Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tanzania Dhidi Ya DR Congo Ni Vita Ya Kujuana
    Africa | CAF

    Tanzania Dhidi Ya DR Congo Ni Vita Ya Kujuana

    MhaririBy MhaririJanuary 24, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji wa Tanzania
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Wakati macho na masikio ya wengi hii leo ni kuona namna gani kama yataendelea maajabu ambayo yamekua yakijitokeza katika michuano ya mataifa barani Afrika huku mechi kubwa kadhaa zikipigwa lakini inayozungumzwa zaidi ni ya Tanzania dhidi ya DR Congo ambao ni mchezo wa mwisho kabisa hatua ya makundi kutoka kundi F.

    Mchezo wa leo ambao kikanuni ni kwamba DR Congo yuko ugenini kwani mwenyeji wa mchezo huu ni Tanzania ambaye  yuko nyumbani katika uwanja wa Amadou Gon Coulibaly wenye uwezo wa kuingiza takribani watazamaji elfu ishirini.

    Kila mmoja ana mtazamo wake juu ya mchezo huu ambao Tanzania anaingia akiwa hana cha kupoteza akihitajika kupata ushindi ili aweze kufuzu hatua inayofuata ya 16 bora katika michuano hii ambayo ni mara ya 3 kwa Taifa Stars kufuzu.

    Bila shaka wengi wanaamini kuwa endapo hii leo wachezaji wa Taifa Stars wataongeza nguvu zaidi ya ile ambayo waliionesha kwa Zambia basi wana nafasi kubwa ya kufanya vizuri mbele ya timu ya Taifa ya DR Congo ambayo imesheheni wachezaji wakubwa kutoka ligi kubwa barani Ulaya.

    Unajua nasema kwanini Stars wanaingia katika vita ya kujuana dhidi ya DR Congo? Kumekua na wachezaji kadhaa ambao wanacheza na ambao waliwahi kucheza ambao wanaweza kutumika kutoa siri ya jinsi ya baadhi ya wachezaji wanavyocheza. Tutazame vita hii ya kujuana katika namna hii

    Mwamnyeto&Bacca dhidi ya Mayele

    Hawa ni wachezajia ambao wanafamiana vya kutosha kwani wameshacheza Pamoja mara nyingi katika kikosi cha Yanga kabla ya Mayele kuuzwa katika klabu ya Pyramid nchini Misri. Katika kikosi cha Tanzania,Mwamnyeto na Bacca ndio mabeki wa kati ambao wamecheza dakika 180 kwenye mechi mbili za Afcon katika michuano ya mwaka huu wakiruhusu mabao manne na straika wa Pyramids, Fiston Mayele yeye amecheza dakika 39 pekee.

    Mayele kama ataanza katika mechi hii basi mabeki wa Stars wanapaswa kumchunga nyota huyo wa zamani wa Yanga kwani anawafahamu vizuri akiwa amewahi kucheza Tanzania kwa misimu miwili mfululizo.

    Feitoto&Kibu dhidi ya Inonga

    Hapa wanakutana wachezaji wa klabu ya Simba yaani Kibu na Inonga Pamoja na mchezaji wa Azam ambaye waliwahi kukutana katika baadhi ya mechi za ligi kuu Tanzania Bara. Kama wote watacheza mechi hiyo huenda ikashuhudiwa vita kutokana na kujuana vyema kwenye Ligi Kuu.

    SOMA ZAIDI: Mauritania Na Simulizi Yao Mpaka Kumtoa Algeria AFCON

     

     

    AFCON 2023 dr congo afcon tanzania

    1 Comment

    1. Pingback: Huyu Ndio Beki Katili Wa Nyavu AFCON - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.