Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » TFF Ni Wakati Wa Kuwafungulia Fursa Nje Makocha Wazawa
    Africa | CAF

    TFF Ni Wakati Wa Kuwafungulia Fursa Nje Makocha Wazawa

    MhaririBy MhaririJanuary 25, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Makocha wazawa Hemed Morocco na Juma Mgunda
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ukiuzungumzia mpira wa miguu Tanzania basi huwezi kuacha kulitaja Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya Rais wake Wallace Karia ambaye anaingia katika orodha ya marais wa shirikisho hilo kwa mafanikio mengi makubwa ambayo ameyapata wakati wa uongozi wake akiwa na Katibu wake Wilfred Kidao ambao wamechukua hatua muhimu katika kuendeleza mchezo wa soka Tanzania.

    Kwa sasa huwezi kuacha kutaja namna ambayo kumekua na ligi bora yenye ushindani lakini pia kukiwa na wadhamini wa kutosha wanaoendelea kuipa nguvu ligi yenyewe kuanzia ile ya Wanaume na ligi kuu ya wanawake ambayo pia imekua na ushindani mzuri tu.

    Tumeona kile ambacho wamekifanya makocha wazawa Hemed Morocco akisaidiana na Juma Mgunda katika michuano ya mataifa barani Afrika kwa mechi 2 za mwisho ambazo walizikaimu baada ya kufungiwa kwa kocha mkuu Adel Amrouche. Nadhani ni wakati sahihi kuwa na njia hii ya kuwapa fursa makocha wazawa kujifunza zaidi nje ya nchi, hasa katika mataifa yaliyoendelea kwani hii ni hatua muhimu ambayo inaweza kuleta mabadiliko chanya katika maendeleo ya soka nchini.

    TFF wanapaswa kufahamu kuwa kwa kuwapa fursa makocha wazawa kwenda kujifunza nje ya nchi kunawezesha upatikanaji wa maarifa mapya ya kufundisha soka kwani mataifa yaliyoendelea mara nyingi yanajulikana kwa mifumo bora ya mafunzo ya soka na teknolojia ya hali ya juu katika maendeleo ya wachezaji. Makocha wazawa wakipata fursa ya kujifunza katika mazingira haya, wanaweza kurudi na maarifa mapya na mbinu za kufundishia, hivyo kuboresha ubora wa mafunzo wanayotoa.

    Makocha wetu wazawa wakishiriki katika programu za kimataifa kunawawezesha kujenga mtandao wa kimataifa na wenzao duniani kote. Hii inaweza kusaidia kuleta ushirikiano katika maendeleo ya soka, kubadilishana uzoefu, na hata kuanzisha mikataba ya ushirikiano na taasisi za kimataifa. Mtandao huu unaweza kuwa muhimu katika kuvutia rasilimali na fursa za maendeleo ya soka nchini.

    Tufahamu kuwa maendeleo ya soka yanaweza kuvutia wadhamini na uwekezaji. Kwa kuboresha ubora wa mafunzo na kuongeza ushindani, Tanzania inaweza kuwa na soko lenye thamani kubwa kwa wadhamini na wawekezaji kuja kuwekeza katika ligi zetu lakini pia na miundombinu ya michezo na kupelekea kujenga msingi imara wa soka la kitaifa.

    Kuwapa makocha wazawa nafasi ya kujifunza nje ya nchi ni uamuzi wa busara ambao unalenga kuleta mabadiliko chanya katika soka la Tanzania na matumaini yangu ni kuwa mkakati huu utachangia kukuza vipaji na kuleta mafanikio katika ngazi ya kitaifa na kimataifa.

    SOMA ZAIDI: Yanga Walikua Sahihi Kumpiga Kitanzi Ibrahim Bacca

    hemed morocco juma mgunda kocha mzawa
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.