Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Matokeo Ya Kidato Cha Nne 2025

    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 11, 2024Updated:October 28, 202424 Comments9 Mins Read8K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mvua ilikuwa ikinyesha, moyo wangu ulijawa na tabasamu kubwaย  sana, nilijinyoosha ili kuianza siku mpya ambayo ilianza kwaย  hali ya hewa kuwa nzuri yenye ubaridi. Niliposhika simu yanguย  niliona picha ya Mwanaume niliyempenda sana. Niliiweka kwenyeย  kioo cha simu yangu, alikuwa akiitwa Mosses, alikuwa niย  mwanaume aliyeuteka moyo wangu sana, nilimpenda kwa nguvuย  zangu zote, hisia zangu ziliniambia Mosses ndiye Mume wangu.ย 

    Tabasamu lilikuwa limejaa usoni pangu, nilimpigia Mosses iliย  niweze kusikia sauti yake, sauti ambayo ilikuwa ndiyo tulizoย  pekee la nafsi yangu!ย 

    “Hello My love” Nilisikia sauti ya Mosses ikisema, basi moyoย  wangu ulifurahi sana, wewe msomaji unaweza kuwa shahidi waย  hili ile furaha unayoipata unapoongea na mpenzi wako nyakatiย  za asubuhi basi ndiyo iliyonivaa wakati huo. Kwanza nilihemaย  kidogo ili niweze kumjibu Mossesย 

    “Mambo Mpenzi, bado haujaamka?” Nilimuuliza Mosses kwa sautiย  iliyojaa bashasha. Mosses alinijibuย 

    “Ndiyo naamka Mpenzi, yaani huwezi amini nimetoka kukuwazaย  muda huu nawe ndiyo unanipigia, hakika tunaishi katika Duniaย  yetu iliyojaa Huba zito Jacklin” Alisema Mosses, mara zoteย  alikuwa na maneno matamu sana kwangu kitu ambacho kilinifanyaย  nizidi kuvutiwa nawe, mara mlango wa chumba changu uligongwa,ย  nilisikia sauti ya Mama ikiwa inaniita.ย 

    “Samahani Mosses, Mama ananiita” nilisemaย 

    “Haya ukimaliza niambie” Alisema Mossesย 

    “Sawa Mume wangu mtarajiwa” Nilisema kisha nilimwambia kuwaย  nampenda sana na kamwe sitoweza kumsaliti. Mara moja nilikataย  simu, nilinyanyuka kitandani na kwenda kuitika wito wa Mamaย 

    “Shikamoo Mama” Nilimsalimia baada ya kuwa nimeshafunguaย  mlango, nilikuwa nafikicha macho yangu kutokana na Mwangaย  uliokuwa ukimulika macho yangu.

    “Marhaba!! Ndiyo unaamka sasa hivi Jacklin? Umesahau kama leoย  unatakiwa kwenda kwenye Interview?” Alisema Mamaย 

    “Oooh Mungu wangu nilishasahau ngoja nijiandae Mama” Nilisemaย  kisha nilikimbilia Bafuni kuoga, siku hiyo ilikuwa ni siku yaย  Jumatatu nilipaswa kwenda kwenye interview ya kazi katikaย  kampuni moja ambayo niliomba nafasi miezi michache iliyopita,ย  Mama alinitazama hadi nazama Bafuni kisha aliingia chumbaniย  kwangu na kuanza kukagua vitu vyangu.ย 

    Aliona kadi za mapenzi ambazo Mosses alikuwa akinitumia,ย  alitikisa kichwa chake kisha aliondoka chumbani kwangu.ย 

    Asubuhi hiyo hiyo, kwenye moja ya jumba la kifahari alikuwepoย  Mtoto wa kitajiri aliyeitwa Osman, alikuwa mweupe mwenyeย  asili ya uarabu, ndiye mmiliki wa kampuni ambayo Mimiย  nilitakiwa kwenda kufanyiwa usaili kwa ajili ya kazi, huyuย  Osman ni Mwanaume mwenye maumivu makali ndani ya moyo wakeย  kwani miezi miwili iliyopita aliachwa na Mwanamkeย  aliyetarajia kumuowa, Mwanamke huyo aliitwa Zahra, huyo Zahraย  alitoroka na kiasi kikubwa cha pesa kisha kwenda nje ya Nchi,ย  alimtumia ujumbe Osman kuwa hamuhitaji tena katika Maishaย  yake, tokea siku hiyo Osman amekuwa ni Mwanaume mwenyeย  kuutafuta upendo wa kweli.ย 

    Asubuhi hiyo Osman aliondoka kwenye jumba hilo na kuelekeaย  kwenye kampuni ambayo mimi nilikuwa naenda kufanya usaili,ย  kutokana na mvua kubwa kunyesha kulisababisha foleni kubwaย  iliyoniweka kwa zaidi ya dakika hamsini, nilikuwa tayariย ย nimechelewa kwenye Usahili, pembezoni mwangu kulikuwa na gariย  aina ya Benzi nyeusi, alionekana huyo Osman akiwa anaangaliaย  sana saa yake, ilikuwa ndiyo mara ya kwanza namuona, jinsiย  alivyokuwa akihangaika kuangalia saa yake ilinipa moyo kuwaย  siyo mimi tu niliyechelewa kwenye jambo bali tupo wengiย  pasipo kujuwa huyo Mtu ndiye mmiliki wa hiyo kampuni.ย 

    Nikiwa kwenye daladala, Mosses alinipigia akaniuliza nikoย  wapi, kiukweli jinsi nilivyokurupuka nyumbani sikuweza hataย  kumuaga kuwa naenda kwenye Usahili, ilinibidi nimueleze kuwaย  nipo kwenye daladala naelekea kwenye Usahili ila nimechelewa.ย 

    “Kama ni hivyo basi chukua pikipiki nitakutumia pesa kidogoย  ulipe maana hapo utazidi kuchelewa” Alisema Mosses,ย  alinifanya nitabasamu, niliona ndiye Mwanaume anayenijaliย  kuliko Wanaume wote Duniani. Basi nilishuka, nilimuona piaย  Osman naye akishuka kwenye gari, sote tulitazama upande mmojaย  tukaita pikipiki moja iliyokuwa karibu, ilitushangaza kuonaย  sote tunamuita Bodaboda huyo, Osman alinitazama namiย  nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha alinisogelea sababu yuleย Bodaboda alikuwa akija kwangu, si unajuwa tena Mwanamkeย  ananguvu kubwa sana kwa Mwanaume? Basi ndivyo ilivyokuwa kwaย  Bodaboda huyoย 

    “Samahani Dada yangu naomba usubirie Pikipiki nyingine mimiย  nina dharura kuna Watu wananisubiria!” Alisema Osman, manenoย  yake yalinifanya nimuulizeย 

    “Ina maana wewe ndiye mwenye haraka peke yako? Hata Mimiย  nasubiriwa huko ninakoenda hivyo wewe ndiye unayepaswaย  kusubiria nyingine” Nilisema kwa haiba ya kike, ilikuwa ndiyoย  mara ya kwanza namuona Osman, sikujuwa kama ndiye mmiliki waย  hiyo kampuni niliyokuwa naenda kwenye Usahili. Bodabodaย  aliingilia katiย 

    “Kwani wewe Bro unaenda wapi na wewe Sistaa unaenda wapi?”ย  Aliuliza Bodaboda huyoย 

    “JM Motors” Nilisemaย 

    “JM Motors” Alisema Osman, sote tulijikuta tukiitaja sehemuย  moja ambayo ndiyo hiyo kampuni ya Uuzaji wa Magari kutokaย  Dubaiย 

    “Sasa si unaona mlitaka kunikosesha pesa za vichwa viwili,ย  panda sistaa huyo jamaa aje kwa nyuma” Alisema Bodaboda hukuย  manyunyu yakianza tenaย 

    “Siwezi kuanza, apande yeye mimi nitakaa nyuma” Nilisema,ย  Osman alicheka tu kisha alisemaย 

    “Naitwa Osman Dhabi” alinipatia Mkono kwa lengo la kutakaย  kunifahamu pia lakini sikutaka mazoea naye kabisa, sikumpaย  mkono wangu, Osman alitabasamu tu kisha alipanda kwenyeย  pikipiki kisha nami nilifuatia. Safari ilianza kuelekea JMย  Motors, Osman alionekana kuwa muongeaji kiasi, niliwasikiaย  wakiongea kuhusu Wanawake ili sikutaka kujali sana, mwendo waย  dakika kama 30 hivi tulifika JM Motors huku mvua ikianzaย  kuchanganya, Niliposhuka tu nilikimbilia kujihifadhi kwenyeย  maegesho ya Magari nikiwa natetema baridi, Osman alilipa pesaย  ya Pikipiki kisha yule Bodaboda aliondoka, niliangalia simuย  yangu kuona kama Mosses alikuwa amenitumia pesa ya Pikipikiย  lakini alikuwa bado hajatuma.ย 

    Osman alisogea akaniambiaย 

    “Nimeshalipa usijali” Alisema kisha alitabasamu tu, kwanguย  niliona kama amenidharau hivi, nilifungua pochi yangu nikatoaย  elfu tano ambayo ndiyo ilibakia hiyo hiyo ya kurudiaย  nyumbani, nilimpa Osman

    “Huwa sipendi vitu vya Bure” Nilisema kwa hasiraย 

    “Samahani sikujuwa kama ungechukia, upo hapa kwa ajili yaย  Usahili?” Aliniulizaย 

    “Ukijuwa itakusaidia nini? Sihitaji mazoea ya kijinga”ย  Nilisema kisha niliekea ambako Watu walikuwa wakiingia, Osmanย  alitabasamu tu akiwa ndani ya Shati jeupe ambalo lilikuwaย  limeloa na suruali nyeusi iliyomkaa vizuri, moyo wanguย  uliniambia kuwa Mwanaume huyo alikuwa na mvuto sana ilaย  alikuwa na dharau.ย 

    Nilipofika ndani nilielekea mapokezi, niliambiwa kuwa Bosiย  anayepaswa kutufanyia Usahili bado hajafika hivyo nilioneshwaย  chumba ambacho Watu wanaotakiwa kusahiliwa walikuwepo, wakatiย  natembea nilihisi kupoteza kitu. Ndiyo, nilisahau Bahashaย  yenye vyeti vyangu ndani ya ile Daladala.ย 

    Roho iliniuma sana na sikuuona umuhimu wa Usahili tena,ย  nilitamani kuondoka lakini yule Mdada alisemaย 

    “Ingia chumba hicho Bosi huyo anakuja” Alikuwa kamaย  amenishtua hivi, haraka niliekelea kwenye chumba hicho bilaย  kugeuka nyuma.ย 

    Nilijaribu kumtumia ujumbe Mosses lakini hakujibu, nilimpigiaย  lakini hakupokea simu yangu, nilijiona nina mzigo ndani yaย  moyo wangu, nilimpigia Mama kumueleza hali halisi, aliniambiaย  kuwa alibakiwa na pesa ile aliyonipa hivyo labda baadayeย  anaweza akapata kisha akanitumia.ย 

    Osman alielekea ofisini kwake, alibadilisha nguo zake huko,ย  alikuwa ni Kijana wa kisasa na mwenye pesa sana, alikuwaย  akisimamia miradi mingi ya Baba yake Mzee Dhabi aliyekoย  Dubai.ย 

    Tulipaswa kusubiria kwa zaidi ya saa nzima, njaa ilikuwaย  ikizidi kuniuma, Mdada mmoja aliye jirani yangu aliniambiaย 

    “Jinsi ulivyolowa na unasema umesahau vyeti jiandae kwaย  maneno ya shombo, huyo Bosi ni kijana tu, msafi sana, alafuย  mzuri, huoni zimetangazwa nafasi wanawake wengi ndiyoย  waliojitokeza tena wakiwa wamevalia vizuri zaidi yako!”ย  Alisema kwa sauti ya Chini, nilimjibuย 

    “Sikuja kwenye mashindao ya urembo nimekuja kutafuta kazi,ย  kama sitopata nitatafuta kwingine, siwezi kuwa Mtumwa waย  umasikini wangu” Nilimjibu, nilimkata kauli hakusema tena, niย  kweli alichokuwa amekisema Wasichana walikuwa wakijipodoaย sana ili wakiingia huko wakamshawishi huyo Bosi ambaye mimiย  nimetoka kuzozana naye bila kujuwa.ย 

    Jina langu lilikuwa la kwanza kuitwa, niliomba niwe wa mwishoย  sababu nguo zangu zilikuwa zinavuja maji, bahati nzuri Mdadaย  aliyekuja kuniita alinielewa, Basi walianza kwenda hukoย  pasipo kurudi hadi pale nilipobakia peke yangu ndani yaย  Chumba hicho. Maneno ya yule Mdada yalizidi kujirudia kwenyeย  ufahamu wangu, kwa kiasi kikubwa yalianza kunitisha sana.ย  Basi, zamu yangu ilipofika nilivuta pumzi kwa nguvu ndaniย  kisha nilizitoa ili kuondoa hali ya woga ambayo nilionaย  inaanza kuniandama, nilikuwa kama kichaa hivi sababu nguoย  bado zilikuwa mbichi, sikuwa na vyeti vya elimu yangu yaย  Biashara.ย 

    Nilipiga hatua ndogo ndogo kuelekea kwenye ofisi kwa ajili yaย  Usahili, nilipoingia nilipigwa na butwaa, nilimuona Osmanย  akiwa ameinama anaandika jambo, yule Mdada alimwambia Osmanย 

    “Bosi, huyu wa mwisho anaitwa Jacklin, alitakiwa kuwa waย  kwanza ili hakuwa tayari” Alisema, Osman hakunyanyua machoย  yake, alisemaย 

    “Sawa anaweza akaketi” Alisema bila kuniangalia usoni,ย  nilitamani kuondoka maana kwa jinsi nilivyomjibu vibayaย  kuanzia kule barabarani hadi tunafika ofisini kwakeย  sikufikiria kama atanisikiliza, basi niliketi hivyo hivyoย  kama Mtu aliyeyavulia maji nguo, Sharti ayaoge. Nilisubiriaย  kwa sekunde kadhaa, yule Mdada aliondoka, baadaye Osmanย  alinyanyua kichwa chake, aliponiona alinitazama kwaย  kunishangaa kama vile alikuwa hajawahi kuniona.ย 

    “Karibu” Alisema Osman, jicho lake niliona lilikuwa na ujumbeย  fulani kwenye hisia zangu, alinitazama kama vile alikuwaย  akitengeneza kitu alafu akawa anakiangalia kama kipo sawa,ย  nilihisi pengine kwasababu nilikuwa nimeloa na pia nilimsemeaย  vibaya.ย 

    “Asante!” Nilisema kwa sauti iliyojaa aibuย 

    “Naitwa Osman Dhabi, ni Mmiliki wa kampuni hii, Unaitwaย  nani?” Aliniuliza kama vile hakuna kilichotokea baina yetu,ย  ilinifanya niwe na maswali mengi kichwani kwanguย 

    “Naitwa Jacklin Sembu, nimekuja kwa ajili ya Usahili wa kazi”ย  Nilisema nikiwa nimeinamia chini, Osman aliniambiaย 

    “Sina haja ya kukufanyia Usahili sababu nimeshakufanyiaย  tukiwa njiani, sitaki kuingilia Maisha yako Jacklin lakiniย kuna wakati unapaswa kuacha jeuri yako” Alisema kishaย  alichukua barua akaniambiaย 

    “Hii uje nayo baada ya siku saba, nilihitaji nafasi ya Mtuย  mmoja pekee, nimechagua kufanya kazi na wewe” Alisema Osman,ย  nilijikuta nikitabasamu kwa shida sana, ni kweli nilikuwaย  nahitaji hiyo kazi kwa udi na uvumba lakini niliishiwa manenoย  ya kuyasema mbele ya Osman, nilijiona nimeelemewa kabisa,ย  nafsi ilinisuta nikasemaย 

    “Nashukuru na Mungu akubariki”ย 

    “Usijali Jacklin, ubaya haulipwi kwa ubaya katu, ubayaย  hulipwa kwa mazuri yasiyosahaulika” Alisema tena kishaย  alinipa mkono ambao niliukataa kule barabarani, ilinibidiย  niupokee, aliuchezea kidogo mkono wangu kwa kunisabahiย 

    “Nakutakia siku njema” Alisema Osman kisha aliendelea na kaziย  zake, nilinyanyuka kisha niliangalia kiti nilichokaliaย  niliona kimeloa maji ambayo yalikuwa yakinichuruzika,ย  niliondoka ofisini kwa Osman nikiwa mwenye furaha sana.ย  Mosses hakunipigia kabisa wakati alisema angenipa pesa yaย  kulipia usafiri, basi nililazimika kumpigia Mamaย 

    “Jacklin Mwanangu sijapata pesa kama unaweza kusubiria hadiย  jioni sawa” Alisema Mamaย 

    “Usijali Mama nitarudi tu” Nilisema, sikuwa na pesa ya nauliย  ya kurudia nyumbani alafu mvua ilikuwa ikinyesha sana,ย  kulikuwa na hali ya radi pia, nilifikiria kama Osmanย  angelinikuta pale nje ingeleta picha mbaya zaidi, nilifikiriaย  pia ile pesa niliyompa kwa hasira, nilijilaumu sana kwaย  kiburi changu. Basi niliingia kwenye mvua, nilivua viatuย  vyangu. Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Pili Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย 

     

    Pumzi ya mwisho Riwaya ya pumzi mwisho

    24 Comments

    1. Farnoush on October 11, 2024 4:31 pm

      Tamu balaaaa

      Reply
    2. Lus twaxie on October 11, 2024 4:38 pm

      Nshaanza kuipenda

      Reply
      • Jackson on October 11, 2024 7:10 pm

        Hiii mashine

        Reply
        • Narkiso on October 15, 2024 4:45 am

          Nice one

          Reply
    3. Suleiman abduli on October 11, 2024 5:08 pm

      Kama naanza kuielewa hivi

      Reply
    4. Kevin Winton mwasambiri on October 11, 2024 6:38 pm

      Himenifunza kutulia bila papala

      Reply
      • G shirima on October 11, 2024 9:25 pm

        Hii naon itakua ya moto sana alafu wifanye iwe ndefu kidogo sasa na matukio mengi mengi kidogo

        Reply
    5. Tumpe on October 11, 2024 7:02 pm

      Aaah weeh๐Ÿ˜๐Ÿฅฐ

      Reply
    6. Paka mweusi on October 11, 2024 7:11 pm

      Hiii imeenda

      Reply
    7. Ym on October 11, 2024 7:12 pm

      Ipo vizuri

      Reply
    8. Sabitimussa23 on October 12, 2024 12:45 pm

      Najifunza vitu vingi sana kupitia liwaya hizi ๐Ÿ‘Š๐Ÿพ

      Reply
    9. Martin on October 12, 2024 5:03 pm

      https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z

      Reply
    10. Martin on October 12, 2024 5:04 pm

      https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z

      Group la mkeka

      Reply
    11. Le izoneee on October 12, 2024 5:32 pm

      Oa admini iko poah sanaaaa….achiaaa ilooo dudeee lingneee

      Reply
      • Pedma on October 12, 2024 5:44 pm

        Simulizi tamuu sanaa

        Reply
    12. Pedma on October 12, 2024 5:44 pm

      Simulizi tamuu sanaa

      Reply
    13. Prof. Noon saleh17 on October 12, 2024 7:56 pm

      Hii enyewe kabisa๐Ÿ‘Š๐Ÿฝ..

      Reply
    14. Marietha on October 25, 2024 11:28 am

      Nimeipenda

      Reply
    15. ๐Ÿ“ช + 1.794439 BTC.GET - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=f304a77f3b4d5285e0076651168d2e5d& ๐Ÿ“ช on July 3, 2025 9:04 am

      3ttvjp

      Reply
    16. binance referral code on December 3, 2025 5:37 am

      Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?

      Reply
    17. smortergiremal on December 25, 2025 1:57 am

      Perfectly pent content, thanks for information. “In the fight between you and the world, back the world.” by Frank Zappa.

      Reply
    18. watch live formula 1 streaming on January 13, 2026 1:36 am

      Thanks , I’ve just been looking for information approximately this topic for a while and yours is the greatest I have discovered till now. But, what concerning the conclusion? Are you certain about the supply?

      Reply
    19. cfb streaming online on January 13, 2026 10:51 pm

      I got what you mean ,saved to fav, very decent site.

      Reply
    20. zaborna torilon on January 20, 2026 10:59 pm

      I believe other website proprietors should take this internet site as an example , very clean and good user genial pattern.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Stori Mpya January 31, 2026

    Matokeo Ya Kidato Cha Nne 2025

    NECTA yatangaza matokeo ya Kidato cha Nne 2025, kiwango cha ufaulu chafikia asilimia 94.98 Baraza…

    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.