Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Nne (14)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Kumi Na Nne (14)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 28, 2024Updated:October 29, 202424 Comments10 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Scola nijibu alikuja Mgeni si ndiyo?” Nilimuuliza tena baadaย  ya kuona alikuwa hanipi jibuย 

    “Lakini Dada..” alisema Scola, nikahisi kuna jamboย 

    “Sitaki cha lakini nataka uniambie ukweli ni nani alikujaย  hapa?” Nilimkazia sauti na jichoย 

    “Baba alisema nisiseme unanipa wakati mgumu Dada Jacklin”ย  Nilimshika mkono Scola nikamuingiza chumbani kwanguย  nikamwambiaย 

    “Tupo Mimi na wewe naomba unieleze ukweli ni nani alikujaย  hapa”ย  Endeleaย 

    SEHEMU YA KUMI NA NNE

    “Kusema ukweli ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kumuona ilaย  nakumbuka Baba alisema nisikwambie wewe, aliniambia niandaeย  chakula chenye hadhi ya kuliwa na Bilionea. Aliniambia kuwaย  ni Mtoto wa tajiri Mkubwa sana anaitwa Dhabi” Alisema Scolaย 

    “Basi inatosha, Asante!!” Nilimkatisha Scola, nilifunguaย  mlango na kumpa ishara kuwa atoke, alikuwa ameniambia ukweliย  ambao nilifichwa na Lidia na Dokta Simon.ย 

    “Dada naomba Usimwambie Baba” alisema Scolaย 

    “Usijali Scola siwezi kufanya hivyo, nenda nahitajiย  kupumzika” Basi Scola aliondoka zakeย 

    Unajuwa yale maumivu ya kuchomwa na msumari mguuni? Ndiyoย  ambayo nilikuwa nikiyapata kwenye moyo wangu, kulia haikuwaย  tiba, kukaa haikuwa tiba, nilitamani nipate sehemu yenyeย  utulivu nipige ukunga hadi sauti yangu iishe.ย 

    Basi siku mbili zilipita, ilikuwa ni tarehe 25/09 ndiyo sikuย  ambayo iliandikwa kwenye ile kadi, moyo wangu uliniambia kuwaย  ndiyo siku pekee ya kuonana na Osman, nilisoma muda ambaoย  Harusi ilikuwa ikifanyika, ilikuwa ni saa 2 Usiku katikaย  Hoteli ya nyota tano ya BAMOL DE HOTEL, muda nawaza yoteย  ilikuwa ni mchanaย 

    Nilijaza jina langu kwenye ile kadi, nilijuwa tukioย  litawashangaza wengi lakini ili moyo wangu utulie ni lazimaย  nionane na Osman na sehemu peke ilikuwa ni kwenye harusiย  yake.ย 

    Niliandaa gauni langu zuri jeusi, mishale ya saa mojaย  nililivaa, nilijitazama kwenye kioo niliona jinsiย  nilivyopendeza ila nilipofunua gauni nilipata huzuni sana,ย  sikuwa na mguu mmoja wa kuvalia kiatu, mkononi nilikuwaย  nimeshikilia kiatu cheusi cha kupandaย 

    Nilikitupa pembeni, nilikusanya magongo yangu, nilimpitaย  Scola akiwa anaingia jikoni, niliondoka nyumbani Usiku huoย  ili nielekee Hotelini, niliita Tax nikaanza safri huku moyoย  wangu ukiwa na maamuzi mawili ya kuacha au kuendelea naย  safari, niliazimia ni bora niende tu. Nikiwa kwenye Tax Lidiaย  alinipigia simu akaniuliza nipo wapi, nilishangaa sanaย 

    “Nipo njiani narudi nyumbani” nilimjibuย 

    “Ulikuwa wapi?” Aliuliza

    “Nilikuwa kwenye matembezi kidogo nilichoka kukaa tuย  nyumbani”ย 

    “Sawa ukifika nipigie niongee na Scola”ย 

    “Sawa!” Alikata simuย 

    Niliona ni bora niizime simu sikutaka tena kufikiria kuhusuย  wao.ย 

    Nilifika Hotelini mishale ya saa tatu kasoro, palikuwaย  pamepambwa sana kwa nje, ulinzi ulikuwa wa kutosha sanaย  sababu aliyeko ndani alikuwa ni Bilionea Mkubwa sana.ย 

    Niliangalia kadi yangu, niliongoza kuelekea kwenye lango kuuย  ambalo lilikuwa na walinzi, kumbe nyuma yangu alikuwepo Doktaย  Simon alafu sikushtukia ila kwakuwa alikuwa na pirika nyingiย  wala hakuniona, nilimshtukia aliponipita.ย 

    “Kumbe mpo hapa Mjini eeh! Kitakachotokea hamtoamini, kamaย  hamtotaka kuishi na Mimi tena ni sawa tu” nilijisemea ndaniย  ya moyo wangu! Nilionesha kadi yangu pale mlangoniย  nilikaguliwa kisha niliruhusiwa kingia ndani ya Hoteli,ย  nilielekezwa mahali ambapo harusi ilikuwa inafanyika.ย 

    Nilitembea na Magongo yangu kwa tahadhari sana maana kamaย  nitakutana na Lidia au Mume wake mpango ungekufa. Watuย  walikuwa wamependeza sana, ile nakaribia nilimuona Mzee Dhabiย  akizungumza na Simu basi niligeuza haraka kama narudiย  nilipotoka maana kama ningeendelea mbele angeniona, bahatiย  nzuri kulikuwa na chemba upande wa kushoto niliingia hukoย  hadi pale alipomaliza kuongea na kurudi Ukumbini.ย 

    Nilijitoa na kuelekea Ukumbini, kweli ilikuwa ni harusi yaย  Kifahari ambayo hata kwnye Filamu sikupata kuishuhudia, rohoย  iliniuma sababu nilipaswa kuolewa mimi, ilipaswa Mama yanguย  awepo kwa ajili ya furaha ambayo aliipigania.ย 

    Nilitafuta Kiti cha nyuma kabisa ili nisije onekana naย  wanafamilia, Muda ambao nilikuwa nimefika ndio kwanza ilikuwaย  inaanza. Matajiri wenye rangi nyeupe walikuwa wengi mno,ย  nilijitahidi kuangaza huku na kule ili nimuone Osman.ย 

    Kweli nilimuona Osman, huwezi amini nilijikuta nikisimamaย  bila kurajia, nilimtazama Osman akionekana kuwa mwenye furahaย  sana, pembeni yake alikuwepo Zahra naye akiwa mwingi waย  tabasamu. Nilishuka na kuketi bila kutaka, Shughuli ilianzaย  kwa kutambulisha baadhi ya Watu wakubwa waliohudhuria pale,ย  Dokta Simon na Lidia walikuwa wakizungumza jambo hukuย wakionekana kupiga simu bila kupokea majibu, nilijuwa tuย  walikuwa wakinipigia Mimi kujuwa niko wapi naona hata waoย  hofu iliwaingia maana Scola sikumuaga kabisa.ย 

    Nilisubiria muda sahihi wa kuonana na Osman bila kubuguzi mtuย  yeyote wala kuharibu chochote kile ila kadili muda ulivyozidiย  kwenda ndivyo nilivyogundua kuwa hali yangu ya kuhitajiย  kuonana na Osman ilikuwa ikipanda.ย 

    Muda wa Osman kumvisha pete Zahra ulipowadia roho ilizidiย  kuniuma, wengi walisimama na kupiga makofi kwa ajili yaย  tukio, ila macho yangu yalikuwa yakibubujikwa na machoziย  mfululizo, nilijitahidi kujizuia nilishindwa, nilitamaniย  kuondoka pale Ukumbini pia nilishindwa. Katika hali isiyo yaย  kawaida nilihisi kuguswa kwenye bega langu, nilipogeukaย  nilikutana na Lidia. Nilishtuka sana huku chozi likiendeleaย  kunibubujikaย 

    “Jacklin umefuata nini hapa?” Aliniuliza Lidia kwa sauti yaย  Chini ambayo hakuna aliyesikia maana wengi akili yao ilikuwaย  kule mbele. Nilimpiga kofi Lidiaย 

    “Muongo Mkubwa wewe, kama ni furaha kusema uwongo na kufichaย  kilicho kizuri basi furaha yako haiwezi kudumu Lidia, wewe niย  Muongo na mnafiki Mkubwa” Nilisema kwa sauti ya kawaidaย  ambayo baadhi waliisikiaย 

    “Jacklin naomba tutoke tukaongee tusije haribu shughuli yaย  Watu” Alisema Lidiaย 

    “Tayari imesha haribika Lidia, unafikiri nitakubali kuondokaย  bila kumwambia Osman kuwa nipo hai, kumwambia kuwa Mimi niย  kilema wa Mguu, kumwambia kuwa Mama yangu amefariki,ย  kumshukuru na kumuomba Msamaha?” Watu wa karibu walianzaย  kututazama, Lidia alishtukia hilo akasemaย 

    “Nakuelewa Jacklin, naomba tukaongee hilo halina shida”ย  akaanza kutaka kunitoa pale kitu ambacho sikukubaliana nachoย 

    “Niacheeee! Niache Lidia Niache…” nilisema kwa sauti ya Juuย  ambayo ilimshtua kila Mtu, macho yote yalikuja upande wetu.ย  Bahati nzuri nilikuwa nimeonesha mgongo kule waliko akinaย  Osman hivyo aliyeonekana vizuri alikuwa ni Lidia, Dokta Simonย  haraka alikuja baada ya kumuona Mke wakeย 

    “Jacklin hukupaswa kuja hapa kabla mambo hayajaharibikaย  nakuomba urudi nyumbani, yote tutayaongea kule” Alisema Doktaย  Simon

    “Siwezi kuondoka hapa bila kuongea na Osman, hamjui ni jinsiย  gani naumia Mimi, hamjui ni jinsi gani Maisha yangu yamejaaย  majuto, ili moyo wangu uwe sawa ni lazima nionane na Osmanย  leo” nilisema kwa sauti ya Juu, Osman alinisikia, sauti yanguย  aliijuwa, alipiga hatua tatu mbele akiwa ameshikilia pete,ย  Zahra alimshika mkono kumzuia asije upande wangu! Hakunaย  aliyeshtuka kuwa nilikuwa ni Mimiย 

    Upande wa Familia ya Osman wote walisimama, taa ililetwaย  kwangu ili nionekane. Ilibidi nigeuke kutazama mbele ambakoย  Osman na Watu wengine walikuwepo, Mzee Dhabi alishtuka sanaย  kuniona, Osman alitumbua macho yake kwa Mshangao, hakutegemeaย  kama angeniona tena katika Maisha yake.ย 

    Dokta Simon na Mke wake walitazamana ni wazi hawakufurahiaย  Mimi kuwepo pale, chozi lilikuwa likinivuja, nilimtazma Osmanย  ambaye naye alikuwa bize kunitazama, Zahra aliuacha Mkono waย  Osman. Ukumbi mzima ulikuwa kimya sanaย 

    Nilichukua magongo yangu nikaanza kujongea kuelekeaย  aliposimama Osman, nilimuona akiwa mwenye mshituko mkubwaย  baada ya kugundua kuwa nilikuwa kilema wa mguu, hata Mzeeย  Dhabi na Mke wake nao walishangaa sana.ย 

    Nilisogea karibu na Osman nikiwa natabasamu kwa maumivuย  makali sana, Osman alidondosha chozi lakeย 

    “Jacklin?” Aliniita, niliitika kwa kutumia kichwa maana mdomoย  ulikuwa mzito sanaย 

    “Upo hai? Ulipatwa na nini, umepoteza Mguu?” Aliniuliza kwaย  hisia kali sana, nilitoa tabasamu lenye maumivu nikamwambiaย 

    “Nilipata ajali” nilitokwa na machozi nilishindwa kujizuiaย  kabisaย 

    “Mama yupo wapi?”ย 

    “Mama amefariki Osman”ย 

    “Mungu wangu! Mlienda wapi?” Aliuliza Osman, nilitaka moyoย  wangu uwe safi, nilimuonesha kidole Baba yakeย 

    “Baba yako alitufukuza kwenye ile nyumba, tulirudi Mtaaniย  ndipo yalipotukuta haya yote, naomba unisamehe Osman,ย  nilihitaji kukusaidia sana ila nilichelewa” Watu woteย  walimtazama Mzee Dhabi, ilitosha kuidhihirishia Dunia kuwaย  Baba yake Osman alitutendea Unyama!! Osman alimgeukia Babaย  yake akamuuliza

    “Baba ni kweli?” Aliuliza Osman akiwa anatiririkwa naย  machozi, Mzee Dhabi hakuwa na jibu zaidi ya kuinamia chini.ย 

    “Baba ulisema waliuza kila kitu na kuhama Mji, ulisemaย  haijulikani kama wapo hai au wamekufa, walikukosea nini Baba?ย  Kumbe mkatili kiasi hicho Baba yangu! Mungu ameamuaย  kukudhihirisha mbele za Watu wanaokuheshimu na kutaka kuwaย  kama wewe, ulitaka iwe hivi si ndiyo?” Alisema Osman kwaย  hisia kali ambayo hakuna aliyeweza kumzuiaย 

    “Osman imeshatokea! Hayo yamepita, nahitaji msamaha wako tu”ย  Nilisema.ย 

    “Jacklin nilishakusamehe tokea ile siku ambayo ulikataa kuwaย  Mke wangu, niliheshimu maamuzi na mawazo yako” Alisema Osman,ย  huzuni ilitanda pale ukumbini, wenye mioyo midogo waliliaย 

    “Baba ulitaka nimuowe Zahra kwasababu alikubali kutoa figoย  yake kwa ajili yangu? Ukasahau ndiye aliyesababisha jerahaย  ndani ya Moyo wangu, aliniacha katika wakati ambao nilikuwaย  sina chaguo lingine. Maumivu na mateso niliyoyapta ameyalipaย  kwa kutoa Figo lake, Hata Moyo wangu Baba unajuwa kuwaย  nampenda Jacklin, namuhitaji ila ulijaribu kumuweka mbali naย  Maisha yangu!” Alisema Osman kisha alinikumbatia, Huweziย  amini Zahra alilia sana pale chini, alitoka mbio akakimbiliaย  njeย 

    Mzee Dhabi na Mke wake walilia kwa maumivu makali sana.ย  Nilivyomkumbatia Osman nilihisi akiwa anapumua kwa shidaย  sana, alikuwa akitaka kusema neno ambalo nilitamaniย  kulisikia, neno ambalo hadi hivi leo sijui alikuwa anatakaย  kuniambia nini, alisizi kwenye mwili wangu bila kuhema tena,ย  ilikuwa ndiyo Pumzi ya Mwisho ya Osman katika hii Dunia,ย  hakuna aliyejuwa kuwa Osman alifia kwenye mwili wangu. Mzeeย  Dhabi alisogea na kupiga magoti akasemaย 

    “Osman! Nisamehe Mwanangu,,nisamehe kwa yote, nilifanya kwaย  hasira baada ya kuona amekataa kusaidia Maisha yako, nimekupaย  hasara Jacklin umempoteza Mama yako na Mguu wako naombaย  mnisamehe” Alisema Mzee Dhabi, ukimya wa Osman ulianza kunipaย  wasiwasi, nilimuacha lakini cha ajabu alienda chini kamaย  Mzigo, haraka gari ya wagonjwa ilifika, Osman alipelekwaย  Hospitalini. Sote tulienda kusubiria hatma ya Osman, kilaย  mmoja alikuwa kimya, nilikuwa mwingi wa kulia tu.ย 

    Masaa matatu Baadaye Dokta Simon alitoka chumba cha Wagonjwaย  mahututi, alitupa taarifa iliyoondoa uhai wa Bilionea Dhabiย  pale pale, Ndio, Osman alikuwa amefariki kwa mshituko naย  mfadhahiko. Mzee Dhabi na Osman walizikwa nyumbani kwaย Osman,,,nilimshukuru Mungu kwa kila jambo lililonifika kwenyeย  Maisha yangu. Nilipoteza kila kitu lakini Mke wa Bilioneaย  Dhabi aliniambia kuwa ananipa Nusu ya mali zote za Bilioneaย  Dhabi.ย 

    Nilipewa kila kitu nilichoahidiwa, japo havikuwa na thamaniย  ya kuzidi uhai wa Osman, Bilionea Dhabi, Mama na Mguu wangu.ย  Nilijiapiza kuwa sitokuja kupenda tena katika Maishaย  yangu.,,,,Miezi mingi ilipita, maumivu ndani yangu yalianzaย  kupona, niliwekewa mguu wa Bandia.ย 

    Siku moja asubuhi nikiwa naelekea JM Motors nikiwa kamaย  mmiliki wa kampuni hiyo ya Uuzaji wa magari, nilijikutaย  katika foleni eneo lile lile ambalo nilijikuta kwenye Foleniย  siku ya kwanza kabisa ambayo nilikuwa naenda JM Motors kuombaย  kazi, ndiyo siku ambayo nilikutana na Osman. Moyo wanguย  uliingiwa na maumivu makali sana, nikiwa nasubiria gariย  zianze kutembea, Mtu mmoja ambaye ni ombaomba aligonga kiooย  cha gari yangu! Nilikuwa ni Mtu ninayezijuwa shida sanaย  kutokana na Maisha niliyopitia, nilifungua kioo, moyoย  uliniripuka sana. Aliyegonga kioo alikuwa ni Mosses Mwanaumeย  niliyekuwa nampenda sana katika Maisha yangu, alikuwa haoniย  yaani kipofu wa macho yote mawili hivyo yeye hakujuwa alikuwaย  akimuomba pesa nani, sikujuwa alikuwa amekutwa na nini ilaย  hata vidole vyake vilikuwa vimekatika.ย 

    Nilimpa noti ya Shilingi Elfu tano, kisha aliondoka zake,ย  unajuwa kwanini nilimpa noti ya Elfu tano? Ni kwasababu ileย  siku aliniahdi kunitumia pesa ya pikipiki alafu hakunitumiaย  wakati huo Elfu tano yangu nilimpa marehemu Osman, nilisemaย 

    “Malipo ni hapa hapa Duniani Mosses, Kwaheri ya kuonana”ย  Nilifunga kioo kisha niliondowa gari yangu.ย 

    โ€ขโ€ขMWISHOโ€ขโ€ขโ€ข

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kununua SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxย  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho

    ย ย 

    Pumzi ya mwisho

    24 Comments

    1. Salma Tanga on October 28, 2024 5:08 pm

      Ongera nimeipenda

      Reply
    2. Siwema on October 28, 2024 5:11 pm

      Ila wewe dada!!!!

      Reply
    3. Fawziya Hassan on October 28, 2024 5:12 pm

      So sad ๐Ÿ˜ข
      Mapenzi ni ugonjwa usio na dawa
      Eeee Mwenyezi Mungu naomba unipe atakae nipenda kwa dhati kama mapenzi ya Osman kwa Jacklin.
      Stori ya kuhuzunisha yenye Mafundisho tosha na maumivu makali ndani yake.๐Ÿ˜ญ

      Reply
    4. Fawziya Hassan on October 28, 2024 5:14 pm

      Maskini Jacklin kapoteza kila kitu maishani mwake๐Ÿ˜ข

      Reply
    5. catherine Arod on October 28, 2024 5:14 pm

      ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญDah wow asee nimeipenda sana๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ hii episode imeniuma sana

      Reply
    6. Asaphnaah on October 28, 2024 5:15 pm

      ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
      • Sharo love malkx ๐Ÿ’– on October 28, 2024 5:39 pm

        Una jua yale maumivu ya kuchomwa msumari kwenye isia feck ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

        Reply
    7. AleFa on October 28, 2024 5:23 pm

      ๐Ÿ’ซ๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ซ

      Reply
    8. Charz jr๐Ÿ˜Ž on October 28, 2024 5:24 pm

      Appriciated @Kaka mkubwa
      Live long…uzidi kutupa madude mkuu๐Ÿ˜Ž๐Ÿค

      Reply
    9. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on October 28, 2024 5:38 pm

      Una jua yale maumivu ya kuchomwa msumari kwenye isia feck ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

      Reply
    10. Wahda on October 28, 2024 7:50 pm

      Nampa pongezi mwandishi kalamu yake amejua kuitendea haki Yuko vizuri ๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜๐Ÿ˜˜

      Reply
      • Minah on October 28, 2024 8:30 pm

        Kiukweli nimejifunza kitu asante mwandishi unajua unastahiri mauwa yako

        Reply
    11. G shirima on October 28, 2024 11:46 pm

      Tamu sana inajenga hisia fulani

      Reply
    12. G shirima on October 28, 2024 11:47 pm

      Chukua๐ŸŒน๐ŸŒบ๐ŸŒท๐Ÿฅ€ yako

      Reply
    13. Xalvan on October 29, 2024 1:14 am

      Kali kinoma

      Reply
    14. Hamza Mwalyawa on October 29, 2024 8:04 am

      Kaka mkubwa KWELI wewe ni kaka mkubwa umeumba ulimwengu wa kufikirika mpaka basi……. SASA WATENGENEZA FILAMU MPOWAPI? HAMONI MNANGOJA NINI?…SHIRIKIANENI NA KAKA MKUBWA!!! MTUTENGENEZEE DUDE JAMANIEE

      Reply
    15. Victor on October 29, 2024 1:49 pm

      Inagoma nkitaka kutuma hela….inasema no hii haijathibitishws

      Reply
    16. Jlarch on October 29, 2024 9:19 pm

      Aiseee hii simulizi ni nzuri sanaa ๐Ÿ†

      Reply
    17. Masotojo on October 29, 2024 11:55 pm

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H

      Reply
    18. Pangkid on October 31, 2024 8:42 pm

      SIMULIZI|Jinsi paka alivyomaliza familia yetu.
      Sehemu ya 1 na 2
      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/10/simulizipaka-wa-familia-sehemu-ya-pili.html

      Reply
    19. Pangkid on October 31, 2024 8:43 pm

      SIMULIZI|Jinsi paka alivyomaliza familia yetu.
      Sehemu ya 1 na 2
      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/10/simulizipaka-wa-familia-sehemu-ya-pili.html

      Reply
    20. Lilian on January 23, 2025 4:01 pm

      Simuliz nzuri sanaaa

      Reply
    21. John on January 23, 2025 4:33 pm

      Umetisha

      Reply
    22. Lycent on February 7, 2025 8:10 am

      Daaah nilitaman iendelee ila pongezi Kwa mwandishi kazi umeifanya vyema

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.