Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Azam na Simba Inawarahisishia Yanga Kuchukua Tena Ubingwa?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Azam na Simba Inawarahisishia Yanga Kuchukua Tena Ubingwa?

    MhaririBy MhaririMarch 7, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kwenye msimamo wa Ligi Kuu ni tofauti michezo minne kati ya Azam FC na Yanga SC, Azam wanaongoza Ligi wakiwa na jumla na alama 44 huku Yanga SC wakiwa na alama 43. Hapo Yanga ina michezo minne mbele, wapinzani wake pamoja na Simba SC ni kama wameanza kutupa mashuka kwenye huu mpambano na ikitokea wamemfunga Namungo FC unaweza kusema Yanga SC hawana mpinzani kwenye kuutetea Ubingwa wao msimu 2023/2024. Niambie, Chama asifafanishwe na mchezaji yoyote?

    Ukiwatazama Simba ni wazi kuwa kuna mambo mengi sana ambayo bila shaka huwezi kuwalaumu wachezaji zaidi sana lazima uwalaumu viongozi na ndio hapo nasema kuwa kutokana na kwamba kuna  maamuzi mengi sana ambayo lawama zote zinaangukia katika uongozi.

    Simba iliuchagua uwanja wa Jamhuri Morogoro kama uwanja wake wa nyumbani ila cha kushangaza, wachezaji wa Simba wameenda kwenye mechi dhidi ya Prisons huku wakiwa hawajafanya mazoezi kabisa katika uwanja huo. Timu kubwa itafanyaje kosa kubwa la kiufundi kama hilo?

    Baada ya kuwatesa vya kutosha mashabiki wa Dar es Salaam hadi mpaka leo wengi sana wameikatia timu tamaa, sasa uongozi umeamua kuwapelekea uchungu mashabiki wa Simba wa mikoani. Sababu ya kuukimbia Chamazi siyo ishu za kuhujumiwa kama wanavyodai, ni kwa sababu mashabiki wa Dar hawana mwamko sana na hii timu kwa sasa. Bado huko mikoani unaweza kuwaokota okota wakajaza uwanja ila sio kama zamani.

    Tukiendelea hivi, na hao wa mikoani nao watakata tamaa na hii timu na baada ya miaka 2 Simba itakuwa timu ya kawaida sana katika ligi. Huwezi kutegemea ubingwa Kama timu yako haina mwendelezo wa kupata matokeo, Leo timu inapata sare kesho inapigwa keshokutwa inashinda!

    Timu zinazocheza kibingwa zinapata matokeo hata zikiwa kwenye hali ngumu kudondosha alama ni kitu wanapambana kisitokee kwanza kuchagua uwanja wako wa nyumbani ambao hizi timu za mikoani zinakuwa na advantage kucheza kwenye viwanja Kama vile alafu unataka utoboe.

    Mwana kulitaka mwana kulipewa!

    SOMA ZAIDI: Simba Waliichukulia Poa Prisons Wameadabishwa

    ligi kuu bara msimamo wa ligi kuu

    1 Comment

    1. Pingback: Kuondoka Kwa Benchikha Tuitegemee Simba Hii Yenye Matola - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.