Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ni Wakati Wake Sishangai Haya Mapambio Kumhusu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Ni Wakati Wake Sishangai Haya Mapambio Kumhusu

    MhaririBy MhaririMarch 9, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wakati wa Pacome
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni wakati wake tukumbushane jambo katika haya maisha kuna kitu kinaitwa wakati yaani time yako imefika na wengine muda wao hupita, hapa hua tunachanganya sana na kushindwa kutofautisha zama na nyakati. watakuita chawa, potelea mbali.

    Tuseme ukweli kwasasa katika ligi yetu tumeletewa mwenye wakati wake kiungo fundi na mwenye kujua mpira tena kwenye viwango vya juu sana. tusibishane tulete fact. facts zangu ni namna Pacome Zouazoua alivyotuonyesha kwa vitendo namna ya kucheza na kushinda mechi.

    Hesabu 23:23 inasema “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, wala hapana uganga juu ya Israeli. sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, ni mambo gani aliyokutendea mungu!” kucheza ligi kuu ya Ivory Coast kisha kuwa MVP siyo kitu rahisi, mwamba alipokuwa akiitumikia Asec Mimosas aliivusha timu na kwenda nusu fainali ligi ya mabingwa Afrika sasa unaweza kutumia lugha rahisi alipotoka alifanikiwa sana na timu yake hiyo ya Asec Mimosas na hapa Yanga sc napo anatuonyesha pia uwezo na ubora wake.

    Kitendo cha Clatous Chama kushindwa kufanya kitu dhidi ya wajelajela ni ile ya kukuonyesha ni zama zimekwisha kwani ukiiondoa mechi dhidi ya Jwaneng galaxy hakuwa kwenye kiwango kile tulichokizoea lakini wanasema timu hua zinatofautiana na Tanzania Prisons wametujibu kwa vitendo.

    Zama hizi ni za viungo wengine ni Pacome Zouazoua hata kama itawatoa roho baadhi ya watu lakini ukifika ukweli tunakubali tu. Yanga sc walikuwa na Haruna Hakizimana Niyonzima zama zake zilipita likaja jina la Clatous Chota Chama.

    Ukiwatazama Simba sc waliwahi kuwa na Haruna Moshi Boban naye alipita kisha baadae alikuja marehemu Patrick Mutesa Mafisango na ni wakati wa kuwakumbusha kuwa tutunze kumbukumbu ndugu.

    SOMA ZAIDI: Sitegemei Mapya Kwa Benchikha Kama Wachezaji Ni Hawa

    pacome yanga sc

    1 Comment

    1. Pingback: Simba Wangeanza Na Huyu Anayeleta Wachezaji - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.