Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tumsubiri Kramo Au Ni Wakati Wa Kutafuta Mchezaji Mwingine?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Tumsubiri Kramo Au Ni Wakati Wa Kutafuta Mchezaji Mwingine?

    Oscar EvodiusBy Oscar EvodiusMay 24, 2024Updated:May 24, 202412 Comments2 Mins Read563 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Aubin Kramo Kouamé
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Aubin Kramo Kouamé(28) ni miongoni mwa majina ambayo Msimu huu wa mashindano unaomalizika mashabiki wa Simba na wadau wengi wa soka walitamani kumuona uwanjani, watu walitaka kuona ni kitu gani cha tofauti atapeleka ndani ya Msimbazi hasa katika eneo la ubunifu ambalo Timu inahitaji wachezaji wengi ili kuzalisha idadi kubwa ya magoli

    Pale Ligi Kuu ya Ivory Coast ukitaja jina la Aubin Kramo basi utakuwa umetaja miongoni mwa majina ya wachezaji wachache sana wenye vipaji vikubwa sana ambao wamepita ndani ya Ligi hiyo, pale wamtambua Aubin Kramo kama mchezaji ambaye alipaswa kuwa kwenye orodha ya wachezaji ambao wapo Ulaya kama Karim Konate, Sankara Kalamoko na wengineo waliotoka pale

    Kama ambavyo Stephane Aziz Ki na Pacome Zouzoua walikuwa MVP wa Ligi Kuu ya Ivory Coast basi Aubin Kramo alifanya hivyo pia kwa Msimu wa Mwaka 2022-23, Kramo wakati anaingia Simba aliingia kama MVP wa Ligi Kuu y Ivory Coast na katika wakati ambao watu wanatamani kuona miguu yake inaleta kitu gani ndani ya uwanja basi ndio wakati ambao anapata majeraha

    Majeraha ambayo amepata Aubin Kramo muda mwingi yamemuweka nje ya uwanja na Msimu huu unamalizika ikiwa Simba SC haijaona hata Robo ya Ubora wake aliotoka nao ndani ya Ivory Coast akiwa kama MVP! Hapa ukiacha Benchi jipya la Ufundi, Utamaduni, Ada ya Usajili, Wachezaji anaowakuta mchezaji husika na vitu vingine basi majeraha pia ni miongoni mwa vitu ambavyo hufanya mchezaji aonekane amefeli ndani ya Timu fulani

    Binafsi bado naamini kama ambavyo nilishasema hapo awali AUBIN KRAMO KOUAMÉ ndio Usajili Bora ambao Simba walifanya katika Dirisha kubwa la Usajili lililopita ni vile majeraha yamefanya amekuwa nje muda mwingi kuliko uwanjani, kama Simba ingepata hata Robo Tatu ya Ubora wake ambao alitoa ndani ya Asec Mimosas basi kuna sehemu kubwa sana wangesogea kutokana na uwezo alionao

    Simply! Mkataba wa Aubin Kramo unamalizika June 30 Mwaka 2025 na Kwakuwa Msimu mpya unaanza hivi karibuni basi tusubiri ataleta kitu gani ndani ya uwanja, pia kama yupo vizuri kurejea uwanjani na Simba wakabaki naye huenda basi wakapata kitu bora sana ambacho walihitaji kutoka kwenye ubongo na miguu yake.

    SOMA ZAIDI: Al Ahly Na Maajabu Ya Jezi Namba 72 Kabla Ya Mechi

    Aubin Kramo Simba Sc Usajili mpya simba sc wachezaji wapya simba sc

    12 Comments

    1. Finias petro on May 24, 2024 12:07 pm

      Aachwe

      Reply
    2. Enock on May 24, 2024 12:20 pm

      Upande wangu mm naona aachwe tu tuangalie namna nyingine ya kupata mchezaji atakae onekana kwenye kiwanja na sio msimu mnzima majeruhi
      Inachosha anakula tu hela bila kuitendea kazi
      Enough it’s enough

      Reply
      • Abraham on May 24, 2024 1:02 pm

        Aachwe ili iweje,
        Unamuachaje MVP wewe c utakuwa mwehu..
        Msimu wote umemvumilia leo unataka kumuacha akiwa hata hajakufanyia lolote Zaid ya kumlipa mshahara…
        Ana kitu,ulivuta subra juu yake hvy wakat wa mavuno kwa huyo mwamba unakaribia

        Reply
    3. Beca Daud on May 24, 2024 12:59 pm

      Kwakuwa bado anamkataba na simba sivyema aondoke..inabidi abaki uenda akaleta matunda bora msimu ujao.
      #Nguvu moja

      Reply
    4. Abraham on May 24, 2024 1:04 pm

      Kramo ni Simba na Simba ni kramo…
      Msimu ujao watafute watu na huyo MVP awepo mbona boli litembee tu

      Reply
    5. Slavius nguvumali on May 24, 2024 1:42 pm

      Mimi naona atafute changa moto sehem ningine anakaa injury sana adi anasahaulika

      Reply
    6. Azizh on May 24, 2024 2:03 pm

      Kramo ni bora kuliko pacome kuliko Aziz ki kilicholeta shida no majeruhi tu kwakua anaendelea na mazoez sioni sababu yakumuacha anavitu vingi Sana vyakutupa na tunamdai… Umakini uwepo kweny usajili kuna majipu yakutumbua lakin sio kramo
      #nguvumoja

      Reply
    7. Mathias on May 24, 2024 2:06 pm

      Shida yetu Tanzania hatuna uvumilivu kramo ni fundi kila mwanasimba anatambua Hilo wanapaswa wampe muda amprove kile alichonacho I think tutamkubali tu

      Reply
    8. Rance on May 24, 2024 2:09 pm

      kramo ni mchezaji mzuri sana injuries ni sehem ya maisha ya wachezaji mimi naona wanasimba tumpe muda kwa tulimsajili aje kuitumikia simba na sio kuja na kuondoka tumpe muda tuone uwezo wake ni mapema sana kumkatia tamaa mchezaji kama Aubin kramo
      #Nguvu moja

      Reply
    9. T J on May 24, 2024 2:28 pm

      Kama bench la ufundi na madaktari wamethibitisha kuwa yupo sawa kiafya ni bora aendelee kubaki kwa msimu mmoja pengin subra ikawalipa

      Reply
    10. Mpaka mafuta on May 24, 2024 4:30 pm

      Wananchi tunasubiri gwaride kwa mkapa🔥🔥 sisi tuna pacome, aziz ki aucho wao wana nani??💚💛

      Reply
    11. Pingback: Uso Wa Saido Ntibazonkiza Unazungumza Mengi

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.