Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba Ni Daraja La Makocha Kupata Umaarufu?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Simba Ni Daraja La Makocha Kupata Umaarufu?

    Living ShayoBy Living ShayoJuly 22, 2024Updated:July 22, 20247 Comments3 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Kocha mpya wa klabu ya Simba Fadlu Davids
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Moja ya makocha ambao watakumbukwa sana ndani ya Simba SC kwa miaka ya karibuni basi ni Patrick Aussems “Uchebe” pamoja na Sven, kumbukumbu bora ua mafanikio ya Simba SC ilitengenezwa na Aussems huku Sven akimalizia msimu bora wa mataji na mpira safi wa kuburudisha.

    Aliacha kikosi cha Simba SC kikiwa na furaha ya ushindi wa goli 4-0 dhidi ya FC Platinum na kiwango bora sana kwa kikosi cha timu hiyo ambacho mpaka leo hakijawahi kutokea wala kuonekana tena, namna wachezaji walivyocheza muunganiko bora wa kikosi kuanzia goli, eneo la ulinzi, kiungo mpaka ushambuliaji.

    Sven aliitengeneza timu ambayo ilikuwa ikicheza kwa muunganiko na kila mchezaji akifanya majukumu yake kwa usahihi, alitengeneza kikosi ambacho kilikuwa ngumu kuruhusu goli kirahisi na hiyo ilimpa jina kubwa sana nchini.

    Licha ya kufanya hayo hakudumu na kikosi cha timu hiyo kwa muda mrefu na hiyo inatupeleka hadi kwenye wasifu wake ambao hautofautiani sana na kocha mpya wa sasa wa Simba SC kwani wakati Sven anaajiriwa Simba SC kama Kocha mkuu alikotoka kote baada ya kuacha kucheza mpira alikuwa Kocha msaidizi ambayo hata Fadlu wa sasa naye ni hivuo hivyo.

    Sven alizaliwa Belgium na alikuwa na Leseni ya “Uefa Pro Licence” ambayo ilimuwezesha kufundisha soka eneo lolote duniani,baada ya kutamatisha safari yake ya uchezaji mwaka 2010 aligeukia kwenye ukocha na mwaka 2014 alikuwa msaidizi kwenye kikosi cha Niko Volou hadi 2018 aliendelea kuwa msaidizi kwenye timu kadhaa na alifanikiwa kuchukua ubingwa wa AFCON na kikosi cha Cameroon kabla ya kutangazwa na Simba SC na alikuwa muumini wa mfumo wa 4-2-3-1.

    Kwa upande wa Fadlu Davids alianza kucheza soka na 2012 aliacha kusakata kabumbu na kuamia kwenye ukocha ambapo mwaka alianza kuwa kocha msaidizi wa Maritzburg akipita vilabu vingine vingi kama msaidizi na mwaka 2023/2024 alikuwa Kocha msaidizi wa kikosi cha Raja Casablanca ambacho walichukua nayo ubingwa wa Ligi kuu Morocco na baada ya hapo alitangazwa kuwa Kocha mkuu wa kikosi cha Dimba SC huku pia nawe akipendelea zaidi mfumo wa 4-2-3-1.

    Safari yake na Sven Vandenbroeck haina tofauti kubwa sana na wote wanatangazwa kuwa makocha wa Simba SC huku wakiwa hawana jina kubwa kwenye uoande wa Soka Barani Afrika, kumbukumbu nzuri kwa upande wa Sven ni kuwa baada ya kuachana na timu hiyo alifundisha vilabu kadhaa vikubwa Afrika FAR Rabat, CR Belouzdad, Wydad AC na sasa ni Kocha mkuu wa timu ya Zulte Waregem inayoshiriki Ligi kuu ya Ubelgiji.

    Ni wakati sasa kusubiri kuona aliyofanya Sven Vandenbroeck na Simba SC na Fadlu Davids akiyafanya na baada ya hapo kuwa Kocha mkubwa barani Afrika na kupelekea kupata nafasi ya kufundisha vilabu vikubwa, jibu pekee ni swala la muda kusubiri utudhihirishie ilo na kutujibia swali letu Simba SC ni daraja kwa makocha kuoata umaarufu?

    SOMA ZAIDI: Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    simba sc leo simba sc tanzania

    7 Comments

    1. Thabit Njapuka on July 22, 2024 10:48 am

      Mimi nasoma tu komenti

      Reply
    2. Valence on July 22, 2024 10:50 am

      Umaarufu gani tena mbona ghafla hv?

      Reply
    3. Beca Daud on July 22, 2024 10:52 am

      Tuna Imani na Fadlu..ubaya ubwela 🔥🔥
      #simba tz
      #Nguvu moja

      Reply
    4. Kicc on July 22, 2024 11:32 am

      umaarufu kwamba iyo ni Madrid🤨

      Reply
    5. Michael on July 22, 2024 1:57 pm

      Yote maisha! Huo wote ni mtazamo wa peg hii

      Reply
    6. King on July 22, 2024 3:33 pm

      Nyui wahuni waongo sana mnasema eti mikeka ni ya kweli kumbe hola mnataka kutupiga ela zetu sio poa wazeee afu mnasema kiniwr kina ongea hamna lolote kama mtu binafsi naweza suka mikeka inayo eleweka bora mbaki na mikeka yenu tuu

      Reply
      • Mhariri on July 23, 2024 12:39 pm

        Habari Mwana Kijiweni… Sisi tunaweka mategemeo ya mkeka na wala hatutoi codes bali tunaweka Tips za jinsi unaweza suka mkeka wako na una uhuru wa kubadilisha kwa kile ambacho sisi tunakua tumepost kwenye MKEKA WA LEO endelea kuwa Kijiweni kwani hapa Mtaa Unaongea

        Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.