Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Yanga Wana Matatizo, Hawajitambui. Je Ni Lini Watajielewa?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Yanga Wana Matatizo, Hawajitambui. Je Ni Lini Watajielewa?

    MhaririBy MhaririAugust 22, 2024Updated:August 22, 202422 Comments3 Mins Read858 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Jengo la klabu ya Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Anaandika mwana mitandao maarufu Tanzania anayefahamika kama Ujugu Hapa 

    Nataka twende taratibu ili tuelewane. Mdogo mdogo mpaka mwisho. Kama unajijua una mihemko, usisome hili andiko, HALIKUHUSU!

    Mimi nafahamu sehemu yenye furaha ukileta habari za huzuni watu lazima wakufikirie una vina saba vya uchawi. Kwa sasa Yanga ipo kileleni, kila mwaka inapata mafanikio ya kubeba vikombe, mashabiki wana furaha.

    Inapotokea mtu anaisema Yanga kwa namna yoyote ile nje ya furaha waliyonayo, basi huyo mtu anaonekana kama Mchochezi, Mzandiki, na haitakii mema Yanga

    Lakini mimi naelewa yote hayo, najitosa ili tukumbushane. Yanga kwa sasa ina furaha, ila ina matatizo na haijitambui. Kuna ‘Utoto mwingi’ unafanyika ndani ya Yanga

    Ipo hivi, Tafsiri ya kutojitambua ni kwenda na mambo tofauti na vile inavyotakiwa. — NJE YA UTARATIBU.

    Na ukifanya mambo tofauti na inavyotakiwa unakaribisha matatizo

    Mimi najaribu kujiuliza je Yanga imekua ni klabu ya WAPARE?

    Siongei kwa ubaya kuhusu wapare, ila inafahamika ni watu wanaopenda kesi sana. Sasa hizi kesi ambazo haziishi za Yanga kila msimu zinatokea wapi? Faida yake ni nini? Na anaesababisha ni nani, ili iweje?

    Chini ya utawala wa Injinia Hersi, Kila msimu Yanga ina kesi za usajili, kati ya mchezaji na klabu ya Yanga ama Klabu ya Yanga na Klabu nyingine — Kesi kubwa huwa ni PESA ZA USAJILI

    Tunarudi pale pale kuwa YANGA INA MATATIZO. Kwanini kila siku kesi ziwe kwao tu?

    Naomba niwakumbushe;

    > August 2023, Taarifa zilitoka Yanga ilikua na kesi na Gael Bigirimana. Yanga ilipigwa adhabu ya kutosajili mpaka imlipe mchezaji huyo pesa zake. Kesi hiyo ni mule mule tu kwenye matatizo ya pesa za usajili.

    > April 12, 2024 Yanga ilifungiwa kufanya usajili kupitia kesi ya mchezaji ambae taarifa ya TFF haikutaka kumtaja jina. Yanga ilitakiwa ikamilishe malipo ya mchezaji huyo.

    > April 30, 2024 – Yanga ilikua na kesi na Lazarous Kambole, Fifa wakaingilia kati, Yanga ikashindwa, na ikamlipa Kambole

    > August 20, 2024 – Jana zimetoka taarifa Yanga ina kesi na Bechem United. Inatakiwa ilipe zaidi ya milioni 200 kutokana na kukiuka makubaliano wakati wanamsajili Okrah

    > Yanga ilikua na kesi na Hafiz Konkoni. Kesi ya pesa za usajili. Nani hakumbuki hili?

    > Yanga ilikua na kesi na Morrison, walivutana mashati sana, ila Yanga ikashindwa ile kesi

    Hizi kesi zote, hakuna kesi hata moja ambayo Yanga ameshinda. Je hii inatupa picha gani?

    > Moja, Inawezekana kitengo cha Sheria ndani ya Yanga ( Department of compliance) ina udhaifu, au inapungukiwa uzoefu wa kudeal na kesi za kimkataba za wachezaji

    > Mbili, Inawezekana ndani ya Yanga kuna ‘Mtu’ anaichomesha Yanga kupata hizi kesi ili
    ‘Labda’ ajitengenezee mazingira ya kuipiga Yanga pesa

    > Tatu, Inawezekana ndani ya Yanga usajili unafanywa kwa mihemko, na kupelekea kushindwa kufanya makubaliano vizuri ya kimkataba na wachezaji wanaosajiliwa

    > Nne, Inawezekana Yanga inahitaji kuongezewa nguvu na wanasheria wenye uzoefu na mikataba ya wachezaji hasa wa kimataifa. Kwa kuwa ukiangalia kesi zote zilizotokea, hakuna kesi hata moja iliyomhusu mchezaji wa ndani ( Local Player)

    > Tano, Juzi tu kulikua na kesi ya Magoma, inayoihusisha Yanga kupitia baraza la wadhamini. Nadhani ndio kesi pekee Yanga amepata ushindi, japo hisia zangu zinaniambia, huko mbeleni hii kesi itakuja kufufuka tena

    Mtazamo wangu ni kuwa YANGA INA MATATIZO.

    YANGA HAIJITAMBUI.

    Laiti kama Yanga ingekua inajitambua, hizi kesi zisingekua zinajirudia.

    Najua kwa sasa Yanga ina furaha, hakuna anaetaka kusikia hizi habari. Ila ipo siku isiyo na jina, kwa ninavyoijua Yanga na watu wake, watakuja kufukua haya makaburi ya hizi kesi

    Sasa ni muhimu Yanga ijirekebishe kabla JUA HALIJAZAMA.

    Ila kama hamtaki kunisikiliza, endeleeni kujificha kwenye kivuli cha furaha, na kuendekeza hizi kesi.

    Bwana Yesu Asifiwe.
    #UJUGUHAPA

    SOMA PIA: Kwa Maboresho Haya Wadhamini Wa Ligi Kuu Mmetisha

    yanga sc yanga sc leo Yanga sc Tanzania

    22 Comments

    1. Kylian on August 22, 2024 12:48 pm

      Kwahy wewe ni kama nan? Na unatakaje haya wewe unaejitambua uko wap na unafanya nn kama watu wanhelasi uwaache

      Reply
      • Sanjawa on August 22, 2024 1:17 pm

        Acha akili mbovu ndo maana mwanzo kasema mtu mwenye mihemuko na asiye elewa kama ww asisome

        Reply
        • Adalberth on August 22, 2024 7:51 pm

          Sahihi

          Reply
    2. Bplm1664 on August 22, 2024 12:51 pm

      Uko ma fact Sanaa Mr UJUGU HAPA

      Reply
    3. Paschal on August 22, 2024 12:52 pm

      Kama umemaliza kuandika Kojoa ukalale

      Reply
    4. TIGER on August 22, 2024 12:56 pm

      Ni kweli lakini wewe yanakuhusu nini?

      Reply
    5. Baisar s Mjobwe on August 22, 2024 12:57 pm

      UJUGU UMEONGEA POINT SANA,SEMA KITU KIMOJA KIBAYA SANA ULICHOKITUMIA KWAMBA YANGA HAIJITAMBUI,NAFIKIRI UKASO.E VIZURI MAANA YA NENO KUJITAMBUA
      MAKOSA YANAYOTOKEA NI KWELI LAKINI HATA WW UMEANDIKA KWA MIHEMKO SANA

      Reply
    6. [email protected] on August 22, 2024 1:10 pm

      Of coz ujugu yupo sahihi mimi simpingi

      Reply
    7. Baxeo Africa on August 22, 2024 1:10 pm

      Siku zote mti wenye matunda hupigwa mawe .mm ninachokijua ni kwamba haya mambo ipo siku yatakaa sawa na matatizo siku zote hayaepukiki 1113.
      Naiombea dua management ya young Africa iendelee kusimama imara ili mwisho wa siku Kila kitu kitakaa sawa.

      Reply
      • Kashinje Mussa on August 23, 2024 10:50 am

        Safii sana tunaiombea pia kila kitu huwa kina mwisho na huwezi pata mafanikio bila changa moto ndogo ndogo naimani yanga African itakuwa itakuwa imala tu kwene mambo kama hayo

        Reply
    8. Valence on August 22, 2024 1:42 pm

      Huyu aliyeandika nadhani anaweza kuwa na hoja ila akatumia maneno ya kimihemuko kuiwasilisha hvyo kuonekana yeye ndo hajitambui

      Reply
    9. BigPoppa09 on August 22, 2024 2:10 pm

      Mwang umeongea fact ,,

      Reply
    10. Teacher JayJay on August 22, 2024 2:51 pm

      Hakika umeeleza ukweli mchungu, yanga tunajitbua ila njaa ndugu yangu ndio tatizo kubwa…..

      Reply
      • Teacher JayJay on August 22, 2024 2:53 pm

        Tunatbua=tunajitambua

        Reply
    11. Rweyemamu on August 22, 2024 3:21 pm

      Upo sahihi brother lkn unapokosoa tumia lugha nzuri iyo ya hatujitambui siyo nzuri, mimi nakubaliana na wewe kwenye kitengo cha sheria cha klabu yetu kina madhaifu sana,ngoja tujifanye hatuoni tufurahi muda wa kuteseka ukifika tutateseka.

      Reply
    12. Chris Mlangwa on August 22, 2024 4:03 pm

      Mr UJUGU HAPA upo sahihi , mathalani hata kwa kutumia neno HAWAJITAMBUI , kwa maana kwao waona ni kawaida kuwa na mfululizo wa kesi , la hasha ! walipaswa watatue mapema lakini kwakuwa zinaendelea basi nadiriki kusema HAWAJITAMBUI KABISA 📌

      Reply
    13. John on August 22, 2024 4:33 pm

      To

      Reply
    14. Mzava 255 on August 22, 2024 6:33 pm

      Ivi ni akili yako?fikiria kwanza kabla ya kuongelea makabila ya wa2

      Reply
    15. Livan James on August 22, 2024 8:44 pm

      Yan unachoongea hakijawahi kuepukika kwa Tim yoyote ile hapa dunian kila club huwa na matatizo ya kiusajili lakin kwa ulivyo iongelea yanga naona kabisa yanga inakuumiza kichwa kwa makali yake

      Reply
    16. Mackmillan on August 24, 2024 8:43 pm

      Dhuu sindano ya moto hii😢😢

      Reply
    17. Pingback: Takwimu Na Rekodi Za CBE SA Wapinzani Wa Yanga Ligi Ya Mabingwa Afrika

    18. Willy on August 29, 2024 9:01 pm

      Kama wewe unajitambua kawe mtu wa sheria wa yanga ila naona wew ndo hujitambui na hujui sheria kila tu ana haki ya kushitaki na kushitakiwa ,? Na pia inaonesha dhahiliii hujui kama iyo timu yako ambayo hujaitaja jina kam na yenyewe huwa inashitakiwa vile vile #JITAMBUE NDO USEME

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.