Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba Yamvuta Chemba Bruno Gomes, Kuondoka Singida BS?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Simba Yamvuta Chemba Bruno Gomes, Kuondoka Singida BS?

    David MohamedBy David MohamedJune 16, 20231 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Simba Wana Jambo lao..! Kiungo mshambuliaji wa Singida, raia wa Brazil Bruno Gomes ameitwa jijini  Dar es Salaam  kwa ajili ya kumalizana na mabosi hao wa Msimbazi kabla ya kutangazwa kuwa mmoja ya nyota wapya wa timu hiyo kwa msimu ujao ambao Wekundu wamepania kurejesha heshima.

    Tayari Bruno aliyefunga mabao 10 msimu huu kwenye ligi, yuko Dar es Salaam akiambatana na viongozi wa Singida na kama mambo yataenda kama ilivyopangwa atasaini mkataba wa miaka miwili.

    Mbrazili huyo pia ni pendekezo la Robertinho ambaye aliwaambia vigogo wa Simba anamtaka ili akasaidiane na Clatous Chama, Saidi Ntibazonkiza na Mzamiru Yassin eneo la kiungo.

    Moja ya vigogo wa Simba alithibitisha  nakusema “Onana na Gomes ni shabaha yetu na kuanzia kesho mnaweza kuona tarifa rasmi kuhusu wao,” alisema kigogo huyo na kufafanua;

    “Tayari huyo winga (Onana) tumemalizana naye na sasa tupo kwenye hatua za mwisho kumsainisha Bruno kwani tupo naye hapa Dar es Salaam, ikiwa ni mwanzo wa pazia la usajili kwa kikosi kijasho.”

    Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alithibtisha timu yake msimu huu itachukua mchezaji inayemtaka kwenye timu yoyote.

    “Siwezi kuweka wazi tumemsajili nani na nani lakini unachotakiwa kujua ni kwamba kila mchezaji tunayemtaka tutampata bila shida yeyote. Simba ni timu kubwa,” alisema Ahmed.

    Kwa taarifa zaidi za michezo, tufuatilie hapa.

    bruno gomes fountain gate ligi kuu tanzania bara Simba simba sc singida big stars

    1 Comment

    1. Anya112en on May 9, 2025 4:03 pm

      Hello team!
      I came across a 112 very cool page that I think you should browse.
      This tool is packed with a lot of useful information that you might find valuable.
      It has everything you could possibly need, so be sure to give it a visit!
      [url=https://www.hermitgamer.com/5-best-strategy-games-for-your-pc/]https://www.hermitgamer.com/5-best-strategy-games-for-your-pc/[/url]

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.