Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tuendelee Kuuamini Ukuta Wa Yerikho Simba SC?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Tuendelee Kuuamini Ukuta Wa Yerikho Simba SC?

    Living ShayoBy Living ShayoMarch 13, 20242 Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji wa klabu ya Simba Fabrice Ngoma
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ulikuwa ni ushindi muhimu kwa Simba SC na kuendelea kuwapa nafasi nzuri kwenye Ligi na kuendelea kuwapa Furaha mashabiki wao, ila kama ni msimu ambao hawatausahau kwa miaka hii ya karibuni basi ni msimu huu wamepata matokeo ila hawakuwa na mchezo mzuri, Singida Fountain Gate FC ni kama mtumbwi umezidiwa na maji wamepoteza mchezo wa tano mfululizo ndani Ya michezo sita hawajaambulia ushindi kwa muda mrefu sasa.

    Kipindi cha kwanza, kilikuwa zaidi kwa Simba SC wakianza na Viungo wakabaji wawili Mzamiru Yassin n Fabrice Ngoma na kuwapa nafasi zaidi Chama, Ntibazonkiza na Kibu kuwa huru na kutengeneza nafasi ambapo waliweza kutengeneza nafasi nyingi zaidi ila matumizi yakawa sahihi kwa nafasi tatu tu, Simba SC walianzaje? 4-2-3-1 jambo ambalo walikuwa zaidi kwenye nusu Ya Singida FG muda mwingi wa kipindi cha kwanza, nini sababu ? Ni Singida FG kuamua kufunguka mapema sana mwa mchezo jambo ambalo lilipelekea wachezaji wengi wa Simba SC kuwa huru kucheza na kupiga pasi na kupelekea kuzaa magoli matatu.

    Bado Simba SC walikuwa wazi sana hususa eneo la kati ya uwanja muda mwingi sana Fabrice Ngoma na Mzamiru Yassin walikuwa wakitoka kwenye maeneo yao na ilipelekea baadhi Ya uanzilishi wa mashambulizi kwa Singida FG kufanikiwa kupitia eneo ilo, Kwa Singida FG eneo lao la ulinzi ndiyo lilikuwa Active zaidi kwa kipindi cha kwanza huku Yusuph Kagoma akikosa msaidizi wa kukaba eneo la kati.

    Kipindi cha pili kilikuwa upande wa Singida FG zaidi na kivipi wakifanikiwa? kwanza waliaamua kukimbia eneo kubwa la uwanja kuliko wachezaji wa Simba SC jambo ambalo liliwasaidia zaidi kumiliki mpira, pili walifanya “Press” Kwa nguvu sana na hiyo iliwanyima nafasi Simba SC kuwa huru kama kipindi cha kwanza, kitendo hicho kiliwapa presha wachezaji wa Simba SC na kupelekea kutotulia na mpira muda mrefu na tatu wakiamua kutumia mabeki wengi sana hususa eneo la pembeni walimtumia Amos Charles na Yahya Mbegu upande mmoja pamoja na Nicolas Gyan na Nicolaus Wadada upande wa pili.

    Changamoto yao ilikuwa wapi ? Baada Ya kufanya “press” na kumiliki mpira maamuzi mengi hayakuwa sahihi kwao hususa kwenye eneo Lao la mwisho walikuwa wakipoteza mipira kwanini ? Walikuwa wakitumia zaidi wachezaji wenye asili ya kukaba na hata mabadiliko ya kuingia Thomas Ulimwengu na Kasengu Kazadi kidogo kulionyesha ishara Ya uoatikanaji bao.

    1. Ayoub Lakred alikuwa na siku nzuri kiwanjani save tatu za Hatari
    2. Chama ni kama alihitaji kutoka na Assist Leo ila wenzake walishindwa kutumia nafasi 4 alizotengeneza
    3. Yusuph kagoma kwenye kiwango bora sana

    Full Time || Simba SC 3-1 Singida Fountain Gate FC

    SOMA ZAIDI: Kwanini Mdhamini Mmoja Timu 6 Ligi Moja?

    benchikha simba ligi kuu

    2 Comments

    1. Pingback: FIFA SERIES 2024 Ni Michuano Gani? Na Inafanyikaje? - Kijiweni

    2. Pingback: Barua Ya Wazi Kwako Dickson Job “Big Brain Defender” - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.