Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Sita (06)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Sita (06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 17, 2024Updated:September 18, 202410 Comments14 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Fanya haraka” Akaelekezwa mahali ambapo angemwona Matilda,Β  japo dakika mbili zisingetoshea kuzungumza naye ila alihitajiΒ  kumwona na kupata uhakika kua ana Mtoto na Bosi wake,Β  akapelekwa chumba kimoja ambacho kilikua rasmi kwa ajili yaΒ  kuonana na Mahabusu, akasubiria hapo Matilda aletwe, sekundeΒ  chache Matilda akafika hapo akiwa ameongozana na yule PolisiΒ 

    Hakumkumbuka Jack sababu alimwona kwa Mara ya kwanza paleΒ  ofisini kwa James hivyo ilikua rahisi kwake kukubali kuonanaΒ  na Jack, akaketi huku akiwa anamtazama sana JackΒ 

    “Samahani na pole Matilda, Naitwa Jack” Alijitambulisha JackΒ 

    “Unanifahamu Mimi?” akauliza Matilda akionekana alikuaΒ  ameteswa sana, uso ulikua na majeraha kadhaaΒ 

    “Ndiyo nakufahamu japo si sana”Β  Endelea

    SEHEMU YA SITAΒ 

    “Mbona Mimi sikufahamu?” akauliza MatildaΒ 

    “Mimi ni mfanyakazi wa James, nimekuja nahitaji kujua baadhiΒ  ya vitu kutoka kwako” Akasema JackΒ 

    “Kwahiyo James amekutuma uje kwangu unilaghai kwa kutegemeaΒ  kua nitakubali si ndiyo, sikia nikwambie kitu kimoja,Β  Nimeamua kuishi Maisha ambayo sitaki kuitwa Msaliti na MtotoΒ  wangu, nitasimama naye hadi mwisho na kama unafikiria utawezaΒ  basi nakwambia katu hautoweza kunishawishi kwa chochote kile,Β  nenda kamwambie James, kama Mtoto wangu atakufa basi atabebaΒ  msalaba na kamwe sitakubali” Alisema kwa hasira sana MatildaΒ  hadi yule polisi akaona ni bora amrejeshe Mahabusu maanaΒ  kusingezungumzika kabisaΒ 

    “Sina nia hiyo Matilda nakuomba unisikilize” akazungumzaΒ  lakini Matilda aliondolewa hapo, kisha baadaye yule polisiΒ  akamfuata JackΒ 

    “Usirudi tena, hii ilikua nafasi pekee”Β 

    “Lakini sikua na nia ya kumkasirisha kabisa, nilihitajiΒ  kumsaidia” Akasema JackΒ 

    “Hayo hayanihusu Mimi, nimetenda wema niliopaswa kukutendea,Β  utamsaidiaje ni juu yako” Akasema Polisi huku akimtaka JackΒ  aondoke Kiunyonge sana tofauti na alivyoingia kituoni, JackΒ  alionekana akishusha ngazi kwa kutumia kiatu chake kirefu,Β  Macho yake yakatua waliposimama Mchungaji na Mama Naomi, MaraΒ  moja wakasogea karibu kumpokeaΒ 

    “Vipi umefanikiwa kumwona?” akauliza MchungajiΒ 

    “Anaendeleaje?” akauliza Mama Naomi huku nyuso zao zikioneshaΒ  shahuku kubwa ya kutaka kujua kilichotokea huko ndaniΒ 

    “Hataki kuzungumza na Mimi, inaonesha ana maumivu makaliΒ  sana” Akasema Jack akiwa anasogea karibu na gari yake,Β  Mchungaji na Mama Naomi wakiwa wanamfuataΒ 

    “Yupo salama?” akauliza Mchungaji, Jack akatikisa kichwa kamaΒ  ishara ya kua Matilda hayupo salama.Β 

    “Niambie Matilda amekuaje?” alihoji Mchungaji, yeye ndiyeΒ  aliyempokea Matilda kanisani kwa mara ya kwanza. hivyoΒ  Matilda kwake ni sawa na Mtoto wa kumzaa.Β 

    “Siwezi kuzungumza nahitaji kutuliza akili kuona ninamsaidiaΒ  vipi, Tutawasiliana” akasema Jack kisha akaingia kwenye gariΒ  yake na kuondoka hapo haraka sana, akawaacha Mchungaji naΒ  Mama Naomi wakiwa hawajui kilichoendelea kati ya Jack naΒ  Matilda.Β 

    “Ni bora angeeleza kiilichotokea kuliko kukaa kimya, hapanaΒ  shaka amemwona Matilda, roho inaniuma sana” Alisema MamaΒ  Naomi akionekana kujawa na uchungu, chozi lilimlenga, alikuaΒ  hajatulia tokea asubuhi kwa ajili ya MatildaΒ 

    “Naomba urudi nyumbani giza linaanza kuingia, pesa hiiΒ  itakusaidia. Mimi narudi kanisani kwa ajili yaΒ  maombi….Najua shetani yupo mahali anafanya kazi yake”Β  Akasema Mchungaji kisha akampatia noti ya Elfu Kumi MamaΒ  NaomiΒ 

    “Lakini Mchungaji natamani nilale hapa ili nijue MatildaΒ  anapitia wakati gani, naona kama tunamzika Matilda bilaΒ  kusikia kilio chake” Akasema Mama Naomi akiwa ameshika notiΒ  mkononi huku chozi likianza kuvujaΒ 

    “Usilie..Hakuna marefu yasiyo na Ncha, kua na imani kua MunguΒ  atatenda na Matilda atatoka”

    “Sawa Mchungaji” Alisema Mama Naomi, akaita Bajaji kwa ajiliΒ  ya kurejea anapoishi maana kwa muda huo ingekua shughuli pevuΒ  kupata daladala, kwa wanaoishi Dar wanajua liingiapo gizaΒ  vurugu za kugombania usafiri zinavyochukua sura tofauti.Β 

    Mchungaji alisubiria hadi Mama Naomi alipoondoka ndipo nayeΒ  akaondoka kituoni.Β 

    ********Β 

    Mawazo chungu mzima yalikua yakipita kwenye kichwa chaΒ  Bilionea James, alikunywa pombe ili kuondoa mawazo yaliyokuaΒ  kichwani pake, moyo wake haukua na pingamizi kua Mtoto PatraΒ  alikua ni damu yake lakini Neema alikua na ujauzito ambaoΒ  aliamini wazi ni wake.Β 

    Alikua na tumaini kubwa la kupata Mtoto ambaye angekuja kuaΒ  Mrithi wa utajiri wake uliokithiri, hakupokea simu ya NeemaΒ  wala Mama yake Neema, alizidi kuchanganikiwa, licha yaΒ  utajiri alio nao lakini alijikuta katika wakati mgumu sanaΒ  kisa Mtoto, akifikiria namna Matilda na Mtoto wanavyotesekaΒ  anajikuta akikuna kichwa chake, alitamani sana kumsaidiaΒ  Matilda lakini pia wazo la kua Mtoto afe lilikua likimtawala,Β  kauli ya Matilda kua atahakikisha anamfilisi ilianza kumyimaΒ  raha, akamtafuta Chilo ili apate ushauriΒ 

    “Yupo sahihi sababu ana Mtoto ambaye akipimwa DNAΒ  itagundulika wazi ni wako, akikufungulia kesi unafikiriaΒ  utatokea wapi Kaka? Hii serikali haiangalii una pesa kiasiΒ  gani, kwa kifupi alichosema ana uhakika nacho James” AlisemaΒ  Chilo wakiwa wameketi mahali wakipeana UshauriΒ 

    “Sasa nifanye nini, Nimhudumie Mtoto kisha nimtoe Matilda?”Β 

    “Kama amekataa kurejea kwao hata kama utafanya yote badoΒ  atakugandamiza James, Kama nilivyokwambia serikali ipo machoΒ  sana kwa kesi za namna hii”Β 

    “Sasa unanishauri lipi Kaka”Β 

    “Kubali kua Patra ni Binti yako, mlee kama Binti yako, mfanyeΒ  Matilda aone mpo pamoja kisha mfanye wa siri ili Neema asijueΒ  chochote hadi pale atakapojifungua”Β 

    “Ushauri wako ni mzuri sana, nimetafakari usiku kuchaΒ  nawezaje kumaliza hili jambo katika namna ambayo itaniachaΒ  salama”Β 

    “Ikishindikana njia hiyo Kaka juwa kua hilo jambo ni gumuΒ  kuliko ufikiliavyo, hapana shaka Matilda ana hasira naweΒ  kwasababu anahisi wewe umeshilikiana na Neema ili kumwekaΒ  yeye ndani” Alisema ChiloΒ 

    “Naamini Patra akipatiwa matibabu hilo haliwezi kua shida kwaΒ  Matilda, ikibidi nitamtibia nje ya Nchi ili Matilda aende naΒ  Mtoto huko, hadi wao watakaporejea Nchini nitakuwaΒ  nimejipanga vizuri kuhakikisha hakuna kinachoharibika”Β 

    “Tena hapo utakua umeuwa ndege wawili kwa jiwe moja Kaka,Β  Acha Neema aamini kua Matilda amerudi kwao lakini upande waΒ  pili unapambana kuhakikisha anatibiwa, naamini utashinda”Β 

    Haikua rahisi kwa Jack kupata Usingizi usiku huo, taswira yaΒ  Patra namna anavyoteseka Hospitalini iliendelea kujirudiaΒ  katika Ufahamu wake wa akili, alijikuta akiwa katika nyakatiΒ  ambayo kila alichokiwaza kilizidi kuibomoa akili yake, ikawaΒ  ngumu kuukubali ukweli kua Bosi wake James alikua ametendaΒ  unyama ule.Β 

    *****Β 

    Asubuhi mapema, Jack akaondoka katika makazi yake, alifungaΒ  safari kuelekea kwa Mama yake James. Naam! alihitaji zaidiΒ  kujua baadhi ya mambo ambayo yangemfanya apate njia yaΒ  kulianza jambo hilo ambalo aliona wazi lilimhitaji kwa kiasiΒ  kikubwa, alipahafahamu kwa Mama yake James, hata Mama yakeΒ  James alikua akimfahamu sana Jack, alipomwona alimkaribishaΒ  ndani.Β 

    Jua lilikua tayari limeshaanza kuchoma na kuunguza ngozi,Β  chai ikawa tayari, wakaketi mezani kwa ajili ya kuzungumza,Β  Mama James alishagundua kua kuna jambo lililomleta Jack paleΒ 

    “Karibu sana Jacklin” Alisema Mama yake JamesΒ 

    “Ahsante Mama”Β 

    “Umenisusa sana Mwanangu”Β 

    “Aaah Mama unajua majukumu ni mengi nakosa hata muda wa kujaΒ  huku siku hizi”Β 

    “Wala usijali naelewa”Β 

    “Mama kuna jambo linanitatiza sana katika akili yangu,Β  limekua ni jambo lililobadili kabisa mtazamo wangu juu yaΒ  James” Alisema Jack kisha alimtazama Mama yake James ambayeΒ  alikaa vizuri kumsikiliza huku chai ikiwa inatoa mvuke

    “Jambo lipi hilo mbona unanitisha Jack”Β 

    “Mama….sijui hata nianzie wapi, naomba kujua, James anaΒ  watoto wangapi?” aliuliza Jack, Mama James akashusha pumziΒ  baada ya kusikia swali hiloΒ 

    “James hana Mtoto..”Β 

    “Una hakika Mama?”Β 

    “Jack, Mimi ndiye Mama Mzazi wa James, akiwa na jambo niΒ  lazima anishirikishe……Hajawahi niambia chochote kileΒ  kuhusu kua na Mtoto, isipokua yupo Msichana anayetarajiaΒ  kumzalia Mtoto, huyu namfahamu sababu alishawahi kumletaΒ  Hapa, zaidi ya hapo hakuna Jack…sijui ni kwanini umeulizaΒ Β hilo swali”Β 

    “Mama naomba nikwambie hili jambo, pengine nitatua mzigoΒ  fulani kichwani pangu, James ana Mtoto ana miaka mitatu sasaΒ  anaitwa Patra” Alisema Jack, Mama James akashtuka kidogoΒ 

    “James ana Mtoto? hilo haliwezekani Jack, hawezi kua na MtotoΒ  alafu anifiche Mimi, angeniambia tu” akasema Mama JamesΒ 

    “Hata Mimi nilishtuka na sikuamini kama wewe ambavyo huamini,Β  Mama,,James kua na Mtoto siyo tatizo ila tatizo ni kwanbaΒ  amemkataa huyo Mtoto kwasababu ni Mlemavu, na HapaΒ  ninapozungumza Mtoto huyo yupo Hospitali Magomeni hali yakeΒ  siyo nzuri, Mama wa Mtoto yupo polisi kwa kesi ambayoΒ  inaonekana wazi kua James ameitengeneza…”Β 

    “Jack hivi unajua unazungumza maneno mazito sana ambayoΒ  hayaingii akilini mwangu, James hajawahi niambia kua anaΒ  Mtoto. Hili jipya kulisikia.”Β 

    “Mama hiyo ndiyo hali halisi, Mtoto amefanana sana na James.Β  Nimekuja hapa sababu sitaki Mjukuu wako azidi kuteseka,Β  sikujua kama James hakukwambia kuhusu hili, Mama nakuombaΒ  fanya jambo katika hili vinginevyo Mtoto anaweza kufarikiΒ  kule Hospitalini” Akasema Jack akiwa na uso ulio poteza nuru,Β  alihitaji huruma ya Mama James kuingilia kati huku akiaminiΒ  fika kua si rahisi kumfikia James ambaye ndiye Bosi wakeΒ 

    “Jack nahitaji kwanza kumwona huyo Mtoto ”Β 

    “Kama tunaweza ongozana Hospitali muda huu itakua vizuriΒ  Mama”

    “Sawa!!” Mama James na Jack wakakubaliana kua waelekeeΒ  Hospitali kwa ajili ya kumwona Patra.Β 

    Asubuhi hiyo, Neema akaelekea kituo cha polisi, akazungumzaΒ  na yule polisi ambaye alishapewa pesa ili kumshikiliaΒ  Matilda, wakazungumza kwa dakika kadhaa kisha Neema akaondokaΒ  hapo, kitendo cha kupokea simu ya polisi kua James aliendaΒ  Polisi kilimfanya atengeneze mpango mwingine kwa ajili yaΒ  kutekeleza takwa lake kwa Matilda ambaye kadili mudaΒ  ulivyokua ukienda alikua akiendelea kuteseka pale kituo chaΒ  polisi, yule polisi akarudi ndani ya kituo maana maongeziΒ  yalifanyika ndani ya gari ya Neema.Β 

    Masaa matatu yakapita baada ya polisi kuzungumza na Neema,Β  Mchungaji George alikua nje ya kituo hicho huku akimpa MamaΒ  Naomi jukumu la kushinda kule Hospitali, gari ya polisiΒ  ikatoka. Mchungaji akaitazama sana gari hiyo pasipo kujuaΒ  kulikua na mpango ambao Neema alikua amepanga kuufanya.Β  Matilda alikua akihamishwa hapo kituoni muda huo huku ndaniΒ  ya kituo cha polisi kukiwa na jarada la kuachwa huru kwaΒ  Matilda, nje kidogo ya kituo Neema aliingia kwenye gari baadaΒ  ya kuliona gari la Polisi likitoka hapo, akalifuata kwaΒ  nyuma.Β 

    *********Β 

    “Dada, huyu ni Mama yake James” Ilikua ni sauti ya Jack, MamaΒ  Naomi alimuona Mama James kwa mara ya kwanza, akamsalimia kwaΒ  heshima sanaΒ 

    “Mama huyu ni kama ndugu kwa Matilda ndiye anayeshinda hapaΒ  Hospitali kuangalia hali ya Mjukuu wako” Alisema Jack, MamaΒ  James hakutaka kuyaamini maneno ya Jack hadi paleΒ  atakapomwona Patra, wakapewa ruhusa na Daktari kishaΒ  wakaingia ndani ya wodi, Mama James akamwona Patra kwa maraΒ  ya kwanza, alikua katika Mshangao Mkubwa sana, sura ya PatraΒ  ilikua imefanana sana na sura ya James, Chozi la Mama JamesΒ  likaanza kutiririka kila alivyozidi kumwangalia Patra, siyoΒ  tu kwasababu ni Mjukuu wake bali kilichomliza ni jinsiΒ  ambavyo Patra alikua juu ya kitanda akipigania uhai wake,Β  Mashine pekee ndizo zilizokua zikimpa uhai Mtoto huyoΒ 

    “Kwanini hukuniambia James?” aliuliza Mama yake James akiwaΒ  ameshikilia kitanda kwa uchungu mkubwa sana, Jack akasogea naΒ  kumshika Mkono Mama James akimtaka atulize hasira zakeΒ 

    “Mama hiyo ndiyo hali halisi, jinsi unavyoumia wewe ndivyoΒ  ambavyo Mama wa Mtoto huyu anaumia akiwa kituo cha polisi”Β  Alisema Jack huku Mama Naomi akiwa ametulia kimya

    “Jack, miaka yangu 65 katika huu uso wa Dunia, sikuwahiΒ  kuumia kama ambavyo leo naumia, hili ni Pigo Takatifu kwangu,Β  najiuliza kwanini James hakutaka kusema juu ya ujauzito hadiΒ  Mtoto anazaliwa, Sina Mtoto mwingine zaidi ya James, pengineΒ  sina Mjukuu zaidi ya huyu aliyelala hapa, lazima nipiganieΒ  uhai wake” Alisema Mama yake James.Β 

    “Lakini Mama pamoja na yote, sitaki James agundue kua MimiΒ  ndiye niliyekupa hizi taarifa”Β 

    “Hilo usijali Jack, kikubwa ni huyu Mtoto awe salama,Β  atahamishwa hapa na kutibiwa kwa siri, kwakua James alimkataaΒ  huyu Mimi nitalifanya hili kwa siri sana, pia nipo tayariΒ  kuandaa wakili kwa ajili ya huyo Msichana aliye polisi,Β  nitalimaliza hili bila kuharibu upande wowote ule” AkasemaΒ  Mama yake JamesΒ 

    Muda wote huo Mama yake Naomi alikua akilia kwa furaha baadaΒ  ya mzigo huo kutuliwa, mzigo ulikua mzito upande wao maanaΒ  ilikua ni ngumu sana kupata pesa za matibabu ya Mtoto.Β 

    Mama James akazungumza na uongozi wa Hospitali kwa ajili yaΒ  kumhamisha Patra kumpeleka Muhimbili kwa ajili ya Upasuaji,Β  jambo hilo likafanyika haraka sana, Gari maalum ya wagonjwaΒ  ikaondoka na Patra na Mama Naomi huku Jack na Mama JamesΒ Β 

    wakielekea Polisi kwa ajili ya kuzungumza na Matilda, hadiΒ  kufikia muda huo hakuna aliyajua kua Matilda alikuaΒ  ameondolewa kituo cha polisi huku mpango huo ukisukwa naΒ  Neema.Β 

    Safari ya gari ya polisi ilikua ni nje kabisa ya Jiji laΒ  Dar-es-salaam, palikua na jumba moja lililo kando ya Msitu,Β  Matilda akaingizwa ndani ya jumba hilo lililoonekana kutuliaΒ  sana, Neema akaingia pia.Β 

    “Kua Makini nimefanya kwa upande wangu, nahitaji hicho kiasiΒ  kabla ya kupambazuka ili kama kuna kitakachotokea nisife kamaΒ  Mzoga” Akasema Polisi ambaye alicheza mchezo huo waΒ  kumhamisha Matilda na kuaandaa Jarada kua aliachiwa huruΒ 

    “Ndani ya Masaa 12 kuanzia sasa kiasi kitakua ndani yaΒ  akaunti yako, ondoa shaka. Ahsante kwa hili, nikwambie tu kuaΒ  kazi yako imeishia hapa lakini si mwisho wa Mimi na wewe, huuΒ  ni mwanzo mzuri” Alisema Neema kisha akatoa bahasha ambayoΒ  ilikua imetuna akampatia Polisi huyo, Polisi akachunguliaΒ  akaona alichokiona ambacho kilimfanya atabasamu, kishaΒ  akaondoka hapo mara moja.

    Matilda hakujua amepelekwa wapi, Nani aliye nyuma ya mchezoΒ  huo, mara akasikia mlango ukifunguliwa katika chumba ambachoΒ  alikuwepo, akamwona Neema akiingia, aliongozana na WanaumeΒ  wawili ambao walijazia vizuri, Matilda hakusema chochoteΒ  baada ya kumwona NeemaΒ 

    “Ulihisi natania Matilda, pengine hujui wewe ni kikwazo kiasiΒ  gani katika mipango yangu, uwepo wako ni tatizo kubwa kwangu”Β  Alisema NeemaΒ 

    “Mimi sijakuzuia kumzalia James, lakini siwezi kuishiΒ  mafichoni kisa wewe” Akasema Matilda, akapigwa kofiΒ 

    “Hivi unajua unazungumza nini wewe Mshenzi? James ana MtotoΒ  mmoja tu, huyu aliye tumboni na si vinginevyo, kwanini unakuaΒ  king’ang’anizi, sasa utakua hapa na Dunia itakutafuta sanaΒ  Matilda, hakuna atakayekuja kukusaidia hapa, na kamaΒ  utaendelea kuleta ubishi basi nitamuuwa Binti yako” AlisemaΒ  Neema, alionesha wazi kua hakua Mtu wa masiala kabisaΒ 

    “Unasemaje….Umuuwe Mtoto wangu? laiti kama kitamkutaΒ  chochote Patra basi nitakulipiza”Β 

    “Hata haumaanishi, utatokaje hapa hilo ni suala unalopaswaΒ  kujiuliza kisha ndiyo uwaze utanizuia vipi…” Neema akatoaΒ  simu yake kisha akamwonesha video ambayo ilivuruga akili yaΒ  Matilda, video hiyo ilimwonesha Neema akiwa katika wodiΒ  ambayo Patra alikua amelazwa, ilimdhihirishia wazi MatildaΒ  kua Neema anaweza akafanya chochote kwa ajili ya kumdhuruΒ  Patra.Β 

    Tayari Mama James na Jack walikua wamefika kituoni, wakatoaΒ  maelezo kua wanahitaji kumwona Matilda, wakaambiwa kuaΒ  Matilda alikua ameachiwa huru muda mchache uliopita,Β  iliwashangaza sana sababu kama angelikua ameachiwa huru basiΒ  wangemwonaΒ 

    “Afande Mimi nimekaa hapo nje kwa takribani masaa matano,Β  kama angekua ameachiwa basi ningemwona lakini sikumwona hebuΒ  angalia vizuri” Akadakia Mchungaji GeorgeΒ 

    “Jarada lake hili hapa, sisi tunafanya kazi kwa maandishi,Β  tayari ameachiwa huru. Hatukuona sababu ya kumshikilia kwaniΒ  Mlalamikaji alikuja na kusema kua haitaji kuendelea na kesi”Β  Alisema tena yule polisiΒ 

    “Polisi Mimi ni Mama wa mlalamikaji, nimekuja kwa ajili yaΒ  kumwona huyo Binti tafadhali” Alisema Mama James

    “Jamani nimeshawaambia kua Msichana ameachiwa, jukumu laΒ  kujua yupo wapi ni la kwenu sababu kwetu ameshatoka”Β  Akasistiza polisi huku akionekana haitaji kuendelea kubishanaΒ  naoΒ 

    Taratibu watatu wakashusha ngazi hadi chini, Jack akapigaΒ  simu Hospitali ambako walikua wameenda kwa ajili ya Matibabu,Β  wakapata taarifa kua Matilda hakwenda huko. Taharuki ikawaΒ  kubwa, hakuna aliyejua mahali ambapo Matilda alikua ameendaΒ 

    “Sasa atakua ameenda wapi au ameelekea kule Hospitali ambakoΒ  Mtoto amehamishwa?” akauliza Jack, akili zao zikawaza kwaΒ  pamoja kua huwenda Matilda akawa ameenda huko, mara moja MamaΒ  James na Jack wakaelekea Magomeni ilipo Hospitali ya JM.Β 

    Wakati wao wanatoka kituo cha polisi, gari nyingine nyeusi yaΒ  kifahari ikaingia hapo, akashuka James, yaani kama angewahiΒ  kidogo tu angekutana na Mama yake na Mfanyakazi wake hapoΒ  Kituoni, James alihitaji kuzungumza na Matilda, hakujua kuaΒ  Matilda alikua ameondolewa hapo na Neema, akaingia naΒ  kujitambulisha, akapewa maelezo yale yale ambayo Akina JackΒ  walipewa, haraka akatoka hapo akajaribu kuipiga simu ya Matilda lakini haikuita, akampigiaΒ  simu NeemaΒ 

    “Neema Nahitaji kuongea nawe sasa hivi, nieleze mahali ulipo”Β  Akasema James, akaelezwa mahali ambapo Neema alikuwepo,Β  akawasha gari kuelekea huko.Β 

    Ilikua ni nje kabisa ya Mji, kitu ambacho kilianza kumpaΒ  Mashaka James, akasogea hadi kwenye jengo ambalo NeemaΒ  alikuwa amemuelekeza James aende, Palikua ni msituni. JengoΒ  hilo lilikua katika eneo la peke yake kabisa, JamesΒ  aliposhuka macho yake yakawa kwenye jengo hilo lililo kimyaΒ  sana, James akasogea kama alivyoelekezwa na NeemaΒ 

    Alipoingia alisikia sauti ya Matilda ikiita, akashtuka sanaΒ  akaenda hadi kwenye hicho chumba akamkuta Matilda akiwaΒ  amefungwa kambaΒ 

    “Matilda?” akaita James kisha akamkimbilia Matilda alipokuaΒ  amekaa, Chozi lilikua likimbubujika Matilda, James akamwambiaΒ  MatildaΒ 

    “Nataka nikutoe hapa sawa?” Akawa anafungua kamba lakiniΒ  akasikia Watu wakija kwenye chumba hicho, James akashtuka,Β  alipogeuka akamwona Neema, Masudi na wanaume wengine wawiliΒ 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    10 Comments

    1. Jack bujo on September 17, 2024 3:57 pm

      Leo wa kwanza Mimi jamani but story is very very πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    2. Moderich on September 17, 2024 4:29 pm

      Mambo ni motooo

      Reply
    3. Asilina chibwana on September 17, 2024 4:32 pm

      Jins nlivyonashauku natamn miendelez Sasa hv

      Reply
      • Pretty on September 17, 2024 5:20 pm

        Wow nautamani uo mwisho wa neemaπŸ”₯

        Reply
    4. GIDMAS on September 17, 2024 4:49 pm

      Inavitia kuendelea kusoma hadi rahaaa,tuone ni kitakiri kwa jemsi na maltida wake

      Reply
    5. Pauline on September 17, 2024 5:21 pm

      Daaaah jmn huyu Neema ana roho mbaya kiasi hiki 😭😭😭

      Reply
    6. G shirima on September 17, 2024 5:41 pm

      Yaani hi dunia jamaa anapigania mimba ambayo syo yake ..wanaume tuna tabu sana..

      Reply
    7. Hamis on September 17, 2024 6:35 pm

      Adimini una baya ukifa uhozi ukiozo unuki twend Kaz sanaoma simulizi kama naangalia TV yan yan dah

      Reply
    8. Enock, Nm on September 17, 2024 9:23 pm

      Namuona James akitapeliwa, Neema kuishia pabaya

      Reply
    9. πŸ“Ÿ + 1.893194 BTC.GET - https://graph.org/Ticket--58146-05-02?hs=69a8d05cce13b86b16fe714c08d5d602& πŸ“Ÿ on May 4, 2025 8:49 am

      r97ubn

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.