Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI – 10
    Hadithi

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI – 10

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 7, 2024Updated:May 7, 202462 Comments6 Mins Read8K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia ” Dakika saba pekee zilitosha kwa Marcus kupata mahali pa kuanza Uchunguzi wake, walitolewa vijana hao wakiwa wamevimba sehemu mbalimbali za Miili yao.”

    Tuendelee Sasa 

    SEHEMU YA KUMI 


    Wiki mbili baada kifo cha Mzee Yusuf.

    Adela alikua ameketi chumbani kwake huku mkononi akiwa ameshikilia kadi moja, aliikumbuka kadi hiyo alipewa na Babu Yake Marehemu Bilionea Yusuf. Kadi ilikua na Namba na Jina lililoandikwa Susan Mbeno.

    Aliitafakari kadi hiyo, Mungu aliweka akili ya kiutu uzima kwa Binti huyu wa Kitajiri. Kipawa cha kufikiri kilikua juu sana tofauti na umri wake, aliitazama kwa zaidi ya dakika sita huku akitafakari ni kwanini Babu yake alimpatia kadi hiyo, moyo ulimdunda.

    Akaielekea simu ya Mezani na kuipiga namba hiyo akiamini Babu yake alihitaji yeye azungumze na huyo Susan Mbeno, akiwa anasubiria simu ipokelewe alikua akitetemeka huku akijawa na woga wa ajabu sana, kabla hata haijapokelewa aliikata.

     Akaketi kitandani akiwa analia huku akisema

    “Sitaki, sitaki, staki” sauti hii ilipenya kwenye masikio ya Bi Choro aliyekua akipiga deki sakafu kando ya chumba cha Adela, ikampeleka hadi chumbani humo na kumkuta akiwa analia. 

    “Adela unalia nini?” alihoji Bi Choro kwa upole sana

    “Bibi sitaki kusema, sitaki Mimi” alisema Adela akimkumbatia Bi Choro

    “Hutaki kusema nini?”

    “Bibi sitaki Mimi” alisema akiwa analia, Bi Choro alijitahidi sana kumhoji Adela lakini hakusema kingine zaidi ya kudondosha chozi.

    “Basi pumzika Adela, usiwe na hofu, usiogope. Mlinzi yupo, Mimi nipo hakuna mwingine 

    atakayekuja, upo salama sawa?” alisema Bi Choro, aliamini kifo cha Mzee Yusuf ndiyo sababu ya Binti huyo kulia kwani kipindi hicho alikua akisakamwa sana na wapelelezi.

     

     Baadaye Adela akapitiwa na Usingizi, Bi Choro akamlaza vizuri kisha akatoka.

    ***

    “Mapigo yake ya moyo yanazidi kushuka, jitihada zifanyike haraka” ilikua ni sauti ya Dokta 

    akiwaelekeza Madaktari na Manesi ambao walikua ndani ya chumba kimoja alicholazwa Adela, 

    mitambo ilionesha kushuka sana kwa mapigo yake hali iliyoonesha wazi kuwa angefariki muda 

    mchache Ujao. Alikua akishindwa kuhema, macho yalimtoka pima. 

    “Mwanangu Mimi, Adelaaaa” Sofia alikua akimlilia Binti yake, walikesha hapo kwa usiku mzima na nusu ya siku mpya, Hamza hakumwacha Dada yake.

     Akamweleza kua Madaktari wanafanya jitihada ili kuokoa Maisha ya Binti huyo lakini hiyo haikutosha kumtuliza, alilia mfululizo.

    Jioni saa 10:12 Daktari aliandika muda ambao Mtoto Adela alifariki Dunia, taarifa iliyomfanya Sofia apoteze fahamu zaidi ya mara tano. Kifo cha Binti huyo kiliandikwa na Daktari aliyekua akimtibia kua alifariki kwa mshituko wa moyo uliotokana na njozi aliyokua ameiyota Binti huyo, sisi tunaifahamu ndoto ya Binti huyo lakini taarifa ya kifo hicho kiliwashangaza walio wengi.

    Maneno ya chini chini yakawa mengi, familia hiyo ikatajwa na walioifahamu kuwa inaandamwa na mzimu wa kifo, wengine wakihusisha vifo hivyo na imani za Freemason lakini kwa mpelelezi Daudi Mbaga aliyeko Kigoma aliuona urejeo wa Muuwaji ndani ya familia hiyo, saa 12:00 kengele ya Kanisa la Roma ilipokua ikigonga, Daudi Mbaga alimpigia tena simu Jasusi Marcus aliyekua kituo cha Polisi walipohifadhiwa wale Wanachuo.

    “Nitazungumza nao baadae, warudishe Mahabusu” aliagiza Marcus huku simu ya Daudi Mbaga 

    ikiwa hewani, akakimbilia nje sehemu ambayo aliamini ni salama zaidi kuipokea

    “Nasikiliza” alisema Marcus

    “Binti Adela amefariki, mwili upo St. Augustino Hospital Kinondoni, wahi ukauchunguze Marcus” 

    Ilikua ni taarifa iliyomshtua Marcus, Adela alikua ni miongoni mwa Watu walio katika listi yake ya upelelezi ikiaminika kuwa ndiye aliyemuona Muuwaji kwa mujibu wa ripoti ya Daudi Mbaga.

    “Yule Binti amefariki?”

    “Ndiyo, nasikia kifo chake kimetokana na ndoto aliyoiota, hii haiwezekani Marcus, lipo jambo nyuma yake” 

    “Sawa, natoka hewani” alisema Marcus kisha alikata simu. Alichezesha kope za macho yake huku akiwa amejawa na Mshangao, watasemaje amefariki kutokana na ndoto tu? Hata yeye akatia walakini kua Muuwaji amerudi tena, hii ikaongeza joto zaidi la kuamini Sakina hakua Muuwaji halisi.

    Saa moja mbele, Marcus anafika Hospitali Kinondoni alipoelekezwa na Daudi Mbaga. Hakuwapigia simu wafiwa, alifika na kuuliza Mapokezi, kwanza alijitambulisha kua ni Askari polisi kisha alisema

    “Nimekuja kumtazama Mgonjwa anaitwa Adela kutoka katika familia ya Bilionea Yusuf” alisema, kwa heshima ya kazi yake, Binti aliye mapokezi akachota taarifa haraka kwenye kompyuta ili kujua kama walikua na Mgonjwa anayeitwa Adela kutokea kwenye familia ya kitajiri. 

    “Samahani, ameshafariki”

    “Mwili wake uko wapi?”

    “Mochwari daraja la kwanza”

    “Ahsante” akasema Jasusi Marcus, Yule Mdada akamuelekeza mahali ilipo Mochwari daraja la 

    kwanza ambalo Miili ya watu matajiri iliwekwa huko tena ilikua michache mno. Akaishika korido aliyoelekezwa, akiwa amebakisha hatua kadhaa kufika alipishana na Daktari Mmoja, akamsimamisha.

    Lengo la Marcus lilikua ni kumsalimia kisha amuulize kama Mochwari kuna waangalizi wa maiti, Daktari huyo alionekana kuwa mwenye hofu sana, mkononi alikua na Bahasha ya kaki iliyotuna.

    “Samahani, Naitwa Marcus ni afisa wa polisi. Nauliza kama muda huu kuna waangalizi wa maiti” alisema Marcus, yule Daktari wa kiume akawa anababaika kumjibu Marcus akionekana kujawa na woga fulani ndani yake hadi Marcus alishangaa, mara ile bahasha ilianguka na bunda moja la pesa likatoka, haraka yule Daktari akaliokota na kulirudisha kwenye Bahasha akioneka kuwa na hofu sana kisha akaondoka bila kumpa jibu la Uhakika.

    “Daktari anapata wapi bunda la pesa tena akiwa sehemu ya kazi?” alijiuliza Marcus kabla ya 

    kupuuzia, mawazo na akili yake yakawa kuelekea Mochwari. 

    Akafika mbele ya Mlango wa Mochwari, aliona mlango ulikua na upenyo fulani wa wazi ambao 

    ulionesha ndani, ilionekana aliyeingia au kutoka aliacha Mlango wazi, wakati analitafakari hilo 

    alimwona Mtu aliyefunika sura kwa kutumia kofia ya koti jeusi akiwa ana randa randa Mochwari 

    tena hakuonekana kabisa kuwa Daktari. 

    Mavazi pekee yalimfanya Marcus achomoe Bastola yake kisha taratibu akaufungua mlango huo 

    ambao ulionekana kumpa taarifa Mtu aliye ndani ya chumba hicho, naye akaganda huku akiwa 

    ameshikilia jokofu moja la kuhifadhia Maiti. 

    “Wewe ni Nani?” aliuliza Marcus, lakini Mtu huyo alionesha wazi kua ni Mwoga. Alikua akitetemeka, alikua amempa mgongo Marcus aliye mita kadhaa.

    “Nakuuliza tena, wewe ni Nani?” akahoji Marcus huku akiwa amenyoosha vizuri Bastola yake, kama alivyoambiwa na Daudi Mbaga naye hisia zake akazihamishia hivyo hivyo kua kifo cha Mtoto Adela si kifo cha Mshituko kama ambavyo ripoti ya Daktari ilisema, alihisi uwepo wa mambo yasiyo ya kawaida.

    “Geuka taratibu mikono ikiwa juu” akapaza sauti Marcus huku akiamini moja kwa moja kua huyo Mtu si Mzuri ndiyo maana alikua akipekua kwenye Majokofu hayo. Mtu huyo akageuka huku kichwa akiwa amekiinamishia chini, Marcus akamtaka ainue kichwa chake.

    Taratibu akainua kichwa akiwa anatetemeka, Marcus hakuyaamini macho yake. Mtu huyo alikua nani? ZIKIFIKA COMMENTS 100 naahia sehemu ya 11

     

    Jiunge WhatsApp Channel Ya KIJIWENI Ili Kuwa Wa Kwanza Kupata Updates Za RIWAYA Hii Kwa Kubonyeza Hapa 

    SOMA Uchambuzi Na Makala Mbalimbali Kwa Kubonyeza Hapa

     



     

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.