Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Tatu (13)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Tatu (13)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 27, 2024Updated:October 29, 20247 Comments14 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Kwanza pole sana Jacklin, Dunia yako imekugeuka lakiniΒ  ndivyo ilivyo sababu siyo Watu wote wanakuwa na simulizi tamuΒ  za Maisha yao, yako chungu sana. Osman alikutafuta sana,Β  ilisadikika kuwa Mlikuwa mmeuza kila kitu na kuondoka”Β  Alisema Dokta Simon, stori yake ilikuwa ngeni masikioniΒ  mwanguΒ 

    “Tuliuza kila kitu?” NilimuulizaΒ 

    “Ndiyo! Mzee Dhabi pia alihangaika kuwatafuta bila mafanikio,Β  mwisho alikata tamaa baada ya kupata taarifa kuwa mliuzaΒ  nyumba na kuondoka wewe na Mama yako!”Β 

    Haraka niligundua kuwa Mzee Dhabi alifanya yote pasipo OsmanΒ  kujuwa. Endelea

    Sehemu Ya Kumi Na Tatu

    “Hapana Baba yake Osman alitumia hasira zake kutuondoshaΒ  kwenye ile nyumba na kuchukua kila kitu tulichonunuliwa naΒ  Osman, hatukuuza nyumba wala mali yoyote ile vyoteΒ  vilichukuliwa na Mzee Dhabi, tuliishi Maisha ya mateso sanaΒ  Mimi na Mama yangu” nilisema, nilishindwa kuzuia uchungu ulioΒ  ndani ya moyo wangu, nililia sana tena kwa kwikwiΒ 

    “Usilie Jacklin, kwasasa unaishi wapi?” Alihoji Dokta Simon,Β  nilifuta chozi langu nilitulia kwa sekunde kadhaa kishaΒ  nilimjibuΒ 

    “Uswahilini, tulikuwa tunaishi kwa kuuza Mboga mboga mtaani.Β  Na hii hali yangu nitaweza vipi kuendesha Maisha yanguΒ  Dokta!” Chozi liliendelea kunibubujikaΒ 

    “Usijali nitakuchukua utaishi kwangu Jacklin wakati tunafanyaΒ  utaratibu mwingine” Alisema DoktaΒ 

    “Samahani hivi Osman yupo wapi?” NiliulizaΒ 

    “Osman anaishi Marekani..” Alijibu Dokta Simon huku akioneshaΒ  kutaka kusema kitu kingine ambacho alijizuia asikisemeΒ 

    “Anaishi na Zahra?” NilimuulizaΒ 

    Alishusha pumzi zake kisha alinitazama akanijibuΒ 

    “Ndio, wanatarajia kufunga ndoa miezi mitatu ijayo hapaΒ  Nchini” Alisema Dokta SimonΒ 

    “Natamani kumuona Osman ili nimwambie kuwa sikukataa kuokoaΒ  Maisha yake ila nilikuwa nimechelewa” Nilisema kwa kilioΒ  kikubwaΒ 

    “Jacklin, hayo yameshapita, kwasasa tuangalie Afya yakoΒ  kwanza ndiyo jambo lenye umuhimu zaidi kuliko chochote kile”Β  Alisema Dokta Simon, nilimkubalia. Hakuchelewa sana aliondokaΒ  wodiniΒ 

    Hakuna aliyekuja kuniona kwa siku nilizokuwa Hospitalini,Β  moyo ulijaa upweke na maumivu makali, nilimkumbuka Mama yanguΒ  jinsi alivyonilea na kunipigani katika nyakati zote.Β  Nilitokwa na machozi kila wakati, Mama yangu aliondoka bilaΒ  hata kuniaga, ilinipa shida sana hadi kuwa sawa. Dokta SimonΒ  alijitahidi sana kila alipopata muda alikuja kuniangalia naΒ  kunipa faraja kwa kuniambia maneno yaliyojaa matumainiΒ  makubwa sana japo nilishajuwa kuwa thamani ya Maisha yanguΒ  ilikuwa imeshaondoka.

    Bili za Hospitali alizilipa mwenyewe Dokta Simon,Β  nilimshukuru sana kwa ubindamu aliouonyesha kwangu.Β  Alinichukua na kunipeleka nyumbani kwake baada ya mwezi mmojaΒ  kupita, alikuwa akiishi na Mke wake aliyeitwa Lidia. NiliishiΒ  kwa upendo na amani ya hali ya juu sana, Mke wa Dokta SimonΒ  alikuwa na moyo kama wa Mume wake ndio maana ndege hawaΒ  wawili waliruka pamoja sababu walifanana kwa kila kituΒ 

    “Usijali Jacklin Mungu atakupa ufalme mwingine kupitiaΒ  maumivu yako” Alisema Mke wa Dokta Simon wakati nilipokuwaΒ  najifunza kutembea kwa kutumia MagongoΒ 

    “Nashukuru kwa ukarimu wenu Lidia, mmenionesha thamani kubwaΒ  iliyo ndani yangu ambayo niliona imeondoka, nilihisiΒ  sitotabasamu tena. Mwisho ninekubali hali halisi kuwa siweziΒ  kutembea hivyo nashukuru kwa kila kitu Lidia” Nilisema tukiwaΒ  tumesimama kando ya Barabara.Β 

    “Dokta Simon alinieleza kuhusu wewe na Osman, alikutolea figoΒ  na kuokoa Maisha yako”Β 

    “Ni kweli, katika vitu ambavyo ninajuta katika Maisha yanguΒ  ni kutomshukuru Osman kwa wema wake alionitendea na kumuombaΒ  Msamaha sababu sikuweza kuokoa uhai wake, nilishindwa kulipaΒ  fadhila za Ubinadamu wake” Nilisema, nilihisi choziΒ  likinilenga taratibuΒ 

    “Usijali Jacklin, hayo yameshapita. Haina haja tena kuingiaΒ  kwenye Maisha ya Mtu nwingine na kumkumbusha yaliyopita.Β  Sahau tu na Maisha yaendelee ” Alisema Lidia, tuliendelea naΒ  mazoeziΒ 

    “Pamoja na yote ila uzuri wako Jacklin upo pale pale, wewe niΒ  mzuri sana” Alisema Lidia,, alinifanya nitabasamuΒ 

    “Unanichokoza?” Nilisema kwa utani kisha tulicheka, tulikuwaΒ  marafiki wakubwa sana kwa kipindi kifupi ambacho niliishiΒ  nyumbani kwao, walijitahidi kuniondoa upweke, walinisaidiaΒ  sana sikuwa na mawazo kama Mwanzo.Β 

    Usiku mmoja nikiwa nimelala, kutokana na dawa kali nilizokuwaΒ  nameza kwa ajili ya kupunguza maumivu nilijikuta nikizamaΒ  ndotoni. Ndoto ilianza kwa furaha sana, Niliota TukiwaΒ  tunacheka na Osman, ghafla alikuja Mwanamke akiwa ameshikiliaΒ  Bastola, Mwanamke huyo sikuiyona sura yake ila alisemaΒ 

    “Jacklin una muda mchache sana wa kuendelea kupumua, siweziΒ  kukubali furaha yangu ukaiharibu kirahisi, Pumzi yako yaΒ  Mwisho sema neno moja kabla sijakumaliza” Alisema MwanamkeΒ huyo, nilimtazama Osman ambaye alikuwa akishangaa tukio hilo,Β  nilisemaΒ 

    “Nakupenda Osman” Lilikuwa ndiyo neneo langu la Mwisho katikaΒ  pumzi yangu ya Mwisho, alinipiga risasi. Ghafla nilishtukaΒ  kutoka Usingizini, nilihema sana, Jasho lilikuwaΒ  likinibubujika, niliamka na kwenda kuwasha taa. Jumba laΒ  kifahari la Dokta Simon lilikuwa kimya sana, sikutakaΒ  kuwasunbua ila ndoto niliyoiota ilinishtua mno.Β 

    Nilijiuliza ndoto hiyo ilikuwa na maana gani, nilisali iliΒ  Mungu aniweke mbali na hatari hiyo kabisa. NilikeshaΒ  nikimuomba Mungu, Usingizi ulinichukua Alfajiri, AsubuhiΒ  nilimsimulia Lidia kuhusu ndoto yangu, alicheka tuu kishaΒ  alisemaΒ 

    “Tatizo rafiki yangu unawaza sana kiasi kwamba unatengenezaΒ  hadi picha ya Uwongo kwenye akili yako, kumbuka kilaΒ  unachokifikiria hutokea hivyo acha kutengeneza Maisha mabayaΒ  ya Baadaye” Alisema akiwa ananiandalia chai, alikuwaΒ  akinichukulia kama Mtoto mdogo yani kwa jinsi alivyokuwaΒ  akinidekezaΒ 

    “Nimekuelewa Lidia” Nilisema.Β 

    • β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Osman aliwasili Nchini kwa ndege ya shirika la Fly EmirateΒ  akitokea Marekani. Alirudi Nchini kwa ajili ya kufunga ndoaΒ  na Zahra, tangu alipoondoka kwa ajili ya matibabu miezi kdhaaΒ  iliyopita hakurudi tena. Aliwasiliana na Rafiki yake DoktaΒ  Simon, ilikuwa ni furaha kwa marafiki hao kukutana tena OsmanΒ  akiwa mwenye Afya, katika Maongezi yao Osman aliniuliziaΒ  lakini Dokta Simon hakutaka kumwambia Osman kuwa Mimi nipoΒ  nyumbani kwake, sina Mguu. Alifanya hivyo ili kuruhusu kilaΒ  kilichopita kasirudi tena.Β 

    Nilishangaa siku hiyo Lidia aliniambia kuwa twende ShambaΒ  tukakague, sikuwa na pingamizi sababu nilikuwa sina kaziΒ  yoyote ile kumbe ndiyo siku ambayo Osman alikuwa anakujaΒ  kutembelea nyumbani kwa Dokta Simon, hawakutaka nionane naΒ  Osman, hawakutaka nijisikie vibaya. Basi tulipoondoka nyumaΒ  Osman alienda nyumbani kwa Dokta Simon kwa ajili ya kupataΒ  chakula cha Mchana na mazungumzo mengine ya kirafiki.Β 

    Tukiwa njiani tunaenda Shamba nilihisi kama kuna kitu hakipoΒ  sawa kwangu, sikuwa na furaha ya kwenda huko shamba,Β  nilimwambia Lidia kuwa sijisikii vizuri kuendelea na safariΒ  hivyo turudi nyumbani.

    “Unaumwa?” Aliniuliza LidiaΒ 

    “Hapana, sihisi kama natakiwa kuwa sehemu ya safari hii,Β  samahani Lidia” nilisema ili kama nitakuwa nitakuwaΒ  nimemkwaza anisamehe, Lidia alisemaΒ 

    “Mbona tumekaribia Jacklin jamani, ni hapo tu wala siyo mbaliΒ  hata hivyo hatuchelewi” Alisema Lidia, nilizungumza sasa kamaΒ  Binadamu ambaye sijatumia viungo vya mwili, si unajuwa vilemaΒ  jinsi ambavyo wanapenda kujiongelea madhaifu yaoΒ 

    “Turudi Bwana au sababu unajuwa siwezi kutembea ndiyoΒ  uniringie hivyo? Sijisikii na safari” Nilisema kishaΒ  niliuchuna, niliegemea kwenye kioo huku moyo ukiniambiaΒ  niwahi kurudi nyumbani, hata mwenyewe sikujuwa ni kwaniniΒ  nilikuwa nataka kurudi nyumbani wakati tulikubaliana kuwaΒ  twende Shambani.Β 

    “Usiseme hivyo Jacklin, Usimkufuru Mungu kiasi hicho, hayaΒ  turudi” alisema Lidia kisha aligeuza gari, moyo ulianzaΒ  kuchanuaΒ 

    Sasa kingine nilichokigundua ni kuwa Lidia alikuwa bizeΒ  kupiga simu mahali alafu simu ilikuwa haiiti, nilijaribuΒ  kuchungulia niliona alikuwa akimpigia Mume wake, nilijulizaΒ  alikuwa anataka kumwambia nini?Β 

    Sikuwa na kifua cha kuweza kukaa na dukuduku, nilimuulizaΒ 

    “Unampigia nani?” Niliuliza makusudi tu wakati nilishaonaΒ  alikuwa akimpigia Mume wake Dokta SimonΒ 

    “Nampigia Dada atuandalie chakula” Alisema kwa tabasamuΒ  ambalo hata yeye mwenyewe aligundua kuwa alikuwa akiongopa,Β  niligunaΒ 

    “Mh! Haya” Wala sikutaka eti kumuuliza zaidi wakati nilionaΒ  alikuwa akimpigia Mume wake, hali ile iliendelea kwa mudaΒ  mrefu, sijui sasa simu ilikuwa inaita alafu haipokelewi auΒ  vipi, sikutaka kuhoji zaidi bali nilihisi jambo ambalo sikuwaΒ  na uhakika nalo. Tulipofika Mjini kulikuwa na foleni kiasiΒ  hivyo angalau nilimuona akitabasamu hadi nilishangaa yaaniΒ  Watu wanakasirika kisa foleni yeye anafurahiaΒ 

    Nilicheka chini chini baada ya kugundua alikuwa amepagawa,Β  Basi haikutukuchukuwa muda mrefu kufika nyumbani. NiliiyonaΒ  gari ya kifahari ikiwa imeegeshwa karibu na Bustani ya Mauwa,Β  ilikuwa ya kifahari sana.

    “Ile gari ni ya Nani?” Niliuliza maana sikuwahi kuiyona paleΒ  nyumbaniΒ 

    “Aaah ile?” Aliuliza Lidia kama vile hakuwa na jibu laΒ  kunipa, nilimkaziaΒ 

    “Ndiyo! Ile nyeusi sijapata kuiyona hapa nyumbani, inaonekanaΒ  ni ya kifahari sana.” Nilisema huku Lidia akiwa anasogezaΒ  gari eneo la maegesho.Β 

    Kumbe Dokta Simon alikuwa tayari amewasiliana na Mke wake kwaΒ  njia ya ujumbe mfupi, lengo lao lilikuwa ni kutotaka Mimi naΒ  Osman tuonane pale. Huko ndani sasa ambako Osman na DoktaΒ  Simon walikuwepo walikuwa wakizungumza mambo yao ilaΒ  waliposikia ngurumo ya gari, Osman alitaka kuchungulia hukuΒ  akimuuliza Dokta SimonΒ 

    “Shemeji Lidia huyo?” Simon alipoulizwa hivi alibakia akiwaΒ  anajiuma meno asijuwe ajibu vipi, ni kweli tulikuwa Mimi naΒ  Lidia sasa angemjibi vipi ikiwa hataki Mimi na Osman tuonane?Β 

    “Ndi…ndi…oo”Β 

    “Mh! Mbona unajibu kama hauna uhakika, ni bora ukaangalieΒ  kama ni yeye maana muda wangu umeisha hapa ingawa nilihitajiΒ  sana kumuona” Alisema OsmanΒ 

    “Sawa ngoja nikaangalie, jisikie huru rafiki yangu” alisemaΒ  Dokta Simon kisha alikuja kwenye Maegesho akatukuta mimi naΒ  Lidia tukizozana maana alikuwa hataki nishuke kwenye gariΒ 

    “Bora hata Shemu umefika yaani Mkeo simuelewi kabisa, huweziΒ  amini ananizuia kushuka kwenye gari” nilisemaΒ 

    “Aaah Mke wangu kwanini unafanya hivyo?” Aliuliza Dokta SimonΒ 

    “Jacklin hajanielewa, nilikuwa nimemwambia asubirie weweΒ  ufike ili ukamuoneshe sapraizi yake” Alisema Lidia,Β  nilijikuta nikitabasamu kusikia kuna SapraizΒ 

    “Sapraiz gani hiyo?” Niliuliza, mkononi Dokta Simon alikuwaΒ  na kitambaa cheusi akaniambia anifunge machoniΒ 

    “Jamani jamani Sapraizi gani hiyo mbona mnanitisha” NilisemaΒ 

    “Hebu kwanza nikufunge ili ukaiangalie Sapraiz itakayoΒ  kufanya upagawe” Alisema Dokta Simon, Basi nilikubaliΒ  kufungwa kitambaa kumbe lengo lao lilikuwa Nisimuone Osman,Β  Walinipeleka nyuma ya nyumba

    “Jamani nna hamu ya kuona hiyo Sapraiz” NilisemaΒ 

    “Haya hebu nikufungue” Alisema Dokta Simon, moyo wanguΒ  ulijawa na furaha sana nilipomuona Kasuku akiwa kwenye kiziziΒ  chake, nilikuwa napenda sana Kasuku, sikuwaza chochote tena.Β  Nilivuta Magongo yangu na kulisogelea Zizi la Kasuku, DoktaΒ  Simon alimpa Ishara Mke wake kuwa anatoka, muda huo akiliΒ  yangu wala haikuwa hapo, walinipeleka sehemu ambayo hataΒ  nisingeliweza kusikia sauti ya gariΒ 

    Osman alikuwa akimsubiria Dokta Simon ndani, alipofikaΒ  alimdaka kwa swaliΒ 

    “Ni yeye?”Β 

    “Mke wangu?”Β 

    “Ndiyo!”Β 

    “Aah hapana, ni Kijana wangu wa kazi alikuwa akileta gari”Β 

    “Oooh! Sawa Basi ngoja Mimi niende” Osman aliaga, alielekeaΒ  lilipo gari lake kisha aliondoka pale nyumbani bila kuhisiΒ  wala kujuwa kuwa nilikuwa pale.Β 

    Nilikuwa nacheza na kasuku wangu mzuri niliyepewa kamaΒ  zawadi, nilisahau kila kitu. Lidia na Mume wake waliingiaΒ  ndaniΒ 

    “Hajashtuka chochote” aliuliza LidiaΒ 

    “Hapana sijui Jacklin!”Β 

    “Hapana japo alikuwa na wasiwasi kama nilivyokutumia mesejiΒ  kuwa hatukufika shambami aligaili njiani” Alisema LidiaΒ 

    “Mmmh kuna namna hawa Watu wawili wanawasiliana kifikra,Β  sitaki waonane, sitaki turudi tulipotoka. Osman ameamuaΒ  kuendelea na Maisha yake, nataka Jacklin naye aendelee naΒ  Maisha yake, atapata Mtu atakaye mpenda kwa jinsi alivyo”Β  Alisema Dokta Simon, alikuwa ni Mtu safi sana, roho yakeΒ  ilikuwa nzuri iliyojaa hurumaΒ 

    “Cha Msingi ni kuendelea kuhakikisha hajisikii mpweke”Β  Alimalizia Dokta Simon.Β 

    Hayo ndiyo yalikuwa Maisha yangu, mipango ya Harusi ya OsmanΒ  iliendelea kufanyika, kumbe katika kipindi hicho chote OsmanΒ  alikuwa hajakata tamaa ya kunitafuta japo Baba yakeΒ alimuongopea kuwa tuliuza nyumba na kuhama mji, alinitafutaΒ  bila mafanikio lakini alijipa tumaini kuwa ipo siku ataniona,Β 

    Masikini hakujuwa kama Mimi ni kilema wa Mguu, hakujuwa kuwaΒ  Mama yangu ambaye alikuwa akihangaika naye kunitafutia figoΒ  alikuwa amefariki siku nyingi. Hakujuwa kama nilikuwaΒ  nikiishi kwa rafiki yake.Β 

    Wazazi wa Osman walikuja kutoka Dubai, Harusi ilipangwa kwaΒ  kuzingatia heshima aliyonayo Mzee Dhabi, umaarufu na utajiriΒ  wake. Moyo wa Mzee Dhabi ulificha unyama ambao alitutendeaΒ  Mimi na Mama yangu.Β 

    Lidia na Osman walikuwa ni miongoni Mwa Watu wa karibu waΒ  Familia ya Mzee Dhabi, walishiriki maandalizi kisiri sanaΒ  bila Mimi kujuwa kwa kipindi chote, walikuwa wakiingia naΒ  kutoka alafu hakukuwa na stori zozote kuhusu Ndoa ya Osman,Β Β nakumbuka siku moja nilimuuliza Dokta Simon kama ndoa yaΒ  Osman ilikuwa imepitaΒ 

    “Imeshapita, walitaka kufanyia huku lakini walighaili,Β  imefanyika huko Dubai ambako anaishi kwasasa” NdichoΒ  alichonijibu Dokta Simon, nilikuwa mnyonge baada ya kusikiaΒ  hivyoΒ 

    “Usijali Jacklin, haikuwa ridhki yako ndiyo maana yalitokeaΒ  yaliyotokea, sahau kila kitu Maisha yaendelee sawa?” AlisemaΒ  tena Dokta SimonΒ 

    “Sawa” Nilijibu huku moyo wangu ukiwa na maumivu makali sana,Β  Osman kuowa haikuwa shida kwangu ila kilichoniuma zaidiΒ  ilikuwa ni kushindwa kumshukuru na kumwambia kuwa nipo HaiΒ  anisamehe kwa kila kitu.Β 

    Nilikaa na picha ya Osman kwa muda mrefu, siku mojaΒ  niliichoma moto, nilifungua ukurasa mpya wa Maisha yangu,Β  niliyapotezea maumivu kwa kucheza na Kasuku wangu, sikutakaΒ  kabisa kumfikiria Osman wala kukumbuka kilichomfika MamaΒ  yangu maana mambo hayo mawili yalikuwa yakinifanya nakuwaΒ  mnyonge sana. Niliamua kujisahaulisha hata alichonifanyiaΒ  Mosses..Β 

    Siku moja ilikuwa Mchana nilimpigia simu Lidia nikamwambiaΒ  kuwa nina hamu ya kula Ice Cream, alikuwa kazini hivyoΒ  alinitaka nivumilie kidogo, baadaye alimtuma dereva taxi ajeΒ  kunichukua anipeleke mahali ambapo Lidia alikuwepo iliΒ  tukanunue Ice Cream. Nilipofika niliingia kwenye gari yaΒ  Lidia, tulielekea kwenye Ice Cream huku tukipiga stori zaΒ  hapa na pale ambazo zilituburudisha kwa kiasi fulani.

    Kutoka nilipomkuta Lidia hadi sehemu ambayo Ice creamΒ  zilikuwa zinauzwa hapakuwa mbali sana, mwendo mfupi tuΒ  tulikuwa tumefika. Kutokana na hali ya Mguu wangu LidiaΒ  aliniomba nisishuke kwenye gari badala yake nimsubirie! BasiΒ  Lidia alishuka na kuingia zinapouzwa Ice cream ambazoΒ  nilikuwa nikizipenda sana, alichelewa sana hadi nilianzaΒ  kujiona mpweke ndani ya gariΒ 

    Nilitamani kushuka lakini kabla wazo la kushuka halijaniingiaΒ  sawa sawa, simu ya Lidia iliita, iliita kwa muda mrefu sanaΒ  hadi nilitamani kuangalia ni nani alikuwa akipiga ilaΒ  nilihisi uvivu fulani, sasa katika angalia angalia nilionaΒ  kitu kama kadi hivi. Nilipata shahuku ya kuiangalia,Β  nilinyoosha mkono na kuichukua.Β 

    Nilianza kuisoma, ilikuwa ni kadi ya harusi ya Osman naΒ  Zahra, moyo uliniripuka paa! Nikaangalia mlango ambao LidiaΒ  aliingia hakukuwa na Mtu aliyekuwa akitoka nikaendeleaΒ  kuisoma. Cha ajabu kadi ile ilikuwa haijatumika kabisa yaaniΒ  tarehe iliyoandikwa ilikuwa ni siku mbili mbele, zilikuwaΒ  kadi kama tano hivi zenye majina ila hiyo moja ilikuwa hainaΒ  jina basi niliiweka kwenye mkoba wangu haraka ili nikituliaΒ  niisome vizuri, nilijikuta nikianza kuwa na huzuni sana.Β 

    Punde Lidia alirejea ndani ya gari akiwa na Ice Cream,Β  nilimtazama sana hadi aliniulizaΒ 

    “Vipi kuna tatizo?” Aliniuliza akiwa ananipatia Ice Cream,Β  nilitabasamu tu baada ya kugundua kuwa nilikuwa nikifichwaΒ  jambo maana Dokta Simon alisema Harusi imeshapita ila chaΒ  ajabu kadi zile zilisema kuwa ni siku mbili baadayeΒ 

    “Hakuna shida” nilimjibuΒ 

    “Nimepata hiyo ile nyingine unayoipenda haipo” Alisema LidiaΒ 

    “Hata hii siyo mbaya kikubwa ni Ice Cream” nilimjibu kishaΒ  nilianza kufakamia Ice Cream, nilikula kwa hasira sana baadaΒ  ya kugundua Lidia na Mume wake hawakuwa wakweliΒ 

    “Tunarudi nyumbani au kuna mahali unataka twende” aliulizaΒ  Lidia akiwa anawasha gariΒ 

    “Nafikiri turudi nyumbani tu” Basi Tulirudi nyumbani.Β 

    Tulipofika nilielekea chumbani kwangu nilihakikisha nimefungaΒ  mlango vizuri ili niweze kuisoma ile kadi kwa utulivu,Β  nilikaa kitandani, niliitoa na kuanza kuisoma tena. KibayaΒ  zaidi ni kuwa waliokuwa wakizisambaza zile kadi walikuwa niΒ  Dokta Simon na Mke wake Lidia.

    Nilitamani kulia kwa uchungu ambao nilikuwa nikiusikia kwenyeΒ  moyo wangu, mara nyingi nilikuwa nikiwauliza kuhusu OsmanΒ  lakini walikuwa wakinipa majibu ya Hatuna mawasiliano nayeΒ  sana kwa sasaΒ 

    Nililia sana, niliona nimenyimwa haki ya kumuomba msamaha naΒ  kumshukuru Osman, niliihifadhi ile kadi kwenye Begi langu laΒ  nguo. Sikutaka kuwauliza chochote kile, siku hiyo Usiku LidiaΒ  alikuja chumbani kwangu na kuniambia kuwa anasafiri na MumeΒ  wake kwenda Nje ya Jiji watarudi baada ya wiki mojaΒ 

    “Nitawamiss sana jamani” nilisemaΒ 

    “Usijali Jacklin hata sisi tutakumiss mno, ubaki salama naΒ  kwa chochote usisite kutupigia simu” Alisema LidiaΒ 

    Alipoondoka nilitafakari nifanye nini maana nilijuwa tuΒ  walitengeneza safri feki ili kunizuga kuhusu Ndoa ya Osman.Β  Kweli siku iliyofuata asubuhi mapema waliniaga rasmi,Β  waliingia kwenye gari niliwapungia mkono wa kuwaaga,Β  waliniacha na Mdada wa kazi na Mlinzi.Β 

    Walipoondoka nilimfuata Mdada wa Kazi aliyekuwa anaitwa ScolaΒ  nikamuulizaΒ 

    “Unakunbuka siku ambayo Mimi na Lidia tulienda Shambani? IleΒ  siku ya mwisho?..” nilimuuliza alionekana kutafakari sanaΒ 

    “Ndio nakumbuka” alinijibu baada ya kuwa tayari amemalizaΒ  kutafakariΒ 

    “Kuna mgeni alikuja hapa si ndiyo?” Scola alinitolea machoΒ  yake MakubwaΒ 

    “Scola nijibu alikuja Mgeni si ndiyo?” Nilimuuliza tena baadaΒ  ya kuona alikuwa hanipi jibuΒ 

    “Lakini Dada..” alisema Scola, nikahisi kuna jamboΒ 

    “Sitaki cha lakini nataka uniambie ukweli ni nani alikujaΒ  hapa?” Nilimkazia sauti na jichoΒ 

    “Baba alisema nisiseme unanipa wakati mgumu Dada Jacklin”Β  Nilimshika mkono Scola nikamuingiza chumbani kwanguΒ  nikamwambiaΒ 

    “Tupo Mimi na wewe naomba unieleze ukweli ni nani alikujaΒ  hapa”Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya KUMI NA NNE Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho

    Β Β 

    Pumzi ya mwisho

    7 Comments

    1. Fawziya Hassan on October 27, 2024 6:45 pm

      Jamani Jackline😒
      Mapenzi mabaya sana yasikie tu kwa mwenzako omba yasikukute

      Reply
    2. Sir, Yowas on October 27, 2024 7:06 pm

      Leo umejitahidi sana admini

      Reply
    3. Michael on October 27, 2024 8:39 pm

      πŸ˜‡πŸ˜‡πŸ˜‡πŸ˜‡

      Reply
    4. Roddrigo on October 29, 2024 7:43 pm

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H

      Maisha Kitaa WhatsApp channel

      Reply
    5. 🏷 Ticket: + 1,511285 BTC. Continue >>> https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=28c4065c9c3246a1862a07f5a6441ef0& 🏷 on May 25, 2025 6:14 am

      uk4exa

      Reply
    6. πŸ”’ πŸ“₯ Wallet Notification: 0.33 BTC detected. Secure transfer => https://graph.org/ACCESS-CRYPTO-REWARDS-07-23?hs=28c4065c9c3246a1862a07f5a6441ef0& πŸ”’ on August 20, 2025 6:56 pm

      j2zpta

      Reply
    7. Binance账户 on January 7, 2026 5:39 am

      Can you be more specific about the content of your article? After reading it, I still have some doubts. Hope you can help me. https://www.binance.com/es-MX/register?ref=GJY4VW8W

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    AFCON
    Africa | CAF January 1, 2026

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya michuano ya TotalEnergies CAF AFCON Morocco 2025 imekamilika…

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.