Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Pacome Na Aucho Ni Pasua Kichwa Dhidi Ya Mamelodi?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Pacome Na Aucho Ni Pasua Kichwa Dhidi Ya Mamelodi?

    MhaririBy MhaririMarch 18, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pacome
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Moja ya kitu ambacho wana Yanga wengi hawaombei ni majeraha ya kiungo Pacome Zouzoua, na kupona haraka kwa Khalid Aucho na kama ikitokea hawatorejea mapema basi wataenda kutia ugumu kwenye mchezo dhidi ya Mamelodi Sundowns. Sitaki kusema Yanga SC wanakikosi finyu hapana ila katika ushindi wa Yanga kwenye michuano ya kimataifa basi Pacome na Khalid Aucho wana mchango mkubwa zaidi.

    Naamini kama ungekutana na kocha Miguel Gamondi na ukamuuliza ni kitu gani ulikuwa ukihitaji Kwa sasa?Nadhani kubwa atakalokuambia ni kupona kwa wachezaji wake ambao ni majeruhi mnaona namna wachezaji wa Yanga SC wanavyocheza Kwa tahadhari kubwa wakikwepa majeraha lakini wachezaji wa Azam wao wanaamini hawana cha kupoteza.

    Kabla ya kwenda kuwalaumu waamuzi wetu na sisi turejee nyuma kwenye zile ajenda mfu kwani hampaswi kusahau haraka namna hiyo.

    Kabla ya huu mchezo mtakumbuka vizuri propaganda zilivyotembea kuwa Yanga wakishinda dhidi ya Azam FC unakuwa siyo ushindi wa kweli. Yaani kama kuna namna ambayo inafanyika ili Yanga ishinde.

    Sasa katika mazingira ya kawaida kama mwanadamu unafikiri utafanya kitu gani kama siyo kuingia kwenye mchezo na presha kubwa watasema yule Heri Sasii ni Yanga kabisa au Simba wakutupwa na ikitokea hivyo refalii anaingia uwanjani na anashindwa kutekeleza majukumu yake.

    Ukweli ni kwamba mpira wetu unachezwa sana Instagram zaidi kuliko sehemu nyingine ile, yaani kalamu zinatumika zaidi na tunaacha kuufanya mpira uchezwe.

    Leo mashabiki wa Yanga wanatoka mbele na kuanza kumlaumu Kocha wao Miguel Gamondi amekosea kupanga kikosi chake lakini wanasahau namna ratiba ilivyo ngumu mbele yake, siku 17 mechi 5 wewe kuwezaaaa. Nakuuliza wewe ungeweza wapi.

    Sawa wanasema ratiba imepangwa lazima wachezaji wacheze lakini na wao ni binadamu na wakati mwili nao unachoka na majeraha ya hapa na pale. Tatizo hapa kwetu kama wewe siyo Yanga SC basi Simba SC Mnyama. Ukweli unafichwa na unafki unatembea.

    SOMA ZAIDI: GUEDE Amemponza GAMONDI Kwenye Mfumo Wa Azam Na Sababu Kubwa 

    azam vs yanga magoli yote yanga dhidi ya azam
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.