Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Msimlaumu Onana, Senegal Wana Timu Bora Sana
    Africa | CAF

    Msimlaumu Onana, Senegal Wana Timu Bora Sana

    MhaririBy MhaririJanuary 19, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Andre Onana
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) imekuwa jukwaa la kuonesha vipaji vya wachezaji wa soka kutoka bara la Afrika. Katika toleo la hivi karibuni la AFCON, Senegal imeonyesha uwezo wake wa kipekee, na kuvutia macho ya wapenzi wa soka duniani kote.

    Ukitazama katika mitandao ya kijamii baada ya mchezo wa Senegal dhidi ya Cameroon ambao Simba wa Teranga wamewafunga Simba wasiofungika mabao 3:1 huku golini akiwa golikipa wa klabu ya Man Utd kutoka katika ligi kuu ya Uingereza anayejadiliwa sana ni golikipa Andre Onana.Kuna wakati unajiuliza kwanini sasa wakati aina ya magoli ambayo amefungwa ni uzembe wa mabeki wake

    André Onana amekuwa nguzo muhimu katika ushindi na mafanikio ya Timu ya Taifa Cameroon katika baadhi ya mechi ingawa mchezo dhidi ya Senegal ni mchezo wake wa kwanza katika michuano ya AFCON mwaka huu. Akiwa kama golikipa, ameonesha ustadi wake wa hali ya juu katika kuokoa michomo hatari, kutoa mabao na kuwa kiongozi langoni lakini pia kupangwa kwake kuanza leo ni pamoja na uzoefu wake katika ligi za Ulaya, hasa akiwa na Man Utd, umemfanya awe mchezaji wa kuaminika na mwenye uzoefu.

    Hata hivyo, kuna wakati ambapo Onana amekutana na changamoto na kushutumiwa kwa baadhi ya makosa yake langoni. Hii ni sehemu ya mchezo wa soka, na hata wachezaji bora wanaweza kukutana na nyakati ngumu. Ni muhimu kuelewa kwamba sio Onana pekee anayepaswa kulaumiwa wakati mambo yanapokwenda vibaya.

    Ukiitazama nchi ya Senegal ambao ni mabingwa watetezi ina timu imara yenye vipaji vingi katika kila idara. Washambuliaji kama Sadio Mané, na mabeki imara kama Koulibaly wameifanya Senegal kuwa mojawapo ya timu bora katika bara la Afrika. Hivyo basi, ni muhimu kuelewa kuwa matokeo mabaya hayawezi kumlazimu lawama Onana pekee.

    SOMA ZAIDI:Tusahau Kuhusu Morocco, Tunaingiaje Kwa Zambia?

    afcon AFCON 2023 onana ONANA CAMEROON
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.