Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba Yamshushia Kipigo Kizito Kagera Sugar
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Simba Yamshushia Kipigo Kizito Kagera Sugar

    MhaririBy MhaririDecember 15, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji Saido Ntibazonkiza kutoka klabu ya Simba.
    Mchezaji wa klabu ya Simba Saido Ntibazonkiza akipiga mpira wa penati katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar.
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Klabu ya soka ya Simba imeibuka na ushindi wa mabao 3:0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliofanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar Es Salaam.

    Mchezo huo uliokua wa kuvutia ulimalizika kwa kipindi cha kwanza klabu ya Simba kuondoka na ushindi wa bao 1:0 lililofungwa na kiungo wake Saido Ntibazonkiza kwa njia ya mkwaju wa penati.

    Dakika ya 75 wekundu wa msimbazi waliongeza uongozi kwa bao safi la kichwa lilofungwa na kiungo mmali Sadio Kanoute huku Mshambuliaji na kapteni wa klabu hiyo John Raphael Bocco akishindilia msumari wa moto kwa kufunga bao la 3 dakika ya 90 ya mchezo.

    Ushindi huo unaifanya Simba ifikishe pointi 22, ingawa inabaki nafasi ya tatu, ikizidwa pointi mbili na mabingwa watetezi, Yanga baada ya wote kucheza mechi tisa na wote wapo nyuma ya Azam FC yenye pointi 28 za mechi 12.
    Kwa upande wa Kagera Sugar baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 13 za mechi 12 nafasi ya 12.

    Aidha baada ya mchezo huo kocha mkuu wa klabu ya Simba, Abdelhak Benchikha ameweza kuwasifu wachezaji wake kwa ushindi walioupata lakini akilia na ubovu wa sehemu ya kuchezea wa Uwanja wa Uhuru huku kocha wa Kagera Sugar Mecky Mexime akisema kuwa wanaendelea kujipanga kuhakika wanarekebisha makosa ya leo na kushinda mchezo unaofuata.

    Kwenye msimamo anaeongoza ni Azam Fc akiwa na alama 28 na mechi 12 alizocheza huku anayemfuatia ni Yanga ambae amecheza michezo 9 na alama 24 huku wa tatu ni klabu ya Simba ambae amejikusanyia alama 22 katika mechi 9 alizocheza.

    Klabu za Geita Gold , Mashujaa na Mtibwa Sugar zikiwa chini kabisa ya msimamo wa ligi kuu Tanania Bara.

    Kwa taarifa zaidi za michezo unaweza kuendelea kwa kusoma hapa.

    simba sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.