Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mayele Ana Laana Ya Ligi Kuu?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mayele Ana Laana Ya Ligi Kuu?

    MhaririBy MhaririFebruary 12, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mayele
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kumekua na maandiko mengi mtandaoni haswa baada ya kile ambacho amekiandika mchezaji wa kimataifa wa timu ya taifa ya DR Congo na klabu ya Pyramids kutoka nchini Misri Fiston Kalala Mayele,haswa kuhusu namna ambavyo amekua akipokea kauli za matusi kutoka kwa mashabiki wa soka wa Tanzania na akaja wazi na kusema kuwa anawafahamu kuwa wenye hiyo tabia ni mashabiki wa klabu ya Yanga.

    Utakua unajiuliza kama mimi kwanini inafikia hivyo na mpaka anawasema mashabiki ambao wamempa heshima na thamani kubwa baada ya mafanikio makubwa ambayo klabu ya Yanga imeyapata hivi karibuni ikichagizwa na kiwango chake kikubwa ambacho amekionesha na kuisaidia klabu hii.

    Kuna jambo ambalo ngoja niliweke wazi na nadhani ni kwamba bado Mayele hajakijua kuhusu mpira wa bongo ni kuwa siku zote ukiondoka katika ligi ya Tanzania usianze mbwembwe hazisaidii kitu wewe fanya kazi yako ukimaliza umepata timu nyingine nenda kafanye kazi huko pia kama ambavyo ulikua ukifanya ukiwa Tanzania.

    Mashabiki wa soka bongo wanajua kukuza na kuwafanya wachezaji mastaa na jambo kama hili Mayele amelipata kwahiyo ni wakati wake sasa kuvumilia kwa kile ambacho alikua akipitia kuliko kukiweka mtandaoni na kuzua taharuki kwangu mimi nimemuona mchezaji wa kwanza kufanya hivyo na hii ni kuwakosea heshima mashabiki wa klabu iliyokutambulisha vyema alipo sasa.

    Kuna kitu kinaitwa laana ya ligi kuu, mchezaji akishapita bongo hakuna namna anaweza kutoboa ligi nyingine Afrika na sababu ni moja tu, hype na heshima anayopewa na mashabiki wa klabu mbili za Kariakoo haipo sehemu yoyote. Mayele awaige Chama na Miquissone arudi nyumbani Inawezekana kuna watu wamemjaza maneno ya fitna kwa siku nyingi leo ndio kaamua kulipuka

    SOMA ZAIDI:Ligi Kuu Imerejea Marefa Kuweni Na Msimamo

    Fiston Mayele Mayele

    2 Comments

    1. Pingback: Ningeshangaa Sana Kama Simba Wasingeshinda - Kijiweni

    2. Pingback: Ahsante John Bocco Umeiona Fursa Kwa Soka La Tanzania - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.