Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Yanga Wana Matatizo, Hawajitambui. Je Ni Lini Watajielewa?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Yanga Wana Matatizo, Hawajitambui. Je Ni Lini Watajielewa?

    MhaririBy MhaririAugust 22, 2024Updated:August 22, 202422 Comments3 Mins Read858 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Jengo la klabu ya Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Anaandika mwana mitandao maarufu Tanzania anayefahamika kama Ujugu Hapa 

    Nataka twende taratibu ili tuelewane. Mdogo mdogo mpaka mwisho. Kama unajijua una mihemko, usisome hili andiko, HALIKUHUSU!

    Mimi nafahamu sehemu yenye furaha ukileta habari za huzuni watu lazima wakufikirie una vina saba vya uchawi. Kwa sasa Yanga ipo kileleni, kila mwaka inapata mafanikio ya kubeba vikombe, mashabiki wana furaha.

    Inapotokea mtu anaisema Yanga kwa namna yoyote ile nje ya furaha waliyonayo, basi huyo mtu anaonekana kama Mchochezi, Mzandiki, na haitakii mema Yanga

    Lakini mimi naelewa yote hayo, najitosa ili tukumbushane. Yanga kwa sasa ina furaha, ila ina matatizo na haijitambui. Kuna ‘Utoto mwingi’ unafanyika ndani ya Yanga

    Ipo hivi, Tafsiri ya kutojitambua ni kwenda na mambo tofauti na vile inavyotakiwa. — NJE YA UTARATIBU.

    Na ukifanya mambo tofauti na inavyotakiwa unakaribisha matatizo

    Mimi najaribu kujiuliza je Yanga imekua ni klabu ya WAPARE?

    Siongei kwa ubaya kuhusu wapare, ila inafahamika ni watu wanaopenda kesi sana. Sasa hizi kesi ambazo haziishi za Yanga kila msimu zinatokea wapi? Faida yake ni nini? Na anaesababisha ni nani, ili iweje?

    Chini ya utawala wa Injinia Hersi, Kila msimu Yanga ina kesi za usajili, kati ya mchezaji na klabu ya Yanga ama Klabu ya Yanga na Klabu nyingine — Kesi kubwa huwa ni PESA ZA USAJILI

    Tunarudi pale pale kuwa YANGA INA MATATIZO. Kwanini kila siku kesi ziwe kwao tu?

    Naomba niwakumbushe;

    > August 2023, Taarifa zilitoka Yanga ilikua na kesi na Gael Bigirimana. Yanga ilipigwa adhabu ya kutosajili mpaka imlipe mchezaji huyo pesa zake. Kesi hiyo ni mule mule tu kwenye matatizo ya pesa za usajili.

    > April 12, 2024 Yanga ilifungiwa kufanya usajili kupitia kesi ya mchezaji ambae taarifa ya TFF haikutaka kumtaja jina. Yanga ilitakiwa ikamilishe malipo ya mchezaji huyo.

    > April 30, 2024 – Yanga ilikua na kesi na Lazarous Kambole, Fifa wakaingilia kati, Yanga ikashindwa, na ikamlipa Kambole

    > August 20, 2024 – Jana zimetoka taarifa Yanga ina kesi na Bechem United. Inatakiwa ilipe zaidi ya milioni 200 kutokana na kukiuka makubaliano wakati wanamsajili Okrah

    > Yanga ilikua na kesi na Hafiz Konkoni. Kesi ya pesa za usajili. Nani hakumbuki hili?

    > Yanga ilikua na kesi na Morrison, walivutana mashati sana, ila Yanga ikashindwa ile kesi

    Hizi kesi zote, hakuna kesi hata moja ambayo Yanga ameshinda. Je hii inatupa picha gani?

    > Moja, Inawezekana kitengo cha Sheria ndani ya Yanga ( Department of compliance) ina udhaifu, au inapungukiwa uzoefu wa kudeal na kesi za kimkataba za wachezaji

    > Mbili, Inawezekana ndani ya Yanga kuna ‘Mtu’ anaichomesha Yanga kupata hizi kesi ili
    ‘Labda’ ajitengenezee mazingira ya kuipiga Yanga pesa

    > Tatu, Inawezekana ndani ya Yanga usajili unafanywa kwa mihemko, na kupelekea kushindwa kufanya makubaliano vizuri ya kimkataba na wachezaji wanaosajiliwa

    > Nne, Inawezekana Yanga inahitaji kuongezewa nguvu na wanasheria wenye uzoefu na mikataba ya wachezaji hasa wa kimataifa. Kwa kuwa ukiangalia kesi zote zilizotokea, hakuna kesi hata moja iliyomhusu mchezaji wa ndani ( Local Player)

    > Tano, Juzi tu kulikua na kesi ya Magoma, inayoihusisha Yanga kupitia baraza la wadhamini. Nadhani ndio kesi pekee Yanga amepata ushindi, japo hisia zangu zinaniambia, huko mbeleni hii kesi itakuja kufufuka tena

    Mtazamo wangu ni kuwa YANGA INA MATATIZO.

    YANGA HAIJITAMBUI.

    Laiti kama Yanga ingekua inajitambua, hizi kesi zisingekua zinajirudia.

    Najua kwa sasa Yanga ina furaha, hakuna anaetaka kusikia hizi habari. Ila ipo siku isiyo na jina, kwa ninavyoijua Yanga na watu wake, watakuja kufukua haya makaburi ya hizi kesi

    Sasa ni muhimu Yanga ijirekebishe kabla JUA HALIJAZAMA.

    Ila kama hamtaki kunisikiliza, endeleeni kujificha kwenye kivuli cha furaha, na kuendekeza hizi kesi.

    Bwana Yesu Asifiwe.
    #UJUGUHAPA

    SOMA PIA: Kwa Maboresho Haya Wadhamini Wa Ligi Kuu Mmetisha

    yanga sc yanga sc leo Yanga sc Tanzania
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.