Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Naamini Kuwa Mchawi wa Simba ni Wanasimba Wenyewe
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Naamini Kuwa Mchawi wa Simba ni Wanasimba Wenyewe

    MhaririBy MhaririApril 12, 2024Updated:April 12, 20246 Comments2 Mins Read604 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mashabiki wa klabu ya Simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Utulivu ndani ya klabu ni timu kutwaa mataji kama hilo likikosekana lazima mchafuko utokee tu na ndio hicho ambacho kinawatafuna klabu ya Simba kwa sasa. Mo Dewji anatolewa Mbuzi wa kafara eti hatoi pesa tena siyo sehemu ya kuhudumia timu lakini maswali ni machache tu, mbona Viongozi walinyamaza kimyaa walisubiri mambo yatokee vibayaa waanze kuvujisha Siri za namna hiyo. Hii imetoka ndani humo hakuna mwingine wakutambua kama tajiri hatoi hizo huduma.

    Huu siyo muda wakuyaanza haya mambo siyo nyakati nzuri za kupopoana wenyewe kwa wenyewe, timu ikishinda mshinde wote na ikipoteza mmpoteze wote baadae Viongozi mnaketi na kujitafakari upya.

    Hakuna unafki mbaya kama hapa sasa watu wanatoka pembeni na kuanza kusengenya atasemwa yule na kusemwa huyu Sasa kwanini msiseme ukweli kuwa usajli ndio ulioidondosha timu, si lilikuja dirisha dogo je kipi kilifanyika cha maana zaidi ya kuleta wachezaji ambao nao walihitajika kuvumiliwa.

    Kwa Simba SC ilipofika ilihitaji wachezaji wa kuvamiliwa? Tena ambalo liliwashangaza wengi ni kuwaacha wachezaji ambao wangeendelea kuisaidia timu na wakaletwa wachezaji ambao msaada wao haujakidhi mahitaji ya timu.

    Lazima tukubali hapa ni sahihii sana kuwa wavumilivu msimu umalizike na kurudi kwenye uwanja wa usajli kucheki mapungufu ni yapi na kuyafanyia kazi hii itasaidia sana kuliko hili la kuanza kumtafuta mchawi kwangu hakuna afya.

    Ukweli mtupu wachezaji wengi waliopo Simba SC umri umeshawatupa mkono na wengine wametumika miili imechoka kwaiyo wanashindwa kutoa kitu kipya. Mfano mdogo Saido Ntibanzokiza yule unataka akupe kipi zaidi, mchezaji ameshamaliza saizi ni Kama anajisukuma tu sasa unahitaji uchawi au Elimu ya Chuo kuliona hili.

    Mimi nimemaliza, Mchawi wa Simba ni Wanasimba wenyewe.

    Unaweza kutuma andiko au chapisho lako ili lisomwe hapa KIJIWENI kupitia [email protected]

    SOMA ZAIDI: Mashabiki SIMBA Wanahitaji Mabadiliko Makubwa Sio Propaganda

    habari za simba mo dewji simba

    6 Comments

    1. Yohana on April 12, 2024 9:11 am

      Simba saiv ni kama uyoga leo mboga kesho sumu

      Reply
    2. Imani on April 12, 2024 9:12 am

      Kweli mchawi wao wao wenyewe

      Reply
    3. Baxeo Africa on April 12, 2024 9:34 am

      Wajifunze kutoka kwa uongozi wa yanga,viongozi ambao wana jitoa kwa AJILI ya team na wanajenga uzalendo na hisia za uzalendo kwa wachezaji wao wote

      Reply
    4. Oberd banyikwa on April 12, 2024 9:58 am

      Simba viongozi wana njaa

      Reply
    5. Zeyy Tabasamu✨🥰 on April 12, 2024 10:00 am

      Nikweli kbsa🙌Usajili haukulipa hatuna wachezaji Hatuna Timu 🥺Wasianze kuchafuana ila hata Uongozi nao Mbovu sababu wao ndo wanaotulea Onana Na Yule Mtoto mwenye Kwashakooo jobe 💔Pesa zinatoka wananufaisha mitumbo yao

      Reply
    6. Jankcmaphoto on April 12, 2024 12:26 pm

      Mtuachie My wetu

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.