Ilipoishia “Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaΒ Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaΒ pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaΒ palepale.Β
Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaΒ nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,Β alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaΒ nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaΒ nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoΒ nyumbani. Endelea
SEHEMU YA TANO
“Haya Mama nitaendelea kumtafuta” Alisema Osman, alipokataΒ simu alijiuliza nilikuwa nimeenda wapi, alishikwa na wivuΒ fulani hata kazi hakufanya naye aliondoka. Mida ya Jioni kamaΒ saa moja kasoro hivi ndiyo niliamka, nilikuta MossesΒ ameniandalia supu, nilikunywa kisha aliniulizaΒ
“Osman ndiyo Nani? Amepiga sana simu, ilipokata yake iliingiaΒ ya Mama yako, walikuwa wakipiga kwa kupokezana” Aliniuliza naΒ kuelezea kuhusu simu zilizokuwa zimeingiaΒ
“Osman ni Bosi wangu labda amenipigia sababu kuna faili zipoΒ kwangu, ngoja nimpigie Mama” Nilisema, alinisogezea simu maraΒ moja kisha nilimpigia Mama, alipokea na kinishushia swali juuΒ
“Jacklin uko wapi?” Aliuliza kwa sauti iliyoonesha kuwaΒ alikuwa na shahuku ya kujuwa nilipoΒ
“Mama mimi siyo Mtoto sasa swali gani hilo alafu kama vileΒ una hasira na Mimi!”Β
“Ndiyo wewe siyo Mtoto lakini kwanini uondoke kazini kabla yaΒ muda wa kazi kuisha? Osman amenipigia simu kujuwa kama upoΒ sawa na upo wapi”Β
“Ulimjibuje Mama”Β
“Nilimwambia kuwa sijui ulipo sasa kwanini niwe muongo kwaΒ kijana wa Watu, mwisho wote tuje kuonekana hatuna maana?”Β
“Ok Mama usiongee sana nipo kwa Mosses hata hivyo narudi mudaΒ siyo mrefu” Nilisema, Mama alikata simu.Β
“Huyo Mama yako jinsi anavyonichukia usikute amekasirika hukoΒ kisa wewe kuja kwangu” Alisema MossesΒ
“Ah! Mama yangu nimeshamzoea love, ngoja nirudi tu nyumbaniΒ ila fanya kama tulivyoongea tafuta nyumba kesho unipe jibu”Β Nilisema kisha nilizama kwenye waleti yangu nikampa MossesΒ laki na nusuΒ
“Hiyo itakusaidia” Nilisema kisha niliondoka zangu pale.Β
Nilipofika nyumbani nilimkuta Mama akiwa amefura kama churaΒ mwenye njaa, alikuwa amekaa nje akinisubiria. NilipomfikiaΒ aliniuliza swali gumu sanaΒ
“Umesahau kila kitu sababu leo upo hai, huyo Mosses alikataaΒ kusaidia Maisha yako, alinijibu jeuri lakini wewe unamuona waΒ maana sana kwako, nimefanya makosa kukupigania Jacklin?”Β
Lilikuwa ni swali gumu kuwahi kuulizwa katika Maisha yangu,Β Mama alidondosha chozi lililochuruzika hadi kwenye mashavuΒ yake, ilinibidi nikae kwanzaΒ
“Mama ndiyo maneno gani hayo? Binadamu tunakosea naΒ kujirekebisha, usimuhukumu Mosses kwa kosa moja tu yule niΒ Binadamu hajakamilika Mama, hilo haliwezi kuuondoa uthamaniΒ wake kwangu” Nilimjibu Mama kwa kujikaza sana, hakuna kituΒ nilikuwa sipendi kama kumuona Mama akilia kwa ajili yangu,Β anagalau ningekuwa mgonjwa lakini ni mzima na analia kwaΒ ajili yanguΒ
“Mama yako nilisemewa vibaya, Kijana wa Watu alikusaidiaΒ hakuangalia nyuma. Bila Osman ingekuwa inasimuliwa hadithiΒ yako Jacklin, lakini leo Mtu aliyekusaidia akabadilisha naΒ Maisha yetu kututoa kwenye umasikini hadi kwenye hali hiiΒ haupokei simu zake, unaacha kazi yake na kwenda kwa Mosses?”Β Alisema Mama, nilihema kwa uchungu na maumivu, ni kweli OsmanΒ alisaidia Maisha yangu lakini hakusaidia ili niwe mtumwaΒ kwakeΒ
“Mama msaada ambao unakuwa Mtumwa ni msaada wa kizandiki tuu,Β kama alinisaidia kwa moyo wake hakupaswa kuhitaji malipo,Β mbona anajuwa kila kitu sasa kwanini apige simu kwako?Β Amenikosea sana”Β
“Unajisikiliza Jacklin au unaongea kwasababu unayo nafasi yaΒ kufanya hivyo? Hajakusaidia tu bali ameweka maisha yakeΒ rehani, anatembea na figo moja kwa ajili yako, hupaswiΒ kumsumbua hivi kijana wa Watu na kama huitaji kazi basiΒ mwambie ili amtafute Mtu mwingine” Mama alisema kwa hisiaΒ kaliΒ
“Sawa Mama sipendi ukwazike kwa ajili yangu. NitamuombaΒ msamaha Osman, kuwa na amani Mama nakupenda sana” NilisemaΒ kisha nilinyanyuka na kuingia ndani, nilimuacha Mama akiwaΒ amekaa nje peke yake, najuwa jinsi alivyokuwa anajisikia ilaΒ ningefanya nini wakati moyo wangu upo kwa mwingine? NilizionaΒ ishara zote kuwa Osman ananipenda ila tayari hisia zangu zipoΒ kwa Mosses.Β
Nilipofika chumbani kwangu niliyatafakari maneno ya MamaΒ ambayo ni wazi aliyasema kutoka ndani ya nafsi yake,Β nilijisikia vibaya, nilitamani kumtumia meseji Osman nimuombeΒ msamaha ila niliona ni bora nimuombe msamaha kesho yakeΒ Ofisini, nilizitazama Missed Calls zake nilimuonea hurumaΒ Kijana wa Watu, nilifunua shati langu nikaangalia eneo laΒ tumbo, nilitabasamu tu hata sijui kwanini nilifanya hivyo.
Kesho yake kabla ya kwenda ofisini nilipitia duka la MauaΒ nikanunua ua zuri kwa ajili ya kumpatia Osman ili anisameheΒ kwa kilichotokea. Nilichagua ua zuri ambalo niliamini litampaΒ furaha Osman, mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha, hali yaΒ hewa ilikuwa nzuri sana ikanikumbusha siku ya kwanzaΒ Nilipoanza kuumwa nikasaidiwa na Osman, nilianza kutabasamuΒ tu hadi Muuza Maua alinishtukia akasemaΒ
“Inaelekea unampenda sana Mtu ambaye unampelekea ua hili,Β Nawaombea penzi lenu lichipue mithiri ya Mtende jangwani”Β Alisema kisha alinitazama usoni, ghafla sura yangu ilikosaΒ uchangamfu. Sijui kwanini kila nilipomfikiria OsmanΒ nilijikuta nikiishia kwenye huzuni. Mara muda huo huo OsmanΒ alipiga simu kama vile alikuwa akijuwa nilikuwa nikimuwaza,Β niliiacha iite kidogo kisha niliipokea huku yule Muuza dukaΒ akinitazama tuΒ
“Hello Osman” Nilimsalimia Osman mara baada ya kuwaΒ nimeshapokea simu na kusikia sauti yakeΒ
“Jacklin, leo sijisikii vizuri naomba usimamie kazi zakoΒ vizuri” Alisema Osman, ni kweli hata sauti yake haikuwa naΒ uchangamfuΒ
“Una shida gani Osman?” NilimuulizaΒ
“Nahisi hali ya Homa tuu Jacklin” Alisema tena OsmanΒ
“Haya nitafanya hivyo lakini baadaye….” Nilitaka kumwambiaΒ kuwa nahitaji kuonana naye ila nilisita nikamwambiaΒ
“Ugua pole Osman” Nilisema kisha simu ilikatika, nilirudiΒ kulipia ua lile kisha niliondoka nalo hadi kazini.Β
Mdada wa mapokezi aliponiona alinisimamisha, alinifuataΒ niliposimama akaniulizaΒ
“Umempa nini Bosi Osman? Yaani alivyo mkali yule lakini janaΒ alinywea kabisa, aliposikia haupo naye aliondoka naΒ alionekana hana raha” Alisema, dakika moja tu ilitoshaΒ kumtambua alikuwa ni Mtu wa aina gani, alionekana kuwaΒ mshakunaku, nilitabasamu kisha nikamwambiaΒ
“Kazi njema” nilimuacha akiwa ameduwaa, pengine alitegemeaΒ ningemwambua Mimi ni Mwanamke wa Osman nahisi ndichoΒ alichokuwa anataka kukisikia.Β
Niliketi kwenye kiti, nilishusha pumzi zangu, niliona jinsiΒ maisha yangu yalivyobadilika. Mara simu yangu iliita,Β aliyekuwa akinipigia alikuwa ni Mosses, aliniambia kuwaΒ amepata nyumba hivyo ilikuwa ikihitaji pesa kiasi cha MilioniΒ 14, nilimwambia jioni nitampatia pesa hiyo.Β
Siku hiyo, Osman alienda Hospitalini kuangalia afya yake,Β alienda kwenye Hospitali ya Dokta Simon, Wawili hawa walikuwaΒ wakifahamiana sana. Alipofika Dokta Simon alimfanyiaΒ uchunguzi, kwakuwa alikuwa akimfahamu vizuri Osman alijuwa niΒ kitu gani kilikuwa kikimsumbua Osman, waliketi baada yaΒ vipimoΒ
“Osman! Nilikuonya kuhusu kutoa figo yako hukutaka kunisikia”Β Alisema Dokta Simon, Osman alikaa kimya kumsikiliza DoktaΒ SimonΒ
“Nilikataa usifanye vile sababu ya tatizo lako, figo mojaΒ ilikuwa na matatizo hivyo ulikuwa ukitumia zaidi figo mojaΒ tuu, sasa ile nzima umeiondoa hii iliyobakia inafanya kaziΒ kwa kiwango kidogo sana na haitokuwa na muda mrefu nayoΒ itakufa” Alisema Dokta SimonΒ
“Kwanini umeamua kuhatarisha Maisha yako Osman? Wewe niΒ Bilionea mkubwa hapa Nchini, una pesa ya kutosha,Β unaheshimika kila kona” Aliendelea kusema Dokta SimonΒ
“Nilifanya vile kwasababu ya upendo wangu kwa Jacklin,Β nilikuwa na Maisha yaliyojaa huzuni sana baada ya ZahraΒ kunitenda vibaya, ghafla sura yangu ilijawa tabasamu maraΒ baada ya kumuona Jacklin, niliapa sitopenda tena ila baada yaΒ Jacklin kuja katika Maisha yangu nimejihisi tofauti kabisa”Β Alisema Osman kisha alishusha pumzi zakeΒ
“Kwa mara ya kwanza namuona Bilionea dhahifu zaidi katikaΒ Maisha yangu, unahatarisha Maisha yako kwa ajili ya MwanamkeΒ ambaye unajuwa fika ana Mwanaume wake? Unahatarisha MaishaΒ kwa ajili ya Mwanamke ambaye hata hujawahi kumtamkiaΒ chochote? Hiyo ni akili yako Osman?? Laiti kama Mzee DhabiΒ akilijuwa hili ulilofanya ataipoteza familia ya Jacklin naΒ haitokuja ionekane tena, wewe ni Mtoto wa pekee wa yule Mzee,Β siku akiligundua hili anaweza hata akaniuwa Mimi” AlisemaΒ Dokta SimonΒ
“Sikia Dokta Simon, naomba hili jambo liwe siri Baina yetu.Β Baba yangu asijuwe chochote wakati ambao tunatafuta Figo kwaΒ ajili ya kunipandikiza” Alisema OsmanΒ
“Naweza kulificha lakini hali yako inaweza ikaniumbua mbeleΒ ya Baba yako, vyote nitafanya lakini vipi kama JacklinΒ akazikataa hisia zako huoni kama utakuwa umekula hasara wewe?” Alimuuliza swali gumu sana, Osman alikunbuka namnaΒ tukivyogombana kule Dubai, aliona Swali la Dokta SimonΒ lilikuwa na mashiko sana.Β
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PUMZI YA MWISHO
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMΒ Β
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ
Β
10 Comments
Asante mtunzi, endelea kutupa burudani
Huyu demu ovyoo sanaππ
Mungu naomb jackline atambue kuw mosses hampend arudi kwa osman
Ivi ni kweli kina mwanamke wa ivi
Noma nomaa…..dis iz goin to be badπ₯²π₯² osman his going to lose his lifeπ₯Ίπ₯Ί
Asitisha mapenzi Kwa Jacklin bn me nakadirishwa na uyu dada duuh
Jacklin hakir hana
endelezen bas
tm1nmm
08l9lu