Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Vigogo Azam kumng’oa Peter Banda Simba
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Vigogo Azam kumng’oa Peter Banda Simba

    David MohamedBy David MohamedJune 12, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Vigogo wa Azam Hawajamaliza! Saa chache baada ya kumalizana na Yanga na kumbeba, kiungo Feisal Salum ‘Fei Toto’ iliyompa mkataba wa miaka mitatu, klabu ya Azam imehamia Msimbazi ikianza mazungumzo ya kumnyakua winga, Peter Banda.

    Azam imeanza mazungumzo na wawakilishi wa nyota huyo wa kimataifa kutoka Malawi mwenye miaka 22 na kwa hatua waliyofikia kuna uwezekano mkubwa, Banda akavaa uzi wa Azam msimu ujao kutokana na Simba kuwa tayari kumuuza au kumtoa kwa mkopo kipindi hiki akiwa amebakiza mkataba wa  mwaka mmoja.

    Nyota huyo tegemeo wa timu ya taifa ya Malawi, hayupo kwenye mipango ya kocha mkuu, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ aliyowapa mabosi wa chama hilo na Azam inatumia mwanya huo ili kumshawishi atue viunga vya Chamazi yalipo maskani ya klabu hiyo.

    Moja ya Vigogo Azam FC, aliyeomba jina lake kuhifadhiwa amethibitisha kuwa wanamhitaji Banda kutokana na uwezo na umri alionao.

    “Pale Simba tutang’oa mtu, kama tulivyowapa wao wachezaji miaka ya nyuma na sisi watatupa mastaa wao, mmoja wao ni yule winga Banda, kama wanaona hawafai, sisi atatufaa na tunajua tutamtumiaje.” alisema mtu huyo na kuongeza;

    “Kuna mazungumzo tumefanya na wawakilishi wa mchezaji lakini pia tunajiandaa kwenda mezani kwa Simba kumuomba Banda, baada ya hapo tutakachojibiwa tutakifanyia kazi.”

    Banda alijiunga na Simba mwanzoni mwa msimu uliopita kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Nyassa Big Bullets ya kwao Malawi, lakini tangu ametua kwa Wanamsimbazi hao, hakuwa na muendelezo  mzuri wa kiwango chake huku Majeraha ya mara kwa mara yakitajwa kuwa sababu.

    Azam azam fc habari za usajili peter banda simba sc tetesi za usajili usajili usajili ligi kuu
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.