Ilipoishia Sehemu Ya Pili
“Kazi imeisha!” Alisema Diana kwa njia ya simu
“Waoo Good Girl ( Vizuri Msichana mzuri ) ” ilisikika sauti nzito ya kizee
“Rudi Tanzania” Alimalizia kusema Mwanaume huyo kwa njia ya simu, simu hiyo ilikatika, tayali polisi walishafika nje ya Hoteli hiyo, Diana alichofanya ni kuingia kwenye chemba ya maji machafu akaenda kutokea mbali na eneo hilo. Endelea
SEHEMU YA TATU
Tayali ilifahamika ni wapi ambapo Faudhia angepatikana ni mpaka wa Namanga, ilihitaji auawe kabla hajafika Tanzania.
Mishale ya saa 11 Alfajiri vijana wa Khalid Bangala walijaribu kumtafuta Bosi wao bila mafanikio, hawakujuwa wafanye nini sababu maelekezo yote walikuwa wakipewa na Bosi wao ambaye alikuwa ameshauawa Hotelini, majadiliano yao yalimuamsha Faudhia akiwa ndani ya Sanduku.
“Unafikiri tutafanya nini, Simu ya Khalid haipatikani, tufanyaje na tunakaribia eneo lenye askari” Alisema mmoja wa Vijana hao, Faudhia aliposikia hivi alihisi kuna hatari, kutokana na mafunzo aliyoyapitia aligundua pengine kuna jambo halipo sawa, aligonga afunguliwe huku akisema amebanwa sana na Haja. Vijana hao walisimamisha gari hilo, walikuwa juu ya mlima, kulikuwa kunapambazuka na iliwahitaji kutembea chini ya Kilometa 15 kufika Mpakani. Faudhia hakutaka kujionesha kuwa amehisi jambo lisilo la kawaida, hakutaka kuwaamini moja kwa moja, walikuwa na bunduki ambazo walizificha, mmoja alimsindikiza Faudhia kujisaidia huku akiwa amemshikilia Bunduki kwasababu alikuwa bado hajawalipa
“Pale ni wapi?” Alihoji Faudhia akiwa anazidi kusogea sehemu ya kujisaidia
“Longido” alijibu Mwanaume huyo
“Unamaanisha Tanzania?”
“Ndio, unapaswa kutulipa kwanza sababu umeshafika eneo husika ambalo sisi hatuwezi kusogea huko, kuna ulinzi wa Askari wa mpakani.” Alisema Mwanume huyo
“Simama hapo basi au unataka kunichungulia!” Aliuliza Faudhia na kumfanya Mwanaume huyo asimame lakini akiwa anamuonesha Bunduki Faudhia ambaye alikuwa tayali ameashaanza kujisaidia.
Akiwa anajisaidia alisikia milio ya Risasi za haraka kisha ukimya ulitanda, yule aliyemsindikiza alirudi kule haraka akakuta wenzake tayari wameuawa, lilikuwepo kundi la watu tano ambalo lilitokea msituni na kumtaka Mwanaume huyo anyanyue mikono yake juu. Wanaume hao walikuwa wakiongea rafudhi ya Kenya, haraka Faudhia alifungua kibegi chake kidogo akatoa bastola yake, ukimya ulitawala, Faudhia alijaribu kuchungulia eneo la tukio ndipo alipowaona Wanaume hao, haraka alizama kwenye kichaka
“Msichana yupo wapi?” Alihoji mmoja wa Watu hao huku akiwa amenyooshea bastola yule kijana wa Khalid aliyebakia, yule Mwanaume hakuwa na chaguo ilibidi aoneshe mahali ambapo Faudhia alikuwa ameingia kwa ajili ya kujisaidia, alipigwa risasi yule Mwanaume kisha lile kundi liliongoza mahali ambapo Faudhia alikuwa ameingia, ilikuwa inakaribia saa 12 asubuhi, kulishaanza kupambazuka.
Faudhia alishajuwa hali ya hatari ilikuwa imenukia eneo hilo, alichofanya ni kuanza kukimbia kuelekea mpaka wa Namanga upande wa kaskazini ambako ndipo ilipo Wilaya ya Longido, alikuwa na maelekezo maalum ya eneo gani anapaswa kupita ambalo litakuwa salama lakini kutokana na milio ya Risasi kusikika iliwashtua askari wa mpakani wakatoka kwa ajili ya kuangalia kulikuwa na tatizo gani.
“Yule pale” Alisema kiongozi wa kundi hilo la Watu watano, walipewa amri ya kumuuwa Faudhia kutoka kwa Mtu ambaye hakujulikana hadi kufikia wakati huo, ila Faudhia alijuwa ni kwanini Watu hao walikuwa wakimfuatilia ila hakujua wametumwa na nani.
Milio ya Risasi iliendelea kurindima msituni hapo, Faudhia alijitahidi kukimbia ili kuokoa Maisha yake. Ulikuwa ni mtafutano wa zaidi ya dakika 10 bila mafanikio kwa Wanaume wa kundi hilo kumpata Faudhia ambaye alishahitimu mafunzo ya ujasusi huko Mexico, Faudhia alifuata maelekezo maalum ili aonane na Mtu mwenye gari msituni hapo, bahati mbaya akiwa anakaribia alikutana na Askari wa mpakani ambao walikuwa wakifuatilia milio ya Risasi, Faudhia alisimama kwa sekunde kadhaa huku akiwa anatazama na Askari hao ambao walikuwa mbele yake Mita kadhaa tuu kutokea aliposimama, pumzi za Faudhia zilimwambia kuwa hatuna jinsi bali kufa au kujikamatisha mikononi mwa Askari hao.
“Weka silaha yako chini” Alisema mmoja wa Askari hao, Kila hesabu aliyokuwa anaipiga Faudhia haikumpa jibu linalotakiwa, alijikuta akijisalimisha mwenyewe, Askari walianza kusogea taratibu kwa makini sana eneo ambalo Faudhia alikuwa amesimama, wale wanaume wa kundi la Kigaidi hawakujua kuwa Faudhia alikuwa amesimama mbele ya kundi la Askari polisi, walitokea eneo hilo na kushtukizwa na askari polisi kisha mashambulizi ya Risasi yalianza kusikika huku haraka Faudhia akichumpa na kujitupa kwenye poromoko dogo, Milio ya Risasi iliendelea kusikika lakini haikufamfanya Faudhia asimame wala arudi nyuma, alizidi kusonga mbele hadi alipofika mpaka wa Namanga, alivuka na kuingia Tanzania.
Mashambulizi baina ya Askari polisi wa mpakani na Lile kundi yaliendelea na kumpa uhuru Faudhia kukutana na Mtu aliyepangiwa kukutana naye mpakani hapo
“Ingia kwenye gari haraka tuondoke eneo hili” alisema Mwanaume mmoja ambaye ndiye aliyetakiwa kumchukua Faudhia mpakani na kumfikisha Arusha Mjini, Faudhia aliingia ndani ya gari na safari ilianza kuelekea Arusha Mjini.
•••••••••••••••••••••••••••••••••
Jeshi la polisi liliizunguka Benki kuu ( B.O.T ) ili kuhakikisha hakuna anayetoka humo benki, ndani ya Benki hiyo alikuwepo Mtu hatari aliyeitwa Chogo, tayari alikuwa amemteka Mke wa Gavana na Gavana mwenyewe ambao wote walikutwa ndani ya Benki hiyo, nje ya Benki zilionekana maiti za Askari kadhaa ambao walikuwa wakitaka kufanya jaribio la kushambuliana na Magaidi hao ambao walionekana kuzungumza kiswahili kizuri, ilikuwa ni mishale ya saa 1 asubuhi jua lilikuwa likichomoza, ukimya uliendelea kutawala na hakukuwa na Raia aliyekuwa akifanya safari. Muda huo huo Mzee Shayo aliwasili akiwa na gari yake, alikutana na Mkuu wa operesheni hiyo aliyeitwa Sir Jeff, waliitana chemba kwa ajili ya mazungumzo, wote walionekana kuanza kukata tamaa kwa jinsi Magaidi hao walivyokuwa na mbinu kali za kukabiliana na Askari.
“Niambie mpango unaendaje?” Aliuliza Mzee Shayo huku akitazama saa yake
“Gavana na Mke wake wameshikiliwa ndani ya Benki” alijibu Sir Jeff akiwa anamtazama Mzee Shayo
“Hawajasema wanataka nini?” Aliuliza tena Mzee Shayo
“Hakuna hata mmoja aliyezungumza hadi hivi sasa zaidi ya ishara tu kupitia kioo kikubwa”
“Shenzi sana!!” alisema Mzee Shayo, punde simu yake iliita, alipoangalia aliona ni Faudhia alikuwa akimpigia kwa njia ya Whatssap, alisogea pembeni kuipokea sababu hakutaka kunshirikisha yeyote juu ya Ujio wa Faudhia
“Baba!! Nipo Arusha” Alisema Faudhia, hivi ndivyo ambavyo Faudhia alikuwa akimchukulia Mzee Shayo, alimchukulia kama Baba yake mzazi baada ya kumsaidia kumtoa kwenye mikono hatari ya Mzee Shomari miaka mingi iliyopita
“Sawa Faudhia! Nakutumia picha, nataka uchunguze huyo Mtu anafahamika vipi hapo Arusha, ndiye mshukiwa namba Moja wa tukio hili la Ugaidi” Alisema Mzee Shayo kisha alimtumia picha Faudhia, ilikuwa ni picha ya Martin Gimbo ambaye alijitambulisha kwa askari kama Chogo. Mara moja Faudhia alianza kazi ndani ya Jiji la Arusha. Mfumo wa serikali ulishawekwa kwenye kiganja cha Faudhia, alitumia kompyuta mpakato ambayo alitumiwa na Mzee Shayo kupitia jamaa aliyemchukua pale Mpakani, kompyuta hiyo ilikuwa na mawasiliano na Kitengo cha Usalama wa Taifa, muda huo Faudhia alikuwa Hotelini akiifanya kazi hiyo
Aliingiza picha kwenye mtandao wa Idara ya Usalama wa Taifa, alimuona jamaa huyo aliyeitwa Martin Gimbo. Taarifa za Jamaa huyo zilionesha kuwa alizaliwa Arusha Mjini, aliona ni wapi alisoma hivyo ilikuwa ni kazi rahisi kwa Faudhia, jua lilikuwa limeshaweka makazi katika anga kwa ajili ya kuimulika Dunia, Faudhia aliutumia usafiri wa gari waliyotoka nayo mpakani akiwa na jamaa aliyeitwa Mohd, walienda kwenye shule ambayo waliona kuwa Martin Gimbo alisoma, bahati nzuri ilikuwa ni siku ya Shule, waliingia hadi ofisi ya Mwalimu Mkuu, walienda shule ya Sekondari ambapo waliamini taarifa za Martin zingepatikana.
Walikaribishwa na Mwalimu mkuu wa shule hiyo ambaye muda mchache baadaye aliketi kuwasikiliza huku akionekana kuzishangaa sura za akina Faudhia
“Naitwa Undercover Mohd kutoka kitengo cha Usalama wa Taifa” alijitambulisha yule jamaa huku Faudhia akiwa kimya, Mohd alitoa kitambulisho ili kumuaminisha Mwalimu huyo ambaye alikuwa akitetemeka kutokana na woga sababu taarifa za ugaidi zilizizima katika Miji mikuu ya Dodoma na Dar-es-salaam. Baada ya kujiridhisha Mwalimu huyo alishusha pumzi zake kisha aliondoa mawani
“Haikuwa rahisi kuwaamini sababu Wanafunzi na Waalimu wameanza kukimbia Mji huu kwasababu ya uvumi kuwa baada ya Dodoma na Dar utafuata Mji huu kuwa chini ya Magaidi” alisema Mwalimu huyo kisha alishushia maji yaliyo ndani ya chupa, alionekana kuwa na mengi ya kusema, alinyanyuka na kwenda kufunga mlango kisha ndani kukawa giza aliwasha taa
“Niwasaidie nini vijana?” Aliuliza Mwalimu huyo ambaye alikuwa na mvi kiasi kuashiria kuwa umri wake ulikuwa umeenda. Faudhia alitoa picha ya Chogo akamuonesha Mwalimu huyo, Mwalimu aliichukua picha hiyo kisha aliisogeza kwenye Mwanga, alishtuka baada ya kumuona chogo kisha alimpatia picha Faudhia
“Unamfahamu huyo Mtu?” Alihoji Mohd
“Hapana” Alijibu Mwalimu baada ya kukaa kimya kwa sekunde kadhaa
“Mwalimu, ukweli wako utaliweka Taifa hili huru. Sura yako inaonesha unamfahamu, tuambie anaishi wapi na unamfahamu vipi?” Alidakia Faudhia
“Nimesema simjui mnanilazimisha ili iweje? Simjui huyo Mtu hebu nendeni” alisema Mwalimu kwa hasira huku akifoka mithiri ya chatu aliyejeruhiwa
“Unamjuwa huyu Mtu ndio maana unajaribu kuficha, Mwalimu tuambie huyu Mtu anaishi wapi na unamfahamu vipi?” Alisema Mohd kwa sauti iliyokauka
“Nimesema simjui, hebu ondokeni ofisini kwangu haraka sana” Alisema Mwalimu kwa sauti ile ile huku akinyanyuka kitini mfano wa Mtu aliyetaka kuondoka ofisini hapo, Faudhia alichomoa bastola na kumuonesha Mwalimu huyo.
Bastola ilimfanya Mwalimu anywee kidogo
“Endapo utaendelea kukanusha nitapasua ubongo wako sasa hivi, unamjuwa huyu Mtu anaitwa Martin Gimbo. Alisoma hapa kwa miaka minne” Alisema Faudhia akiwa amemshikilia Bastola Mwalimu,
“Sisi siyo Watu wabaya ila unatulazimisha kufanya huo ubaya, kama hutaki kusema hebu tupatie faili la Martin” Alisema Mohd
Mwalimu hakuwa na neno jasho lilikuwa likimtiririka, alivuta droo la meza alitoa faili lenye maelezo yanayomuhusu Martin Gimbo, Faudhia alipolifunua Faili hilo, halikuwa na picha ya
Martin, halikuwa na maelezo kuwa Martin alikuwa akiishi sehemu gani
“Taarifa zimeenda wapi?” Alihoji Faudhia
“Msijaribu kulifuatilia hilo jambo, hamtafanikiwa nawaambia, mtakufa kabla ya kujuwa chochote kile” Alisema Mwalimu huyo
“Ona hii” Alisema Mohd baada ya kuangalia kwa makini waliona namba ya simu nyuma ya faili hilo, ilibidi walichukue faili hilo, Mohd alichukua bastola na kumpiga mwalimu huyo.
“Kwanini unauwa?” Alihoji Faudhia
“Hana faida yoyote” Alisema Mohd
“Tuondoke haraka sana” Aliongeza Mohd kisha waliingia ndani ya gari na kutoweka eneo hilo, wakiwa ndani ya gari waliipiga namba hiyo, ilipokelewa na Mwanamke mwenye sauti dhaifu sana, ilionekana alikuwa mgonjwa maana alikuwa akikohoa sana
Faudhia aliutumia ujanja wa mafunzo yake, walielekezwa alipo mpokeaji wa simu hiyo, walienda kuonana naye lakini njiani Faudhia alijiuliza Kwanini Mohd alimuuwa Mwalimu Mkuu baada ya kuyatamka maneno yale? Hakutaka kuyapa kipaumbele, walisogea hadi eneo husika, walikutana na Mama mmoja dhaifu sana wa mwili wake, alikuwa akiishi na Mjukuu wake wa miaka 16
Walimsalimia Mama huyo kisha walimuuliza
“Hapa ni nyumbani kwa Martin Gimbo?” Alipouliza hivi huyo Mama alipata nguvu hata ya kukaa, Mjukuu wake alishangaa sana kwa Mama huyo kuketi mwenyewe wakati mara zote alikuwa akimsaidia kukaa, Mama huyo alikaa kimya sana
“Je? Wewe ni Mama yake Martin?” Alihoji Faudhia, Mama huyo aliwatazama kisha aliwauliza
“Mnamuulizia Martin Gimbo?” Aliuliza kama vile Mtu aliyetaka kupata uthibitisho wa alichokisikia
“Ndio, Martin Gimbo, unamfahamu?” Alihoji Mohd
“Ndio, ni Mwanangu! Miaka mingi sasa tangia Martin alipofariki kwa ajali ya gari akiwa anaelekea Mjini, tangu siku hiyo sikuwahi kuamka na kukaa tena hata ongea yangu ilikuwa ya shida, Martin alikuwa ndiyo Mwanangu wa pekee niliyempenda, tumaini la Maisha yangu lilikuwa kwa Kijana wangu Martin baada ya Baba yake kufukiwa na kifusi huko Merelani akiwa anafanya kazi za mgodi” Alisema Mama huyo, kisha alimuomba Mjukuu wake amsindikize mahali.
“Nifuateni” Alisema Mama huyo ambaye alijitambulisha kama Mama yake Martin Gimbo ambaye alikuwa akitajwa kama gaidi kiongozi wa kundi la ESS .
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NNE
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
16 Comments
https://shorturl.fm/m8ueY
Hii Ik0 0n 🔥
Noma sana
Inakuja Kwa Wakati Saana Jamani Hadi Raha Ahsante Admn
Wanaenda kufanywa nn… Kama ye ndo mkuu wa kitengo 🙆🏽♂️🙆🏽♂️🙆🏽♂️🥱🥱
Tupe nyingine admin
Nzuri sana Admin
Hii ya Moto Sana Admin
Mama anajambo lake,🤓 admin tunahitaji mwendelezo kwa wakati tafadhal,,,simulizi nzuri sana👍
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/TbTre
https://shorturl.fm/9fnIC
https://shorturl.fm/6539m
https://shorturl.fm/xlGWd
https://shorturl.fm/f4TEQ
https://shorturl.fm/nqe5E