Mvua ilikuwa ikinyesha, moyo wangu ulijawa na tabasamu kubwaย sana, nilijinyoosha ili kuianza siku mpya ambayo ilianza kwaย hali ya hewa kuwa nzuri yenye ubaridi. Niliposhika simu yanguย niliona picha ya Mwanaume niliyempenda sana. Niliiweka kwenyeย kioo cha simu yangu, alikuwa akiitwa Mosses, alikuwa niย mwanaume aliyeuteka moyo wangu sana, nilimpenda kwa nguvuย zangu zote, hisia zangu ziliniambia Mosses ndiye Mume wangu.ย
Tabasamu lilikuwa limejaa usoni pangu, nilimpigia Mosses iliย niweze kusikia sauti yake, sauti ambayo ilikuwa ndiyo tulizoย pekee la nafsi yangu!ย
“Hello My love” Nilisikia sauti ya Mosses ikisema, basi moyoย wangu ulifurahi sana, wewe msomaji unaweza kuwa shahidi waย hili ile furaha unayoipata unapoongea na mpenzi wako nyakatiย za asubuhi basi ndiyo iliyonivaa wakati huo. Kwanza nilihemaย kidogo ili niweze kumjibu Mossesย
“Mambo Mpenzi, bado haujaamka?” Nilimuuliza Mosses kwa sautiย iliyojaa bashasha. Mosses alinijibuย
“Ndiyo naamka Mpenzi, yaani huwezi amini nimetoka kukuwazaย muda huu nawe ndiyo unanipigia, hakika tunaishi katika Duniaย yetu iliyojaa Huba zito Jacklin” Alisema Mosses, mara zoteย alikuwa na maneno matamu sana kwangu kitu ambacho kilinifanyaย nizidi kuvutiwa nawe, mara mlango wa chumba changu uligongwa,ย nilisikia sauti ya Mama ikiwa inaniita.ย
“Samahani Mosses, Mama ananiita” nilisemaย
“Haya ukimaliza niambie” Alisema Mossesย
“Sawa Mume wangu mtarajiwa” Nilisema kisha nilimwambia kuwaย nampenda sana na kamwe sitoweza kumsaliti. Mara moja nilikataย simu, nilinyanyuka kitandani na kwenda kuitika wito wa Mamaย
“Shikamoo Mama” Nilimsalimia baada ya kuwa nimeshafunguaย mlango, nilikuwa nafikicha macho yangu kutokana na Mwangaย uliokuwa ukimulika macho yangu.
“Marhaba!! Ndiyo unaamka sasa hivi Jacklin? Umesahau kama leoย unatakiwa kwenda kwenye Interview?” Alisema Mamaย
“Oooh Mungu wangu nilishasahau ngoja nijiandae Mama” Nilisemaย kisha nilikimbilia Bafuni kuoga, siku hiyo ilikuwa ni siku yaย Jumatatu nilipaswa kwenda kwenye interview ya kazi katikaย kampuni moja ambayo niliomba nafasi miezi michache iliyopita,ย Mama alinitazama hadi nazama Bafuni kisha aliingia chumbaniย kwangu na kuanza kukagua vitu vyangu.ย
Aliona kadi za mapenzi ambazo Mosses alikuwa akinitumia,ย alitikisa kichwa chake kisha aliondoka chumbani kwangu.ย
Asubuhi hiyo hiyo, kwenye moja ya jumba la kifahari alikuwepoย Mtoto wa kitajiri aliyeitwa Osman, alikuwa mweupe mwenyeย asili ya uarabu, ndiye mmiliki wa kampuni ambayo Mimiย nilitakiwa kwenda kufanyiwa usaili kwa ajili ya kazi, huyuย Osman ni Mwanaume mwenye maumivu makali ndani ya moyo wakeย kwani miezi miwili iliyopita aliachwa na Mwanamkeย aliyetarajia kumuowa, Mwanamke huyo aliitwa Zahra, huyo Zahraย alitoroka na kiasi kikubwa cha pesa kisha kwenda nje ya Nchi,ย alimtumia ujumbe Osman kuwa hamuhitaji tena katika Maishaย yake, tokea siku hiyo Osman amekuwa ni Mwanaume mwenyeย kuutafuta upendo wa kweli.ย
Asubuhi hiyo Osman aliondoka kwenye jumba hilo na kuelekeaย kwenye kampuni ambayo mimi nilikuwa naenda kufanya usaili,ย kutokana na mvua kubwa kunyesha kulisababisha foleni kubwaย iliyoniweka kwa zaidi ya dakika hamsini, nilikuwa tayariย ย nimechelewa kwenye Usahili, pembezoni mwangu kulikuwa na gariย aina ya Benzi nyeusi, alionekana huyo Osman akiwa anaangaliaย sana saa yake, ilikuwa ndiyo mara ya kwanza namuona, jinsiย alivyokuwa akihangaika kuangalia saa yake ilinipa moyo kuwaย siyo mimi tu niliyechelewa kwenye jambo bali tupo wengiย pasipo kujuwa huyo Mtu ndiye mmiliki wa hiyo kampuni.ย
Nikiwa kwenye daladala, Mosses alinipigia akaniuliza nikoย wapi, kiukweli jinsi nilivyokurupuka nyumbani sikuweza hataย kumuaga kuwa naenda kwenye Usahili, ilinibidi nimueleze kuwaย nipo kwenye daladala naelekea kwenye Usahili ila nimechelewa.ย
“Kama ni hivyo basi chukua pikipiki nitakutumia pesa kidogoย ulipe maana hapo utazidi kuchelewa” Alisema Mosses,ย alinifanya nitabasamu, niliona ndiye Mwanaume anayenijaliย kuliko Wanaume wote Duniani. Basi nilishuka, nilimuona piaย Osman naye akishuka kwenye gari, sote tulitazama upande mmojaย tukaita pikipiki moja iliyokuwa karibu, ilitushangaza kuonaย sote tunamuita Bodaboda huyo, Osman alinitazama namiย nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha alinisogelea sababu yuleย Bodaboda alikuwa akija kwangu, si unajuwa tena Mwanamkeย ananguvu kubwa sana kwa Mwanaume? Basi ndivyo ilivyokuwa kwaย Bodaboda huyoย
“Samahani Dada yangu naomba usubirie Pikipiki nyingine mimiย nina dharura kuna Watu wananisubiria!” Alisema Osman, manenoย yake yalinifanya nimuulizeย
“Ina maana wewe ndiye mwenye haraka peke yako? Hata Mimiย nasubiriwa huko ninakoenda hivyo wewe ndiye unayepaswaย kusubiria nyingine” Nilisema kwa haiba ya kike, ilikuwa ndiyoย mara ya kwanza namuona Osman, sikujuwa kama ndiye mmiliki waย hiyo kampuni niliyokuwa naenda kwenye Usahili. Bodabodaย aliingilia katiย
“Kwani wewe Bro unaenda wapi na wewe Sistaa unaenda wapi?”ย Aliuliza Bodaboda huyoย
“JM Motors” Nilisemaย
“JM Motors” Alisema Osman, sote tulijikuta tukiitaja sehemuย moja ambayo ndiyo hiyo kampuni ya Uuzaji wa Magari kutokaย Dubaiย
“Sasa si unaona mlitaka kunikosesha pesa za vichwa viwili,ย panda sistaa huyo jamaa aje kwa nyuma” Alisema Bodaboda hukuย manyunyu yakianza tenaย
“Siwezi kuanza, apande yeye mimi nitakaa nyuma” Nilisema,ย Osman alicheka tu kisha alisemaย
“Naitwa Osman Dhabi” alinipatia Mkono kwa lengo la kutakaย kunifahamu pia lakini sikutaka mazoea naye kabisa, sikumpaย mkono wangu, Osman alitabasamu tu kisha alipanda kwenyeย pikipiki kisha nami nilifuatia. Safari ilianza kuelekea JMย Motors, Osman alionekana kuwa muongeaji kiasi, niliwasikiaย wakiongea kuhusu Wanawake ili sikutaka kujali sana, mwendo waย dakika kama 30 hivi tulifika JM Motors huku mvua ikianzaย kuchanganya, Niliposhuka tu nilikimbilia kujihifadhi kwenyeย maegesho ya Magari nikiwa natetema baridi, Osman alilipa pesaย ya Pikipiki kisha yule Bodaboda aliondoka, niliangalia simuย yangu kuona kama Mosses alikuwa amenitumia pesa ya Pikipikiย lakini alikuwa bado hajatuma.ย
Osman alisogea akaniambiaย
“Nimeshalipa usijali” Alisema kisha alitabasamu tu, kwanguย niliona kama amenidharau hivi, nilifungua pochi yangu nikatoaย elfu tano ambayo ndiyo ilibakia hiyo hiyo ya kurudiaย nyumbani, nilimpa Osman
“Huwa sipendi vitu vya Bure” Nilisema kwa hasiraย
“Samahani sikujuwa kama ungechukia, upo hapa kwa ajili yaย Usahili?” Aliniulizaย
“Ukijuwa itakusaidia nini? Sihitaji mazoea ya kijinga”ย Nilisema kisha niliekea ambako Watu walikuwa wakiingia, Osmanย alitabasamu tu akiwa ndani ya Shati jeupe ambalo lilikuwaย limeloa na suruali nyeusi iliyomkaa vizuri, moyo wanguย uliniambia kuwa Mwanaume huyo alikuwa na mvuto sana ilaย alikuwa na dharau.ย
Nilipofika ndani nilielekea mapokezi, niliambiwa kuwa Bosiย anayepaswa kutufanyia Usahili bado hajafika hivyo nilioneshwaย chumba ambacho Watu wanaotakiwa kusahiliwa walikuwepo, wakatiย natembea nilihisi kupoteza kitu. Ndiyo, nilisahau Bahashaย yenye vyeti vyangu ndani ya ile Daladala.ย
Roho iliniuma sana na sikuuona umuhimu wa Usahili tena,ย nilitamani kuondoka lakini yule Mdada alisemaย
“Ingia chumba hicho Bosi huyo anakuja” Alikuwa kamaย amenishtua hivi, haraka niliekelea kwenye chumba hicho bilaย kugeuka nyuma.ย
Nilijaribu kumtumia ujumbe Mosses lakini hakujibu, nilimpigiaย lakini hakupokea simu yangu, nilijiona nina mzigo ndani yaย moyo wangu, nilimpigia Mama kumueleza hali halisi, aliniambiaย kuwa alibakiwa na pesa ile aliyonipa hivyo labda baadayeย anaweza akapata kisha akanitumia.ย
Osman alielekea ofisini kwake, alibadilisha nguo zake huko,ย alikuwa ni Kijana wa kisasa na mwenye pesa sana, alikuwaย akisimamia miradi mingi ya Baba yake Mzee Dhabi aliyekoย Dubai.ย
Tulipaswa kusubiria kwa zaidi ya saa nzima, njaa ilikuwaย ikizidi kuniuma, Mdada mmoja aliye jirani yangu aliniambiaย
“Jinsi ulivyolowa na unasema umesahau vyeti jiandae kwaย maneno ya shombo, huyo Bosi ni kijana tu, msafi sana, alafuย mzuri, huoni zimetangazwa nafasi wanawake wengi ndiyoย waliojitokeza tena wakiwa wamevalia vizuri zaidi yako!”ย Alisema kwa sauti ya Chini, nilimjibuย
“Sikuja kwenye mashindao ya urembo nimekuja kutafuta kazi,ย kama sitopata nitatafuta kwingine, siwezi kuwa Mtumwa waย umasikini wangu” Nilimjibu, nilimkata kauli hakusema tena, niย kweli alichokuwa amekisema Wasichana walikuwa wakijipodoaย sana ili wakiingia huko wakamshawishi huyo Bosi ambaye mimiย nimetoka kuzozana naye bila kujuwa.ย
Jina langu lilikuwa la kwanza kuitwa, niliomba niwe wa mwishoย sababu nguo zangu zilikuwa zinavuja maji, bahati nzuri Mdadaย aliyekuja kuniita alinielewa, Basi walianza kwenda hukoย pasipo kurudi hadi pale nilipobakia peke yangu ndani yaย Chumba hicho. Maneno ya yule Mdada yalizidi kujirudia kwenyeย ufahamu wangu, kwa kiasi kikubwa yalianza kunitisha sana.ย Basi, zamu yangu ilipofika nilivuta pumzi kwa nguvu ndaniย kisha nilizitoa ili kuondoa hali ya woga ambayo nilionaย inaanza kuniandama, nilikuwa kama kichaa hivi sababu nguoย bado zilikuwa mbichi, sikuwa na vyeti vya elimu yangu yaย Biashara.ย
Nilipiga hatua ndogo ndogo kuelekea kwenye ofisi kwa ajili yaย Usahili, nilipoingia nilipigwa na butwaa, nilimuona Osmanย akiwa ameinama anaandika jambo, yule Mdada alimwambia Osmanย
“Bosi, huyu wa mwisho anaitwa Jacklin, alitakiwa kuwa waย kwanza ili hakuwa tayari” Alisema, Osman hakunyanyua machoย yake, alisemaย
“Sawa anaweza akaketi” Alisema bila kuniangalia usoni,ย nilitamani kuondoka maana kwa jinsi nilivyomjibu vibayaย kuanzia kule barabarani hadi tunafika ofisini kwakeย sikufikiria kama atanisikiliza, basi niliketi hivyo hivyoย kama Mtu aliyeyavulia maji nguo, Sharti ayaoge. Nilisubiriaย kwa sekunde kadhaa, yule Mdada aliondoka, baadaye Osmanย alinyanyua kichwa chake, aliponiona alinitazama kwaย kunishangaa kama vile alikuwa hajawahi kuniona.ย
“Karibu” Alisema Osman, jicho lake niliona lilikuwa na ujumbeย fulani kwenye hisia zangu, alinitazama kama vile alikuwaย akitengeneza kitu alafu akawa anakiangalia kama kipo sawa,ย nilihisi pengine kwasababu nilikuwa nimeloa na pia nilimsemeaย vibaya.ย
“Asante!” Nilisema kwa sauti iliyojaa aibuย
“Naitwa Osman Dhabi, ni Mmiliki wa kampuni hii, Unaitwaย nani?” Aliniuliza kama vile hakuna kilichotokea baina yetu,ย ilinifanya niwe na maswali mengi kichwani kwanguย
“Naitwa Jacklin Sembu, nimekuja kwa ajili ya Usahili wa kazi”ย Nilisema nikiwa nimeinamia chini, Osman aliniambiaย
“Sina haja ya kukufanyia Usahili sababu nimeshakufanyiaย tukiwa njiani, sitaki kuingilia Maisha yako Jacklin lakiniย kuna wakati unapaswa kuacha jeuri yako” Alisema kishaย alichukua barua akaniambiaย
“Hii uje nayo baada ya siku saba, nilihitaji nafasi ya Mtuย mmoja pekee, nimechagua kufanya kazi na wewe” Alisema Osman,ย nilijikuta nikitabasamu kwa shida sana, ni kweli nilikuwaย nahitaji hiyo kazi kwa udi na uvumba lakini niliishiwa manenoย ya kuyasema mbele ya Osman, nilijiona nimeelemewa kabisa,ย nafsi ilinisuta nikasemaย
“Nashukuru na Mungu akubariki”ย
“Usijali Jacklin, ubaya haulipwi kwa ubaya katu, ubayaย hulipwa kwa mazuri yasiyosahaulika” Alisema tena kishaย alinipa mkono ambao niliukataa kule barabarani, ilinibidiย niupokee, aliuchezea kidogo mkono wangu kwa kunisabahiย
“Nakutakia siku njema” Alisema Osman kisha aliendelea na kaziย zake, nilinyanyuka kisha niliangalia kiti nilichokaliaย niliona kimeloa maji ambayo yalikuwa yakinichuruzika,ย niliondoka ofisini kwa Osman nikiwa mwenye furaha sana.ย Mosses hakunipigia kabisa wakati alisema angenipa pesa yaย kulipia usafiri, basi nililazimika kumpigia Mamaย
“Jacklin Mwanangu sijapata pesa kama unaweza kusubiria hadiย jioni sawa” Alisema Mamaย
“Usijali Mama nitarudi tu” Nilisema, sikuwa na pesa ya nauliย ya kurudia nyumbani alafu mvua ilikuwa ikinyesha sana,ย kulikuwa na hali ya radi pia, nilifikiria kama Osmanย angelinikuta pale nje ingeleta picha mbaya zaidi, nilifikiriaย pia ile pesa niliyompa kwa hasira, nilijilaumu sana kwaย kiburi changu. Basi niliingia kwenye mvua, nilivua viatuย vyangu. Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Pili Ya PUMZI YA MWISHO
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMย ย
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย




24 Comments
Tamu balaaaa
Nshaanza kuipenda
Hiii mashine
Nice one
Kama naanza kuielewa hivi
Himenifunza kutulia bila papala
Hii naon itakua ya moto sana alafu wifanye iwe ndefu kidogo sasa na matukio mengi mengi kidogo
Aaah weeh๐๐ฅฐ
Hiii imeenda
Ipo vizuri
Najifunza vitu vingi sana kupitia liwaya hizi ๐๐พ
https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z
https://chat.whatsapp.com/K7bQpacPX2oGwBOn19mQ7z
Group la mkeka
Oa admini iko poah sanaaaa….achiaaa ilooo dudeee lingneee
Simulizi tamuu sanaa
Simulizi tamuu sanaa
Hii enyewe kabisa๐๐ฝ..
Nimeipenda
3ttvjp
Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?
Perfectly pent content, thanks for information. “In the fight between you and the world, back the world.” by Frank Zappa.
Thanks , I’ve just been looking for information approximately this topic for a while and yours is the greatest I have discovered till now. But, what concerning the conclusion? Are you certain about the supply?
I got what you mean ,saved to fav, very decent site.
I believe other website proprietors should take this internet site as an example , very clean and good user genial pattern.