Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Freddy Anahitaji Msaikolojia, Ana Tatizo Hili Kubwa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Freddy Anahitaji Msaikolojia, Ana Tatizo Hili Kubwa

    MhaririBy MhaririFebruary 29, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Freddy Michael kutoka Simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ukimtazama ni wazi kuwa huwezi kukataa ya kuwa ni mchezaji ambaye ana umbo halisi la mshambualiaji na naweza kusema kuwa Freddy Michael ni usajili mzuri lakini umekutana na changamoto ya presha ya timu kubwa ya klabu ya Simba.

    Ameshindwa kuidhibiti presha iliyopo pale katika klabu ya Simba ambayo unaona kabisa ni miongoni mwa zile timu kubwa ambazo ukisajiliwa ni wazi utakua na presha kubwa sana ukiachana na presha ya mechi husika ambayo utakua umepangwa.

    Naon ani wazi kuwa presha ndicho kitu cha kwanza kinamtafuna zaidi na kushindwa kufanya vizuri, kuweka mpira wavuni na nafikiri kuwa Abdelhak Benchikha na Daktari wake wa saikolojia wakae na Freddy Michael ili kutatua tatizo lake la kutokuwa na utimamu mzuri anapokua uwanjani, kuna vitu vya kupata kutoka kwa kocha na jitihada za mchezaji kufanya vya kutosha.

    Ni mchezaji mzuri anajua kukaa kwenye nafasi nzuri uwanjani lakini pia anakua na changamoto ya umaliziaji pekee huku akiwa na njia nzuri ya kuwa na hatari zaidi kwenye mpira lakini tatizo kubwa zaidi ameshindwa kuimeza na kuidhibiti presha iliyopo pale Msimbazi, ikiwa kinyume yake maana atakuwa tegemeo.

    Kuna wachezaji wengi wazuri tu ambao baada ya kusajiliwa katika klabu hizi kubwa za Kariakoo wameonekana kutokua sawa katika viwango vyao lakini wakiondoka huwa wanakua na balaa la maana tun a uzuri mifano ya wachezaji ipo.

    Ni wakati sasa kwa mashabiki kumpa moyo zaidi wa kupambana lakini pia na benchi la ufundi kumtaftia mtaalam wa saikolojia ili aweze kumweka sawa kupambana na maisha ya kitanzania ili aweze kuanya vyema katika klabu yake ya Simba.

    SOMA ZAIDI: Tunamkosea Heshima GSM Tuuzungumze Ukweli Tu

     

    freddy simba

    1 Comment

    1. Pingback: Barua Hii Ikufikie Barbara Gonzalenz - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.