Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kuhusu Uwanja Yanga Fanyeni Kweli Acheni Siasa Za Mpira
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kuhusu Uwanja Yanga Fanyeni Kweli Acheni Siasa Za Mpira

    MhaririBy MhaririFebruary 13, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Uwanja wa Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni wazi kuwa klabu ya Yanga imetimiza miaka 89 tangu kuanzishwa kwake ikiwa ni moja kati ya klabu kongwe nchini Tanzania ambayo makazi yake ni mitaa ya Jangwani zilipo ofisi za kiutendaji za klabu hii.

    Ukiachilia mbali kuwa na jengo ambalo limemebeba historia kubwa ya klabu hiyo lakini pia kuna uwanja wao unaoitwa uwanja wa Kaunda ambao umekua ukikumbwa na changamoto ya mafuriko mara kadhaa kunapokua kunatokea mafuriko na jitihada mbalimbali zikafanyika kuweka vifusi ili kuwe juu na kwa hilo wakafanikiwa.

    Naweza kusema moja kati ya kilio kikubwa cha mashabiki na wanachama wat imu hii kubwa ni kuhusiana na uwepo wa uwanja wao ambao wao wanatamani ujengwe palepale Jangwani zilipo karibu na ofisi za timu hiyo na sio mara moja kusikia viongozi mbalimbali wa klabu ya yanga wakizungumza kuhusiana kujengwa kwa uwanja huu.

    Wakati wa sherehe za kutimiza miaka 89 ya klabu ya Yanga kulikua na taarifa kuhusiana na kuwa mdhamini na mfadhili wa klabu ya Yanga, Gharib Said Mohammed (GSM) ameridhia kujenga uwanja katika eneo la makao makuu ya klabu hiyo Jangwani Dar es Salaam taarifa ambayo ilitolewa na Rais wa Yanga, Hersi Said na kusema kuwa uongozi wa Yanga upo tayari kumpa ushirikiano GSM katika mchakato wote wa ujenzi wa uwanja huo.

    Tumeona namna ambavyo viongozi mbalimbali waliopita Yanga wakizungumza kuhusu ujenzi wa uwanja huo na kushindwa kutekeleza jukumu hili kubwa zaidi ambalo bila shaka kwa ambaye atafanikiwa kulitimiza katika uongozi wa klabu hii ataacha historia kubwa sana katika maisha ya soka ya klabu hii huku siasa za mpira zikitawala zaidi.

    Kwenu viongozi wa Yanga tumeona hatua zenu mbalimbali mlizoamua kuzichukua kuhusu klabu hii lakini ni wakati sasa wa kuthibitisha kuwa ni kitu ambacho kinawezekana na kinaweza kufanywa na nyie kuwa wa kwanza kuonesha mmeamua kukifanya nacho ni kuwa na uwanja wenu rasmi mtakaoutumia katia mechi zenu.

    SOMA ZAIDI : Ahsante John Bocco Umeiona Fursa Kwa Soka La Tanzania

    habari za yanga taarifa za yanga Uwanja wa yanga

    1 Comment

    1. Pingback: Wachezaji Hatari Wa Kuchungwa Ligi Kuu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.