Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » YANGA Watajilaumu Kwa MEDEAMA , Kundi Linazidi Kuvurugika
    Africa | CAF

    YANGA Watajilaumu Kwa MEDEAMA , Kundi Linazidi Kuvurugika

    MhaririBy MhaririDecember 8, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pacome na Musonda Medeama vs Yanga
    Mchezaji wa Yanga Pacome Zouzua akishangilia goli na mchezaji mwenzie wa Yanga Kennedy Musonda
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mechi iliyotarajiwa kuwa nzuri lakini mwenendo wa mwamuzi uliharibu ladha nzima ya mechi! Mwamuzi alikuwa wa kiwango cha chini mno! Kila timu iliona inammudu mwenzie tu na makosa yalikuwa mengi.

    Medeama walikuja na mpango wa kujitoa, kufika miguuni na wanafurahia mpira wa kugongana! Wana madhaifu mengi kiufundi na Yanga wangekuwa na matumizi mazuri ya nafasi wangefurahia zaidi.

    Yanga kila mchezo wanacheza vyema, wanatengeneza nafasi nyingi ila matumizi yake ni butu mno! Musonda ana papara, Mzize anajigovya govya! Ndio kitu pekee kinachowatafuna mechi baada ya mechi.

    Well played Kwadwo Amoako yule jezi namba 4 mchezaji mzuri sana! Mipira yake ya kutenga ni balaa mnoAna uwezo mzuri sana wa kupiga pasi pia na uvumilivu wake mchezoni ni mkubwa sana.

    Yule Pacome Zouzoua anajua mpira Anajiamini kutembea na mpira kwenye nyakati usizotarajia. Lile goli na movement ile angekuwa mchezaji mwingine angelazimisha kupasia! Ndiye Man of the Match wangu leo.

    Jonathan Sowah achana na goli lake la penati anajua sana kulinda mpira! Juu anaenda, chini anacheza kwa timing nzuri sana. Nilipenda energy yake kwenye kuwania mpira.

    Ibrahim Abdullah Hamad ‘Bacca’ na leo tena kwenye ubora wake ule ule kwenye msitari wa safu ya ulinzi Alitembeza mkong’oto vyema tu.

    Kipa Felix Kyei ana ‘footwork’ nzuri sana na wenzie wanamwamini sana inapohitajika mazingira ya kujisitiri kwani Mguuni kwake mazungumzo yamo.

    Khalid Aucho kwenye mfumo wa mabeki watatu wa kati anajikuta anatembea eneo kubwa peke yake… Anafanya kazi ya ngamia sana kwa sasa.

    Yanga wanammiss sana Lomalisa! Kibabage sio mbaya na anaingia kwenye boksi vyema tu ila maamuzi yake akiwa kwenye boksi ni dhaifu mno! Hana uhakika wa anachotaka kufanya!

    Yanga leo kuna muda walionekana kama wamechoka kwenye muda ambao Medeama wamechoka!

    Kundi hili linazidi kuvurugika! Yanga wameshindwa hii mechi wanapaswa kujilaumu wao wenyewe! Ni experience nzuri na ngumu wanaipata! Kazi imebaki kwenye mikono yao! Soma zaidi

    medeama leo yanga sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.