Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Haller Kutoka Kupambana Na Saratani Mpaka Bingwa AFCON
    Africa | CAF

    Haller Kutoka Kupambana Na Saratani Mpaka Bingwa AFCON

    MhaririBy MhaririFebruary 12, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Sebastian Haller
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Achana na njia ngumu waliyopita Ivory Coast hadi kuwa mabingwa wa AFCON 2023 kuna njia nyingine ngumu aliyopita mfungaji wa bao la ushindi, Sebastian Haller kwani aliyaanza mashindano haya akiwa na majeraha ya kifundo cha mguu na hii ndiyo maana mechi za mwanzo alizikosa na baadaye akawa anatokea benchi huku mechi yake ya kwanza kuanza ilikuwa nusu fainali dhidi ya DR Congo ambapo alifunga bao la ushindi.

    Na kwenye fainali pia akafunga bao lililobakisha kombe nyumbani litakalodumu katika vichwa vya wananchi wa Ivory Coast bila kusahau na mashabiki wa soka barani Afrika ambao walikua wakiitazama fainali kati yao na Nigeria.

    Lakini hilo sio jambo kubwa zaidi kwake kwani moja kati ya kitu kikubwa na cha kishujaa ni ile ya kurudi uwanjani baada ya kushinda vita dhidi ya ugonjwa hatari wa saratani ambapo Julai 2022, baada tu ya kujiunga na Dortmund akitokea Ajax, Sebastian Haller aligundulika kuwa na saratani ya korodani.

    Akafanyiwa upasuaji mara mbili na kupigwa mionzi mara nne ili kuondoa mfumo wake wote wa korodani ulioathirika na saratani ambapo kila tiba moja katika hizo ilichukua siku tano za kulazwa hospitali lakini Septemba 2022 akatoka hospitali na Oktoba mwaka huo huo akahudhuria sherehe za utoaji tuzo za Ballon d’Or jijini Paris ambapo yeye mwenyewe alikuwa mmoja wa wanaowania tuzo hiyo na alishika nafasi ya 13 kutokana na mafanikio yake akiwa na Ajax ikiwa pamoja na kuwa mfungaii bora wa ligi ya Uholanzi.

    Alipewa nafasi ya kupanda jukwaani kukabidhi tuzo ya Yashin kwa kipa bora, Thibaut Courtois. Haller alionekana kuathirika na mionzi ya tiba na nywele zake zilinyonyoka vibaya.Siku hiyo ambayo mtangazaji wa Balon d’Or, Didier Drogba, ambaye ni shujaa wake, akamuomba aseme kitu kuhusu maendeleo ya afya yake. Akasema anaendelea vizuri na anatarajia kurudi uwanjani.

    Mwezi wa 12 Sebastian Haller akarudi hospitali kufanya tena vipimo na madaktari wakamthibitishia kwamba amepona kabisa hivyo akajiunga na kambi ya timu yake kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi na Januari 22, 2023 akacheza mechi yake ya kwanza rasmi tangu ajiunge na Dortmund ambapo ilikuwa mechi ya ushindi wa 4-3 dhidi ya Augsburg kwenye Bundesliga na Haller aliingia dakika ya 60 akivaa viatu vilivyoandikwa “F*CK CANCER”.

    Februari 2024 anaisaidia Ivory Coast kushinda AFCON baada ya kuwavusha hatua ya nusu fainali na kufunga bao la 2 la ushindi katika hatua ya fainali dhidi ya Nigeria.

    SOMA ZAIDI: Takwimu Na Rekodi Zote AFCON Unazopaswa Kuzifahamu

    afcon haller ivory coast sebastian haller
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.