Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Timu Zinazoongoza Kwa Udhamini Ligi Kuu Ya Nbc
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Timu Zinazoongoza Kwa Udhamini Ligi Kuu Ya Nbc

    Living ShayoBy Living ShayoMarch 5, 20241 Comment4 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    timu za ligi kuu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kama ni wakati kwetu na mambo kubadilika basi ni ili la timu zetu kuanza kujikwamua kwenye swala la kujenga nembo bora na jina bora la timu ambalo imekuwa rahisi kupata wadhamini wengi kwa muda mfupi, ndani ya Ligi kuu ya NBC kuna timu 16 na hakuna timu hata moja ambayo haina udhamini wowote kwani kuna udhamini wa kampuni tatu tofautia Azam TV, TBC na NBC Bank ambazo zinatoa hela kwa kila timu zote shiriki.

    Tofauti ni kuwa nje ya udhamini rasmi wa Ligi nzima vilabu vingi vimejipatia wadhamini kadhaa kupitia ubora wa kikosi chao wanaonyesha uwanjani, vilabu zaidi ya 10 vinaudhamini kuanzia mmoja na zaidi na kama inavyojieleza kuwa vilabu vya Simba SC na Yanga SC ndiyo vilabu vyenye “Engagement” kubwa zaidi kuliko vilabu vyote nchini na hiyo imetokana na ukubwa wao kuanzia majina ya wachezaji wanaowamiliki na hata wafuasi wake pia kuwa wengi kuliko vilabu vyote nchini.

    Ila usichokijua ni kuwa vilabu hivyo vimepitwa na klabu ya Singida Fountain Gate FC kuwa na wadhamini wengi kuliko wakubwa hao kutokana na ilo hii ndiyo orodha ya vilabu vyenye wadhamini wengi Ligi kuu ya NBC.

     

    1.Singida Fountain Gate Fc

    Makazi yake rasmi yalikuwa mkoani Singida kama jina lake linavyosomeka ila kwa sasa imebadilisha na kuwa inapatikana Mwanza. Hii ndiyo klabu yenye wadhamini wengi Ligi kuu ya NBC ikiwa na jumla ya wadhamini 9 wengi zaidi kuliko klabu yoyote ile.

    Mdhamini mkuu wa klabu hiyo ni SportPesa huku wadhamini wengine wakiwa ni Haier, Azam TV, Coral Paints, Airtel, Vunjabei, Uhai, Nassco, Precision Air pamoja na Jet&Son ambao ni mdhamini wa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa klabu hiyo.

     

    2.Simba Sc Tanzania

    Kariakoo mtaa wa Msimbazi ndiyo makao rasmi ya klabu hiyo iliyo na zaidi ya miaka 80 tokea kuanzishwa kwake, imefanya makubwa sana nje na nchi na hiyo imefanya kutengeneza jina na kupata wafuasi wengi na wadhamini wakutosha, kwa sasa ina jumla ya wamiliki 8.

    Mdhamini mkuu ni M-bet huku wadhamini wengine wakiwa ni Sandaland The only one ambaye anahusika na Jezi, Azam TV, Air Tanzania, MobiAd, MoXtra, Mo Assuarance pamoja na Pilsner Lager.

     

    3.Yanga Sport Club

    Ikiwa na miaka 89 tokea kuanzishwa kwake ikiwa maskani yake ni Dar es Salaam mitaa ya Jangwani ikiwa na jumla ya wadhamini 7 kutoka kampuni mbalimbali.

    Mdhamini mkuu wa klabu hiyo ni SportPesa huku ikiwa na NIC kama mdhamini wa tuzo ya Mchezani bora wa mwezi, Haier, GSM, Azam TV, Hero pamoja na Whizmo kama mdhamini mkuu wa kikosi hicho kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

     

    4.Coastal Union

    Inaweza ikawa imekushangaza ila ndiyo klabu ya nne nchini kuwa na wadhamini wengi ikiwa na jumla ya wadhamini sita (6) ikiwa na maskani yake mkoani Tanga.

    Mdhamini mkuu wa timu hiyo ni kampuni ya Elsewedy Cables huku wadhamini wengine wakiwa ni SleekSingh, Haier, K Security pamoja na Azam TV

     

    5.Namungo Fc

    Haina misimu mingi sana ila ni klabu ambayo kwa muda mfupi tu tokea ipande Ligi kuu ya NBC imefanikiwa kushiriki michuano ya Shirikisho Afrika CAFCC na kufuzu hatua ya makundi ambapi maskani yake ni mkoani Lindi ikiwa na jumla ya wadhamini watano (5) tu.

    Mdhamini mkuu wa timu hiyo ni SportPesa huku ikiwa na wadhamini wengine ambao ni Azam TV, Coral Paints, Haier, Lodhia Industries pamoja na Swahili wote.

    Hivyo ndivyo vilabu vyenye wadhamini wengi ndani ya Ligi kuu ya NBC ambapo masikio ya wengi ilikuwa ni ngumu kudhania kuwa Singida Fountain Gate FC ana wadhamini wengi kuliko Simba SC na Yanga SC ila tofauti kubwa ni kuwa Wadhamini wengi wanaoingia mkataba wa kuvidhamini vilabu hivyo wamekuwa wakisaini mikataba yenye thamani kubwa kuliko mikataba ambayo inasainiwa na wengine na hiyo ndiyo tofauti pekee tu, dhamani ya Simba SC na Yanga SC imebebwa na jina na ukubwa wao huku pia na ushiriki wao kwenye michuano ya Afrika.

    SOMA ZAIDI: Ni Mwaka Wao Watachukua Tuzo Nyingi Sana Msimu Huu

    ligi kuu ligi kuu tanzania bara

    1 Comment

    1. Pingback: Azam FC Mmetengeneza Ugonjwa Utakaosumbua Ligi Kuu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.