Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Ya Wazi Kwako Dickson Job “Big Brain Defender”
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Ya Wazi Kwako Dickson Job “Big Brain Defender”

    MhaririBy MhaririMarch 14, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Barua kwako Dickson Job
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kamanda

    Bila shaka uko poa kabisa na unaendelea na maandalizi yako ya upambanaji hapo kwa Watoto wa mitaa ya Twiga na Jangwani yalipo makao makuu ya klabu ya Wananchi Yanga. Hii ni barua ya wazi kwako niliyoona nikuandikie baada ya kuona haya mengi yanayoendelea mitandaoni.

    Nikiri wazi kuwa kwa kiwango cha beki wa kati kwa sasa, kama sio Ibrahim Bacca basi ni wewe kamanda Dickson Job kwa wachezaji wazawa na nisema kuwa ndio nakubali yupo Bakari Mwamnyeto lakini ni kama kiwango chake kimeshuka kiasi au amekosa kujiamini kuliko wewe.

    Baada ya kuona kikosi cha Kocha wa Taifa Stars Hemedi Suleiman Morocco kama mwanamichezo nimeshtuka kuona jina lako halipo hapo yaani katika orodha ya wachezaji 23 watakaosafiri na Taifa Stars kwenda Azerbaijan jina lako Dickson Job halipo?

    Imenipa maswali mengi haswa kutokana na kiwango chako ambacho unacho kwa sasa katika kikosi cha wananchi lakini naomba kukuuliza swali, hivi hizi tuhuma ni za kweli? Na kama ni kweli kwanini uliamua kufanya hivyo?

    Binafsi mimi ni mtu wa mwisho kuamini kuwa ulikataa kucheza beki namba 2 jambo ambalo linaonekna kuwa ulidharau maamuzi ya kocha na kubwa zaidi wapo ambao wanasema kuwa umekosa uzalendo na taifa lako wewe unajiskiaje kwa sasa?

    Kamanda, kama ni kweli basi tambua kuwa umeninyong’onyesha sana kwa kitendo hiki kwani hakika ile ilikua mechi yetu muhimu sana kwa Taifa. Kama si kweli basi tuendelee kuwapigia kelelee watu ambao wamekuwa wakifanya machaguo ya wachezaji wawe wanaangalia umuhimu na uhitaji kwenye kikosi cha Taifa Star siyo tu kuita wachezaji kwasababu una maslahi nao.

    SOMA ZAIDI: Tuendelee Kuuamini Ukuta Wa Yerikho Simba SC?

     

    dickson job job taifa stars
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.