Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 11, 2024Updated:October 28, 202419 Comments9 Mins Read8K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mvua ilikuwa ikinyesha, moyo wangu ulijawa na tabasamu kubwaΒ  sana, nilijinyoosha ili kuianza siku mpya ambayo ilianza kwaΒ  hali ya hewa kuwa nzuri yenye ubaridi. Niliposhika simu yanguΒ  niliona picha ya Mwanaume niliyempenda sana. Niliiweka kwenyeΒ  kioo cha simu yangu, alikuwa akiitwa Mosses, alikuwa niΒ  mwanaume aliyeuteka moyo wangu sana, nilimpenda kwa nguvuΒ  zangu zote, hisia zangu ziliniambia Mosses ndiye Mume wangu.Β 

    Tabasamu lilikuwa limejaa usoni pangu, nilimpigia Mosses iliΒ  niweze kusikia sauti yake, sauti ambayo ilikuwa ndiyo tulizoΒ  pekee la nafsi yangu!Β 

    “Hello My love” Nilisikia sauti ya Mosses ikisema, basi moyoΒ  wangu ulifurahi sana, wewe msomaji unaweza kuwa shahidi waΒ  hili ile furaha unayoipata unapoongea na mpenzi wako nyakatiΒ  za asubuhi basi ndiyo iliyonivaa wakati huo. Kwanza nilihemaΒ  kidogo ili niweze kumjibu MossesΒ 

    “Mambo Mpenzi, bado haujaamka?” Nilimuuliza Mosses kwa sautiΒ  iliyojaa bashasha. Mosses alinijibuΒ 

    “Ndiyo naamka Mpenzi, yaani huwezi amini nimetoka kukuwazaΒ  muda huu nawe ndiyo unanipigia, hakika tunaishi katika DuniaΒ  yetu iliyojaa Huba zito Jacklin” Alisema Mosses, mara zoteΒ  alikuwa na maneno matamu sana kwangu kitu ambacho kilinifanyaΒ  nizidi kuvutiwa nawe, mara mlango wa chumba changu uligongwa,Β  nilisikia sauti ya Mama ikiwa inaniita.Β 

    “Samahani Mosses, Mama ananiita” nilisemaΒ 

    “Haya ukimaliza niambie” Alisema MossesΒ 

    “Sawa Mume wangu mtarajiwa” Nilisema kisha nilimwambia kuwaΒ  nampenda sana na kamwe sitoweza kumsaliti. Mara moja nilikataΒ  simu, nilinyanyuka kitandani na kwenda kuitika wito wa MamaΒ 

    “Shikamoo Mama” Nilimsalimia baada ya kuwa nimeshafunguaΒ  mlango, nilikuwa nafikicha macho yangu kutokana na MwangaΒ  uliokuwa ukimulika macho yangu.

    “Marhaba!! Ndiyo unaamka sasa hivi Jacklin? Umesahau kama leoΒ  unatakiwa kwenda kwenye Interview?” Alisema MamaΒ 

    “Oooh Mungu wangu nilishasahau ngoja nijiandae Mama” NilisemaΒ  kisha nilikimbilia Bafuni kuoga, siku hiyo ilikuwa ni siku yaΒ  Jumatatu nilipaswa kwenda kwenye interview ya kazi katikaΒ  kampuni moja ambayo niliomba nafasi miezi michache iliyopita,Β  Mama alinitazama hadi nazama Bafuni kisha aliingia chumbaniΒ  kwangu na kuanza kukagua vitu vyangu.Β 

    Aliona kadi za mapenzi ambazo Mosses alikuwa akinitumia,Β  alitikisa kichwa chake kisha aliondoka chumbani kwangu.Β 

    Asubuhi hiyo hiyo, kwenye moja ya jumba la kifahari alikuwepoΒ  Mtoto wa kitajiri aliyeitwa Osman, alikuwa mweupe mwenyeΒ  asili ya uarabu, ndiye mmiliki wa kampuni ambayo MimiΒ  nilitakiwa kwenda kufanyiwa usaili kwa ajili ya kazi, huyuΒ  Osman ni Mwanaume mwenye maumivu makali ndani ya moyo wakeΒ  kwani miezi miwili iliyopita aliachwa na MwanamkeΒ  aliyetarajia kumuowa, Mwanamke huyo aliitwa Zahra, huyo ZahraΒ  alitoroka na kiasi kikubwa cha pesa kisha kwenda nje ya Nchi,Β  alimtumia ujumbe Osman kuwa hamuhitaji tena katika MaishaΒ  yake, tokea siku hiyo Osman amekuwa ni Mwanaume mwenyeΒ  kuutafuta upendo wa kweli.Β 

    Asubuhi hiyo Osman aliondoka kwenye jumba hilo na kuelekeaΒ  kwenye kampuni ambayo mimi nilikuwa naenda kufanya usaili,Β  kutokana na mvua kubwa kunyesha kulisababisha foleni kubwaΒ  iliyoniweka kwa zaidi ya dakika hamsini, nilikuwa tayariΒ Β nimechelewa kwenye Usahili, pembezoni mwangu kulikuwa na gariΒ  aina ya Benzi nyeusi, alionekana huyo Osman akiwa anaangaliaΒ  sana saa yake, ilikuwa ndiyo mara ya kwanza namuona, jinsiΒ  alivyokuwa akihangaika kuangalia saa yake ilinipa moyo kuwaΒ  siyo mimi tu niliyechelewa kwenye jambo bali tupo wengiΒ  pasipo kujuwa huyo Mtu ndiye mmiliki wa hiyo kampuni.Β 

    Nikiwa kwenye daladala, Mosses alinipigia akaniuliza nikoΒ  wapi, kiukweli jinsi nilivyokurupuka nyumbani sikuweza hataΒ  kumuaga kuwa naenda kwenye Usahili, ilinibidi nimueleze kuwaΒ  nipo kwenye daladala naelekea kwenye Usahili ila nimechelewa.Β 

    “Kama ni hivyo basi chukua pikipiki nitakutumia pesa kidogoΒ  ulipe maana hapo utazidi kuchelewa” Alisema Mosses,Β  alinifanya nitabasamu, niliona ndiye Mwanaume anayenijaliΒ  kuliko Wanaume wote Duniani. Basi nilishuka, nilimuona piaΒ  Osman naye akishuka kwenye gari, sote tulitazama upande mmojaΒ  tukaita pikipiki moja iliyokuwa karibu, ilitushangaza kuonaΒ  sote tunamuita Bodaboda huyo, Osman alinitazama namiΒ  nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha alinisogelea sababu yuleΒ Bodaboda alikuwa akija kwangu, si unajuwa tena MwanamkeΒ  ananguvu kubwa sana kwa Mwanaume? Basi ndivyo ilivyokuwa kwaΒ  Bodaboda huyoΒ 

    “Samahani Dada yangu naomba usubirie Pikipiki nyingine mimiΒ  nina dharura kuna Watu wananisubiria!” Alisema Osman, manenoΒ  yake yalinifanya nimuulizeΒ 

    “Ina maana wewe ndiye mwenye haraka peke yako? Hata MimiΒ  nasubiriwa huko ninakoenda hivyo wewe ndiye unayepaswaΒ  kusubiria nyingine” Nilisema kwa haiba ya kike, ilikuwa ndiyoΒ  mara ya kwanza namuona Osman, sikujuwa kama ndiye mmiliki waΒ  hiyo kampuni niliyokuwa naenda kwenye Usahili. BodabodaΒ  aliingilia katiΒ 

    “Kwani wewe Bro unaenda wapi na wewe Sistaa unaenda wapi?”Β  Aliuliza Bodaboda huyoΒ 

    “JM Motors” NilisemaΒ 

    “JM Motors” Alisema Osman, sote tulijikuta tukiitaja sehemuΒ  moja ambayo ndiyo hiyo kampuni ya Uuzaji wa Magari kutokaΒ  DubaiΒ 

    “Sasa si unaona mlitaka kunikosesha pesa za vichwa viwili,Β  panda sistaa huyo jamaa aje kwa nyuma” Alisema Bodaboda hukuΒ  manyunyu yakianza tenaΒ 

    “Siwezi kuanza, apande yeye mimi nitakaa nyuma” Nilisema,Β  Osman alicheka tu kisha alisemaΒ 

    “Naitwa Osman Dhabi” alinipatia Mkono kwa lengo la kutakaΒ  kunifahamu pia lakini sikutaka mazoea naye kabisa, sikumpaΒ  mkono wangu, Osman alitabasamu tu kisha alipanda kwenyeΒ  pikipiki kisha nami nilifuatia. Safari ilianza kuelekea JMΒ  Motors, Osman alionekana kuwa muongeaji kiasi, niliwasikiaΒ  wakiongea kuhusu Wanawake ili sikutaka kujali sana, mwendo waΒ  dakika kama 30 hivi tulifika JM Motors huku mvua ikianzaΒ  kuchanganya, Niliposhuka tu nilikimbilia kujihifadhi kwenyeΒ  maegesho ya Magari nikiwa natetema baridi, Osman alilipa pesaΒ  ya Pikipiki kisha yule Bodaboda aliondoka, niliangalia simuΒ  yangu kuona kama Mosses alikuwa amenitumia pesa ya PikipikiΒ  lakini alikuwa bado hajatuma.Β 

    Osman alisogea akaniambiaΒ 

    “Nimeshalipa usijali” Alisema kisha alitabasamu tu, kwanguΒ  niliona kama amenidharau hivi, nilifungua pochi yangu nikatoaΒ  elfu tano ambayo ndiyo ilibakia hiyo hiyo ya kurudiaΒ  nyumbani, nilimpa Osman

    “Huwa sipendi vitu vya Bure” Nilisema kwa hasiraΒ 

    “Samahani sikujuwa kama ungechukia, upo hapa kwa ajili yaΒ  Usahili?” AliniulizaΒ 

    “Ukijuwa itakusaidia nini? Sihitaji mazoea ya kijinga”Β  Nilisema kisha niliekea ambako Watu walikuwa wakiingia, OsmanΒ  alitabasamu tu akiwa ndani ya Shati jeupe ambalo lilikuwaΒ  limeloa na suruali nyeusi iliyomkaa vizuri, moyo wanguΒ  uliniambia kuwa Mwanaume huyo alikuwa na mvuto sana ilaΒ  alikuwa na dharau.Β 

    Nilipofika ndani nilielekea mapokezi, niliambiwa kuwa BosiΒ  anayepaswa kutufanyia Usahili bado hajafika hivyo nilioneshwaΒ  chumba ambacho Watu wanaotakiwa kusahiliwa walikuwepo, wakatiΒ  natembea nilihisi kupoteza kitu. Ndiyo, nilisahau BahashaΒ  yenye vyeti vyangu ndani ya ile Daladala.Β 

    Roho iliniuma sana na sikuuona umuhimu wa Usahili tena,Β  nilitamani kuondoka lakini yule Mdada alisemaΒ 

    “Ingia chumba hicho Bosi huyo anakuja” Alikuwa kamaΒ  amenishtua hivi, haraka niliekelea kwenye chumba hicho bilaΒ  kugeuka nyuma.Β 

    Nilijaribu kumtumia ujumbe Mosses lakini hakujibu, nilimpigiaΒ  lakini hakupokea simu yangu, nilijiona nina mzigo ndani yaΒ  moyo wangu, nilimpigia Mama kumueleza hali halisi, aliniambiaΒ  kuwa alibakiwa na pesa ile aliyonipa hivyo labda baadayeΒ  anaweza akapata kisha akanitumia.Β 

    Osman alielekea ofisini kwake, alibadilisha nguo zake huko,Β  alikuwa ni Kijana wa kisasa na mwenye pesa sana, alikuwaΒ  akisimamia miradi mingi ya Baba yake Mzee Dhabi aliyekoΒ  Dubai.Β 

    Tulipaswa kusubiria kwa zaidi ya saa nzima, njaa ilikuwaΒ  ikizidi kuniuma, Mdada mmoja aliye jirani yangu aliniambiaΒ 

    “Jinsi ulivyolowa na unasema umesahau vyeti jiandae kwaΒ  maneno ya shombo, huyo Bosi ni kijana tu, msafi sana, alafuΒ  mzuri, huoni zimetangazwa nafasi wanawake wengi ndiyoΒ  waliojitokeza tena wakiwa wamevalia vizuri zaidi yako!”Β  Alisema kwa sauti ya Chini, nilimjibuΒ 

    “Sikuja kwenye mashindao ya urembo nimekuja kutafuta kazi,Β  kama sitopata nitatafuta kwingine, siwezi kuwa Mtumwa waΒ  umasikini wangu” Nilimjibu, nilimkata kauli hakusema tena, niΒ  kweli alichokuwa amekisema Wasichana walikuwa wakijipodoaΒ sana ili wakiingia huko wakamshawishi huyo Bosi ambaye mimiΒ  nimetoka kuzozana naye bila kujuwa.Β 

    Jina langu lilikuwa la kwanza kuitwa, niliomba niwe wa mwishoΒ  sababu nguo zangu zilikuwa zinavuja maji, bahati nzuri MdadaΒ  aliyekuja kuniita alinielewa, Basi walianza kwenda hukoΒ  pasipo kurudi hadi pale nilipobakia peke yangu ndani yaΒ  Chumba hicho. Maneno ya yule Mdada yalizidi kujirudia kwenyeΒ  ufahamu wangu, kwa kiasi kikubwa yalianza kunitisha sana.Β  Basi, zamu yangu ilipofika nilivuta pumzi kwa nguvu ndaniΒ  kisha nilizitoa ili kuondoa hali ya woga ambayo nilionaΒ  inaanza kuniandama, nilikuwa kama kichaa hivi sababu nguoΒ  bado zilikuwa mbichi, sikuwa na vyeti vya elimu yangu yaΒ  Biashara.Β 

    Nilipiga hatua ndogo ndogo kuelekea kwenye ofisi kwa ajili yaΒ  Usahili, nilipoingia nilipigwa na butwaa, nilimuona OsmanΒ  akiwa ameinama anaandika jambo, yule Mdada alimwambia OsmanΒ 

    “Bosi, huyu wa mwisho anaitwa Jacklin, alitakiwa kuwa waΒ  kwanza ili hakuwa tayari” Alisema, Osman hakunyanyua machoΒ  yake, alisemaΒ 

    “Sawa anaweza akaketi” Alisema bila kuniangalia usoni,Β  nilitamani kuondoka maana kwa jinsi nilivyomjibu vibayaΒ  kuanzia kule barabarani hadi tunafika ofisini kwakeΒ  sikufikiria kama atanisikiliza, basi niliketi hivyo hivyoΒ  kama Mtu aliyeyavulia maji nguo, Sharti ayaoge. NilisubiriaΒ  kwa sekunde kadhaa, yule Mdada aliondoka, baadaye OsmanΒ  alinyanyua kichwa chake, aliponiona alinitazama kwaΒ  kunishangaa kama vile alikuwa hajawahi kuniona.Β 

    “Karibu” Alisema Osman, jicho lake niliona lilikuwa na ujumbeΒ  fulani kwenye hisia zangu, alinitazama kama vile alikuwaΒ  akitengeneza kitu alafu akawa anakiangalia kama kipo sawa,Β  nilihisi pengine kwasababu nilikuwa nimeloa na pia nilimsemeaΒ  vibaya.Β 

    “Asante!” Nilisema kwa sauti iliyojaa aibuΒ 

    “Naitwa Osman Dhabi, ni Mmiliki wa kampuni hii, UnaitwaΒ  nani?” Aliniuliza kama vile hakuna kilichotokea baina yetu,Β  ilinifanya niwe na maswali mengi kichwani kwanguΒ 

    “Naitwa Jacklin Sembu, nimekuja kwa ajili ya Usahili wa kazi”Β  Nilisema nikiwa nimeinamia chini, Osman aliniambiaΒ 

    “Sina haja ya kukufanyia Usahili sababu nimeshakufanyiaΒ  tukiwa njiani, sitaki kuingilia Maisha yako Jacklin lakiniΒ kuna wakati unapaswa kuacha jeuri yako” Alisema kishaΒ  alichukua barua akaniambiaΒ 

    “Hii uje nayo baada ya siku saba, nilihitaji nafasi ya MtuΒ  mmoja pekee, nimechagua kufanya kazi na wewe” Alisema Osman,Β  nilijikuta nikitabasamu kwa shida sana, ni kweli nilikuwaΒ  nahitaji hiyo kazi kwa udi na uvumba lakini niliishiwa manenoΒ  ya kuyasema mbele ya Osman, nilijiona nimeelemewa kabisa,Β  nafsi ilinisuta nikasemaΒ 

    “Nashukuru na Mungu akubariki”Β 

    “Usijali Jacklin, ubaya haulipwi kwa ubaya katu, ubayaΒ  hulipwa kwa mazuri yasiyosahaulika” Alisema tena kishaΒ  alinipa mkono ambao niliukataa kule barabarani, ilinibidiΒ  niupokee, aliuchezea kidogo mkono wangu kwa kunisabahiΒ 

    “Nakutakia siku njema” Alisema Osman kisha aliendelea na kaziΒ  zake, nilinyanyuka kisha niliangalia kiti nilichokaliaΒ  niliona kimeloa maji ambayo yalikuwa yakinichuruzika,Β  niliondoka ofisini kwa Osman nikiwa mwenye furaha sana.Β  Mosses hakunipigia kabisa wakati alisema angenipa pesa yaΒ  kulipia usafiri, basi nililazimika kumpigia MamaΒ 

    “Jacklin Mwanangu sijapata pesa kama unaweza kusubiria hadiΒ  jioni sawa” Alisema MamaΒ 

    “Usijali Mama nitarudi tu” Nilisema, sikuwa na pesa ya nauliΒ  ya kurudia nyumbani alafu mvua ilikuwa ikinyesha sana,Β  kulikuwa na hali ya radi pia, nilifikiria kama OsmanΒ  angelinikuta pale nje ingeleta picha mbaya zaidi, nilifikiriaΒ  pia ile pesa niliyompa kwa hasira, nilijilaumu sana kwaΒ  kiburi changu. Basi niliingia kwenye mvua, nilivua viatuΒ  vyangu. Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Pili Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ 

     

    Pumzi ya mwisho Riwaya ya pumzi mwisho

    19 Comments

    1. Farnoush on October 11, 2024 4:31 pm

      Tamu balaaaa

      Reply
    2. Lus twaxie on October 11, 2024 4:38 pm

      Nshaanza kuipenda

      Reply
      • Jackson on October 11, 2024 7:10 pm

        Hiii mashine

        Reply
        • Narkiso on October 15, 2024 4:45 am

          Nice one

          Reply
    3. Suleiman abduli on October 11, 2024 5:08 pm

      Kama naanza kuielewa hivi

      Reply
    4. Kevin Winton mwasambiri on October 11, 2024 6:38 pm

      Himenifunza kutulia bila papala

      Reply
      • G shirima on October 11, 2024 9:25 pm

        Hii naon itakua ya moto sana alafu wifanye iwe ndefu kidogo sasa na matukio mengi mengi kidogo

        Reply
    5. Tumpe on October 11, 2024 7:02 pm

      Aaah weeh😁πŸ₯°

      Reply
    6. Paka mweusi on October 11, 2024 7:11 pm

      Hiii imeenda

      Reply
    7. Ym on October 11, 2024 7:12 pm

      Ipo vizuri

      Reply
    8. Sabitimussa23 on October 12, 2024 12:45 pm

      Najifunza vitu vingi sana kupitia liwaya hizi πŸ‘ŠπŸΎ

      Reply
    9. Martin on October 12, 2024 5:03 pm

      https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z

      Reply
    10. Martin on October 12, 2024 5:04 pm

      https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z

      Group la mkeka

      Reply
    11. Le izoneee on October 12, 2024 5:32 pm

      Oa admini iko poah sanaaaa….achiaaa ilooo dudeee lingneee

      Reply
      • Pedma on October 12, 2024 5:44 pm

        Simulizi tamuu sanaa

        Reply
    12. Pedma on October 12, 2024 5:44 pm

      Simulizi tamuu sanaa

      Reply
    13. Prof. Noon saleh17 on October 12, 2024 7:56 pm

      Hii enyewe kabisaπŸ‘ŠπŸ½..

      Reply
    14. Marietha on October 25, 2024 11:28 am

      Nimeipenda

      Reply
    15. πŸ“ͺ + 1.794439 BTC.GET - https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=f304a77f3b4d5285e0076651168d2e5d& πŸ“ͺ on July 3, 2025 9:04 am

      3ttvjp

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.