Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Jezi za Cameroon Zilivyostaajabisha AFCON Ya 2002 Na 2004
    Africa | CAF

    Jezi za Cameroon Zilivyostaajabisha AFCON Ya 2002 Na 2004

    MhaririBy MhaririJanuary 9, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    matukio yaliyostaajabisha AFCON
    Wachezaji wa timu ya taifa ya Camerron na jezi zao wakati wa AFCON ya mwaka 2002.
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kuelekea michuano ya mataifa barani Afrika (AFCON) itakayofanyika nchini Ivory Coast, yapo matukio kadhaa ambayo yalishika vichwa vya habari na kuwafanya watu wengi kutaka kuyafuatilia ili kufahamu zaidi kuhusu matukio haya na moja kati ya tukio liloshangaza wengi ni kuhusu jezi za timu ya Taifa ya Cameroon ambazo walivaa katika michuano ya mwaka 2002 na 2004.

    Wakati wa michuano ya AFCON kwa mwaka 2002 Cameroon walishinda michuano ya Kombe la Mataifa Bingwa Afrika 2002 kwa kuwafunga Senegal kupitia mikwaju ya penalti kwenye fainali. Licha ya kuchukua ubingwa lakini kinachokumbukwa sana na wanamichezo barani Afrika ni jezi za Cameroon (Simba Wasioshindwa) ambazo zilikuwa hazina mikono. Baada ya kuchukua ubingwa wa AFCON pia walifuzu kombe la dunia lilofanyika nchini Japan mwaka 2002  wakiwa na kikosi cha wachezaji kama Samuel Etoo, Marc Vivien Foe pamoja na Rigobrt Song walivyotaka kutumia jezi hizi walizuiwa na FIFA kuzivaa kwenye kombe la dunia.

    matukio yaliyostaajabisha AFCON

    Baada ya kushangaza umma na jezi za namna hiyo za kukata, Cameroon wakaendelea tena na vituko vyao ambapo mwaka 2004 wakati wa michuano ya AFCON iliyofanyika nchini Tunisia walikuwa na jipya tena ambapo walivalia jezi moja iliyoshikana – fulana na kaptura.

    Kufuatia jezi hizi mpya ambazo walikuja nazo Cameroon Fifa hawakufurahia, na ikizingatiwa kwamba walikiuka ahadi ya awali ya kuzitumia kucheza mechi za makundi pekee, Fifa waliwapiga faini kwa kucheza mechi ya robo fainali ambayo walishindwa na Nigeria.

    Michuano ya AFCON inatarajiwa kuanza kutimua vumbi nchini Ivory Coast kuanzia tarehe 13/01/2024 mpaka tarehe 11/02/2024 nchini Ivory Coast huku viwanja takribani 6 vikitumika katika mechi mbalimbali.

    Endelea kufuatilia zaidi kuhusu taarifa zinazohusu AFCON kwa kugusa hapa.

     

    1 Comment

    1. Pingback: Mastreka Hatari Wa Kuchungwa AFCON 2023 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.