Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (04)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 8, 2025Updated:January 8, 202512 Comments6 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Shiii‼” Baba Mkwe akanipa ishara katili ya kunitaka nikae kimya vinginevyo kile kisu  kingeingia mwilini mwangu. Kisha akachuchumaa na kuniambia

    “Leo utajuwa ni kwanini uliolewa Binti” Alisema halafu akayaongea maneno fulani  nisiyoyaelewa, nakumbuka kabisa hayakuwa maneno ya lugha ya Kiswahili bali lugha  nisiyoifahamu na wala si Kiingereza wala Kiarabu. Wale Watu wakasimama kisha wakaenda  kupotelea kwenye kona za kile chumba kilichojaa harufu ya Udi. Endelea 

    SEHEMU YA NNE 

    Nilikua kama naangalia filamu vile, hata wewe msomaji unaweza fikiria ilikua ni filamu na  ninakusimulia hapa. Hapana ni Simulizi ya kweli, simulizi hii ikusaidie kufanya chaguo sahihi  wakati wa kuolewa au Kuowa ili usije pitia kama Mimi, haya mambo siyo tu kwa Mwanamke  hata Mwanaume anaweza tendewa hivi. Tuendelee sasa 

    Mate hayakumezeka wala pumzi hazikutulia, yule Mzee alikua amenikata jicho kali kisha  kaniambia kwa maneno yenye vituo vingi kuashiria kuwa anamaanisha anachokisema,  akaniambia 

    “Umeolewa ili uje kuishi na Misukule hapa, huu ndiyo utajiri wangu. Wewe siyo wa kwanza  kuolewa na Salehe, walioenda kinyume walifia humu na kupotea kabisa wao pamoja na Familia  zao” Yaani nilizidi kuishiwa nguvu, Mungu wangu jasho lilinitoka kama nimemwagiwa maji.  Kisha Mzee akaendelea 

    “Hii ni nyumba yangu Mimi siyo ya Salehe, yule ni Mtoto wangu na ndiye anayenisaidia Mimi.  Utakua unafanya mapenzi na Msukule mmoja mmoja Kila baada ya Siku tatu. Usijaribu  kutoroka ndani ya nyumba hii wala kutoa siri popote, narudia kwa Msistizo ili uelewe  ninachomaanisha. Utawaponza Wazazi wako kwa Ujinga wako mwenyewe” Chozi lilizidi  kunitoka kisha yule Mzee akasimama akaninyooshea Kidole 

    “Utafanya niyatakayo ili kuilinda familia yako, hutaruhusiwa kutumia simu na hutatoka nje  isipokua kwa maagizo maalum kutoka Kwangu” kisha yule Mzee aliondoka zake na kunicha  ndani ya kile chumba, wala hakunifungia kuonesha kuwa anajiamini na anachokisema. Kiukweli  Nililia sana kwa kwikwi, nililia Mno sababu niliona wazi kuwa ili wazazi Wangu wawe salama napaswa kutumikia Misukule ya yule Mzee na kama nataka kuwa huru basi nitawapoteza Wazazi  wangu ambao hawakuwa na Hatia yoyote ile. 

    Katika Maisha yangu niliutunza usichana wangu kwa ajili ya Mume wangu lakini nililazinika  kuutoa kwa Misukule, nilijilaumu kwa kumwamini Salehe, nilimlaani sana. Nikiwa ninalia  akaingia tena yule Mzee akiwa amehamaki akaniuliza 

    “Simu yako ipo wapi?” alishikilia kisu mkononi, sikupepesa maneno nilimpa simu mara moja  kisha akaondoka nayo. Wala hakufunga mlango aliuwacha wazi ikiwa ni ishara ya kuniruhusu  kuwa huru ndani ya nyumba lakini siyo kuondoka, ndiyo kwa mara ya kwanza katika Maisha  yangu niliushuhudia Uchawi wa waziwazi. 

    Basi, nilirudi chumbani nikiwa ninalia, nilikua mwenyewe kwenye Maisha yangu. Sikuwa na  Mtu wa kumueeleza ninayopita, sikuwa na msaada na pengine kaburi langu lingekuwa ndani ya ile nyumba. Kitu cha kwanza kufanya kilikua ni kufuta chozi langu, kwanini niliruhusu  lidondoke chozi langu lenye thamani kubwa. Hata ningelia vipi isingelisaidia Mimi kupona  

    Nilijiegemeza kwenye Mto nikatafakari mengi, nikapata jibu la uhakika kabisa kuwa siku ile  nilifanya mapenzi na Msukule na ndiye aliyenitoa Usichana wangu kwa mara ya kwanza  nikifikiria ni Salehe. Kitu fulani cha uchungu kilijaa kifuani pangu, hakika nilitendewa unyama  sana na Salehe na Baba yake. Nilijua Baba na Mama wangekuwa na wasiwasi na Mimi kama  nitakaa kwa siku nyingi pasi na kuwasiliana nao lakini ningefanya nini sasa na ilinibidi nikae nao  mbali ili kuokoa Maisha yao.  

    “Eeh Mungu, umeniptisha kwenye Mtihani gani sasa. Hukuona mitihani mingine rahisi kwangu  isipokua huu?” Nilituma lawama ma maswali kwa Mungu wangu, kumbe ukiona Mtu  anamkufuru Mungu si kwa kutaka bali kwa kukosa majibu sahihi ya kuondoka kwenye matatizo.  

    *** 

    Masaa yalienda, sikupata hata lepe la kuusingizia Usingizi yaani nilikua na kichwa kizito sana  japo Usiku ulikua umeenda. Hakuna sauti ya kutisha niliacha kuisikia Usiku huu, yaani Mzee  Mwinyimkuu alinionesha Uchawi dhahiri kabisa. Sauti za Watoto Wachanga nilizisikia bila  kificho, nyimbo za ajabu ajabu ziliimbwa na kuchezwa nikajiona kama nimeshafika kuzimu.  Nikazikumbuka Riwaya kadhaa nilizokua nazisoma mtandaoni na stori za hapa na pale juu ya  Uchawi, nilikua siziamini lakini hatimaye nilijikuta ndani ya moja ya Riwaya ya kutisha sana. 

    Mimi Saida nilikosa majibu ya maswali yote hata yale madogo niliyojiuliza. Bundi walisikika  Usiku kucha, hadi kuna pambazuka nilikua macho hata taa sikuizima kwa kuhofia kuingiliwa  tena na yule Msukule. Kukesha macho usiku mzima haikua rahisi, macho yalivimba hasa  ukizingatia nililia sana 

    Niliogopa kutoka chumbani, sikuwa na amani kama siku ya kwanza. Nilikaa kitandani nikipiga  Mihayo, mara Mlango uligongwa, nilishtuka nkasema moyoni sasa naenda kupelekwa kwa  Misukule, hofu ikaamka upya ndani yangu lakini nikamsikia Mzee Mwinyimkuu akisema 

    “Amka uandae chai haraka” alisema kwa jazba fulani baada ya kugonga kwa kitambo kisha  nikayasikia makubhasi yake yakifanya safari kutoka mlangoni kwangu. Moyo ulinidunda sana  kiukweli, sikuwa na raha wala amani yoyote ile. Ningefanya nini zaidi ya kuamka na kwenda  kumwandalia chai yule Mzee, Binafsi sikuhisi njaa kabisa licha ya kutokula jana kutwa nzima. 

    Niliufungua Mlango taratibu sana, nikasikia kama Mtu anafanya Usafi hivi, nilipoangalia vizuri  niliona tu ufagio pekee ukifagia bila kumwona aliyeushikilia ule ufagio, nusura nizame tena  ndani kwa woga lakini nikapata kiu ya kuona zaidi. Huuu‼! Uchawi unatisha sana na  nimeushuhudia laivu bila chenga, niliporudisha macho tena sikuona chochote isipokua nyumba  ilikua safi sana

    Basi nikaanza safari fupi ya kupita koridoni na kuelekea jikoni kuandaa chai ya Mzee  Mwinyimkuu. Ile naingia tu nikakutana naye ndunda ndunda. 

    “Muda wote ulikua unafanya nini wewe?” aliniuliza kwa hasira sana kama vile tulikua  tumegombana. Hofu ilinianza upya hata sikuweza kutoa sauti yoyote ile, nikainamia chini,  Jamani nilikuja kushtukizwa na kibao cha shavu la kushoto hadi nikahisi giza. Alinipiga kibao  kizito hadi nikapepesuka pembeni, mateso makali yalianza kwangu 

    Sikuweza kutoa sauti yoyote ile isipokua chozi na maumivu yaliyojaa ndani ya Moyo wangu. 

    “Usiniletee upumbavu, hukuja kulala hapa wala kutembea. Kumbuka maneno yangu, Utafia  humu ukileta kiburi, pesa hii hapa Nunua chapati urudi haraka” alisema Mzee Mwinyimkuu,  akanipa Elfu tano mpya kabisa. Kisha yeye aliondoka zake akaelekea sebleni, alionekana  anajiamini na maneno yake ndiyo maana aliniruhusu nitoke nikamnunulie Chapati, wakati nataka  kutoka akapaza sauti yake akaniambia ninunue chapati za hela yote 

    Sikuwa na maswali mengi kuwa chapati zinaenda kuliwa na Nani sababu hata ule Mchicha  nilikua na uhakika kuwa unaliwa na Misukule niliyoiona Usiku. Nilihisi kukonda kwa siku moja  tu ya hekaheka, nilitoka nikafungua geti kisha nikatoka ndani, taratibu nikawa naeleka kwa yule  Mama anayeuza Chapati nyumba kama ya Nne hivi kutoka nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. 

    Macho yangu yaliitazama sana ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, nje Watu walikua  wakiendelea na shughuli zao, niliamini hakuna anayejuwa kinachoendelea. Nilitamani  nimsimulie Mtu pengine nimwombe msaada lakini nikakumbuka onyo nililopewa na Mzee  Mwinyimkuu, Ah! Hamu iliniisha………. 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TANO YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    12 Comments

    1. Mama eddy on January 8, 2025 3:22 pm

      Duuuh kuna kitu cha kujifunza apa

      Reply
      • Ahmed Ruta on January 8, 2025 3:28 pm

        Ndo Iko nilichowambia ndo Cha kujifunza

        Reply
      • Fatbaloz on January 8, 2025 5:01 pm

        Gud gud

        Reply
    2. Ahmed Ruta on January 8, 2025 3:27 pm

      Kwaiyo apo mabinti mjufunze msitunze bikra nadhan nyie wenyewe mmejionea kwa mwenzenu Saida YANGU NI AYO

      Reply
      • Fawziya Hassan on January 8, 2025 4:11 pm

        Jamani Saida hadi huruma😔😔
        Uchawi upo kweli tuwe makini na wanaume watakao tuowa
        Simulizi ya vitisho yenye maajabu na mafunzo makubwa kwa wanwake na wanaume wanaopenda Mimama.

        Reply
        • LEVI COLISON NDOKOLE on January 8, 2025 10:32 pm

          Huwezi jua tabia za mtu hvihvi tu

          Reply
      • Fawziya Hassan on January 8, 2025 4:21 pm

        Salehe Namba mbili ni Wewe

        Reply
      • [email protected] on January 8, 2025 9:49 pm

        Ya Leo fupi sn Admin jmn Hila ianzidi kunoga . Nawza tu Saida kwann anashinda ht kusema MUNGU nisaidie . Dah! Hapo kwenye kuwapa misukule kwa zamu shindwa shetani .🤭

        Reply
      • [email protected] on January 8, 2025 10:23 pm

        Sa itakuwaje

        Reply
    3. Hamisi halidi on January 8, 2025 6:09 pm

      Yaleo fupi sna boss

      Reply
    4. Frae on January 9, 2025 7:55 am

      Wendelezo kak

      Reply
    5. Cathbert on January 13, 2025 7:42 pm

      Kikubwa kuomba Mungu

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.