Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tuzo za TFF 2022/2023: MAYELE na SAIDO Wang’ara / Hawa hapa Washindi Wote
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Tuzo za TFF 2022/2023: MAYELE na SAIDO Wang’ara / Hawa hapa Washindi Wote

    David MohamedBy David MohamedJune 12, 2023No Comments4 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Tuzo za TFF ni Moto..! Ligi kuu Tanzania bara (NBC Premier League) ikiwa imefikia ukingoni Juni 12, 2023 kwa kumalizika Mechi ya fainali ya Azam Sports Federation Cup iliyokutanisha Azam FC dhidi ya Yanga SC na huku ikimalizika katika Viwanja vya Mkwawani Tanga na Yanga SC kuondoka na ubingwa kwa ushindi wa bao 1-0.

    Licha ya kuwakosa Wachezaji wao muhimu katika kikosi ambao ni Fiston Mayele na Stephane Aziz Ki waliotimkia kutumikia mechi za kimataifa, Bao pekee la ushindi la Yanga SC liliwekwa kambani na Mshambuliaji Kennedy  Musonda dakika ya 13 na kuwafanya wana jangwani hao kutetea tena ubingwa wao msimu huu.

    Baada ya kumalizika kwa michuano hiyo na Ligi kiujumla, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilitamatisha kwa kutolewa kwa Tuzo katika msimu huu wa 2022/2023 zilizofanyika katika Viwanja wa ufundi vya TFF katika vipengele mbalimbali katika soka nchini Tanzania zilizofanyika hapo mkoani Tanga na vigogo mbalimbali wakiondoka na Tuzo usiku huo.

    Hizi hapa ni  baadhi ya Tuzo ambazo ziligonga vichwa vya mashabiki wa soka kutokana na ukubwa wake na hawa ndio washindi waliozinyakua:

    1. Mchezaji bora Umri miaka 20 ni Clement Mzize kutoka Yanga SC
    2. Mchezaji bora 1st League ni Tungu R. Kachinje kutoka Stand United FC
    3. Mchezaji bora ligi ya Championship ni Edward Songo kutoka JKT Tanzania
    4. Timu yenye nidhamu ligi kuu ya wanawake (SWPL) ni Alliance Girls
    5. Mcheaji bora chipukizi Ligi ya wanawake (SWPL) ni Winfrida Charles kutoka Alliance Girls
    6. Golikipa bora Ligi kuu ya wanawake Tanzania bara (SWPL) ni Naitath Abbass kutoka JKT Queens
    7. Muamuzi bora Ligi kuu Tanzania bara ni Jonesya Rukya
    8. Mfungaji bora Ligi kuu ya wanawake Tanzania bara (SWPL) ni  Janeth Shikangwa kutoka Simba Queens
    9. Kipengele cha Kocha bora ligi kuu ya wanawake (SWPL) ni Ally Ally kutoka JKT Queens
    10. Mchezaji bora wa ligi kuu ya wanawake (SWPL) ni Donisia Minja kutoka JKT Queens
    11. Tuzo ya heshima kwenye soka la wanawake nchini Tanzania imekwenda kwa Angela Bilal
    12. Mchezaji Gwiji wa Zamani ni Leopold Taso aliekipiga pia Malindi FC na Timu ya Taifa ya Tanzania na akiwa Meneja wa Taifa stars kwa Miaka 7 Mfululizo
    13. Tuzo ya heshima imekwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake mkubwa kukuza soka nchini
    14. Ester Adalbelt ni Mwamuzi bora Ligi kuu ya wanawake (SWPL)
    15. Kamishna bora wa soka ni Issack Munisi
    16. Seti bora ya waamuzi ligi kuu Janeth Balama, Tatu Malogo, Joneysia Rukya na Mohamed Mkono
    17. Glory Tesha ni mwamuzi bora msaidizi Ligi kuu ya wanawake (SWPL)
    18. Frank Komba ni mwamuzi bora Msaidizi Ligi kuu ya NBC Tanzania bara
    19. Golikipa bora wa mashindano ya Azam Sports Federation Cup ni Djigui Diarra kutoka Yanga SC
    20. Mfungaji bora wa mashindano ya Azam Sports Federation Cup ni Andrew Simchimba kutoka Ihefu Sports Club
    21. Mchezaji bora wa mashindano ya Azam Sports Federation Cup ni Bakari Nondo Mwamnyeto kutoka Yanga SC
    22. Kocha bora wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara ni Nasredine Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga SC
    23. Tukio bora la kiungwana “Fair Play” imekwenda kwa Saido Ntibazonkiza Wa Simba SC katika mechi ya Simba SC Vs Yanga SC
    24. Mchezaji bora chipukizi Ligi kuu Tanzania bara (NBC)  ni Lameck Lawi Kutoka Coastal Union FC
    25. Beki bora Ligi kuu ya Tanzania bara (NBC) ni Dickson Job kutoka Yanga SC
    26. Kiungo bora Ligi kuu ya Tanzania bara (NBC) ni Saido Ntibazonkiza Wa Simba SC
    27. Meneja bora wa uwanja ni Omary Malule, Meneja wa uwanja wa Highland Estate unaotumiwa na Ihefu SC
    28. Golikipa bora wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara ni Djigui Diarra kutoka Yanga SC
    29. Mfungaji bora wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara imekwenda kwa Fiston Mayele wa Yanga SC na Saido Ntibazonkiza wa Simba SC wakilingana wote kwa pamoja kwa Goli 17 Msimu huu wa 2022/23
    30. Goli bora la Ligi kuu ya NBC Tanzania bara Msimu wa 2022/23 inakwenda kwa Fiston Mayele kutoka Yanga SC
    31. Tuzo ya Mchezaji bora, Most Valuable Player (MVP) Ligi kuu ya NBC Tanzania bara imekwenda kwa Fiston Mayele kutoka Yanga SC
    32. Timu yenye nidhamu Ligi kuu NBC Tanzania bara Msimu wa 2022/23 ni KMC FC Kutoka Manispaa ya kinondoni
    33. Kikosi bora cha Ligi kuu ya NBC Tanzania ni  Djigui Diarra (Yanga SC), Dickson Job (Yanga SC), Henock Inonga (Simba SC), Bakar  Mwamnyeto (Yanga SC), Shomari kapombe (Simba SC), Mohamed Hussein (Simba SC), Mzamiru Yassin (Simba SC), Bruno Gomez (Singida BS), Saido Ntibazonkiza (Simba SC), Clatous Chama (Simba SC) na Fiston Mayele (Yanga SC)

    Kwa taarifa zaidi za soka na usajili duniani, endelea kutufuatilia hapa.

    Azam beki bora fistom mayele kipa bora kiungo bora kocha bora ligi kuu ligi kuu bara ligi kuu tanzania bara mchezaji bora mfungaji bora MVP NBC NBC Premier League saido ntibazonkiza Simba singida big stars tanzania tff tff awards tuzo ya mayele tuzo ya saido tuzo za tff usiku wa tuzi tff yanga
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.