Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (04)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 8, 2025Updated:January 8, 202515 Comments6 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Shiiiโ€ผโ€ Baba Mkwe akanipa ishara katili ya kunitaka nikae kimya vinginevyo kile kisuย  kingeingia mwilini mwangu. Kisha akachuchumaa na kuniambia

    โ€œLeo utajuwa ni kwanini uliolewa Bintiโ€ Alisema halafu akayaongea maneno fulaniย  nisiyoyaelewa, nakumbuka kabisa hayakuwa maneno ya lugha ya Kiswahili bali lughaย  nisiyoifahamu na wala si Kiingereza wala Kiarabu. Wale Watu wakasimama kisha wakaendaย  kupotelea kwenye kona za kile chumba kilichojaa harufu ya Udi. Endeleaย 

    SEHEMU YA NNEย 

    Nilikua kama naangalia filamu vile, hata wewe msomaji unaweza fikiria ilikua ni filamu naย  ninakusimulia hapa. Hapana ni Simulizi ya kweli, simulizi hii ikusaidie kufanya chaguo sahihiย  wakati wa kuolewa au Kuowa ili usije pitia kama Mimi, haya mambo siyo tu kwa Mwanamkeย  hata Mwanaume anaweza tendewa hivi. Tuendelee sasaย 

    Mate hayakumezeka wala pumzi hazikutulia, yule Mzee alikua amenikata jicho kali kishaย  kaniambia kwa maneno yenye vituo vingi kuashiria kuwa anamaanisha anachokisema,ย  akaniambiaย 

    โ€œUmeolewa ili uje kuishi na Misukule hapa, huu ndiyo utajiri wangu. Wewe siyo wa kwanzaย  kuolewa na Salehe, walioenda kinyume walifia humu na kupotea kabisa wao pamoja na Familiaย  zaoโ€ Yaani nilizidi kuishiwa nguvu, Mungu wangu jasho lilinitoka kama nimemwagiwa maji.ย  Kisha Mzee akaendeleaย 

    โ€œHii ni nyumba yangu Mimi siyo ya Salehe, yule ni Mtoto wangu na ndiye anayenisaidia Mimi.ย  Utakua unafanya mapenzi na Msukule mmoja mmoja Kila baada ya Siku tatu. Usijaribuย  kutoroka ndani ya nyumba hii wala kutoa siri popote, narudia kwa Msistizo ili ueleweย  ninachomaanisha. Utawaponza Wazazi wako kwa Ujinga wako mwenyeweโ€ Chozi lilizidiย  kunitoka kisha yule Mzee akasimama akaninyooshea Kidoleย 

    โ€œUtafanya niyatakayo ili kuilinda familia yako, hutaruhusiwa kutumia simu na hutatoka njeย  isipokua kwa maagizo maalum kutoka Kwanguโ€ kisha yule Mzee aliondoka zake na kunichaย  ndani ya kile chumba, wala hakunifungia kuonesha kuwa anajiamini na anachokisema. Kiukweliย  Nililia sana kwa kwikwi, nililia Mno sababu niliona wazi kuwa ili wazazi Wangu wawe salama napaswa kutumikia Misukule ya yule Mzee na kama nataka kuwa huru basi nitawapoteza Wazaziย  wangu ambao hawakuwa na Hatia yoyote ile.ย 

    Katika Maisha yangu niliutunza usichana wangu kwa ajili ya Mume wangu lakini nililazinikaย  kuutoa kwa Misukule, nilijilaumu kwa kumwamini Salehe, nilimlaani sana. Nikiwa ninaliaย  akaingia tena yule Mzee akiwa amehamaki akaniulizaย 

    โ€œSimu yako ipo wapi?โ€ alishikilia kisu mkononi, sikupepesa maneno nilimpa simu mara mojaย  kisha akaondoka nayo. Wala hakufunga mlango aliuwacha wazi ikiwa ni ishara ya kuniruhusuย  kuwa huru ndani ya nyumba lakini siyo kuondoka, ndiyo kwa mara ya kwanza katika Maishaย  yangu niliushuhudia Uchawi wa waziwazi.ย 

    Basi, nilirudi chumbani nikiwa ninalia, nilikua mwenyewe kwenye Maisha yangu. Sikuwa naย  Mtu wa kumueeleza ninayopita, sikuwa na msaada na pengine kaburi langu lingekuwa ndani yaย ile nyumba. Kitu cha kwanza kufanya kilikua ni kufuta chozi langu, kwanini niliruhusuย  lidondoke chozi langu lenye thamani kubwa. Hata ningelia vipi isingelisaidia Mimi kuponaย ย 

    Nilijiegemeza kwenye Mto nikatafakari mengi, nikapata jibu la uhakika kabisa kuwa siku ileย  nilifanya mapenzi na Msukule na ndiye aliyenitoa Usichana wangu kwa mara ya kwanzaย  nikifikiria ni Salehe. Kitu fulani cha uchungu kilijaa kifuani pangu, hakika nilitendewa unyamaย  sana na Salehe na Baba yake. Nilijua Baba na Mama wangekuwa na wasiwasi na Mimi kamaย  nitakaa kwa siku nyingi pasi na kuwasiliana nao lakini ningefanya nini sasa na ilinibidi nikae naoย  mbali ili kuokoa Maisha yao.ย ย 

    โ€œEeh Mungu, umeniptisha kwenye Mtihani gani sasa. Hukuona mitihani mingine rahisi kwanguย  isipokua huu?โ€ Nilituma lawama ma maswali kwa Mungu wangu, kumbe ukiona Mtuย  anamkufuru Mungu si kwa kutaka bali kwa kukosa majibu sahihi ya kuondoka kwenye matatizo.ย ย 

    ***ย 

    Masaa yalienda, sikupata hata lepe la kuusingizia Usingizi yaani nilikua na kichwa kizito sanaย  japo Usiku ulikua umeenda. Hakuna sauti ya kutisha niliacha kuisikia Usiku huu, yaani Mzeeย  Mwinyimkuu alinionesha Uchawi dhahiri kabisa. Sauti za Watoto Wachanga nilizisikia bilaย  kificho, nyimbo za ajabu ajabu ziliimbwa na kuchezwa nikajiona kama nimeshafika kuzimu.ย  Nikazikumbuka Riwaya kadhaa nilizokua nazisoma mtandaoni na stori za hapa na pale juu yaย  Uchawi, nilikua siziamini lakini hatimaye nilijikuta ndani ya moja ya Riwaya ya kutisha sana.ย 

    Mimi Saida nilikosa majibu ya maswali yote hata yale madogo niliyojiuliza. Bundi walisikikaย  Usiku kucha, hadi kuna pambazuka nilikua macho hata taa sikuizima kwa kuhofia kuingiliwaย  tena na yule Msukule. Kukesha macho usiku mzima haikua rahisi, macho yalivimba hasaย  ukizingatia nililia sanaย 

    Niliogopa kutoka chumbani, sikuwa na amani kama siku ya kwanza. Nilikaa kitandani nikipigaย  Mihayo, mara Mlango uligongwa, nilishtuka nkasema moyoni sasa naenda kupelekwa kwaย  Misukule, hofu ikaamka upya ndani yangu lakini nikamsikia Mzee Mwinyimkuu akisemaย 

    โ€œAmka uandae chai harakaโ€ alisema kwa jazba fulani baada ya kugonga kwa kitambo kishaย  nikayasikia makubhasi yake yakifanya safari kutoka mlangoni kwangu. Moyo ulinidunda sanaย  kiukweli, sikuwa na raha wala amani yoyote ile. Ningefanya nini zaidi ya kuamka na kwendaย  kumwandalia chai yule Mzee, Binafsi sikuhisi njaa kabisa licha ya kutokula jana kutwa nzima.ย 

    Niliufungua Mlango taratibu sana, nikasikia kama Mtu anafanya Usafi hivi, nilipoangalia vizuriย  niliona tu ufagio pekee ukifagia bila kumwona aliyeushikilia ule ufagio, nusura nizame tenaย  ndani kwa woga lakini nikapata kiu ya kuona zaidi. Huuuโ€ผ! Uchawi unatisha sana naย  nimeushuhudia laivu bila chenga, niliporudisha macho tena sikuona chochote isipokua nyumbaย  ilikua safi sana

    Basi nikaanza safari fupi ya kupita koridoni na kuelekea jikoni kuandaa chai ya Mzeeย  Mwinyimkuu. Ile naingia tu nikakutana naye ndunda ndunda.ย 

    โ€œMuda wote ulikua unafanya nini wewe?โ€ aliniuliza kwa hasira sana kama vile tulikuaย  tumegombana. Hofu ilinianza upya hata sikuweza kutoa sauti yoyote ile, nikainamia chini,ย  Jamani nilikuja kushtukizwa na kibao cha shavu la kushoto hadi nikahisi giza. Alinipiga kibaoย  kizito hadi nikapepesuka pembeni, mateso makali yalianza kwanguย 

    Sikuweza kutoa sauti yoyote ile isipokua chozi na maumivu yaliyojaa ndani ya Moyo wangu.ย 

    โ€œUsiniletee upumbavu, hukuja kulala hapa wala kutembea. Kumbuka maneno yangu, Utafiaย  humu ukileta kiburi, pesa hii hapa Nunua chapati urudi harakaโ€ alisema Mzee Mwinyimkuu,ย  akanipa Elfu tano mpya kabisa. Kisha yeye aliondoka zake akaelekea sebleni, alionekanaย  anajiamini na maneno yake ndiyo maana aliniruhusu nitoke nikamnunulie Chapati, wakati natakaย  kutoka akapaza sauti yake akaniambia ninunue chapati za hela yoteย 

    Sikuwa na maswali mengi kuwa chapati zinaenda kuliwa na Nani sababu hata ule Mchichaย  nilikua na uhakika kuwa unaliwa na Misukule niliyoiona Usiku. Nilihisi kukonda kwa siku mojaย  tu ya hekaheka, nilitoka nikafungua geti kisha nikatoka ndani, taratibu nikawa naeleka kwa yuleย  Mama anayeuza Chapati nyumba kama ya Nne hivi kutoka nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu.ย 

    Macho yangu yaliitazama sana ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, nje Watu walikuaย  wakiendelea na shughuli zao, niliamini hakuna anayejuwa kinachoendelea. Nilitamaniย  nimsimulie Mtu pengine nimwombe msaada lakini nikakumbuka onyo nililopewa na Mzeeย  Mwinyimkuu, Ah! Hamu iliniisha……….ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TANO YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    15 Comments

    1. Mama eddy on January 8, 2025 3:22 pm

      Duuuh kuna kitu cha kujifunza apa

      Reply
      • Ahmed Ruta on January 8, 2025 3:28 pm

        Ndo Iko nilichowambia ndo Cha kujifunza

        Reply
      • Fatbaloz on January 8, 2025 5:01 pm

        Gud gud

        Reply
    2. Ahmed Ruta on January 8, 2025 3:27 pm

      Kwaiyo apo mabinti mjufunze msitunze bikra nadhan nyie wenyewe mmejionea kwa mwenzenu Saida YANGU NI AYO

      Reply
      • Fawziya Hassan on January 8, 2025 4:11 pm

        Jamani Saida hadi huruma๐Ÿ˜”๐Ÿ˜”
        Uchawi upo kweli tuwe makini na wanaume watakao tuowa
        Simulizi ya vitisho yenye maajabu na mafunzo makubwa kwa wanwake na wanaume wanaopenda Mimama.

        Reply
        • LEVI COLISON NDOKOLE on January 8, 2025 10:32 pm

          Huwezi jua tabia za mtu hvihvi tu

          Reply
      • Fawziya Hassan on January 8, 2025 4:21 pm

        Salehe Namba mbili ni Wewe

        Reply
      • [email protected] on January 8, 2025 9:49 pm

        Ya Leo fupi sn Admin jmn Hila ianzidi kunoga . Nawza tu Saida kwann anashinda ht kusema MUNGU nisaidie . Dah! Hapo kwenye kuwapa misukule kwa zamu shindwa shetani .๐Ÿคญ

        Reply
      • [email protected] on January 8, 2025 10:23 pm

        Sa itakuwaje

        Reply
    3. Hamisi halidi on January 8, 2025 6:09 pm

      Yaleo fupi sna boss

      Reply
    4. Frae on January 9, 2025 7:55 am

      Wendelezo kak

      Reply
    5. Cathbert on January 13, 2025 7:42 pm

      Kikubwa kuomba Mungu

      Reply
    6. ๐Ÿ–ฑ Ticket: TRANSACTION 1,569368 BTC. Next >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=0e4476252400ba80a2cc5a0ed1a892cb& ๐Ÿ–ฑ on July 8, 2025 9:34 am

      nc4vte

      Reply
    7. ๐Ÿ“€ System Alert - 1.9 Bitcoin withdrawal attempt. Deny? => https://graph.org/TAKE-YOUR-BITCOIN-07-23?hs=0e4476252400ba80a2cc5a0ed1a892cb& ๐Ÿ“€ on August 12, 2025 5:35 pm

      if7dcv

      Reply
    8. ๐Ÿ“ ๐Ÿ” Security Required - 0.6 BTC transaction held. Proceed here > https://graph.org/UNLOCK-CRYPTO-ASSETS-07-23?hs=0e4476252400ba80a2cc5a0ed1a892cb& ๐Ÿ“ on August 28, 2025 4:51 am

      hrr09y

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.