Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Hakuna Mnyonge Yoyote Anaweza Kuwa Bingwa AFCON 2023
    Africa | CAF

    Hakuna Mnyonge Yoyote Anaweza Kuwa Bingwa AFCON 2023

    MhaririBy MhaririFebruary 7, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mabingwa wa AFCON
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Baada ya mapumziko ya siku kadhaa ni wazi sasa macho na masikio ya wengi ni kuhusiana na michuano ya mataifa barani Afrika (AFCON) ambapo kuanzia hatua ya makundi mpaka hatua ya robo fainali yamekua na mvuto mkubwa sana kwa mashabiki wa soka barani Afrika haswa kutokana na matokeo ya kustaajabisha na vigogo kutolewa.

    Kumbuka kuwa katika hatua hii ya nusu fainali timu zilizofuzu ni wenyeji Ivory Coast, South Africa, DR Congo na Nigeria na wote tayari walishawahi kuwa mabingwa wa michuano hii ya AFCON hivyo ni nusu fainali ambayo sio ya kinyonge sana kwani inawakutanisha mabingwa wa mara kadhaa wa michuano hii mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya timu za taifa na hapa tutazame timu na idadi ya makombe waliyochukua katika michuano hii.

    1. Nigeria

    Amefuzu hatua hii baada ya kumtoa Angola kwa bao 1:0 katika hatua hii ya nusu fainali ndio ambaye anaongoza kwa kuchukua ubingwa mara nyingi zaidi kwa timu zilizofuzu hatua hii ya nusu fainali. Amechukua ubingwa huu mara 3 ambapo ni mwaka 1980, 1994 na mwaka 2013.

    1. Ivory Coast

    Huyu ni mwenyeji wa michuano hii ya mataifa barani Afrika kwa mwaka huu na ameingia hatua hii baada ya kumtoa Mali. Sio mnyonge kwani amechukua michuano hii ya mataifa barani Afria mara 2 ambapo ni mwaka 1992 na mwaka 2015.

    1. DR Congo

    Timu hii ya taifa ambayo ndani yake kuna wachezaji wengi sana kutoka ligi mbalimbali kubwa barani Ulaya wamewahi kuchukua ubingwa huu wa AFCON mara 2 ambapo waliutwaa mwaka 1968 na mwaka 1974 hivyo wana kiu kubwa ya kuweka rekodi ya kuchukua mara ya 3 michuano hii.

    1. South Africa

    Hawa ndio unaweza kusema vibonde ila pia waliwahi kuwa mabingwa wa michuano hii mara moja pekee na swali kubwa ni wataweza kutinga fainali? Kwani hatua hii ya nusu fainali anakutana na Nigeria ambaye ndio mkongwe zaidi katika hatua hii akiwa na ubingwa mara 3.

    Bila shaka tumeona namna ambavyo nusu fainali hii ilivyokua sio ya kinyonge kwa kuona ambavyo wote waliotinga nusu fainali washawahi kuwa mabingwa , kumbuka kuwa Nigeria dhidi ya South Africa huku Ivory Coast dhidi ya DR Congo.

    SOMA ZAIDI: Walioleta VAR AFCON Wana Nafasi Yao Moyoni Mwangu

     

     

    AFCON 2023

    1 Comment

    1. Pingback: Ivory Coast vs DR Congo Suka Hivi Mkeka Wako - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.