Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Jasusi Sehemu Ya Kumi Na Nne (14)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Kumi Na Nne (14)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaDecember 12, 2024Updated:December 13, 202431 Comments13 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia

    Mbaga akajiweka sawa kwa ajili ya kujibu mapigo kutoka kwa Malaika, akabonyea kidogo na kukaa staili ya nyani Mzee anayetaka kurukia Tawi la Mti, kisha akakunja miguu yake sawasawa huku akiwa anamtazama Malaika ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa mwepesi kutokana na umbo lake dogo na jembamba.

    “Nitakuuwa kama nilivyomuuwa mwenzako” Akasema Mbaga ikiwa ni mbinu ya kumtuliza Malaika 

    Endelea 

    SEHEMU YA KUMI NA NNE

    “Risasi inaweza kwenda haraka zaidi kuliko hata mapigo yako, huwa sipigwi na Mtu mtaratibu kama Wewe” Pale pale Mbaga akamfuata Malaika kama Mtu anayekimbia kisha akabendi upande wa kushoto aliporudi kulia akatupa ngumi ambayo ilikwepwa kirahisi na Malaika kisha akapewa ngumi ya shingo alafu akamaliziwa na teke la kifua, Mbaga akaanguka chali, Malaika akajuwa kuwa hatakiwi kumpa Mbaga hata sekunde moja ya mapumziko, akampelekea mvua ya mateke ambayo yalikita zaidi eneo la kifua, Mbaga akarudi tena chini akiwa katika hali ya

    uchovu sana hata moyo wake ukakiri kuwa amekutana na Mtu hatari kuliko alivyofikiria.

    Malaika akajiweka sawa huku akikunja vidole vyake na kuwa mfano wa Uma, Mbaga akajuwa tu endapo atalegea basi anaweza kuuawa hapo na hilo pigo, akasimama ili apambane na Malaika, tayari mguu wa Mbaga ulikuwa na maumivu Makali mno, Malaika akaligundua hilo haraka akaufanyia kazi mguu huo kwa kuuchosha zaidi, akawa anapeleka mapigo ya Mateke kuelekea kwenye Mguu huo ambao ulikuwa mzito kusogea.

    Kila pigo ambalo Malaika alilipeleka kwa Mbaga liliitikiwa na sauti ya kugugumia ya Mbaga na kumfanya Malaika ajuwe kuwa Mapigo yake yote yalikuwa yakifika sehemu husika, hali ya Mbaga ikaanza kuwa Mbaya hasa baada ya mguu wake kuonekana kukosa balansi ya kwenda mbele, dakika moja akajikuta akiwa sakafuni akiwa anatokwa na damu nyingi mdomoni, Mbaga hakuwa na uwezo hata wa kurusha ngumi kwa Malaika hata kunyanyuka.

    “Nilikwambia huwezi kunidhibiti, nitakuuwa ili kulipa kisasi cha Kifo cha Six, nimefanya kazi na Six kwa miaka mingi na haikuwa kutokea hili lililotokea leo. Nitaandikwa katika historia ya vitabu vya Nchi hii kuwa nimemuondoa P55″ Alisema Malaika huku akiwa anacheka kwa maumivu, Six kwake alikuwa ni zaidi ya Mtu wa kufanya naye kazi.

    Akamsogelea Six na kuthibitisha alichokiamini kuwa Six alikuwa ameshakufa kwa kupigwa rusasi moja tu ya Shingo.

    Akamrudia Mbaga kisha akakunja mkono wake na kutengeneza umbo la Uma ambalo lilikuwa ni umbo hatari zaidi, lengo la Malaika lilikuwa ni kuondoa koromeo la Mbaga kwa hasira, wakati huo Mbaga hakuwa na nguvu hata ya kumzuia Malaika, Ghafla Malaika alihisi ubaridi kwenye mgongo wake, ubaridi ambao ulisababisha ahisi maumivu huku akizidi kuhisi giza machoni pake, akajaribu kugeuka nyuma akakutana na sura ya Dawon akiwa ameshikilia Bastola iliyokuwa ikitoa moshi.

    Kabla hajasema chochote akapigwa risasi nyingine eneo lamoyo, akapigwa nyingine eneo la Kichwa, habari ya Malaika ikaishia hapo, akaanguka chini. Mbaga akahema kwa furaha,

    Dawson akamfuata Mbaga

    “Upo salama?” Aliuliza akiwa anamuinua

    “Mungu anajuwa najisikiaje Dawson, sijui hata aliweza vipi kukuamsha kitandani na kukuleta hapa ukanisaidia, huyu Msichana alikuwa ananimaliza hapa” Alisema kisha alikohoa.

    “Hatuna muda wa kupoteza hapa, mpigie Sande Olise tujuwe amefikia wapi, Kisko na Chande wapo Hospitali wanaendelea na matibabu” Alisema Dawson kisha mbaga akatoa redio Call akampigia Sande

    Dakika tano zilizopita, Sande alikuwa ameshanyanyuka ili aangalie uwezekano wa kufika chumbani kwa Rais, akiwa anavuta kitasa akapokelewa na teke kali kutoka kwa Jamaal.

    Akarudishwa nyuma akaangukia kwenye sinki la choo, akajitonesha yale maumivu ya Mbavu zake, akanyanyua macho ili amuone aliyempiga teke hilo akamuona Jamaal ambaye alikuwa na mwili wa mazoezi.

    Kisha Jamaal akaufunga mlango wa choo kwa kutumia funguo alafu funguo akaitia kwenye Tundu la sink la choo

    “Ukiweza kuniuwa utakuwa huru kutoka hapa lakini kama nitakuuwa nitakuzika kwenye chemba ya choo” Alisema Jamaal kisha akamfuata Sande ambaye bado alikuwa haelewi elewi ameweza vipi kushtukiwa.

    Akamkamata Sande na kwenda kumgongesha ukutani, bahati nzuri Sande naye alikuwa Mtu wa

    mazoezi akajiviringisha mikono akajitoa kwenye mwili wa Jamaal, akaona isiwe tabu ni bora apambane na Jamaal

    Wakaanza kurushiana mapigo makali makali ambayo yalimpata kila mmoja wao, uzuri wa Jamaal alikuwa mrefu hivyo aliweza kumpelekea mapigo ya nguvu Sande kuliko Sande alivyopeleka kwa Jamaal, Sande akajikuta amepigwa teke akaangukia kwenye bomba la maji ambalo lilikatika kutokana na uzito wa Sande, maji yakaanza kumwagika chooni hapo huku mengine yakitafuta njia ya kutoka yakawa yanaelekea chumbani kwa Rais

    Bado waliendelea kushambuliana kwa zamu, Jamaal hakutaka kufanya makosa kabisa sababu walishaahidiwa pesa ya kutosha, muda huo simu ya Jamaal iliita na alipoangalia akaona ni Rais ndiye anayepiga akaipokea na kuweka loud Spika

    “Upo wapi mbona kuna kelele hivyo?” Aliuliza Rais

    “Naoga Bosi muda mchache nitakuwa hapo”

    “Haya sawa!” Simu ilikatika, Jamaal akaiweka mfukoni kisha akamfuata Sande Olise na kuanza kumsugua kichwa kwenye ukuta hadi mwisho wa ukuta akiwa amembana vizuri Sande kiasi kwamba hakuwa na uwezo wa kupurukuta. Akawa anampiga vifuti eneo la mgongo na kumfanya Sande azidi kukosa nguvu kisha akamtupia

    kwenye Bwawa dogo lililopo pale chooni, akamfuata na kuanza kumkosesha pumzi kwa kumzamisha kwenye Bwawa hilo

    Purukushani ikawa kubwa kwa jinsi Sande alivyokuwa ananyweshwa yale maji ilionesha ni wazi kuwa alikuwa na muda mchache wa kuendelea kuwa hai. Sande akakumbuka alikuwa na ile staa ya kufungulia dirisha akajitahidi kufungua zipu huku akiendelea kukosa pumzi, akafanikiwa kuitoa staa kisha akamchoma Jamaal eneo la mbavu, Jamaaal akamuacha Sande huku akigugumia kwa maumivu, Sande alikuwa hoi sana.

    Akawa anataka kutoka pale kwenye lile bwawa dogo lakini Jamaal akamshika mguu na kumrudisha akawa anampiga eneo la uso kwa hasira sana. Hali ya Sande ikazidi kuwa mbaya, akaitumia tena ila Staa akamchoma eneo lilelile la mbavu kisha akamchoma tena eneo la mkono kwenye mishipa iliyokuwa na nguvu na kumfanya Jamaal ahisi mkono wake hauna nguvu.

    Sande akaona ni bora amalizane na Jamaal pale pale, akampiga ngumi la uso, akampiga ngumi mfululizo hadi uso wa Jamaal ukaharibika na kusababisha damu nyingi kumwagika, akamchoma na ile staa eneo la shingo ikatokea upande mwingine, habari ya Jamaal ikaishia hapo.

    Sande alikuwa hoi sana, ndipo akasikia simu ikiwa inaita, ilikuwa ndiyo ile simu ambayo Mbaga alikuwa akimpigia, akaipokea huku akiwa anahema juu juu

    “Kulikoni Sande upo salama?” Aliuliza Mbaga

    “Nilikiona kifo changu lakini kwa bahati nzuri nimefanikiwa kuokoka”

    “Umefikia wapi?”

    “Bado nipo Chooni, natoka sasa”

    “Ok! Tunakuja huko sasa hivi kuja kukusaidia” ilisikika sauti ya Mbaga kisha simu ikakatika.

    Ukimya alioupata Rais ulimtishia sana ukizingatia John Brain tayali alishampa taarifa kuwa Six amepigwa riasasi ameuawa, hakuwa na imani na walinzi wa Ikulu kwa namna ambavyo mara nyingi alikuwa akiwatumikisha kufanya mauwaji, moja ya Mauwaji hayo yalikuwa ni mauwaji ya Inspekta Zola, pia kutesa Watu wasio na hatia.

    Akajaribu kumpigia simu Jamaal lakini simu iliita, Sande aliitazama bila kuipokea.

    Rais akaona ni bora aelekee kwenye chumba cha siri ambacho kilikuwa kimehifadhi nyaraka za siri na ile fimbo ya alama ya Urais, akajisachi akakumbuka kuwa funguo aliiacha chumbani kwake kwenye moja ya koti lake, akakimbia haraka kuelekea chumbani, akashangaa kuona maji yakiwa yanatiririka kutokea

    Chooni, akajaribu kuita kidogo

    “Jamaal! Jamaal!” Akajibiwa na ukimya, akalazimika kuelekea mlango wa Choo, akausukuma lakini mlango huo ulikuwa umefungwa, angalau akawa na tumaini kuwa kuna usalama kumbe Sande alikuwa amejificha mahali, akaielekea ile funguo kwenye koti, chumba hicho ambacho Rais anataka kwenda ni chumba cha siri sana ambacho si rahisi ukakiona ( Utanielewa Mbeleni )

    Akawa mbio akaipata funguo lakini akiwa anataka kutoka kuelekea huko wazo likamjia, kufungua choo ili azuie maji yaliyokuwa yakitiririka, Rais huyu alishaondoa ulinzi eneo la ndani kwa kumtegemea Jamaal alipoona hali ni mbaya akawa na mawazo mawili, kuita ulinzi kisha kuelekea chumba cha siri, haraka akachukua funguo ya Chooni ambayo alikuwa ameiunganisha kwenye funguo ya chumba cha siri, akafungua.

    Sande hakutaka kumpa uwazi wa kutaka kukimbia baada ya kumuona Jamaal akiwa ametapakaa damu , akamkamata na kumzamisha Chooni.

    “Sande ni wewe?” Aliuliza Rais

    “Unataka nini sema unachotaka nitakupatia Sande” Alizidi kusema huku akiwa mwenye hofu,

    “Leo unataka niendeleee kuishi wakati ulituma Watu waniuwe?

    Kabla sijafa utatangulia wewe!!” Alisema kisha alimkunja kwa lengo la kumjaza hofu

    “Sande tafadhali usifanye hivyo, kumbuka hapa ni Ikulu na ukifanya chochote kile utajiweka katika mazingira magumu ya kuwa hai, sema unataka nini nitakupa!!”

    “Nautaka Urais wako! Mamlaka kisha nilipe kisasi kwa kifo cha Zola” Rais akawa ameelewa lengo la Sande kufika Ikulu lilikuwa ni nini

    “Sande unajua fika nisingeliweza kumuuwa Huyo Zola, isipokuwa….” akakatizwa na ishara ya Sande

    “Nahitaji unipeleke kwenye chumba cha siri cha Ikulu”

    “Chumba cha siri? Nani amekuambia kuwa hapa kuna chumba cha siri! Hakuna hicho chumba ndani ya Hii Ikulu Sande, utakuwa umekosea” Alijitetea Rais akiwa anatabasamu kwa lengo la kumtoa mchezoni Sande huku macho ya Rais yakiwa yanatazama kipande cha bomba lililoanguka chini, akataka kumshambulia lakini Sande akashtuka akamvuta hadi ukutani akampa ngumi nne za uso ambazo ziliiweka akili ya Rais katika hali sawa!!

    “Nipeleke chumba cha Siri” Rais hakuwa na jinsi ya kufanya akalazimika kuongozana na Sande, kwanza Sande akachomoa Bastola kisha akaiweka kwenye kichwa cha Rais huyo ili ije kuwa kama ngao ya kumlinda. Wakaongozana kuelekea huko huku Rais akijuwa fika kuwa Sande anaweza kumuuwa endapo hatofanya hivyo.

    Mwendo wa taratibu eneo ambalo halikuwa na walinzi, wakafika mahali Rais akamuuliza Sande

    “Unashirikiana na Muasi P55?”

    “Twende sitaki maswali ya Kizandiki” Alisema Sande, wakafika hadi kwenye Ofisi ya Rais huyo, kitendo cha kufika tu Ofisini alamu maalum ikalia baada ya Kamera kuonesha kuwa Rais alikuwa ametekwa humo Ikulu, Askari wakamiminika kuelekea ndani ambako Rais alikuwepo.

    “Funga mlango wako haraka sana” Alisema Sande huku akimtishia kumuuwa Rais, hakuwa na jinsi akafanya kama alivyoelekezwa sababu mlango huo ulikuwa wa umeme na ulikuwa na namba maalum za kuingilia ambazo alikuwa akizifahamu Rais pekee. Simu ya Rais ilikuwa ikiita, mpigaji alikuwa ni John Brain, baada ya kuwapigia vijana wake wote watatu simu haikuweza kupokelewa.

    Sande akaichukua simu akaipokea

    “Rais! kuna Usalama huko?” aliuliza punde simu ilipopokelewa

    “Hakuna usalama sababu Ikulu ipo chini ya Uvamizi” Sauti ya Sande ilipofika kwa John ikampa ujumbe kuwa Rais alikuwa chini ya ulinzi.

    “John! muda wa wewe kuendelea kutekeleza ugaidi Duniani umeisha, Dunia itaenda kuandika Historia Muda mchache ujao tutakapokufuta katika uso wa Dunia” John akawa amechanganikiwa, Sande akaendelea kumueleza

    “Hakuna kijana wako hata mmoja anayepumua hadi kufikia wakati huu, umebaki mwenyewe katika Ardhi ambayo uliamrisha kila kitu kifanywe kwa matakwa yako” Kisha Sande akakata simu hiyo

    “Waambie Askari wako wakae mbali na eneo hili vinginevyo nitakuuwa muda sio mrefu” Akasema Sande, pale pale Rais akabonyeza sehemu ambayo ilikuwa na Maiki akasema na Askari wote wakasikia.

    “Nioneshe kilipo chumba cha siri”

    “Sande hata ukienda huko utakufa sababu Kuna mfumo wa umeme ambao hauwezi kukuruhusu kupenya zaidi” Alieleza Rais, Sande akampiga teke la Mguu Rais kisha akamwambia

    “hakuna muda wa kupoteza nipeleke huko” Rais akaelekea mahali ambapo kulikuwa na kabati kubwa la vitabu akabonyeza sehemu kisha mlango ukafunguka.

    Kila ambacho Mbaga alimueleza Sande kilionekana, ni kweli ndani ya chumba hicho kulikuwa na mionzi iliyokuwa ikipishana “Unaona? ule ni mfumo wa Umeme Sande, unachotaka kipo mbele zaidi ya pale ambapo kuna mionzi utafia huko” Sande akaona Rais huyo anamtia kelele, akamfunga kamba mikononi na miguuni kisha akamuweka chini ya Meza, akatoa kifaa cha kunyonya mionzi ambacho alipewa na Mbaga akakiwasha kikaanza kuhesabu sekunde ambapo baada ya sekunde 30 kupita kitazima hivyo

    Sande alipaswa kutumia muda mfupi kuchukua vitu viwili, Fimbo na nyaraka za siri ambazo alielezwa kuwa zilikuwa zipo pamoja ndani ya chumba hicho.

    Sande akaingia ndani ya chumba hichi kisha akaweka kifaa sehemu ambapo mionzi yote ya umemeikaunganika na kukielekea kifaa hicho, Sande akapata nafasi ya kuzama zaidi ndani ya chumba hicho, akawa anahaingaika jinsi ya kuviona vitu alivyokuwa akivitaka, akajikuta akitumia sekunde 10 bila Mafanikio, kumbe Rais alikuwa na kisu kidogo alichokuwa amekificha kwenye kiatu chake, akawa amejitahidi na kukata kamba hizo. Akaangalia kwenye Kioo ambacho kilikuwa kikitumika kuonesha Video za CCTV, akaona kuna Askari waliokuwa mlangoni, haraka akakimbilia kuwafungulia.

    Sekunde zilikuwa zimeshaisha, Sande alikuwa ameshapata nyaraka na hiyo fimbo kisha haraka akawahi kutoka, mlango ukajifunga. Akakutana Uso kwa uso na Askari wawili waliofunguliwa Mlango na Rais, Aksari hao wakachomoa Bastola zao huku wakiwa wamefunika nyuso zao, Sande akajikuta yupo chini ya Ulinzi wa Askari hao.

    Rais akampokonya Sande vile Vitu kisha akawa anapiga hatua kuelekea kufungua lango la chumba cha Siri, ghafla akashangaa Askari hao wawili wakimnyooshea Bastola, wakavua walichovaa kwenye nyuso zao,

    Rais hakuamini kuwaona Dawson na Mbaga wakiwa ndani ya Mavazi ya kijeshi, akataka kufanya ujanja kufungua mlango ili aingie huko, akapigwa risasi ya mguu.

    Wakavichukua vitu hivyo alafu wakamwambia Rais atangaze katika TV ya Taifa kutokea Ikulu kuwa Nchi ipo chini ya Jeshi. Muda huo John Brain alikuwa akikusanya kila kilicho chake ili aondoke Nchini, akiwa anataka kutoka akasikia Sauti ya Rais kutokea kwnye TV ikiitangazia Nchi kuwa Nchi hiyo ipo chini ya Jeshi, wakaonekana akina Dawson na Mbaga ambao walitajwa kuwa Waasi kwa nyakati tofauti tofauti, wakamlazimisha Rais alekeze kila kitu, akasema kila kitu hata mauwaji ya Makamu wa Rais ni yeye ndiye aliyehusika nayo, vifo vilivyokuwa vikitokea vilitokana na yeye.

    Kisha picha ya John Brain ikaanikwa kwenye TV, Watu ndio wakapata kumjua John Brain ambaye Taifa la Marekani lilikuwa likimsaka. Taarifa hii ilienda mbali zaidi hadi vituo vya Runinga vya Aljazeera vikaitoa.

    John Brain akaondoka Nchini kwa kutumia Helkopta, akatua Uganda ili apande ndege akiwa amevalia sura Bandia. Tayari Marekani walikuwa wameshaipata Taarifa hiyo wakatuma FBI Dunia nzima wakiwa na sampo ya DNA ya John Brain baada ya kumfahamu. John akakamatwa kwenye mpaka wa Somalia akiwa anajiandaa kuonana na Kundi la Alqaeda na Baada ya kupimwa akagundulika kuwa ni yeye, FBI wakarudi Marekani wakiwa na

    John Brain ili awaoneshe Makundi mengine ya Kigaidi.

    Taifa hilo likawataja Mbaga, Sande Olise na Dawson kama Mashujaa wa Dunia kwa kumfichua John Brain ambaye Mataifa mengi yalihangaika kwa muda mrefu, Kama ilivyo ahadi ya Mbaga aliondoka kwenda kuishi Shamba katika Nchi ya Eritrea, akajiwekeza na kilimo huku akiwa ameiacha Nchi hiyo ikiwa inaingia kwenye Uchaguzi wa kuunda Serikali itakayoongozwa kikatiba tofauti na Mwanzo ambavyo Watu walikuwa wakirithi nafasi ya Urais.

    Baada ya miezi mwili Dawson alifariki kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu, Kisko na Chande walichukuliwa na Taifa la Marekani kwa ajili ya mafunzo ya kijeshi, wakati huo Sande akistaafu kazi ya Kijeshi akapanda ndege kwenda Eritrea kuishi pamoja na Mzee Mbaga

    MWISHO

    LEO NATAKA COMMENTS NYINGI KAMA Unataka Mpya Comment MPYA kama Unataka Mpya Ije Mwakani Comment MWAKANI Watakaoshinda Kwa KURA 200 BASI Naachia Mpya 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

      Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx 

    jasusi riwaya za kijasusi

    31 Comments

    1. catherine Arod on December 12, 2024 4:20 pm

      Asantee sana admin story tamu nataman iendelee

      Reply
      • Mhariri on December 12, 2024 4:21 pm

        Huna Baya

        Reply
    2. Joshua laizer on December 12, 2024 6:40 pm

      Tamu kichzi

      Reply
    3. Egibeth on December 12, 2024 6:47 pm

      Mwendo umeumalizaaa salaamaa

      Reply
    4. DIzzoh on December 12, 2024 6:54 pm

      Hot sana

      Reply
    5. Cathbert on December 12, 2024 6:56 pm

      Iko sahihii

      Reply
    6. Kenned on December 12, 2024 7:00 pm

      Guuud sana

      Reply
    7. Anuar on December 12, 2024 7:03 pm

      Mpya

      Reply
    8. Edward on December 12, 2024 7:05 pm

      Mpyaaaa kesho mapemaaaa ijeee

      Reply
      • Lukuman on December 12, 2024 10:36 pm

        Hakika tumefurahi na kujifunza

        Reply
      • Anitha bukuku on December 18, 2024 6:53 pm

        Hakika nimejifunza kitu

        Reply
    9. Wil on December 12, 2024 7:14 pm

      Lete nyingine mapemaaa

      Reply
    10. Ahmed Samir on December 12, 2024 7:33 pm

      Story nzur xan

      Reply
    11. Hamisi halidi on December 12, 2024 7:51 pm

      Una baya kaka wa mastor

      Reply
    12. Sir yowas on December 12, 2024 8:03 pm

      Leta nyingine

      Reply
    13. Elisha on December 12, 2024 8:50 pm

      Mtu wa maana sana wewe respect achia burudani huko studio

      Reply
    14. Scalion on December 12, 2024 8:57 pm

      Sah hii kitu ilikuwa tamu sana sana sanaaaa Big up kwako mtunzi Mungu azidi kukuinua kila kukicha uzidi kupanda viwango zaidi
      Tunaomba ingine mpyaaaaa please 🙏

      Reply
    15. Charz jr😎 on December 12, 2024 9:04 pm

      Why iwe mwakani kaka mkubwa😃😃😃 mbona unatunyanyapaa🥲🥲

      Reply
    16. Fawziya Hassan on December 12, 2024 9:18 pm

      Moyo mweupeee❤️
      Alhamdulillah Mashujaa wamesalimika
      Simulizi yenye maana pana kwa Ulimwengu mzima..
      ❤️❤️

      Reply
    17. G shirima on December 12, 2024 9:45 pm

      New

      Reply
    18. Jack bujo jr on December 12, 2024 9:54 pm

      Alhamdulillah 🙏🙏

      Reply
    19. Angel on December 12, 2024 9:57 pm

      Nataman Zola asingekufaga kabla..hadi pale ambapo angeon alichokipambania kimekuw kwel

      Reply
    20. Ramadhani on December 12, 2024 10:58 pm

      Mpya

      Reply
    21. Kingz on December 13, 2024 12:35 am

      Nakuonba hata hyo nyngne iwe ya kijasusi kwakwel maana zinatufundish uzalendo kwa100%

      Big up Sana kwako mtunzi💞🤏🏽🤏🏽

      Reply
    22. Patricia Lizzy on December 13, 2024 1:46 am

      Ahsnte ADMIN imeisha vzr jamani ahta mwenye kichwa kigumu lazima hameielda ila kwa upande wangu
      Love & pain kwakweli haikuisha story iliishiaa njian tunaombaa mwendekezo wake

      Reply
    23. Patricia Lizzy on December 13, 2024 1:46 am

      Ahsnte ADMIN imeisha vzr jamani ahta mwenye kichwa kigumu lazima hameielda ila kwa upande wangu
      Love & pain kwakweli haikuisha story iliishiaa njian tunaombaa mwendekezo wake

      Reply
    24. Inspector Zola on December 13, 2024 8:45 pm

      > SIMULIZI|BOSS-SEHEMU YA KWANZA
      Isome hapa⤵
      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/12/simuliziboss-sehemu-ya-kwanza_12.html

      Reply
    25. Shimmy on December 17, 2024 7:26 pm

      New

      Reply
    26. Sharo love malkx 💖 on December 18, 2024 11:29 pm

      Stori nzuri kaka
      Mr KIJIWENI

      Reply
    27. Ezyra on January 25, 2025 11:57 am

      Ama kweli hupaswi kukosa kijiweni sio kwa hadithi nzuri kama hizi

      Reply
    28. Emanuely Daudy on May 9, 2025 5:30 pm

      Yaani mimi nilizama kabisa huko kwenye mision mazima hongera sana mtunzi kwa kitu cha kijasusi

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.