Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Takwimu Na Rekodi Zote AFCON Unazopaswa Kuzifahamu
    Africa | CAF

    Takwimu Na Rekodi Zote AFCON Unazopaswa Kuzifahamu

    MhaririBy MhaririFebruary 12, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mabingwa wa AFCON
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni rasmi sasa michuano ya mataifa barani Afrika (AFCON) kwa mwaka huu imekamilika rasmi na mwenyeji akifanikiwa kuuchukua ubingwa na kuubakisha katika ardhi yake ya nyumbani.

    Achilia mbali matokeo ya kushangaza lakini pia na safari ngumu aliyoipata bingwa wa michuano ya AFCON kwa msimu huu ambaye ni mwenyeji Ivory Coast kuna mambo mengi ambayo yamejificha nyuma ya pazia ambayo unaweza kuwa huyafahamu lakini sisi tumekuandalia kwa kina kabisa mambo hayo ili uweze kuyafahamu vizuri kabisa.

    • Kwa mara ya 12 katika historia ya michuano ya mataifa barani Afrika, nchi mwenyeji anachukua ubingwa ambapo mara ya kwanza ilikua Misri mwaka 2006 huku Ivory Coast hili likiwa ni taji lao la 3 baada ya kuchukua mwaka 1992 nchini Senegal na mwaka 2015 nchini Equatorial Guinea.
    • Hii ni mara ya 5 kwa Nigeria kufungwa katika michuano ya AFCON ambapo ilitokea pia mwaka 1984,1988,1990 na mwaka 2000 wakiungana na timu ya taifa ya Ghana kama timu ambayo imefika fainali nyingi za AFCON.
    • Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ivory Coast Emerse Fae, anakua kocha wa kwanza kuweka rekodi ya kuchukua ubingwa wa AFCON bila ya kuanza michuano kama kocha mkuu.
    • Katika mchezo wa fainali, Nigeria amepiga mashuti pekee yaliyolenga goli ikiwa ni mashuti machache zaidi kwao tangu kuanza kwa michuano ya msimu huu.
    • Kapteni na beki wa kati wa Nigeria ameweka rekodi ya kuwa beki wa kwanza wa kati kufunga mabao 3 katika michuano ya AFCON.
    • Ekong wa Nigeria na Haller wa Ivory Coast ni wachezaji wa kwanza kufunga magoli katika mechi za nusu fainali na mechi ya fainali katika michuano ya AFCON tangu afanye Gedo mwaka 2010 nchini Misri.
    • Simon Adingra anaingia katika rekodi za CAF kwa kuwa mchezaji aliytoa pasi mbili za usaidizi katika fainali za michuano hii kwa karne ya 21.
    • Max-Alain Gradel ndio mchezaji mkongwe zaidi kushiriki fainali ya AFCON ambapo amecheza fainali akiwa na miaka 36 na siku 73 tangu itokee kwa Essam El Hadary aliekua na miaka 37 mwaka 2010 na miaka 44 mwaka 2017.

    SOMA ZAIDI: Washindi wa tuzo za AFCON vipengele vyote

    afcon AFCON 2023

    2 Comments

    1. Pingback: Haller Kutoka Kupambana Na Saratani Mpaka Bingwa AFCON - Kijiweni

    2. Pingback: Ratiba Kamili Ligi Ya Mabingwa Afrika Mwezi Huu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.