Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nne 

“Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigonga  kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumi  mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahati  mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoni 

Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu huku  akimwambia 

“Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwa  anaanguka chini. Endelea

SEHEMU YA SITA

Mohd alimsindikiza Faudhia kwa teke kali lililomzimisha  Faudhia, Mohd alitoa kifaa kidogo ambacho kilikuwa na sindano  ya sumu ndani yake, aliitoa kisha alimkita Faudhia eneo la  shingo. 

Baada ya kuhakikisha amemdunga alielekea Kuvuta kochi kisha  aliitafuta simu yake ambayo ndiyo ilikuwa muhimu sana kisha  Bastola yake ambayo ingekuja kuwa ushahidi pale, aliichukua  Bastola na simu kisha aliondoka eneo hilo. 

Sekunde kumi na tano baadaye sindano ya sumu ilianza kufanya  kazi yake, Faudhia alishtuka huku akiwa anateswa na sumu  ambayo ilikuwa ikisambaa kwa kasi mwilini, alijikuta akianza  kuishiwa nguvu, alijivuta kisha alifungua kibegi chake kidogo  alitoa sindano, alivuta dawa haraka kutoka kwenye chupa  kidogo kisha alijidunga sindano akiwa anavuja damu, kisha  alianguka chini na kuzima. 

Usiku huo, Mzee Shomari alikuwa akisubiria simu ya Mohd ili  kumpa taarifa ya kifo cha Faudhia. Alikuwa kwnye kiti cha  walemavu akitembea sebleni ndani ya Jengo la China plaza  jengo ambalo walilifanya kuwa makao yao ya siri walipoanza  kupanga mipango ya Kigaidi, jengo hilo lilikuwa la rafiki  yake aliyeko Uholanzi ambaye ndiye aliyekuwa anafadhili  ugaidi. 

Alianza kukumbuka miaka mingi iliyopita katika Jiji la Mbeya. 

Siku ambayo alikamatwa Baada ya kumuuwa Mama yake Diana,  alimtazama kwa hasira sana Faudhia, alijenga chuki na kisasi  kwa Faudhia. Mzee Shomari alipelekwa Kituo cha polisi,  alipewa mateso makali sana ikiwemo kuwekwa kwenye beseni  lenye maji na kukosa pumzi, alikumbuka jinsi alivyopigwa hadi  kuvunjwa mguu na ndiyo sababu ya yeye kuwa mlamavu ndiyo  maana anatembea kwenye kiti cha walemavu. 

Alipelekwa mahakamani baada ya kupata matibabu ya mguu kisha  alihukumiwa kifungo cha Maisha jela, alipofika huko alikutana  na mzungu aliyeitwa Damian, alijenga urafiki na Mzungu huyo  ambaye alikuwa na kesi ya kusafirisha madini kinyume cha  sheria kutoka Tanzania kwenda Thailand, walishibana wakiwa  gerezani. 

Akiwa anaendelea kuwaza kilichotokea baada ya kufungwa, simu  ya Mzee Shomari iliita alipopokea alisikia sauti ya Mohd  ikimwambia 

“Faudhia ni damu baridi” Alisema akiwa na maana kuwa  ameshamuuwa, Mzee Shomari alishangaa sana kwa jinsi ambavyo  alimuuwa Faudhia kisha alimuuliza

“Upo wapi?” 

“Nipo njiani narudi Dar” Alisema Mohd 

“Tukio lilikuwaje?” Alihoji Mzee Shomari kwa unakini mkubwa  huku akionekana alikuwa mwenye akili sana 

Mohd alimsimulia Mzee Shomari tukio lilivyotokea kisha Mzee  Shomari alisema 

“Ukifika Chalinze utaona kuna prado nyeusi, itumie” Alisema  Mzee Shomari kisha alikata simu. Alisogea na kutazama chini,  aliliona namna jiji la Dar lilivyokuwa likiwaka taa huku  barabara ya kutoka Karume kwenda Kariakoo ikiwa nyeupe hakuna  Mtu wala gari 

Alinyanyua simu yake akapiga simu mahali kisha akasema 

“Case Clossed ( Kesi imeisha ) ” alikata simu akajisukuma na  kuingia kwenye chumba kingine. 

Masaa matano baadaye Mohd alifika Chalinze usiku sana akiwa  na gari yake aina ya Toyota V8, mji ulikuwa kimya kabisa,  alilliona Prado likiwa linawasha hazard kuashiria kuwa  lilikuwa ndiyo gari ambalo Mohd alitakiwa kulitumia, haraka  alishuka na kulielekea gari hilo, alipoingia aliangaza ndani  ya gari hilo ili kuona kama kulikuwa na Mtu lakini gari hilo  halikuwa na Mtu, alivuta funguo na kuiwasha, kitendo cha  kuwasha tu gari hilo lililipuka, Mohd alifia ndani ya gari  hilo, pembezoni kulikuwa na roli, ndani ya Roli kulikuwa na  Mtu ambaye alisikika akiongea na simu akisema 

“Target eliminated ( Mlengwa amemalizwa )” kisha roli hilo  liliwashwa na kueleka Upande wa morogoro. 

Siku iliyofuata, Chogo alipewa kazi na Mzee Shomari ya  kuhakikisha anaifahamu ilipo chemba ya siri ambayo pesa hizo  za Kimarekani zilikuwa zimehifadhiwa, Mtu pekee ambaye  alidhaniwa kuwa anajuwa ilipo alikuwa ni Gavana wa Benki  hiyo. Pesa ambazo akina Chogo walikuwa wanazitaka zilikuwa ni  pesa za siri ambazo Tanzania iliyauzia madini Nchi ya Saudi  Arabia. Chogo alirudi ndani ya chumba ambacho Gavana  alikuwemo na Mke wake, alikuwa ameweka rehani maisha ya mmoja  wa wafanyakazi wa Benki hiyo ili Gavana aseme mahali ambapo  pesa hizo zilikuwa zimehifadhiwa. 

Gavana alimuuliza Chogo amajuwaje kama ndani ya Benki kuna  pesa za siri ambazo zilitokana na mauzo ya madini

“Acha kuuliza maswali ambayo kamwe hutoweza kupata majibu  yake, sema ilipo chemba ya siri vinginevyo namuuwa huyu!!”  Alisema Chogo huku Bastola ikiwa kichwani kwa Mfanyakazi huyo 

Gavana alikaa kimya hakuonekana kumtetea Mfanyakazi asiuawe,  alimtazama Mke wake kisha alirudisha macho kwa chogo. 

“Umejuwaje?” Aliuliza tena kwa mshangao mkubwa sana, Chogo  alionekana kuwa ni Mtu katili mwenye hasira sana, alimpiga  risasi mfanyakazi kisha akamwambia Gavana 

“Nakupa masaa matatu uoneshe ilipo chemba ya siri” Chogo  alisema kisha aliondoka ndani ya chumba hicho. 

Upande wa pili, Mzee Shayo alianza kuingiwa na wasiwasi  kuhusu vijana wake wawili aliowatumainia, simu ya Mohd  haikupatikana baada ya kuuawa ndani ya gari, simu ya Faudhia  iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa, ilimpa mashaka juu ya  usalama wao, alijitahidi sana kupiga simu lakini simu yake  haikuweza kumpa majibu ya nini kilichokuwa kimetokea huko  Arusha kwenye operesheni ya kujuwa kuhusu Chogo, alituma  Askari wengine wa Kitengo kuelekea Arusha kwa ajili ya  kuwatafuta Mohd na Faudhia. 

Punde alipokea simu ya Rais iliyomtaka aende Ikulu haraka  sana, kutoka Kigamboni yalipo makao makuu ya Kitengo cha siri  cha Usalama wa Taifa ilimchukua dakika kadhaa, tayali hali ya  tahadhari ilitangazwa hivyo hakukutakiwa Mtu yeyote kutoka  ndani, Jiji lilikuwa kimya sana kama makazi yaliyotelekezwa,  Mzee Shayo alifika hadi Ikulu kisha alienda kwenye chumba cha  siri ambacho Rais na Waziri Mkuu walikuwa wamehifadhiwa. 

Rais alihitaji kujuwa Mzee Shayo alifikia wapi katika  harakati za kupambana na Kikosi hicho cha Kigaidi, waliketi  watu watatu na kuanza kuzungumza, Mzee Shayo alimwambia Rais  kuwa ametuma vijana kuelekea Arusha mbako inaaminika kuwa  Gaidi namba moja aliyeiteka Benki kuu anatokea huko 

“Huo ni ujinga Shayo! Unafuatilia historia ya Mtu badala ya  kupambana naye sasa hivi, hadi umalize kuijuwa historia yake  pengine gaidi atakuwa amemaliza kazi yake na kuondoka Nchini.  Benki ipo chini yao Shayo, historia histori historia  itasaidia nini?” Aliuliza Rais akionekana kuwa mwenye hasira 

“Mkuu kila jambo linahitaji taaluma katika utendaji, kabla ya  kutatua tatizo ni lazima tuangalie lilipoanzia itatusaidia  kujuwa ukubwa wake!” Alijitetea Mzee Shayo

“Hivi kweli ulistahili kuwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama wa  Taifa? Magaidi wamechukua silaha Lugalo na makambi mengine,  tayari Nchi hii imekuwa kisiwa cha vita unayajuwa madhara  yake? Kiasi kikubwa vita hii utapigana wewe na vijana wako,  jeshi lipo katika hali ngumu ya kujinasua” Alisema Rais huku  akionekana kuanza kususa mazungumzo hayo, Waziri Mkuu  akamwambia Mzee Shayo 

“Kuna hazina kubwa sana pale Benki pengine ndiyo sababu ya  Ugaidi huu, hakikisha unafaulu Shayo, vinginevyo  hatutokuelewa” Alisema Waziri Mkuu kisha Mzee Shayo  alinyanyuka na kuaga, alipoondoka Rais alimuuliza Waziri Mkuu 

“Nani anajuwa ilipo chemba iliyohifadhiwa pesa?” Aliuliza  akiwa makini sana 

“Kuna Mdada wa pale Benki anaitwa Selina, yeye bahati mbaya  yupo ndani ya Benki na ameshikiliwa kama watafanikiwa  kumtambuwa basi mpango wote utavurugika” Alisema Waziri Mkuu  na kumpa muda wa kutafakari Rais 

“Una hakika Gavana hajui chochote?” Aliuliza Rais 

“Gavana anajuwa kuhusu pesa iliyohifadhiwa Benki ila hajui  iliwekwa wapi sababu mpango ulifanywa kuwa siri kama  ulivyoagizwa”. Alijibu Waziri Mkuu 

“Nina uhakika hawawezi kuchukua pesa za Kitanzania watahitaji  zile Dola, hili jambo sitaki lifahamike popote na kama  itatokea Mtu amejuwa basi katisha Maisha yake” Aliagiza Rais 

Naaam!! Mzee Shayo alipotoka Ikulu alihitaji kwenda  kutembelea makazi yake yaliyopo Mikocheni B, alikuwa  akitembea kwa siri sana hadi alipofika, Kisha aliingia kwenye  chumba ambacho alikuwa akikitumia kufanya kazi zake, aliketi  ili kujipa utulivu huku akifikiria afanye nini. 

••••••••••••••••••••••••••••••••• 

Nje kidogo ya Jiji la Arusha, kulionekana gari moja nyeusi  aina ya prado ikiwa imeacha barabara na kukita kwenye Mti 

Tukio hilo lilionekana kutokea muda mrefu uliopita kutokana  na ukimya ambao ulikuwepo, ndani ya gari hiyo alikuwemo  Faudhia akiwa ameegemea usukani, alikurupuka kama Mzimu  kutoka kifo. 

“Uhhhh” alisikia maumivu makali ya kichwa, alionekana kuchoka  sana, alifungua mlango na kutoka ndani ya gari, alijivuta hadi chini ya Mti, aliitoa simu yake kisha aliiangalia  alikuwa ametafutwa na Nani, aliona ni Mkuu wa Kitengo alikuwa  amempigia zaidi ya mara 40, alimpigia Mkuu huyo 

“Aah Baba!!” Alisema Faudhia akionekana kuwa na maumivu  makali kisha alikohoa na kuanza kumtia hofu Mzee Shayo 

“Faudhia upo sawa?” Alihoji Mzee Shayo 

“Nilichungulia mlango wa kuzimu lakini bahati nzuri mafunzo  yamenisaidia kujinasua” Alisema Faudhia 

“Mohd yuko wapi?” Alihoji Mzee Shayo 

“Baba!! Mohd ndiye aliyetaka kunipeleka kuzimu, nimeshtuka  anafanya kazi upande wa Magaidi, anatumika upande huo na  sijui ametumika kwa muda gani, alipewa agizo la kunimaliza”  Alisema Faudhia 

“What? ( Nini? )” aliuliza kwa mshituko sana Mzee Shayo. 

“Ndio…alafu, Mhusika Mkuu wa ugaidi ni Mzee Shomari”  Alisema Faudhia na kumuacha kinywa wazi Mzee Shayo 

“Una uhakika na maneno yako Faudhia? Mzee Shomari si yupo  gerezani?” Aliuliza Mzee Shayo, 

“Hapana, nina uhakika na ninachozungumza na yeye ndiye  aliyetoa maagizo ya kuuawa kwangu, nahisi ni yeye ndiye  aliyehitaji kunimaliza kabla sijavuka mpaka wa Namanga”  Alisema Faudhia 

“Shit!! Sasa kwanini wametumia nguvu kubwa ya kuzuia habari  za Chogo ikiwa gaidi namba moja ni Mzee Shomari?” Aliuliza  Mzee Shayo 

“Kuna mtego mahali, inavyoonekana kuna mchezo unachezwa hapa  Baba” Alisema Faudhia 

“Upo wapi kwa sasa?” Alihoji Mzee Shayo 

“Nipo nje kidogo ya Jiji la Arusha, jiji hili si salama tena  Kwasasa” 

“Sikia Faudhia, ni lazima umalize hiyo kazi, fuatilia ujuwe  ni kwanini Chogo anafichwa, kuna ufunguo wa hili jambo katika  Maisha ya Chogo, hujapata fununu yoyote?”

“Tulionana na Mama yake Chogo, alisema Mwanaye alifariki  Miaka mingi kwa ajali ya gari na alituonesha na kaburi lake,  lakini pia alituonesha picha ya Mtu aliyeleta Maiti ya Chogo  alikuwa ni Mzee Shomari” Alisema Faudhia 

“Hapo kuna taarifa juu ya taarifa, tukio juu ya Tukio, hiyo  picha iliyopigwa Mzee Shomari alikuwa katika pozi lipi?”  Aliuliza Mzee Shayo akiwa nyumbani kwake Mikocheni 

“Ilionekana ni picha iliyopigwa bila Mzee Shomari kujiandaa,  alikuwa akiongea na Mtu mwingine” 

“Yes! Yes! Rudi Arusha haraka sana Faudhia, hakikisha  unafahamu stori nzima, naelekea gerezani kujuwa kuhusu  taarifa ya Mzee Shomari” 

“Sawa Baba” Alisema Faudhia kisha alikata simu, alishusha  pumzi zake, alikuwa na kazi nzito iliyojaa hatari mbele yake. 

Waligawana majukumu, Faudhia alirudi Arusha, Mzee Shayo  alielekea gereza la Segerea haraka sana, alitumia usafiri wa  pikipiki ambao aliamini asingeliweza kuchelewa wala  kudhurika, Watu wachache sana ndio waliokuwa wakifanya safari  za hapa na pale ila shughuli zilikuwa zimesimama kabisa,  ilimchukua takribani dakika 50 kutoka Mikocheni hadi Lilipo  gereza la Segerea, alikuwa akifahamika hivyo aliingia moja  kwa moja hadi kwa Mkuu wa gereza na kumuuliza kuhusu Mzee  Shomari, alichojibiwa kilimchosha sana. Naaam!! Alipewa sasa  simulizi ya Mzee Shomari akiwa gerezani hadi alivyotoweka 

“Baada ya kufungwa alikaa miezi kadhaa tuu, baadaye kulitokea  uvamizi hapa na hatimaye alitoroshwa ila ilifahamika kuwa  baada ya kutoroka aliondoka Nchini na rafiki yake Mzungu  ambaye alikuwa mfungwa mwenzake wakaelekea Uholanzi” Alieleza  Mkuu wa Magereza 

“Shit!” Alisema Mzee Shayo na kukumbuka wakati tukio hilo  linatokea yeye alikuwa mapumziko Nchini Moroco 

“Asante!” Alisema kisha aliondoka gerezani hapo akiwa na  uhakika kuwa maneno ya Faudhia yalikuwa kweli ila alijiuliza  sababu hasa ya ugaidi huo ilikuwa nini. 

Aliondoka hapo kichwa kikiwa kimejaa moto, mzigo mzito wa  kupambana ulikuwa kichwani pake, Rais alikuwa akimkalia kooni  kila wakati asijuwe afanyaje. 

Upande wa Faudhia alikuwa tayari amerejea ndani ya Jiji la  Arusha kuendelea kuutafuta ukweli kuhusu Chogo, alishaambiwa ni Hospitali gani ilitoa gari kwa ajili ya kusafirisha mwili  wa Chogo, gari gani alipata nalo ajali, alifikiria aanzie  wapi, aliona ni bora awasiliane na kampuni ya usafirishaji  ambayo ilidaiwa gari lao ndio lilipata ajali na kupelekea  kifo cha Chogo, alipfika aliambiwa kampuni hiyo imefungwa kwa  muda mrefu. Alikutana na mdada mmoja ambaye alionekana kuwa  mfanyakazi wa kampuni hiyo, alijaribu kumbembeleza ili aseme  chochote lakini mdada huyo aligoma kabisa, aliona ni bora  aondoke. 

Alipofika kwenye gari, aliketi na kutafakari aingilie wapi,  alipata wazo la kwenda Hospitalini. Lakini akiwa anawasha  gari alitazama Side Mirror aliona kuna Mtu akitoka hapo akiwa  na kikaratasi mfano wa tiketi hivi, alishangaa wakati  aliambiwa hakuna huduma katika kampuni hiyo, aliona ni bora  azuge anaondoka, Naam! Alisogeza gari na kuificha mahali  kisha alirudi taratibu na kukuta mlango wa kampuni  umefunguliwa wote wakati mwanzo ulikuwa umefungwa, kulikuwa  na watu kadhaa ambao walikuwa wakitoka hapo, alifikiria  huenda wakawa wateja, alipoona Watu wameisha, aliingia humo  kisha haraka alitoa bastola yake na kumuonesha Mdada huyo.  Faudhia Aligeuza maneno ya kibao kilichoandikwa HUDUMA  INAPATIKANA akaweka TUMEFUNGA KWA MUDA. 

Mdada huyo alionekana kujawa na hofu sana asijuwe anapaswa  kufanya nini, 

“Ulisema huduma zimesitishwa muda sasa lakini kumbe ulikuwa  unajuwa unachokifanya si ndiyo?” Mdada aliendelea kutetemeka  sana 

“Niambie unafahamu nini kuhusu ajali mbaya ya gari iliyotokea  Miaka iliyopita, unamfahamu vipi Chogo? Ukifanya ujanja  wowote nazibua kichwa chako” Alisema Faudhia 

“Naomba tafadhali usiniuwe nina ndugu ambao wananitegemea  Mimi” Alisema Mdada huyo akiwa analia 

“Kama unataka nisikuuwe basi sema ukweli unafahamu nini  kuhusu Chogo na kwanini ulikuwa unaficha jambo?” Aliuliza kwa  masistizo Faudhia huku akijuwa fika kuwa eneo hilo halikuwa  salama sana kwake, kwa hofu ya kuuawa Mdada alianza kufunguka 

“Nitasema kila kitu ila naomba usiniuwe” 

“Mimi ni Undercover wa kitengo, unapaswa kusema ukweli sababu  bila hivyo shingo yako itakuwa halali ya risasi nitakayo  ifyatu hapa” Alisema Faudhia kwa msistizo sana.

“Ilikuwa ni siku ya Jumatano, nilikuwa ndiyo kwanza nimeanza  ajira hapa, alikuja Baba Mmoja mlemavu wa mguu, umri wake  ulikuwa umeenda na kusema kuwa anahitaji kuongea na Bosi  wetu, bahati nzuri Bosi alikuwa ofisini kwake, Baba huyo  alionekana kuwa ni Mtu mwenye fedha nyingi. Alienda kwa Bosi  na sikujuwa kuwa alikuwa anaongea nini na Bosi, baadaye  alitoka kisha aliniaga kuwa anaondoka, Baada ya dakika 15  Bosi alikuja na kuniambia kuwa kuna kijana atakuja kwa ajili  ya kusafiri, nafikiri ndiyo huyo ambaye unamuulizia ila jna  lake siwezi kulikumbuka, aliniambia akija nimuoneshe mahali  pa kwenda kulala, ilikuwa ni ndani ya Ofisi hii kabla  haijajengwa upya. Nilichukulia ni jambo la kawaida tuu,  alipokuja kijana majira ya saa moja usiku nilimkatia tiketi  kisha nilimuonesha mahali pa kwenda kulala, inaonesha Yule  Baba alkuwa akimfuatilia kijana huyo maana baada ya kijana  huyo kwenda kulala yule Baba alikuja” 

“Aliniuliza Kijana yupo wapi, nilimuelekeza alipo sababu  nilimjuwa Baba huyo baada ya kuja mchana na kuzungumza na  Bosi, muda mchache baadaye Bosi naye alikuja kisha aliniuliza  alipo kijana nilimueleza alipo, alielekea huko na ukimya  ulitawala, nilianza kusinzia lakini baadaye nilishtuka baada  ya Bosi kuniita na kuniambia kuwa napaswa kuondoka usiku huo,  nilikuwa na zamu ya kukesha hivyo kuambiwa vile nilifurahi  ili nikalale, lakini nilipoangalia vizuri niligundua yule  Baba alikuwa akimsubiria Bosi nje ila alitoka na begi kubwa  hivi ambalo hata sikuliona wakati linaingia, nilifunga na  kuondoka zangu!!” Alisema Mdada huyo huku akihema juu juu,  Faudhia alishusha Bastola yake baada ya kugudua sasa alikuwa  akiongea ukweli, alijuwa Baba huyo alikuwa ni Mzee Shomari. 

“Enhee ilikuwaje baada ya hapo?”aliuliza tena Faudhia 

“Baada ya hapo, siku iliyofuata niliambiwa nisiende kazini  ila nitalipwa pesa ya siku kitu ambacho kilizidi kunipa  furaha, Mchana kupitia taarifa ya habari nilisikia taarifa  kuwa basi la Kampuni yetu lilipata ajali wakati likiwa  linafanya safari, Hakuna aliyepona katika ajali hiyo…lakini  Bosi alinisistiza sana nisije nikasema chochote kuhusu yule  Baba kuja usiku na yule kijana” Alisimulia Mdada huyo ambaye  alikuwa mnene kiasi 

“Sasa usiri wako umepelekea Nchi kuzama kwenye Lindi la  Ugaidi wa kutisha, muda siyo mrefu jiji hili litakuwa chini  ya ESS, kama unaweza kuongozana na mimi twende” Alisema  Faudhia akimwambia Mdada huyo ambaye alishapukia 

Alionekana kuchanganikiwa, waliingia kwenye gari kisha gari  liliondoka eneo hilo kuelekea yalipokuwa makazi ya Mama yake Martin Gimbo, miili ya Mama Martin na Mjukuu wake ilishaanza  kutoa harufu humo ndani, Faudhia aliingia kutafuta chochote  kitakachomuwezesha kufukua kaburi hilo ambalo lilisemekana  kuwa ni kaburi la Martin Gimbo. 

“Naomba unisaidie hapa, tukishamaliza tunaondoka” Alisema  Faudhia kisha alimpatia chepe mdada huyo, walianza kufukua  kaburi hilo. Iliwachukua zaidi ya saa nzima hadi kumaliza,  chini walikutana na sanduku kubwa ambalo kwa kawaida lilikuwa  ni sanduku la kuhifadhia mwili wakati wa kuzika. Walifanikiwa  kulivuta juu, wakati huo walianza kusikia milio ya Risasi kwa  mbali huku gari za polisi zikiliza ving’ora vyake. 

Faudhia alianza kuligonga ili lifunguke, bahati nzuri alipata  nyundo ndani ya nyumba hiyo kisha alifanikiwa zoezi la  kulifungua Sanduku hilo, yule Mdada alitazama pembeni kwa  hofu ya kuona mabaki ya mwili wa marehemu Martin Gimbo,  bahati mbaya ndani ya Sanduku hilo kulikuwa na brifkesi ndogo  na siyo mifupa wala mabaki ya mwili wa Martin Gimbo 

“Yes! Martin Gimbo ndiye Chogo” Alisema Faudhia huku  akimtazama Mdada huyo ambaye hakulijuwa hata jina lake.  Alilichukua Brifkesi hilo lakini hata kabla hawajapiga hatua  hata moja, Faudhia alisindikizwa chini na teke kali  lililopigwa kwa ustadi wa hali ya juu, ghafla alihisi ganzi  mkono wa kulia, aliliachia brifkesi hilo huku akiwa anaanguka  chini, Sanduku lilidakwa 

Faudhia alishangaa namna upigaji wa teke hilo ulivyotumia  akili na ustadi wa hali ya juu sana, aligeuka kumtazama  aliyekuwa amempiga teke hilo, alikutana na sura aliyoifahamu.  Naaam! Alikuwa ni rafiki yake wa zamani Diana, Diana alikuwa  ndani ya Koti jeusi, sketi nyeusi, pia alikuwa amevalia wigi  jeusi. 

“Diana ni wewe?” Alihoji Faudhia, hakutegemea kukutana na  Diana katika nyakati hizo, aliona kama yupo ndotoni japo  alishatumiwa picha ya Miongoni mwa Watu waliokuwa wakiendesha  ugaidi Tanzania. 

Faudhia alijivuta na kusimama japo kwa maumivu makali, teke  alilopigwa lilimfanya ahisi kizunguzungu. 

“Umewezeje?” Aliuliza Faudhia 

“Kwasababu nimekusubiria kwa zaidi ya miaka 7 Faudhia,  nimekusubiri kwa lengo moja tu la kukupeleka kuzimu” Alisema  Diana kisha aliweka Brifkesi pembeni, yule Mdada alivyoona  hivyo alikimbia eneo hilo sababu alijuwa kuna hatari kubwa  inaenda kutokea hapo muda mchache ujao.

“Ulinisubiria unipeleke kuzimu?” Alihoji Faudhia “Ndiyo! Kwasababu ulimuuwa Mama yangu” alisema Diana 

“Diana itakuwa umekosea njia, mimi nimemuuwa Mama yako? Ina  maana nawe umeingia kwenye mtego wa Mzee Shomari? Diana  mnatumika na huyo Mzee ili atimize lengo lake, nisikilize  rafiki yangu!! Mimi sikuuwa Mama yako bali yeye Mzee Shomari  ndiye aliyefanya hivyo na hiyo ndiyo sababu ya yeye kukaa  jela, amka kutoka usingizini Diana” Alisema Faudhia 

“Leo tutaona Faudhia kati yangu Mimi na wewe nani yupo  Usingizini, Ukifa naondoka na Brifkesi, nikifa unaondoka na  Brifkesi” Alisema Diana huku akijiandaa kupambana na Faudhia 

“Diana hebu nisikilize, hujapoteza kila kitu katika Maisha  yako, una muda wa kubadilisha kila kitu, ungana na Mimi  tumdhibiti Mzee Shomari” Alisema Faudhia, maneno ya Faudhia  hayakubadilisha Chochote, Diana alikaa mkao wa kuanza  kumshambulia Faudhia. Alianza kumfuata Faudhia kama Simba  mwenye njaa huku Faudhia akiwa anarudi nyuma ili afikirie  namna ya kumzuia Diana. 

Faudhia aligundua haraka kuwa Diana alikuwa anatumia pigano  maarufu nchini China linaloitwa Wing Chun, alijuwa sasa kumbe  Diana alikuwa na taaluma ya mapigano ya Martial arts 

Alipomfikia alitua kwenye mapaja ya Faudhia kisha alijirusha  na kumzunguka kwa nyuma kisha aligusa mfupa hadimu sana nyuma  ya mgongo wa Faudhia, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana,  Faudhia alihisi kukatika kwenye uti wa mgongo ila alijikaza  asianguke, alifanya haraka na kumgeukia Diana kisha  alijipanga kupambana naye, alimwambia 

“Acha Diana, Acha unachofanya kumbuka sisi ni marafiki”  Alisema Faudhia 

“Ningekuwa rafiki yako usingelithubutu kuniulia Mama yangu,  alikukosea nini yule?” Alisema Diana huku akionekana kuzidi  kujawa na hasira, alijiandaa tena kumpa pigo lingine la Wing  Chun…Faudhia alijitahidi kuisoma mikimbio ya Diana ambayo  ilikuwa ya haraka mno. 

Alifanya kama vile anamkimbia, alimpa mgongo kisha alipohisi  Diana yupo nyuma karibu na kumnasa alimchumpa na kugusa mguu  mmoja kwenye mti kisha alijipindua na kukutana na Diana  ambaye hakutegemea kama Faudhia angejifyetua kisha Faudhia  alimpa teke la Maana Diana, alisogezwa pembeni huku akitema  damu, ilizidi kumpa hasira, alimfuata tena na kufanya mpambano huo uzidi kuwa mtamu. Ilikuwa ni vita kati ya  marafiki wawili waliogeuka kuwa maadui, ndipo  walipothibitisha kuwa kuna Msitari mwembamba sana kati ya  Upendo na chuki. 

Ulikuwa ni mpambano mkali sana, vita ya kurushiana ngumi  ilitanda, Ilikuwa kama vile walikuwa wakipeana zamu, dakika  tatu kwa Faudhia na dakika tatu kwa Diana. Wakati wanapigana  lile Brifkesi lilikuwa pembeni, Faudhia hakujuwa kulikuwa na  jambo gani ndani ya Bridkesi hilo jeusi. 

Jua lilikuwa likiendelea kuwaka kwa ukali wake. Kutokana na  ile sumu ambayo iliingizwa mwilini mwake na Mohd japo  alijitahidi kuizuia kwa kujichoma sindano ila ilianza  kumletea shida alianza kutokwa jasho, ndio muda ambao Diana  aliutumia kumfanyia kitu mbaya Faudhia. 

Alipeleka ngumi zaidi ya 10 mfululizo, Faudhia alijitahidi  kadiri ya uwezo wake kuzipangua lakini hakuwa na nguvu ya  kuzipangua zote alijikuta akiruhusu mwili wake kukutana na  ngumi nzito za Diana, alijikutana akishuka chini na kupiga  magoti, Diana alilichukua lile brifkesi kisha alimwambia  Faudhia 

“Onja uchungu wa kifo ambao ulimpatia Mama yangu” Alichomoa  sindano ili aweze kumchoma Faudhia 

“Diana! Umesahau kila kitu? Kumbuka wewe ni nani, Mzee  Shomari anakutumia” Alisema Faudhia japo kwa shida sana huku  akihisi kizunguzungu, Diana alitoa kichupa kidogo kisha  alifyonza sumu kwa kutumia sindano 

“Niliwahi kusimuliwa kuwa Mtu anayekaribia kufa huwa na  majuto sana ila nakushangaa wewe Faudhia bado unakaidi kuwa  hukumuuwa Mama yangu” Diana alimsongelea Faudhia, alimshika  nywele na kupindisha shingo kisha alimchoma sindano, kabla  hajaruhusu sumu iweze kusambaa mwilini mwa Faudhia, alipigwa  na kitu kizito kichwani, Diana alishindwa kumalizia zoezi,  alijitahidi kugeuka lakini alishindwa alijikuta akianguka  chini na kupoteza fahamu. Nyuma yake alisimama yule Mdada  ambaye alimpa taarifa ya ajali ya Basi, Naam! Ndiye  aliyempiga na kitu kizito Diana. 

Faudhia alimwambia Mdada huyo kuwa 

“Chukua Brifkesi tuondoke hapa, si unajuwa kuendesha gari?”  Aliuliza 

“Ndio najuwa”

“Tuondoke hapa haraka sana” Alisema Faudhia, hakutaka  kummaliza Diana siku hiyo sababu licha ya uadui bado  alimtambuwa Diana kama rafiki yake, yule Mdada alimsaidia  Faudhia kuingia kwenye gari walilokuja nalo, Milio ya risasi  ilitanda kila kona ya Jiji la Arusha, isingelikuwa salama kwa  Faudhia kuendelea kukaa hapo 

“Tunaenda wapi?” Alihoji mdada akiwa anaingia barabara kuu 

“Dar-es-salaam” Alisema Faudhia huku akilifungua Brifkesi  hilo ili ajuwe ndani yake kulikuwa na nini na kwanini  lilizikwa. 

•••••••••••••••••••••••••••••••• 

Jina la Selina lilifika mikononi mwa Chogo, aliambiwa kuwa  ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri iliyohifadhi kiasi  kikubwa cha pesa, Chogo alitoka kwenye moja ya Chumba baada  ya kumaliza kuzungumza na Mzee Shomari na kupewa taarifa hiyo  kuwa kuna Mwanamke anaitwa Selina na yupo ndani ya Benki,  yeye pekee ndiye anayefahamu ilipo chemba ya siri. Chogo  alitoka akiwa ameshikilia Bunduki aina ya AK47 

Mateka walikuwa wamekaa chini kando ya sehemu ya Mapokezi,  alipofika aliuliza 

“Selina ni nani?” Ilikuwa ni sauti iliyojaa mamlaka sana,  aliuliza kwa kumaanisha kuwa alikuwa akimuhitaji Mdada huyo.  Selina mwenyewe aliposikia hivyo alijuwa ni kitu gani Magaidi  hao walikuwa wakihitaji, baadhi ya Magaidi sura zao  walizificha Ila baadhi hawakuzificha akiweno Chogo ambaye  waliamini hawezi kutambulika kwa urahisi. 

“Selina ni nani?” Aliuliza tena Chogo kisha aliiandaa bunduki  kwa lengo la kuleta kitisho 

“Mimi hapa” alijitokeza huyo aliyeitwa Selina akiwa amevalia  sare za wafanyakazi wa Benki, alikuwa Mwanamke mmoja mzuri  mweusi mwenye rasta asilia. 

“Mleteni” Alisema Chogo, mara moja Selina alisogezwa mahali  aliposimama Chogo, Selina alionekana kuwa muoga sana, Chogo  alimwambia Selina 

“Usiogope sababu una kazi moja tu ya kufanya, ukishamaliza  nitakuacha huru sawa?” Alisema akiwa anatabasamu, Selina  aliitikia kwa woga kisha Chogo alisema

“Tuongozane” Alimpa ishara Selina amfuate kwenye moja ya  chumba. 

Nje ya Benki polisi walizingira benki hiyo wakiwa na silaha  za moto huku wakiwa na tahadhari kubwa, walikuwa wakitumia  kipaza sauti kuzungumza, Chogo alipofika Chumbani na Selina  alimwambia 

“Nisubirie hapa, naenda kuongea na polisi” Alisema kisha  alichukua AK47 na kuelekea nje ya Benki hiyo. 

Kitendo cha Chogo kutoka nje ya Benki kilileta utayari kwa  polisi na vitengo vyote vilivyokuwa makini na Benki, Chogo  alitoka akiwa hajavaa shati, mwili wali wake ulijaa michoro  mingi, alionekana kujiamini sana huku polisi wakiambiana kuwa  wanapaswa kumsikiliza sababu alikuwa na mateka ndani ya Benki 

Chogo alisimama katikati ya Barabara iliyotoka kivukoni  kwenda mjini kisha aliwauliza polisi 

“Mlitaka nitoke ndani, nimeshatoka, mlikuwa mnasemaje?”  Aliuliza kwa ujasiri, kipaza sauti kilisikika 

“Kwanza tunahitaji usalama wa mateka wote walio ndani ya  Benki, pili tunataka kujuwa mnahitaji nini?” 

“Oooh! Siwezi kuuwa Raia ambao hawana kosa lolote, ila  mkileta ujanja nitauwa kila Mtu ndani ya Benki, masaa 24  yajayo nitaiachia Benki hii” Alisema Chogo kisha alirudi  ndani ya Benki, hakuna askari hata mmoja aliyejaribu  kumshambulia Chogo, moja kwa moja alienda kwenye kile chumba  alichomuacha Selina, aliweka Bunduki pembeni kisha alifunga  mlango, Chogo alimtazama Selina kwa jicho la kumtamani sana  ukizingatia sketi ya Selina ilikuwa imepasuka kidogo hivyo  paja lilikuwa nje 

Selina alikuwa mwingi wa kutetemeka, Chogo alimfuata Selina  kisha alimtandika busu, alimshika matiti na Makalio, alimvua  nguo Selina na kumbaka, baada ya kumaliza alimwambia Selina 

“Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapi  ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” Alisema  Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa bado  hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemeka  kwa woga 

“Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipo  Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hii  alibadilisha sura yake na kujaza hasira

“Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema Selina 

LEO NIMEWEKA NDEFU SANA COMMENTS ZIKIWA CHACHE NARUDI KWENYE KUWEKA FUPI

Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SABA

JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

24 Comments

Leave A Reply

Exit mobile version