguliwaย tulisimama mara moja na kutazama.
Tulipomwona Daktari tulisogea aliposimama akituangalia, alikua akitokwa na jasho, alivuaย Barakoa kisha akajishika kiuno. Sura yake ilikosa tumaini, nilijikuta nikilegea mwili mzima.ย Baba akamuulizaย
โHali ya mgonjwa inaendeleaje?โ aliulza Baba kwa shahuku sana, yule Daktari akamtazamaย Baba, akashusha pumzi kidogo akasemaย
โTumejitahidi sanaโ kisha akatikisa kichwa halafu akaendeleaย
โJitihada zimezidi kudra, amefarikiโ sauti ya yule Dakati siwezi kuisahau, yaani ndani ya wikiย moja nilipoteza Watu watatu muhimu sana Maishani mwangu. Nilianza kumpoteza Zena, kishaย Caren, leo nampoteza Mama yangu Mzazi tena kwa mikono yangu Mimi mwenyewe, nilianguaย kilio cha Mtu mzima, nilihitaji nilie kwa uchungu tena kwa sauti kubwa kabisa.ย
Baba alinishikilia maana nilikua ninalia kwa kusaga meno, kilichoniliza zaidi ni kwambaย Mikono yangu ndiyo iliyoondoa Uhai wa Mama yangu, nilimuuwa mwenyewe katika hali yaย kujiokoa. Baba alitokwa na machozi huku akiwa ameufunga mdomo wake, aliitumia mikono yake kunibembeleza lakini haikusaidia.ย
Daktari akamwomesha Baba chumba kitupu ili tukakae huko kwa muda, Baba alinipeleka hukoย na kufunga mlango ili nilie hadi maumivu yaishe, palikua na viti viwili. Baba aliketi na kuniachaย sakafuni nilie hadi nimalize, nililia sana Mimi. Hakuna siku nililia sana kwenye Maisha yanguย kama siku hii, maneno ya yule Jini Bibi kizee yalitimia, nilitambaa hadi miguuni kwa Babaย nikamwambiaย
โNisamehe Babaโ nilisema nikiwa ninalia, japo nilikua ninalia lakini niliona maumivu hayaweziย kwisha kama sitasema ukweli mbele ya Baba yangu aliyekua hajui nini kilitokea, alikuaย akinitazama tu.ย ย
โNisamehe Mimi Baba , ni makosa yanguโ niliendelea kusema, Baba alishangaa inawezekanajeย yakawa ni makosa yangu. Aliniyanyua na kuniulizaย
โInawezekanaje ukasema ni makosa yako Celin?โ nilifuta chozi, nilihitaji ujasiri sasa kumwelezaย ukweli Baba. Nilianza kusema โKifo cha Mama ni Makosa yangu, mikono yangu niliyoipendaย imeondoa uhai wa Mtu ninayempendaโ Baba alihamaki akaniuliza kwa sauti kavuย
โUnasemaje?โย
โBaba, sikukusudia. Nimemuuwa Mama kwa bahati mbaya Mimi, nisamehe Baba Aaaahโผโย niliendelea kulia, nilimweleza Baba ukweli lakini hakuonekana kuukubali kabisa. Alinilea naย kunifundisha tabia njema, akasemaย
โSikukuzaa Muuwaji Celin, sitaki kuyaamini maneno yakoโ alisema Baba kwa uchungu sanaย kisha alipiga hatua za haraka na kwenda kujiinamia ukutani. Nilisikia kilio cha chinichini chaย Baba na manungโuniko, nilielewa ni vita ya ndani kwa ndani ndiyo iliyokua ikiendelea kwake.
Nilijiuliza nimwambie nini Baba yangu aniamini, nilimfuata alipo, hali ilibadilika na mimi ndiyeย niliyekua namtuliza Baba baada ya Baba kunituliza Mimiย
โBabaโผโ nilimwita, alikua amejiinamia. Hakutaka nilione chozi lake kabisa. Nilimwita tenaย akaniambiaย
โCelin, wewe siyo Muuwaji Mwanangu tena huwezi kumuuwa Mama yako Mzazi. Sitaki kusikiaย hizo hadithi, niambie nini kimemkuta Mama yako?โ alisema Baba akiwa ameuficha uso wakeย ukutani, macho yangu yalikua hayakauki chozi hata kidogo, niliendelea kububujisha choziย ย
โBaba, Mwanao nimepitia Mazingira magumu sana tena kwa siri msijue nyinyiโ nilisema, kilioย kilianza upya. Baba aligeuka kunitazama. Macho yake yalikua yamejawa na chozi, alihitajiย kusikia nilichotaka kukisema. Nilimtazama.ย
โChanzo cha yote ni ile nyumba Baba, ina majini na kaburi ambalo ndugu wawili wamezikwaย mle. Hakuna aliyeweza kuishi ndani ya ile nyumba salama, hata kifo cha Mama ni matokeo yaย usiri wanguโ Nilisema jambo ambalo lilimfanya Baba ashangae sanaย
โUmetoa wapi hayo unayoyasema Celin?โ aliniuliza Baba kwa Mshangao mkubwa sana, nilifutaย chozi langu nikaivaa roho ya Ujasiri ili nimsimulie Baba kila kitu. Nilimsimulia kila hatua, kilaย jambo. Hadi namaliza kumweleza Baba alikua ameketi kitini akinitazama kwa uzito sana. Suraย ya majonzi ilimtawala Baba yanguย
โKwanini ulificha jambo kubwa namna hiyo Celin, siri yako imeharibu Maisha yetu, siri yakoย imeondoa uhai wa Mama yako Celinโ alinilaumu Baba, nilikua tayari kupokea lawama zoteย maana tayari maji yalinifika shingoni, nilikua naangamia.ย
โUnafikiria Polisi wataelewa haya?โ aliniuliza Baba, tayari kitengo cha Polisi kilipokea taarifaย ya shambulio la Mama yangu. Walikua wameshafika, mlango ulikua ukigongwaย
Baba alinisogelea akaniambiaย
โKama unaweza kumaliza kila kitu basi maliza Celinโ alisema, kabla hata sijamjibu chochote Baba alielekea mlangoni na kufungua mlango, polisi walikua wamesimama mlangoni.ย
Baba aligeuka na kunitazama kisha alinipa ishara ya tumaini kwa kuniachia tabasamu.ย
โSisi ni maafisa wa Polisi, tunahitaji kuondoka na ninyi kwa ajili ya mahojianoโ alisema Polisiย mmoja, Baba akasemaย
โHaina haja ya kuondoka na sisi, peke yangu nitathibitisha kila kitu. Binti yangu hakuwepo eneoย la tukioโ alisema Baba, kauli yake ya ghafla ilionesha kua alikua ameubeba msalaba wangu.ย Polisi walinitazama kwa sekunde kadhaa huku nikiwa mwoga maana Mimi ndiye Muuwaji,ย kisha waliondoka na Baba yangu. Nililia sana, sikuwa na Mtu karibu yangu wa kuniambiaย maneno ya faraja.
Mama yangu alikua amefariki, Baba alikua mikononi mwa Polisi kwa makosa yangu Mimi. Nilijiinamia baada ya kulia kwa muda mrefu, baadaye nilitoka kwenye kile chumba. Nilipataย Ujasiri wa kuuliza namna ya kuipata Maiti ya Mama kwa ajili ya Maziko. Utaratibu ulikua niย lazima tulipie pesa kidogo ndipo watupatie maiti, sikua na pesa nilimwambia Daktari natakiwaย kurudi nyumbani kuchukua pesa. Akaniangalia kisha akaniambiaย
โUsijali Msichana, tayari maiti imelipiwaโ nilishangaa sana, ni Nani anayeweza kuilipia maiti yaย Mama yangu ili itoke Hospitalini. Nilimtazama kwa Mshangao halafu nikamuulizaย
โHivi nimekusikia ipasavyo?โย ย
โNdiyo, Mjomba wako amelipiaโ alipomaliza kusema nikamwona Mjomba Mgina akiwaย anakuja tulipokua tumesimama na Daktari. Huzuni iliniingia Upya kabisa, nilimkimbiliaย Mjomba na Kumkumbatia kwa Uchungu sana.ย
โPole Celin, pole sana Mjombaโ alisema huku akinipiga piga taratibu mgongoni katika hali yaย kunipoza machungu. Chozi lilinibubujika tena, kwakua tayari nilikua nimemueleza kila kituย Baba yangu sikutaka kuleta tena Mkanganyiko.ย
โInaniuma Mjomba, Mama amekufa kikatili sanaโ nilisema, maumivu yaliyokua yamejaaย moyoni mwangu yalikua yakinichoma mithiri ya sidano.ย
Basi, tuliitoa Maiti Hospitalini na kuipeleka nyumbani kwa Mjomba Mgina. Palitawala Majonziย na vilio, maswali yasiyo na Majibu. Uvumi kua Baba yangu alikua amemuuwa Mama yanguย ulianza kusambaa miongoni mwa waombolezaji, kila Mtu alimwita jina baya Baba yangu.ย
Nilizidi kuumia ndani ya Nafsi yangu, Baba yangu aliitwa Muuwaji kwa sababu ya kunisaidiaย Mimi. Alijivesha ngozi yangu kunificha Muuwaji halisi, nililia kwa mambo mengi yasiyo naย Majibu. Macho yalinivimba, kesho yake tulimzika Mama kwenye Makaburi ya Jiji.ย
Hatimaye Mama yangu aliungana na Zena na Caren kwenye makazi ya milele. Kilichokuaย kimebakia kwangu kilikua fumbo kubwa, hakuna aliyejua kuhusu ile nyumba yenye kaburi naย jini anayeuwa.ย
Sikutaka kumwambia yeyote, moyo wangu ulijawa na kisasi. Sikuuona umuhimu wa kuendeleaย kuishi ikiwa nimepoteza Wapendwa wangu kwa usiri wangu. Baba alifikishwa Mahakamani sikuย Nne baada ya kumzika Mama, alikiri mbele ya Mahakama kua alitenda Mauwaji hayo kwaย mikono yake kwa kile alichokiita wivu wa Mapenzi.ย
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NANE
COMMENTS ZIWE NYINGI SASAย
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx
18 Comments
Good https://is.gd/N1ikS2
Awesome https://is.gd/N1ikS2
Good https://is.gd/N1ikS2
Very good https://is.gd/N1ikS2
Aisee admin story timu kinomaaaaaa shusaa ya 8
ishiii mbna marudioo mzee
Admin mm ndy wa kwanza hii st0ry ip0 0n ๐ฅ asee
Good https://is.gd/N1ikS2
Aisee story timu admin yaan leta ya 8
Tunasubiri sehemu ya 8
Marudio hii admin
Marudio hii umetufowadia ya tarehe 1 .
ishiii mbna marudioo mzee
Story ni ๐ฅ๐ฅ sanaa,,tupe ya 8 bhas
Admin umenikamata aiseee story tamuuu
๐ฅ
Naomba group
yp2bmc