Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Taifa Stars Ilikosa Kujiamini Hakukua Na Mipango Sahihi
    Africa | CAF

    Taifa Stars Ilikosa Kujiamini Hakukua Na Mipango Sahihi

    MhaririBy MhaririJanuary 25, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    kikosi cha Taifa Stars
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni rasmi kuwa sasa Taifa Stars imeaga michuano ya mataifa barani Afrika baada ya kumaliza katika kundi wakiwa nafasi ya 4 na alama 2 pekee kwani wamefungwa mchezo mmoja dhidi ya Morocco na kupata sare katika michezo 2 ambao ni dhidi ya Zambia na wa mwisho dhidi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.

    Ukiitazama namna ambavyo Taifa Stars ilivyocheza katika baadhi ya mechi za katika michuano hii utagundua kuwa kama timu ilikosa kujiamini yaani walipoteza kabisa ile hali ya kuwa na Imani na ujasiri kuwa wanaweza kufanya kitu bila kusita au kuwa na shaka yoyote ile.

    Kuanzia katika maamuzi ambayo makocha wa timu ya Taifa yalikua yakionesha wazi kuwa hawakua na ile ari ya kujiamini katika baadhi ya mambo waliyokua ya msingi kabisa japokua tunafamu namna ilivyo ngumu kwa kazi ya kuusoma mchezo kwa makocha n ani moja kati ya mambo ambayo hayapingiki ndio maana baadhi ya vilabu vikubwa vinaajiri wasoma mchezo kwa ajili ya kutathmini na kutoa mapendekezo zaidi.

    Nadhani ni wakati sasa wa kuwa na imani ya kwamba hatupaswi kuwaacha makocha hasa wale wa kigeni kufanya maamuzi makubwa bila usimamizi mkubwa na wa karibu bila ya kuwa na wakufunzi ambao ni wabobezi wa kitanzania kwani watajifunza kitu.

    Unajua katika nchi yetu kuna wakufunzi wengi sana wa kiufundi na tunafahamu kuwa baada ya AFCON ya Morocco inayofuata ni ya kwetu tujipange mapema kabisa na tusione ubaya katika kujifunza. Kwa Tanzania, AFCON ndo Kombe la Dunia na CHAN ni AFCON kwetu na tulimpa kocha mamlaka makubwa mno, tukaacha kujiamini leo tunalalamika.

    Katika mchezo dhidi ya DR Congo ilikuwa mechi yetu ya kufa au kupona, kwahiyo tulipaswa kuwa na mpango wa kushambulia kuliko mpango wa kupasıana sana kuelekea langoni kwetu, walimu wana imani yao. Nina imani pia kwamba pamoja na mpango wetu mzuri wa kujilinda ila tulipaswa kuwa na mpango mzuri pia wa kushambulia na kuwa na wachezaji wenye asili ya kushambulia zaidi wa kufanya hilo. Namna tulivyocheza haikuakisi sana kwamba tunataka kuvuka na tuna mpango mzuri wa kushambulia. Siamini kwamba hatukuwa na wachezaji hao ila hatukuwa na mpango huo, mabadiliko yalivyofanyika yanaakisi imani yangu.

    SOMA ZAIDI: Huyu Ndio Beki Katili Wa Nyavu AFCON

    taifa stars

    1 Comment

    1. Pingback: Ratiba Kamili Ya AFCON Hatua Ya 16 Bora - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.