Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 15, 2024Updated:October 28, 202410 Comments7 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaย  Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaย  pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaย  palepale.ย 

    Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaย  nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,ย  alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaย  nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaย  nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoย  nyumbani. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    “Haya Mama nitaendelea kumtafuta” Alisema Osman, alipokataย  simu alijiuliza nilikuwa nimeenda wapi, alishikwa na wivuย  fulani hata kazi hakufanya naye aliondoka. Mida ya Jioni kamaย  saa moja kasoro hivi ndiyo niliamka, nilikuta Mossesย  ameniandalia supu, nilikunywa kisha aliniulizaย 

    “Osman ndiyo Nani? Amepiga sana simu, ilipokata yake iliingiaย  ya Mama yako, walikuwa wakipiga kwa kupokezana” Aliniuliza naย  kuelezea kuhusu simu zilizokuwa zimeingiaย 

    “Osman ni Bosi wangu labda amenipigia sababu kuna faili zipoย  kwangu, ngoja nimpigie Mama” Nilisema, alinisogezea simu maraย  moja kisha nilimpigia Mama, alipokea na kinishushia swali juuย 

    “Jacklin uko wapi?” Aliuliza kwa sauti iliyoonesha kuwaย  alikuwa na shahuku ya kujuwa nilipoย 

    “Mama mimi siyo Mtoto sasa swali gani hilo alafu kama vileย  una hasira na Mimi!”ย 

    “Ndiyo wewe siyo Mtoto lakini kwanini uondoke kazini kabla yaย  muda wa kazi kuisha? Osman amenipigia simu kujuwa kama upoย  sawa na upo wapi”ย 

    “Ulimjibuje Mama”ย 

    “Nilimwambia kuwa sijui ulipo sasa kwanini niwe muongo kwaย  kijana wa Watu, mwisho wote tuje kuonekana hatuna maana?”ย 

    “Ok Mama usiongee sana nipo kwa Mosses hata hivyo narudi mudaย  siyo mrefu” Nilisema, Mama alikata simu.ย 

    “Huyo Mama yako jinsi anavyonichukia usikute amekasirika hukoย  kisa wewe kuja kwangu” Alisema Mossesย 

    “Ah! Mama yangu nimeshamzoea love, ngoja nirudi tu nyumbaniย  ila fanya kama tulivyoongea tafuta nyumba kesho unipe jibu”ย  Nilisema kisha nilizama kwenye waleti yangu nikampa Mossesย  laki na nusuย 

    “Hiyo itakusaidia” Nilisema kisha niliondoka zangu pale.ย 

    Nilipofika nyumbani nilimkuta Mama akiwa amefura kama churaย  mwenye njaa, alikuwa amekaa nje akinisubiria. Nilipomfikiaย  aliniuliza swali gumu sanaย 

    “Umesahau kila kitu sababu leo upo hai, huyo Mosses alikataaย  kusaidia Maisha yako, alinijibu jeuri lakini wewe unamuona waย  maana sana kwako, nimefanya makosa kukupigania Jacklin?”ย 

    Lilikuwa ni swali gumu kuwahi kuulizwa katika Maisha yangu,ย  Mama alidondosha chozi lililochuruzika hadi kwenye mashavuย  yake, ilinibidi nikae kwanzaย 

    “Mama ndiyo maneno gani hayo? Binadamu tunakosea naย  kujirekebisha, usimuhukumu Mosses kwa kosa moja tu yule niย  Binadamu hajakamilika Mama, hilo haliwezi kuuondoa uthamaniย  wake kwangu” Nilimjibu Mama kwa kujikaza sana, hakuna kituย  nilikuwa sipendi kama kumuona Mama akilia kwa ajili yangu,ย  anagalau ningekuwa mgonjwa lakini ni mzima na analia kwaย  ajili yanguย 

    “Mama yako nilisemewa vibaya, Kijana wa Watu alikusaidiaย  hakuangalia nyuma. Bila Osman ingekuwa inasimuliwa hadithiย  yako Jacklin, lakini leo Mtu aliyekusaidia akabadilisha naย  Maisha yetu kututoa kwenye umasikini hadi kwenye hali hiiย  haupokei simu zake, unaacha kazi yake na kwenda kwa Mosses?”ย  Alisema Mama, nilihema kwa uchungu na maumivu, ni kweli Osmanย  alisaidia Maisha yangu lakini hakusaidia ili niwe mtumwaย  kwakeย 

    “Mama msaada ambao unakuwa Mtumwa ni msaada wa kizandiki tuu,ย  kama alinisaidia kwa moyo wake hakupaswa kuhitaji malipo,ย  mbona anajuwa kila kitu sasa kwanini apige simu kwako?ย  Amenikosea sana”ย 

    “Unajisikiliza Jacklin au unaongea kwasababu unayo nafasi yaย  kufanya hivyo? Hajakusaidia tu bali ameweka maisha yakeย  rehani, anatembea na figo moja kwa ajili yako, hupaswiย  kumsumbua hivi kijana wa Watu na kama huitaji kazi basiย  mwambie ili amtafute Mtu mwingine” Mama alisema kwa hisiaย  kaliย 

    “Sawa Mama sipendi ukwazike kwa ajili yangu. Nitamuombaย  msamaha Osman, kuwa na amani Mama nakupenda sana” Nilisemaย  kisha nilinyanyuka na kuingia ndani, nilimuacha Mama akiwaย  amekaa nje peke yake, najuwa jinsi alivyokuwa anajisikia ilaย  ningefanya nini wakati moyo wangu upo kwa mwingine? Nilizionaย  ishara zote kuwa Osman ananipenda ila tayari hisia zangu zipoย  kwa Mosses.ย 

    Nilipofika chumbani kwangu niliyatafakari maneno ya Mamaย  ambayo ni wazi aliyasema kutoka ndani ya nafsi yake,ย  nilijisikia vibaya, nilitamani kumtumia meseji Osman nimuombeย  msamaha ila niliona ni bora nimuombe msamaha kesho yakeย  Ofisini, nilizitazama Missed Calls zake nilimuonea hurumaย  Kijana wa Watu, nilifunua shati langu nikaangalia eneo laย  tumbo, nilitabasamu tu hata sijui kwanini nilifanya hivyo.

    Kesho yake kabla ya kwenda ofisini nilipitia duka la Mauaย  nikanunua ua zuri kwa ajili ya kumpatia Osman ili anisameheย  kwa kilichotokea. Nilichagua ua zuri ambalo niliamini litampaย  furaha Osman, mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha, hali yaย  hewa ilikuwa nzuri sana ikanikumbusha siku ya kwanzaย  Nilipoanza kuumwa nikasaidiwa na Osman, nilianza kutabasamuย  tu hadi Muuza Maua alinishtukia akasemaย 

    “Inaelekea unampenda sana Mtu ambaye unampelekea ua hili,ย  Nawaombea penzi lenu lichipue mithiri ya Mtende jangwani”ย  Alisema kisha alinitazama usoni, ghafla sura yangu ilikosaย  uchangamfu. Sijui kwanini kila nilipomfikiria Osmanย  nilijikuta nikiishia kwenye huzuni. Mara muda huo huo Osmanย  alipiga simu kama vile alikuwa akijuwa nilikuwa nikimuwaza,ย  niliiacha iite kidogo kisha niliipokea huku yule Muuza dukaย  akinitazama tuย 

    “Hello Osman” Nilimsalimia Osman mara baada ya kuwaย  nimeshapokea simu na kusikia sauti yakeย 

    “Jacklin, leo sijisikii vizuri naomba usimamie kazi zakoย  vizuri” Alisema Osman, ni kweli hata sauti yake haikuwa naย  uchangamfuย 

    “Una shida gani Osman?” Nilimuulizaย 

    “Nahisi hali ya Homa tuu Jacklin” Alisema tena Osmanย 

    “Haya nitafanya hivyo lakini baadaye….” Nilitaka kumwambiaย  kuwa nahitaji kuonana naye ila nilisita nikamwambiaย 

    “Ugua pole Osman” Nilisema kisha simu ilikatika, nilirudiย  kulipia ua lile kisha niliondoka nalo hadi kazini.ย 

    Mdada wa mapokezi aliponiona alinisimamisha, alinifuataย  niliposimama akaniulizaย 

    “Umempa nini Bosi Osman? Yaani alivyo mkali yule lakini janaย  alinywea kabisa, aliposikia haupo naye aliondoka naย  alionekana hana raha” Alisema, dakika moja tu ilitoshaย  kumtambua alikuwa ni Mtu wa aina gani, alionekana kuwaย  mshakunaku, nilitabasamu kisha nikamwambiaย 

    “Kazi njema” nilimuacha akiwa ameduwaa, pengine alitegemeaย  ningemwambua Mimi ni Mwanamke wa Osman nahisi ndichoย  alichokuwa anataka kukisikia.ย 

    Niliketi kwenye kiti, nilishusha pumzi zangu, niliona jinsiย  maisha yangu yalivyobadilika. Mara simu yangu iliita,ย  aliyekuwa akinipigia alikuwa ni Mosses, aliniambia kuwaย  amepata nyumba hivyo ilikuwa ikihitaji pesa kiasi cha Milioniย  14, nilimwambia jioni nitampatia pesa hiyo.ย 

    Siku hiyo, Osman alienda Hospitalini kuangalia afya yake,ย  alienda kwenye Hospitali ya Dokta Simon, Wawili hawa walikuwaย  wakifahamiana sana. Alipofika Dokta Simon alimfanyiaย  uchunguzi, kwakuwa alikuwa akimfahamu vizuri Osman alijuwa niย  kitu gani kilikuwa kikimsumbua Osman, waliketi baada yaย  vipimoย 

    “Osman! Nilikuonya kuhusu kutoa figo yako hukutaka kunisikia”ย  Alisema Dokta Simon, Osman alikaa kimya kumsikiliza Doktaย  Simonย 

    “Nilikataa usifanye vile sababu ya tatizo lako, figo mojaย  ilikuwa na matatizo hivyo ulikuwa ukitumia zaidi figo mojaย  tuu, sasa ile nzima umeiondoa hii iliyobakia inafanya kaziย  kwa kiwango kidogo sana na haitokuwa na muda mrefu nayoย  itakufa” Alisema Dokta Simonย 

    “Kwanini umeamua kuhatarisha Maisha yako Osman? Wewe niย  Bilionea mkubwa hapa Nchini, una pesa ya kutosha,ย  unaheshimika kila kona” Aliendelea kusema Dokta Simonย 

    “Nilifanya vile kwasababu ya upendo wangu kwa Jacklin,ย  nilikuwa na Maisha yaliyojaa huzuni sana baada ya Zahraย  kunitenda vibaya, ghafla sura yangu ilijawa tabasamu maraย  baada ya kumuona Jacklin, niliapa sitopenda tena ila baada yaย  Jacklin kuja katika Maisha yangu nimejihisi tofauti kabisa”ย  Alisema Osman kisha alishusha pumzi zakeย 

    “Kwa mara ya kwanza namuona Bilionea dhahifu zaidi katikaย  Maisha yangu, unahatarisha Maisha yako kwa ajili ya Mwanamkeย  ambaye unajuwa fika ana Mwanaume wake? Unahatarisha Maishaย  kwa ajili ya Mwanamke ambaye hata hujawahi kumtamkiaย  chochote? Hiyo ni akili yako Osman?? Laiti kama Mzee Dhabiย  akilijuwa hili ulilofanya ataipoteza familia ya Jacklin naย  haitokuja ionekane tena, wewe ni Mtoto wa pekee wa yule Mzee,ย  siku akiligundua hili anaweza hata akaniuwa Mimi” Alisemaย  Dokta Simonย 

    “Sikia Dokta Simon, naomba hili jambo liwe siri Baina yetu.ย  Baba yangu asijuwe chochote wakati ambao tunatafuta Figo kwaย  ajili ya kunipandikiza” Alisema Osmanย 

    “Naweza kulificha lakini hali yako inaweza ikaniumbua mbeleย  ya Baba yako, vyote nitafanya lakini vipi kama Jacklinย  akazikataa hisia zako huoni kama utakuwa umekula hasara wewe?” Alimuuliza swali gumu sana, Osman alikunbuka namnaย  tukivyogombana kule Dubai, aliona Swali la Dokta Simonย  lilikuwa na mashiko sana.ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย 

    ย 

    Pumzi ya mwisho

    10 Comments

    1. Sir, Yowas on October 15, 2024 9:00 pm

      Asante mtunzi, endelea kutupa burudani

      Reply
    2. Johdam on October 15, 2024 9:01 pm

      Huyu demu ovyoo sana๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ

      Reply
    3. Angel on October 15, 2024 9:43 pm

      Mungu naomb jackline atambue kuw mosses hampend arudi kwa osman

      Reply
      • G shirima on October 16, 2024 9:19 am

        Ivi ni kweli kina mwanamke wa ivi

        Reply
    4. Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 15, 2024 9:56 pm

      Noma nomaa…..dis iz goin to be bad๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ osman his going to lose his life๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ

      Reply
    5. Jacqueline Mo on October 15, 2024 11:08 pm

      Asitisha mapenzi Kwa Jacklin bn me nakadirishwa na uyu dada duuh

      Reply
    6. Emmy on October 16, 2024 7:51 pm

      Jacklin hakir hana

      Reply
    7. yahaya on October 19, 2024 9:10 pm

      endelezen bas

      Reply
    8. ๐Ÿ“” + 1.515729 BTC.GET - https://yandex.com/poll/HYTE3DqXnHUqpZMyFqetue?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& ๐Ÿ“” on June 4, 2025 5:22 am

      tm1nmm

      Reply
    9. ๐Ÿ“ง Message; + 1,368618 BTC. Receive >> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& ๐Ÿ“ง on June 6, 2025 10:48 am

      08l9lu

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane โ€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.