Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba Waliichukulia Poa Prisons Wameadabishwa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Simba Waliichukulia Poa Prisons Wameadabishwa

    Living ShayoBy Living ShayoMarch 6, 20241 Comment4 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Simba vs Tanzania Prisons
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilikuwa ni vita Ya kimbinu kwa timu zote mbili Simba SC wakiingia kwa kufunguka zaidi na Tanzania Prisons pia nao wakifanya hivyo huku Simba SC wakiamua kuanzia kutoka nyuma kwenda mbele kwa pasi fupi fupi kitu ambacho kilikuwa tofauti kwa Tanzania Prisons ambao wao waliamua zaidi kupiga pasi ndefu pale wanapokaribia eneo la kati.

    Kipindi cha kwanza timu zote zilitengeneza nafasi kadhaa hususa Simba SC ila namna walivyokuwa wanazuia Tanzania Prisons ilitoa nafasi finyu kwa Simba SC kuwa huru eneo la lango lao na mipira mingi kuwa inapotea inatoka nje au kipa kuidaka. Simba SC wakiwa wanashambulia walikosa mtu ambaye Angekuwa anakutana na mipira yote Ya pili “Second ball” inayookolewa na Tanzania Prisons hivyo mipira mingi iliyokuwa inaokolewa ilikuwa unakutana na wachezaji wa Tanzania Prisons na wanaiondoa kwa urahisi.

    Wakati wanashambuliwa Prisons waliamua kumuacha Samson Mbangula pekee yake eneo la kati la uwanja huku Zabona Hamis Mayombya akitokea pembeni upande wa kulia na Joshua Nyantini akitokea kushoto kitu ambacho kiliwafanya kumiliki mpira na kumsubiri Mussa Haji ambaye mara nyingi alikuwa akipokea mipira ya pili baada ya kuokoa na kuisambaza kushoto kulia au kupita kati kati ya uwanja kutengeneza shambulizi Mara kadhaa walikuwa wanashinda kutokana na eneo la beki wa kati la Simba SC kutotulia na kuacha nafasi “gap” kubwa baina Ya Henock Inonga na Kennedy Juma na hiyo imesababishwa na wachezaji hao kuwa wanafuata mpira na kuacha nafasi kubwa kiufupi hapakuwa na utulivu mkubwa.

    Goli la kwanza la Prisons ilitokana na kushindwa kurudi mapema kwa wachezaji wa Simba SC lakini pia ni uhodari mkubwa kwao kutumia nafasi hiyo, mkimbio “movement” ya goli ilo inaonyesha kiasi gani Prisons waliisoma Simba SC ikiwa inashambulia ndiyo maana baada Ya kuondosha hatari goli kwao ilikuwa rahisi kuwashinda “kuwawin” Simba kwa kuwa na mpambano wa wachezaji wawili kwa wawili kwa timu zote Samson Mbangula na Zabona Hamis dhidi Ya Babaca Sarr na Kennedy Juma na kasi ya Mbangula Samson ilisaidia zaidi kupata goli japokuwa kuna uzembe ambao kama golikipa Aish Manula alipaswa kutoka golini kusaidia kupunguza goli na hata Mbangula aliposhindwa kukokota mpira vizuri ingekuwa rahisi kwake kuokoa kwa kuudak au kuutoa.

    Kipindi cha pili ilikuwa ni vita Ya mipira mirefu kwa timu zote mbili huku Simba SC wakishambulia zaidi kutokea pembeni kuingia ndani huku Tanzania Prisons wakitumia “Caunter Attack” kupitia pembeni na pale wanapoweka mpira chini walikuwa wanajaa wengi kwenye nusu Ya Simba SC na kuwapa presha wachezaji wa Simba SC kitu ambacho kilisababisha goli la pili na Prisons walikuwa wakifurahia kuokoa “transition” za Simba na kumiliki mpira.

    Baada Ya goli la pili Prisons walibadilika kiuchezaji na kubaki eneo Lao zaidi na kitendo cha kumtoa Samson Mbangula iliwapa uhuru zaidi Simba SC kutulia na mpira na kutengeneza nafasi kwa wachezaji wao kukimbia kuelekea kwenye lango la Prisons na ndiyo maana walikuwa langoni mwa Prison kwa muda mrefu na mipira mingi waliyokuwa wakiokoa ilikuwa ikiangukia kwa Clatous Chama na Fabrice Ngoma, ugumu kwa wao kufunga ulikuwepo pale wakikaribia lango la Prisons wachezaji wengi walikuwa walikuwa wamejaa kwenye 18 yao ndani Ya box wakiwa watano na wengine wakiwa nje Ya box lao jambo ambalo mipira mingi waliweza kuikoa.

    Mabadiliko ya Edwin Balua yalisababisha kuharibu eneo la mbele la Prison kwani muda mwingi alikuwa akicheza mbele ya goli la Prison na kumpa nafasi Chama Clatous kugawanya mipira pembeni kwa Ntibazonkiza na Ladack Chasambi wakibadilishana na Shomari Kapombe upande wa kulia na Israel Mwenda huku akisaidiana na Fabrice Ngoma kupiga krosi kutokea upande wa kushoto na wakifanikiwa zaidi kwenye ilo kilichobaki ni kuingiza mpira nyavuni tu.

    Pongezi ni kwa Kocha wa Prisons Amada Ally na benchi zima kwa kuweza kuisoma vizuri Simba SC na wachezaji wao kutumia nafasi chache zilizopatikana, kiufupi Simba SC hawakuwa vizuri eneo Lao la ulinzi na makosa mengi yalikuwa yakitokea hapo na hata magoli yote ni uzembe kushindwa kunusa hatari hususa goli la pili walilofungwa.

    SOMA ZAIDI: Dondoo Na Takwimu Zote Simba Dhidi Ya Tanzania Prisons

    kikosi cha simba simba vs prisons uchambuzi simba vs prisons

    1 Comment

    1. Pingback: Azam na Simba Inawarahisishia Yanga Kuchukua Tena Ubingwa? - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.