Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ufalme Wa Mazombi (Sehemu ya Kwanza-01)
    Hadithi

    Ufalme Wa Mazombi (Sehemu ya Kwanza-01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaApril 14, 2025Updated:April 16, 202517 Comments6 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kwa majina naitwa Bernard Pour. Mimi ni mtoto wa tatu kati ya watoto sita wa Bwana na Bi. Pour David. Yaliyonifanya leo kuwa na uwezo wa kukusimulia simulizi hii ya kusisimua ni yale niliyowahi kuyashuhudia. Mimi na familia yangu tunakaa mkoani Kagera, katika wilaya ya Ngara, ingawa nyumba yetu iko mbali na mji wa Ngara.

    Nakumbuka ilikuwa tarehe 23 ya mwezi wa saba, siku ya Ijumamosi. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya soko, hivyo mimi nilikuwa zamu ya kwenda sokoni kwa ajili ya manunuzi ya vyakula vitakavyotutosha kwa wiki nzima mpaka siku ya soko ijayo, maana soko hili la Kojifa huadhimishwa mara moja kwa wiki.

    Basi, nikaandaa vitu vyangu kwa lengo la kwenda sokoni, nikaandika mahitaji yote muhimu kwa familia yetu kwa hiyo wiki, kisha nikaenda kuchukua kadi ya benki na funguo za gari. Safari ya kwenda sokoni ilianza.

    Nilifika sokoni majira ya saa saba na nusu mchana, kisha nikafanya manunuzi ya bidhaa nilizohitaji. Baada ya kumaliza manunuzi hayo, safari ya kurejea nyumbani ilianza majira ya saa kumi na moja jioni.

    Sikumbuki ni vipi ilivyotokea, lakini ninachokumbuka ni kwamba nilipofika kwenye janki ya wilaya ya Ngara, gari langu lilipinduka baada ya kugongwa na lori ambalo lilikuwa likitoka Kabanga kuelekea Benako. Zaidi ya hapo, sikumbuki kilichotokea maana nilipoteza fahamu palepale.

     

    Nakumbuka siku ambayo nilipata fahamu zangu, nilijikuta nikiwa kitandani nimelala. Harufu kali ya vumbi ilitawala kwenye tundu za pua yangu. Taratibu, nikaamua kufumbua macho yangu, ingawa nilishindwa kutokana na vumbi lililokuwa likinikalia usoni. Baada ya muda, nikaweza kufumbua macho yangu na nikashangaa sana na eneo niliyokuwa nikiishi kwa wakati huo.

    “Mungu wangu! Hapa ni wapi?” nilijiuliza huku nikishangaa mazingira ya mahali niliyokuwa.

    Taratibu, nikainua mkono wangu, kisha mwingine, na kwa pamoja nikainua mwili wangu wote huku nikiwa na uchovu wa ajabu. Nilishuka kitandani huku nikiwa na mshangao mkubwa kutokana na mazingira ya chumba hicho. Nilianza kutazama kuta za chumba hicho, lakini sikuweza kupata majibu ya maswali yote yaliyokuwa najiuliza.

    Kuta zilikuwa zimejaa utando wa buibui na vumbi lilikuwa limejaa kila kona ya chumba hicho. Nilipoangalia kitanda, niliona kimejaa vumbi huku mchoro wa mwili wangu ukiwa umeachwa pale nilipokuwa nimelala.

    “Hapa ni wapi?” nilijiuliza huku nikianza kupiga hatua fupi kuelekea kwenye mlango wa chumba hicho. Lakini kabla sijafika, niliona kioo kilichokuwa kando ya mlango. Taratibu, nikaelekea kwenye kioo hicho.

    “What?” Nilijikuta nikisema neno hilo huku nikiapapasa uso wangu kwa mikono yangu.

    “Nini hiki?” nikajiuliza huku nikiangalia sura yangu kwenye kioo.

    Nywele zangu zilikuwa nyingi sana, ndevu zilikuwa zimetapakaa usoni mwangu kiasi cha kufanya midomo yangu kutoshuhudiwa kutokana na ndevu hizo. Uso wangu ulikuwa umejaa vumbi, kana kwamba sikuwa nimejua maji kwa zaidi ya mwaka au miaka.

    “Mbona sijielewi mimi jamani?” nikazidi kuwaza huku maswali mengine yakijaa akilini mwangu. Mawazo hayo hayakuacha kukatiza katika ubongo wangu, lakini majibu ya maswali hayo hayakuwa na nafasi ndani ya fahamu yangu.

    Taratibu, nikasogea kuelekea mlango wa chumba hicho. Hata kabla sijaufungua, pembeni niliona hotipoti la chakula. Ile hamu ya kufungua mlango ikakata, na taratibu nikaanza kuisogeza hotipoti hiyo ili nitazame kilichokuwa ndani yake.

    Hatua zangu zilitia nanga karibu na hotipoti hilo lililokuwa limejaa vumbi. Taratibu, nikaelekeza mikono yangu kwa hotipoti hiyo, nikafungua na kutazama kilichomo.

    “Mungu wangu!!” nilisema neno hilo baada ya kugundua kwamba chakula kile kimekauka baada ya kuoza.

    “Hiki kitu gani jamani?” nikazidi kuwaza huku nikiwa sina majibu ya kile nilichokuwa nikifikiria. Hatua zangu zikasogea kuelekea mlango wa chumba hicho, maana shauku ya kutaka kujua ni wapi nilikuwa ilijaa kichwani mwangu.

    Taratibu, nikafungua mlango wa chumba hicho huku mawazo yangu yakiwa mengi sana. Ngazi zilizo nje ya chumba hicho zilikumbusha kwamba nilikuwa nyumbani kwetu. Taratibu na kwa tahadhari kubwa, nikaanza kushuka ngazi huku mawazo mengi kichwani mwangu.

    “Kweli, wapo wapi wengine? Mbona hapa ni kimya kiasi hiki?” nilizidi kuwaza huku maswali yangu yakionekana kuwa fumbo kubwa sana.

    Nilisimama nilipofika kwenye sebule ya nyumbani kwetu. Muonekano wa masofa uliniishangaza zaidi, huku mawazo mbalimbali yakijaa kichwani mwangu. Masofa yalikuwa yamejaa vumbi, kana kwamba kwa muda mrefu sana hayakuwa yamefanikiwa kusafishwa wala kukaliwa na watu.

    “Kweli, wapo wapi wengine?” nikazidi kuwaza huku maswali yangu yakizidi kuwa fumbo kubwa kichwani mwangu.

    Taratibu, nikasogea dirishani na kusogeza pazia, huku vumbi likiendelea kusumbua tundu za pua zangu. Chafya ndiyo ilifuata baada ya vumbi kugusa mfumo wangu wa upumuaji.

    Baada ya kufungua dirisha na kuanza kutazama nje ya jengo letu, muonekano wa mazingira ulinishtua sana. Kwanza, kulikuwa kumepoteza ule muonekano wa kuvutia. Majani mazuri ambayo yalikuwa yakipendezesha ardhi ya mtaa wetu hayakuwapo tena; badala yake, yalikuwa yamekauka yote, kana kwamba mvua haikunyesha kwa zaidi ya miaka mitano au zaidi.

    Miti ilikuwa imekauka na kupoteza matawi yake. Majumba yaliyokuwa jirani nasi yalikuwa yamechakaa sana, kana kwamba kwa miaka mingi hayakuwa yakikaliwa na watu.

    “Nini hiki jamani? Mbona sielewi?” nikazidi kuwaza huku majibu ya maswali yangu yakiwa hayapatikani kabisa. Macho yangu niliyaelekeza nje kupitia dirishani, nikitazama muonekano wa majengo na mazingira ya mtaa wetu.

    “We nani? Maana unaonekana hujapatwa na janga hili,” sauti iliyouliza swali niliisikia nyuma yangu. Taratibu, nikageuka maana sauti ile haikuwa ngeni masikioni mwangu.

    Nikageuza uso wangu polepole, nikimtazama aliyeniita, hata kabla sijajibu swali lake. Kumbe alikuwa mdogo wangu, ananyenifuata, nilifahamu hilo baada ya kuutazama uso wake.

    “Sebastian,” niliita kwa hisia.

    “Kumbe ni Bernard, nilikuwa sijakufahamu kwa sababu ya ndevu zako na nywele zako hizo ndefu kama nini,” mdogo wangu alizungumza, na kunifanya niachie tabasamu.

    Pale pale akaanguka chini na kutapika damu.   

    “Seba…!” Niliita jina lake kwa kifupi sana huku nikimsogelea haraka.

    “Usinisogelee,” alisema huku akinitazama kwa makini sana.

    “Kwanini? Na nini kimekukuta?” Niliuliza maswali mawili mfuatano huku nikimtazama kwa umakini sana alivyokuwa akitaabika pale chini.

    “Kwasasa nchi yetu imeharibika kaka,” alisema kwa sauti ya huzuni.

    “Kivipi?” niliuliza, huku nikipiga hatua kumsogelea.

    “Nimekwambia usinisogelee,” alisema kwa hasira, huku akinitazama kwa umakini wa ajabu. Hali hiyo ilinifanya kusimama na kumtazama kwa mshangao.

    “Ka-kaka! Kwasasa ardhi yetu haina makazi. Namaanisha kwamba tangu mwaka mmoja uliopita, virusi visivyo fahamika vimetawala, na sasa watu wengi sana wamekuwa mazombi. Wakikung’ata, lazima uwe zombi. Nampaka sasa, nimebakiza sekunde chache sana niwe zombi,” alisema huku mimi nikiwa sielewi kile anachozungumza. Kuanzia virusi, sijui mwaka mmoja, mpaka yeye kuwa zombi muda si mlefu, nilizidi kuchanganyikiwa huku nikiwa sina majibu kabisa ya kile nilikuwa nikifikiria.

    “Kimbia!” alisema Sebastian huku akinitazama kwa umakini, na sauti aliyoitumia ilikuwa imejaa mamlaka.

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Pili 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx Ufalme wa mazombi xx

    riwaya mpya riwaya za kusisimua ufalme wa mazombi

    17 Comments

    1. Yusuph jr mvanda on April 14, 2025 8:13 pm

      Waoooh nice story

      Reply
      • G shirima on April 14, 2025 9:06 pm

        Kisa Cha kweli bana

        Reply
        • Zaillah Cute on April 15, 2025 1:14 pm

          Jaman nzul mnooo unawez kutungaa

          Reply
      • Joseph kidanha on April 18, 2025 4:53 pm

        BiggerF bro for fantastic story. God bless you at your dream 🌱 and at your plans

        Reply
    2. Fungo on April 14, 2025 8:26 pm

      Noma🔥🔥🔥🙌

      Reply
    3. Anzirani on April 14, 2025 8:55 pm

      Ni

      Reply
    4. Yuster on April 14, 2025 11:15 pm

      Viwango vingine👏

      Reply
    5. Rachel Richard on April 14, 2025 11:27 pm

      Mungu wangu yan kama movie vile ila story tamu

      Reply
    6. Romaney on April 15, 2025 10:57 am

      Vitu vya resident evils
      Au sio

      Reply
    7. Sarah on April 15, 2025 11:44 am

      Nice🙌

      Reply
    8. David ben on April 16, 2025 2:43 pm

      Nzuri mwandishi

      Reply
    9. David ben on April 16, 2025 2:44 pm

      Tunahitaji mwendelezo

      Reply
    10. Joseph kidanha on April 18, 2025 4:55 pm

      BiggerF bro for fantastic story. God bless you at your dream 🌱 and at your plans

      Reply
    11. Dakota2695 on April 27, 2025 1:55 pm

      Good https://t.ly/tndaA

      Reply
    12. Clint2379 on April 29, 2025 6:32 am

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    13. Bill919 on April 30, 2025 11:12 am

      Good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    14. Gail4853 on April 30, 2025 10:33 pm

      Very good https://is.gd/N1ikS2

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.