Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mkude Ni Darasa Zuri Kwa Wachezaji Wetu Bongo?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mkude Ni Darasa Zuri Kwa Wachezaji Wetu Bongo?

    MhaririBy MhaririJune 3, 2024Updated:June 3, 20247 Comments2 Mins Read542 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mkude
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Wachezaji wengi walipaswa kumchukua MKUDE kisha kulifanya darasa huru huyu kwani ni mchezaji wa pekee sana na sijawahi kuwaona wachezaji wa namna hii kwa kipindi kidogo, mwamba alisaini mwaka mmoja Yanga SC kutokea Simba SC.

    Nungunungu kama wanavyomuita alikubali mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Yanga SC wala kwake halikuwa jambo gumu hata kidogo, Jonas Mkude anasaini vipi mkataba wa mwaka mmoja huku akiwa ametokea kwenye timu ambayo status yake kubwa kama hii ya Yanga?

    Maisha ya Mkude ndani ya Yanga ni ya kuvutia sana, kama ikitokea kocha amempa nafasi ya kucheza ni sawa na isipotokea ni sawa pia kwake kwasababu hakuna maneno. Kukaa benchi kwa mchezaji mkubwa kama yeye siyo jambo dogo lakini amechagua kukubali matokoe na hivi ndivyo mchezaji unapaswa kufanya.

    Ondoka yake Simba SC inaweza kuwa rahisi kurudi kwani hakuna KERO wala chuki ameipandikiza, hajawahi kuwakera watu wa Msimbazi kwa namna yoyote ile, ni ukimyaa na upole tu. Leo ukitaja Legend wa Simba SC huwezi kuliacha jina la Jonas Gerald Mkude Nungunungu, huu ni ukweli ambao upo wazi kabisa.

    Ni muda sahihii kwa wachezaji wengine kujifunza namna ya kuzihama timu zao, ukiondoka kwenda sehemu nyingine basi unachagua NIDHAMU siyo majigambo kwani hiyo haitakujenga hata kidogo bali itakuharibia sifa yako maishani mwako. Mkude ni kioo kwa wanaomtazama.

    Bila shaka yoyote sitoshangaa kusikia akiongezewa mkataba mwingine ndani ya Yanga SC, nidhamu, kujituma hivyo vyote vinampa uhalali wa yeye kuendelea kuitumikia Yanga SC. Kila la kheri kaka Yanga SC ichukue iwe yako tembea nayo kaka itakufaa sana.

    SOMA ZAIDI: Wachambuzi Wanamuingiza Feitoto Kwenye Chuki

    Azam crdb bank federation cup final yanga vs azam

    7 Comments

    1. Bplm1664 on June 3, 2024 12:05 pm

      Ni kweli mtupu haina kupingwaaaa

      Reply
    2. Seif Haruna on June 3, 2024 12:12 pm

      Bwana Bwana Bwana Bwana ଆପଣାଆପଣା

      Huyo ndiye mtu pekee anayejua thamani yake na utu wake na sio kujidhalilisha na kuwadhalilisha wengine kwa kujivuna

      Reply
    3. Traveller17 on June 3, 2024 12:43 pm

      Ngoja nimtumie Link ya kijiweni yule mtoto wa michenzani kizmkazi unguja kwa machupa aje asome darasa huru 🤢

      Reply
    4. Tina on June 3, 2024 2:39 pm

      Ukimya ni silaha

      Reply
    5. Elcanblackboy on June 3, 2024 8:03 pm

      Alijua kutafuta jinsi ya kuvaa medali

      Reply
    6. Bintii kimmy on June 4, 2024 8:43 am

      💪💪🤗

      Reply
    7. Michael on June 29, 2024 11:40 pm

      Kabisa ukiskia mchezaji anaueshem mpira ndo vitu anavyo onyesha mukude ni vyema wachezaji wenzake kujifunza

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.