Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Pale Simba Shida Sio Mangungu Ni Wachezaji Hawa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Pale Simba Shida Sio Mangungu Ni Wachezaji Hawa

    Oscar EvodiusBy Oscar EvodiusApril 24, 2024Updated:April 24, 202415 Comments2 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mwenyekiti wa mashabiki wa Simba anayehusika n wachezaji pia
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    August 3 Mwaka 2018 Young Africans iliachana na jumla ya wachezaji 14 kisha wakabaki na majina ya wachezaji wasiozidi 17 ndani ya kikosi chao ambao, katika orodha ile ya wachezaji walioachwa kulikuwa na majina kama David Molinga, Mrisho Ngasa, Jaffary Mohamed, Tariq Seif, Andrew Vicent, Papy Kabamba Tshishimbi na Mohamed Issa ambao mikataba yao ilimalizika na hawakuongezewa

    Kipindi hiko Young Africans ilisitisha mikataba yao ni Raphel Daud, Yikpe Gislain, Ali Ali, Patrick Sibomana, Muharami Issa, Ally Mtoni Sonso(Marehemu) na Eric Kabamba! Hapo katika idadi ile ya wachezaji 17 waliobaki ni wanne tu ndio walikuwa Raia wa Kigeni ambao ni Haruma Niyonzima, Farouk Shikalo, Lamine Moro na Bernard Morrison

    Baada ya hapo Timu ilicheza misimu mitatu(2018/19, 2019/20 na 2020/21) bila Ubingwa wa Ligi Kuu, walikubali kufanya mabadiliko na hata hiyo Miaka mitatu bila Ubingwa bado waliishi kwenye nafasi mbaya na walifanya mabadiliko ya wachezaji wengi sana ndani ya kikosi

    Walicheza ‘Four Seasons’ bila Ubingwa wa Ligi Kuu na waliamua kufanya kitu cha tofauti baada ya kufeli! Kwanza kurudisha mashabiki karibu na Timu yao, kufanya uchaguzi wa Viongozi ambao wana maono ya kupeleka chapa ya klabu yao mbali zaidi na kufanya Usajili wa wachezaji Bora tofauti na walioondoka! Timu ikarudi kwenye mstari mpaka sasa inafanya vizuri

    Simply! Mantiki yangu ni kwamba kwa sasa SIMBA SC wanatakiwa kufanya maamuzi ya haraka hasa ndani ya uwanja, Timu inahitaji kubadili eneo kubwa sana la wachezaji waliopo ambao tayari wameipa Timu nyakati zao bora! Simba inahitaji ‘Quality Players’ wengi ambao wataiaogeza chapa ya MNYAMAA zaidi ya hapo ilipo

    Kwakuwa eneo kubwa la wachezaji inaonekana linatakiwa kupungua pale basi wakati ndio huu! Wachezaji wengi ambao wameingia ndani ya Klabu wamefeli kati ya 100%, naona wamefeli 70% na wamefaulu 30% wamefaulu

    Simba SC iwapo watafeli tena kwenye eneo la Usajili basi hizi nyakati zitaendelea kuishi kwao, Abdelhack Benchikha anahitaji sura mpya ili kurudisha ubora wa Timu na kusukuma ‘Vision & Mission’ ya Klabu hasa kwenye CAF Tournaments! That is Truth about LUNYASI

    SOMA ZAIDI: Waraka Mzito Wa Hamisi Kigwangalla Kuhusu “Kuinunua Simba”

    ligi kuu MUUNGANO CUP Simba

    15 Comments

    1. Michael on April 24, 2024 10:27 am

      Hakika umenrna vyema simba tatizo kubwa lipo uwanjani na sio viongozi hapa naweza kukubaliana na wewe

      Reply
    2. Lenn boe on April 24, 2024 10:31 am

      Hakika mnayoxema ni ya kweli…🤔🤔

      Reply
    3. Sarya Flavian on April 24, 2024 10:31 am

      Yawezekana tusingekuwa kwenye hii hali bila kuuza wale strikers wawili alf ni Dirisha dogo me nafikr uongozi unahusika na huu mwenendo wa timu

      Reply
    4. Mac Allister on April 24, 2024 10:34 am

      Huwezi kuwa na nyumba bora wakati msingi ni mbovu….tatizo linaanzia chini kwa viongozi

      Reply
    5. NAUSHAD on April 24, 2024 10:36 am

      Kwani hao wachezaji wameletwa na nani si akili ya mangungu

      Reply
    6. Legrandez on April 24, 2024 10:36 am

      Ukweli unauma🍃 Kwasababu haiwezekani Team inacheza michezo yote na bado wachezaji wote hawajafikia mabao ya mchezaji alieondoka..hiyo ni kumaanisha kuna upungufu mkubwa wa Quality Players

      Reply
    7. Said on April 24, 2024 10:36 am

      Yes mnyama apunguzee zaidi wazee katika timu ili vijana wapate nafasi kunawatu umri umeendaa inabidi wawache vijanaa na kuongeza sula mpya Runyasi👍👍👍👊🏻

      Reply
    8. Lenn boe on April 24, 2024 10:40 am

      Tatizo lipo kwa viongozi..kuna baadhi ya viongozi wanamilik wachezaji …☝☝

      By Mr..Reporter..

      Reply
    9. Kidullahson HL on April 24, 2024 11:05 am

      Upo sahihi 👊🏻
      Ila mimi kwa mtazamo wangu, viongozi ndio wenye wajibu wa kuleta quality players, wanaofeli sio kwamba hawajitumi ila uwezo wao ndio umeishia hapo, kuna usemi unasema ‘you cannot offer what you don’t have’ so Mangungu na viongozi wenzake Wakatakiwa kuwajibika kwa kuwa kwa misimu yote mitatu wameleta wachezaji wasioendana Na vision za club yq simba sc. Kama hawawezi kuleta wachezaji wanaoweza kuendanq na Maono ya club that’s absurd na wanatakiwa kuwajibika haswaaa 😞😞

      Reply
    10. Mr. Jackoeh on April 24, 2024 11:54 am

      Ukweli ni kwamba …

      Kama wachezaji ni wa low quality na hawawezi kubeba maono ya club imekuaje wakasajiliwa na kuwa part ya club…??
      Kwa tasfiri nyingine na kwa harak harak tu itabidi ufikilie ni wakinanani waliohusika na mchakato mzima huo adi club yetu pendwa kufikia apo ……
      Hapo ndipo itabidi tushughulike na mizizi ya tatzo ilo kabla ya kuchukia matunda yke ndipo tutakapo geukia kwa viongozi na kamati yao kuhusu wachezaji ni swala la mwisho baada ya kushughulikia utendaji wa viongozi ..

      Reply
    11. RUGENGA on April 24, 2024 12:05 pm

      Kwangu Mimi sioni kama wachezaji ndio wanashida🤔 shida Iko kwenye management nzima ya Simba na UKISIKIA kitu management inaanzia juu kuja chini kwahyo huwezi kulahumu wachezaji kuwa ndio wanafelisha timu ya Simba hapana management ndio Ina wajibu wakukaa na kujua tatzo ni Nini ukilahumu wachezaji kwani hawaingii wa uwanjani na je wakiingia hawachezi….mfano mechi ya Yanga Africans na Simba juzi wachezaji walifanya vizuri sana lakini shida ni kwamba management ya Simba inashindwa kuhafikiana hili ikaleta mabadiliko ndani ya timu na kuludi katika mstari

      Reply
    12. Valence on April 24, 2024 12:25 pm

      Mh, mnadhani hii timu mbona imefanya vzuri hadi sasa,, kwani iko nafasi ya ngapi? Au kwakuwa imefungwa na Yanga nje ndani?

      Utafika wakati wao he he he

      Reply
    13. Miraj on April 24, 2024 12:44 pm

      Uongoz wa simba ndo tatizo umesajil wachezaj wa ajabu na wamafungu ,,yanga kipind kile haikua na hela je simba ya sasa haina hela

      Reply
    14. Pingback: Uchambuzi Wa Mechi JKT Tanzania vs Yanga Lawama Uwanja? - Kijiweni

    15. Pingback: Mchezaji Gani Wa Nje Hapa Ligi Kuu Amekuwa Bora Zaidi Kwako? - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.