Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nne
“Na siku zote Muuwaji hawezi kuishi, ndiyo maana nilikutoa gerezani ili uje kuitafuta haki iliyoporwa na Faudhia” Alikazia Mzee Shomari kisha alimruhusu Diana kuelekea ndani ya Benki, mpango wa Mzee Shomari ulikuwa ni Kumuuwa Faudhia, kisha kuiba pesa za kimarekani ambazo zilihifadhiwa ndani ya Benki hiyo katika chemba ya siri, ilikuwa ni zaidi ya Dola Bilioni 900 , alimtumia Chogo kama ngao ya kufanya mambo yake huku akiweka ubia na rafiki yake wa zamani ambaye alikuwa akiishi Uholanzi, ndiye aliyemtoa jela na kumfadhili pesa za kufanya ugaidi Tanzania, hivyo Mzee Shomari alikuwa ndiye Gaidi aliyekuwa akiratibu mipango yote, alikusanya vijana na kuwapatia silaha nzito, akiwemo Diana na Martin Gimbo maarufu kama Chogo
Jinsi alivyowapata Diana na Chogo utakuja kufahamu mbele, hebu tosonge..
Usiku ulikuwa umeingia, ndani ya Jiji la Arusha, Faudhia alikuwa akimlaumu Mohd kwa kosa la Kumuuwa Mama yake na Martin Gimbo.
SEHEMU YA TANO
“Hakukuwa na sababu ya kuuwa Watu wasio na hatia Mohd, umeuwa Mwalimu, umeuwa Bibi na Mjukuu wake” Alisema Faudhia kwa hasira sana
“Unanilaumu kwa kutekeleza mipango yangu ya kazi? Unanilaumu kwa kusafiaha ushahidi wa mwote tulimopita? Faudhia wewe siyo Mfanyakazi wa kanisa au msikiti, wewe ni askari wa siri wa kitengo cha Usalama wa Taifa! Sisi tunauwa kwa ajili ya Taifa” Alijitetea Mohd
“Unauwa kwa ajili ya usalama wa Taifa? Taifa lipi? Kuuwa Watu wasio na hatia ndio majukumu ya Usalama wa Taifa? Pengine umeelewa vibaya mafunzo uliyoyapata, siwezi kuendelea kufanya kazi na wewe Mohd” Alisema Faudhia kisha alipiga simu kwa Mzee Shayo akamwambia ambadilishie Mtu wa kufanya naye kazi
“Kwanini unataka abadilishwe?” Alihoji Mzee Shayo kwa njia ya simu
“Sijisikii uhuru wa kuifanya kazi yangu” Alisema Faudhia huku akiwa anamtazama Mohd ambaye alikuwa na hasira sana akiwa ameketi kwenye kiti
“Faudhia Mwanangu..” kabla hata hajamaliza alikatiswa na Faudhia
“Baba nimesema nibadilishie huyu Mtu” Alisema kwa hasira na sauti ya juu kuonesha msisitizo kuwa alikuwa akimaanisha alichokisema na hakikuwa utani.
“Mpe simu Mohd,” mara moja Mohd alipewa simu na Faudhia, kabla hajaongea na Mzee Shayo alimtazma sana kwa hasira Faudhia.
“Natoa amri ya wewe kurudi Makao Makuu haraka sana” Alisema Mzee Shayo
“Lakini Mkuu..” kabla Mohd hajamaliza kujitetea alikatishwa na Mzee Shayo
“Hakuna cha Lakini Mohd, rudi Makao makuu” Alisistiza Mzee Shayo, mara moja Mohd alimtupia simu Faudhia kisha alichukua koti lake akatoka chumbani hapo lakini kwa bahati mbaya alikuwa amesahau simu yake ambayo ilikuwa kwenye kochi, kitendo cha Mohd kutoka ndani ya chumba hicho, simu yake ilianza kuita, Faudhia alinyanyuka na kuangalia aliyekuwa akipiga
Aliona namba imeandikwa Boss, alifikiria afanye kitu gani aipokee au aiache iendelee kuita hadi ikate, aliichukua na kuchungulia dirishani, alimuona Mohd akilielekea gari lake kwa ajili ya kuondoka, aliona ni bora aipokee simu hiyo sababu alimtilia sana Mashaka kuwa huenda akawa sio Mtu mzuri kutokana na mauwaji ya Watu wasio na hatia ambayo alikuwa akiyafanya.
“Mohd! Muuwe Faudhia sasa hivi kisha urudi hapa” Ilisikika sauti ambayo Faudhia aliitambua, ilikuwa ni sauti ya kizee ya Mzee Shomari, mara moja aligundua kuwa Mohd alikuwa ni askari aliyekuwa akifanya kazi na magaidi, akatambuwa kuwa kilichobakia kwake ni kifo pekee. Alipochungulia tena alimuona Mohd akiwa anapiga hatua kurudi ndani baada ya kugundua kuwa amesahau simu yake, Faudhia alimtazama vizuri Mohd akiwa bado amesimama pale pale, Mohd alikifikia kitasa cha mlango bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa amemshtukia kuwa ni Mamluki anayekisaliti kitengo cha Usalama wa Taifa.
Alipofungua mlango alimkuta Faudhia akiwa amesimama, Unajuwa Mohd alikuwa ni askari wa kitengo cha Usalama wa Taifa hivyo alipoingia tu aligundua kuwa kuna jambo ambalo halikuwa sawa, alimtazama sana Faudhia akiwa ameganda pale mlangoni, walikutanisha macho yao ya Kijasusi huku kila mmoja akiwa anamsoma mwenzake.
Mara simu ya Mohd iliita tena na mpigaji alikuwa ni yule yule Mzee Shomari, aliisikilizia kidogo kisha aliifuata simu lakini kabla hajapokea Faudhia alimnyooshea Mohd Bastola
“Tulia hivyo hivyo Msaliti wewe, kumbe wewe ni mamluki unayefanya kazi na Mzee Shomari? Nilikuwa nakutilia mashaka sana Mohd” Alisema Faudhia, Mohd alikuwa amesimama huku simu ikiendelea kuita mkononi mwake
“Isogeze hiyo simu kwangu” Alisema tena Faudhia huku akihakikisha kuwa Mohd hachomoki wala hafanyi ujanja wa aina yoyote ile. Mohd alimtazama Faudhia kisha alimsoma jinsi alivyokuwa amesimama ila Faudhia alishtuka mapema kuwa Mohd anamsoma kisha akamwambia.
“Ujanja wowote utakaoufanya Mohd napasua kichwa chako” Alisema Faudhia, Mohd aliinama kidogo kisha aliiburuza simu ikafika kwenye miguu ya Faudhia
“Umeanza kutumika upande huo kwa muda gani?” Aliuliza Faudhia huku akizuga ili ainame aichukue simu
“Faudhia! Usifikiri kamwe naweza nikasema chochote au hii siri ikafika makao makuu, katu kitengo hakita ifahamu hii siri” Alisema Mohd kwa kujiamini kisha alishusha mikono yake akamwambia Faudhia
“Si ulikuwa unataka kunitwanga risasi? Fanya hivyo kabla sijakuwahi” Alisema maneno yaliyojaa ulaghai Mkubwa, ilikuwa ngumu kwa Faudhia kumuuwa Mohd, alichotaka ni kufikisha taarifa kwenye kitengo cha Usalama wa Taifa.
Mohd alianza kumsogelea Faudhia taratbu huku akizidi kuongea maneno ambayo yalimchanganya Faudhia
“Wewe ndiyo sababu ya Mama yako kufa, hukustahili kubaki hai kwa uchafu ambao ulikuwa ukimfanyia Mama yako, laiti kama taarifa hizi zitavuja ndani ya kitengo basi hautokuwa na sifa ya kuwa Undercover!! Mtu ambaye amemsaliti Mama yake kwa Baba yake anaweza vipi kutunza siri za Nchi hii” Alisema Mohd huku akizidi kusogea, Maneno ya Mohd yalimtia uchungu sana Faudhia, ni kama alitoneshwa kidonda kilichoanza kukauka
“Acha Mohd! Achaaaaa” Alisema Faudhia kisha aliweka kidole sehemu ya kufyatulia risasi ili ammalize Mohd, haraka Mohd alimuwahi Fadhia na kuushika mkono ambao ulikuwa na Bastola, Faudhia alipofyatua risasi zote zilipiga juu ya dali. Mohd alimkunja Faudhia na kumpa mateke matatu ya Mbavu kabla ya Faudhia kujikunjua
Bastola ilikuwa chini, aliponyanyuka Faudhia alijikuta akiwa mikono mitupu
“Nilikwambia hii siri haiwezi kufika kitengo cha Uslama wa Taifa, kwakuwa nimepigiwa simu nirudi Makao makuu basi wewe utaonekana umeuawa kwa kuvamiwa hapa Hotelini.” Alisema Mohd huku akiwa anakunja Shati lake, alikuwa ni mwanaume mwenye mazoezi na roho ya kikatili sana.
“Mradi wa kukutengeneza wewe uje kuwa Askari wa kitengo unafia hapa rasmi” Alisema Mohd kisha alimfuata Faudhia ambaye alikuwa amejiandaa kukabiliana naye, alirusha ngumi mfululizo ambazo zote Faudhia alizikwepa lakini alifanya ujanja wakati anamaliza kurusha ngumi ya mwisho alikunjua Mguu wa kulia na kumpiga teke la tumbo Faudhia, alijikuta akianguka chini kisha alijinyanyua na kupanga pambano upya.
Wote walikuwa na mafunzo ya Kijeshi hivyo kila mmoja alijuwa namna ya kupambana, Faudhia alijibu mapigo kwa kumpa mateke mawili yaliyofika hadi kwenye kifua cha Mohd, alisogezwa pembeni karibu na mlango ambapo kochi lipo, aliangalia chini kulikuwa na Bastola, pembeni kulikuwa na simu yake yenye siri nzito, aliona ni bora afanye ujanja.
Aliokota mto wa kochi kisha alimtupia Faudhia usomi kisha aliinama ili aichukue bastola lakini Faudhia alikuwa shapu, kabla hajaokota Bastola alipigwa teke la Mgongo kisha Faudhia akaipiga teke ile simu na Bastola vikaingia uvunguni mwa Kochi, alimlazimisha Mohd apambane kwanza.
Mohd aliinuka na kunvaa Faudhia, aliambulia kutupwa chini kutokana na namna Faudhia alivyo Shapu. Kabla hajakaa sawa alipokea ngumi la shingo ambalo lilimsogeza kwenye kochi, kabla hajatulia tena Faudhia alimpelekea Mohd teke ambalo Mohd alilidaka kisha alitumia nguvu kubwa alimsukuma Faudhia ambaye aliangukia kwenye meza
“Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigonga kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumi mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahati mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoni
Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu huku akimwambia
“Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwa anaanguka chini.
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SITA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
11 Comments
Mbona fupi sana jamani
Imeishia patamuu
mbna fupi hvo mzee
Bado mda huko adm, rusha sehemu ya sita. Hii tamu sana kabisa.
Good 👍👍
Admn Ahsante Kwa Story Nzuri Saanaa Hii
Fupi inakera
Fupi innboa sana jmn ….kama utaki acha tu kutuma
Admin hapa umezingua….
Stori ni fupi mnooooo 😯😯😯
Admini hauna vitabu tununue tu
8qqlk0