Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Awesu Tushakujua Wewe Ni “Mchawi” Wa Soka
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Awesu Tushakujua Wewe Ni “Mchawi” Wa Soka

    MhaririBy MhaririFebruary 18, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Awesu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Achilia mbali umbo lake alilonalo na angalia namba ya jezi yake mgongoni kisha soma jina lake vizuri, anaitwa Awesu Awesu, fundi mmoja wa mpira kusema ukweli tu hazungumzwi sana hapa nyumbani lakini  kijana anaujua sana huyu. Katika mechi nyingi ambazo amekua akicheza mtazame kwa umakini kabisa utaelewa kile ambacho ninakuambia hapa.

    Nitaukumbuka msimu ule ambao  kiungo huyu alitakiwa na klabu ya Yanga akaona hatatoboa ambapo aliamua kuitupilia  mbali ofa ile na yeye kutimkia kwa matajiri wa Chamazi, Azam FC na baadae kutolewa kwa mkopo KMC FC akitokea hapo Azam, miguu yake inashawishi kiukweli anajua kuwakunisha vichwa maboss huyu ingawa sijui lakini kama ataendelea kubaki alipo sasa.

    Anavyocheza katika dimba la kati ni wazi unahitaji kuwa na viungo wenye jicho la mapema kugundua jinsi ya kumzuia kwani anaonesha balaa lake alilonalo na jinsi anavyouonesha uchawi wake katika kukaba na kutoa pasi muhimu wakati wa kushambulia.

    Awesu ni miongoni mwa wale wachezaji wa Ligi Kuu Tanzania wanaotuonesha umuhimu wa kutumia juhudi zao binafsi kama chachu ya kufikia ufanisi. Kujituma kwa kufanya mazoezi kwa bidii, kushiriki kikamilifu katika mechi, na kujitolea kwenye mafunzo kunaweza kuwa njia muhimu ya kuboresha uwezo wao na kufikia viwango vya juu vya mpira wa miguu.

    Kwa ujumla mafanikio ya wachezaji wa Ligi Kuu yanaleta heshima kwa taifa kwani wanapofanya vizuri kimataifa au wanapochaguliwa kuwakilisha timu ya taifa, wanachangia katika kujenga taswira chanya ya mpira wa miguu nchini. Hii inaweza kuwahamasisha wachezaji wengine na kuwaleta pamoja Watanzania kusherehekea mafanikio yao.

    Kwa kuhitimisha, kujituma kwa wachezaji kama anavyofanya Awesu ni muhimu sana katika kufikia mafanikio makubwa. Ni jukumu letu kama jamii kuwapongeza na kuwatia moyo, kutoa sifa njema wanazostahili, na kujenga mazingira yanayowawezesha kufikia uwezo wao kamili. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kushuhudia maendeleo makubwa katika soka la Tanzania na kufurahia mafanikio ya wachezaji wetu.

    SOMA ZAIDI: Guede Amebeba Mzigo Mgumu Usioonekana Kikawaida

     

    awesu kmc

    1 Comment

    1. Pingback: Kiburi Cha Chama Kinalindwa Na Mashabiki Wa Simba - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.