Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Yanga, Simba tayari kukabiliana na wapinzani huku CAF ikichagua waamuzi
    Africa | CAF

    Yanga, Simba tayari kukabiliana na wapinzani huku CAF ikichagua waamuzi

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiApril 28, 2023No Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Simba itashuka dimbani leo kuanzia saa tisa alasiri kwa saa za Tanzania kwenye Uwanja wa Stade Mohamed V mjini Casablanca, Morocco. Tayari wachezaji wa Simba wamewasili Casablanca kabla ya pambano lao

    Yanga itashuka dimbani Jumapili kuwakaribisha Rivers United ya Nigeria katika mchezo wa hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Mechi hiyo itaanza saa 7 mchana.

    Dar es Salaam. Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limemteua mwamuzi wa Chad Alhadi Allaou Mahamat kuchezesha mchezo wa robo fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Simba SC ya Tanzania na Wydad Club Athletic ya Morocco.

    Simba itashuka dimbani leo kuanzia saa tisa alasiri kwa saa za Tanzania kwenye Uwanja wa Stade Mohamed V mjini Casablanca, Morocco. Tayari wachezaji wa Simba wamewasili Casablanca kabla ya pambano lao.

    Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, Mahamat atasaidiwa na Elvis Guy Noupue Nguegoue kutoka Cameroon na Issa Yaya, pia kutoka Chad huku afisa wa nne atakuwa Mahmood Ali Mahmood Ismail kutoka Sudan.

    Simba ilishinda bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam na inahitaji sare yoyote ili kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

    Hata hivyo, Simba itakosa huduma ya wachezaji wake watatu, Aishi Manula, kipa chaguo la kwanza ambaye sasa anauguza jeraha lake, Augustine Okrah na Mohamed Ouattara. Kocha mkuu wa timu hiyo, Roberto Oliveira Gonçalves do Carmo almaarufu Robertinho, alisema wataenda kuthibitisha thamani yao katika pambano hilo licha ya kukabiliwa na kibarua kigumu.

    Alisema wachezaji wake wapo katika hali nzuri na wako tayari kufanya vyema katika mechi hiyo.

    Wakati huohuo, mchezo wa marudiano wa hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa Yanga na Rivers United, utachezeshwa na waamuzi wa Morocco.

    Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, Redouane Jiyed atakuwa katikati ya uwanja katika pambano hilo gumu ambalo Yanga inahitaji sare yoyote ili kuweka historia ya kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

    Yanga ilishinda 2-0 ugenini na kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. Jiyed atasaidiwa na Lahcen Azgaou na Mostafa Akarkad huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Jalal Jayed, pia kutoka Morocco.

    Wachezaji wa Yanga wameanza mazoezi jana kujiandaa na mchezo huo unaotarajiwa kuanza saa 7 mchana Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

    Licha ya ushindi wa mabao 2-0 ugenini, Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, alisema wanaichukulia kwa uzito mchezo huo na wanalenga ushindi ili kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ya kifahari.

    Yanga ilishinda 2-0 ugenini na kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. Jiyed atasaidiwa na Lahcen Azgaou na Mostafa Akarkad huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Jalal Jayed, pia kutoka Morocco.

    caf Simba yanga
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.