Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Tisa (09)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Tisa (09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 20, 2024Updated:September 22, 202418 Comments10 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Mama umemyoosha sana”Β 

    “Ndiyo dawa yake, mwache tu. Hawezi kufanya chochote kileΒ  sababu anajua una ujauzito wake, atakapo kuja kufungukaΒ  kiakili utakua umemaliza kila kitu, cha Msingi huyo MsichanaΒ  Mshikilie hadi mwisho.”Β 

    “Asante Mama kwa ushauri wako unanisaidia mno”Β 

    “Nisipokusaidia wewe nimsaidie Nani tena”Β 

    “Nahitaji kujisaidia” Matilda alipaza sauti yake, mara kiatuΒ  kikasikika kikija chumba alichokua amefungiwa, kikafunguliwa,Β  akaingia Mwanaume mmoja.. EndeleaΒ 

     

    SEHEMU YA TISA

    “Nimebwana, naomba kujisaidia” Akasema Matilda huku akianzaΒ  kujikojolea, Mlinzi akamwambia MatildaΒ 

    “Nenda haraka” Akasema na kumsindikiza hadi chooni, chooΒ  hicho kilikua cha ndani.Β 

    Alipoingia huko alikua tayari ameshasoma ni namna ganiΒ  anaweza akaondoka hapo, akapanda juu ya sinki kisha akapitaΒ  katika kitundu kidogo ambacho kilikua juu kilichotumika kamaΒ  Dirisha la Choo, akadondokea chini, yule Mlinzi akaendeleaΒ  kusubiria hapo huku mwenzake akiwa anamwita. Matilda akapataΒ maumivu kadhaa, jua lilikua linaanza kuzama, akatazama mbeleΒ  yake akaona ukuta ambao haukua mrefu sana, akafikiria kutumiaΒ  ukuta ili atimke hapo, akaparamia ukuta.Β 

    Mlinzi akaona dakika zinasogea akagonga mlango, akajibiwa naΒ  ukimya huku akianza kupata mashaka juu ya uwepo wa Matilda,Β  ikabidi afungue mlango, hakumkuta Matilda, akatazama paleΒ  kwenye kitundu akaona dalili za Mtu kupitia hapo, akapandaΒ  kwenye sinki akamwona Matilda akiwa anamalizia kuteremkaΒ  ukuta, akagongana naye macho. Matilda akajiachia, Yule MlinziΒ  akatoka chooni akampa taarifa yule Mlinzi mwingine kishaΒ  wakaelekea nje kwa ajili ya kuhakikisha wanamkamata MatildaΒ  jioni hiyo.Β 

    Matilda akajikuta yupo Msituni, akaanza kukata nyikaΒ  kuwakimbia walinzi hao ili asalimishe maisha yake, WalinziΒ  wakiwa na mbwa wakawa wanamfukuzia Matilda ambaye alionekanaΒ  kua na spidi kubwa sana, alikua kilomita kadhaa kutoka walipoΒ  walinzi. Akaendelea kukata nyika huku giza likiwa linaingia,Β  akawa amechoka sana, alikua hajui ni mahali gani alipo, hivyoΒ  alikua akikimbia kama mwendawazimu tu.

    “Mama nilitereza naomba unisamehe kwa hili, nilikosea kabisa,Β  nipo tayari kulipa kwa hili, nakiri Mimi ni Mtoto mpumbavuΒ  sana” Alisema James akiwa mbele ya Mama yake ambaye alikuaΒ  amekunja uso wake, watu kadhaa walikua wameshafika hapo kwaΒ  ajili ya Msiba wa Patra. Chozi na makamasi yalikua yakimtoka,Β  Mama Naomi akamwonea huruma sana, akamtazama Mama JamesΒ  lakini hakua na nguvu ya kusema chochoteΒ 

    “Mamaaaaa!” akaita James huku akizidi kudondosha chozi, MamaΒ  yake alikua kimya sana akiwa anatazama pembeni, kwa hasiraΒ  aliyokua nayo hakutaka kabisa kumtazama JamesΒ 

    “Mama James, rudisha moyo wako nyuma, huyu ni Mtoto,Β  ameteleza” Akasema Mchungaji George ambaye alikua bega kwaΒ  bega na familiaΒ 

    “Tunazungumzia Maisha ambayo hayawezi kurudi, yule Binti,Β  hawezi kurudi kwa namna yoyote ile, na Mama yake piaΒ  asirudi?” akauliza Mama yake James huku akiwa amekaza machoΒ  yake kwa Mchungaji George, Mchungaji akameza funda la mate,Β  swali aliloulizwa lilimfanya akae kimya.Β 

    Chozi na jasho vilikua vikivuja kwa pamoja, James alijitahidiΒ  sana kumwomba Mama yake amsamehe lakini Mama JamesΒ  akashikilia msimamo kua hawezi kumsamehe hadi MatildaΒ  aonekane. James akaondoka hapo Usiku

    Hekaheka ndani ya Msitu ilikua ikiendelea, Matilda aliendeleaΒ  kuwakimbia wale walinzi wa Neema, alichoka akaamua kujibanzaΒ  nyuma ya Jiwe kubwa, walinzi nao walikua wameshachoka hukuΒ  wakihimizana kua kabla ya jua kuchomoza wahakikishe kuaΒ  wamempata Matilda.Β 

    Matilda akalala hapo Msituni hadi siku iliyofuata, alipoamkaΒ  akaendelea na safari ya kutafuta msaada wa kutoka hapoΒ  Msituni, akakatiza vijito na majabari makubwa na madogo hukuΒ  akiwa hajui ni wapi anaelekea.Β 

    Moyoni mwake akawa anasema na Mungu wake kua amlinde BintiΒ  yake, Masikini hakujua kua Binti yake alikua ameshafariki,Β  ghafla akasikia sauti za Mbwa akajua anapaswa kuongeza mwendoΒ  wa kuendelea kuutafuta Msaada, akakimbia umbali mrefu akiwaΒ  na njaa na kiu ya Maji akajikuta akianguka baada ya kuhisiΒ  kizunguzungu.Β 

    “Eee Mungu nilinde” Akasema Matilda, akahisi giza kishaΒ  akapoteza fahamu.Β 

    “Babu kinachofuata ni kitu gani?” Akauliza Neema, Babu naΒ  Mama yake wakiwa mbele yakeΒ 

    “Mtoto akizikwa habari yake itakua imeisha pia, James anaendaΒ  kua mali yako bila kipingamizi chochote kile, hili ndiyoΒ  jambo kubwa” Akasema Babu yake Neema, wakafurahi sanaΒ 

    “Yaani Babu kama tutafanikisha hili nakuahidi kua nitakupaΒ  zawadi ambayo hutonisahau” Akasema NeemaΒ 

    “Huna haja ya kuahidi sababu wewe ni Mjukuu wangu Neema,Β  kikubwa upate unachohitaji, ukipata wewe Mama yako amepata,Β  basi ndiyo furaha yangu hiyo”Β 

    “Pamoja na hayo Babu nitahakikisha nakujengea nyumba yaΒ  kifahari, nitakua na pesa nyingi” Alisema Neema. Mama NeemaΒ  alikua Mtu wa kutabasamu tu akimwangalia Mwanaye na Babu yakeΒ  wakiwa wanazungumza, kicheko chao kilikua kilio upande waΒ  Mama James ambaye kila alipofikiria jinsi mambo yalivyoendaΒ  alijikuta akiangusha kilio cha Mtu mzima.Β 

    Moyoni alijua kua kuendelea kuzuia Mtoto kuzikwa ni sawa naΒ  kumtesa Mtoto huyo lakini moyoni pia alikua akiumia MtotoΒ  kuzikwa bila Mama yake kuwepo, aliona ni sawa na kuzuia hakiΒ  ya Msingi ya Mama Patra, lakini hakuna aliyejua kilichokuaΒ  kikiendelea, Matilda alikua akipigana vita Msituni.

    “Nipo wapi?” Akauliza Matilda baada ya kujikuta akiwa kwenyeΒ  nyumba moja ambayo ilikua imeezekwa makuti, hakuna aliyeΒ  mbele yake bali kitanda na ukuta uliojengwa kwa udongo waΒ  kugandika. Akakohoa kidogo, haraka akaingia Mzee Mmoja ambayeΒ  alikua na ndevu ndefu, chafu zenye Mg’ao wa fedha, alikua naΒ  rasta pia, Matilda akaogopa sana, wakati anajisogeza pembeniΒ  akajikuta shuka ikiwa inamvuka, ndipo akagundua kua alikuaΒ  hana nguo yoyote ile, akarudisha macho kwa mzee kwa MshangaoΒ 

    Mara, akaingia Bibi mmoja ambaye alionekana wazi kua ni MkeΒ  wa Mzee huyo.Β 

    “Usiogope Binti, Nilikukuta ukiwa hujitambui nikakusaidia”Β  Akasema Mzee huyo, Bibi akaketi pembeniΒ 

    “Na wale watu waliokua wakinifukuzia?” Kwanza Bibi akacheka “Walishambuliwa na jeshi langu” Akasema Mzee huyo “Jeshi lako, unamaanisha nini?”Β 

    “Siafu waliwashambulia walipotaka kukuchukua, wakakimbiaΒ  ndipo nikakusaidia” Hadithi hiyo ikamshtua sana Matilda.Β 

    “Umepoteza fahamu kwa zaidi ya masaa matano, unahitajikaΒ  kupumzika zaidi ili kuvuta nguvu, lakini kwanini wale WatuΒ  walikua wakikufukuzia?” Akauliza BibiΒ 

    “Ni stori ndefu sana” Akasema Matilda baada ya kuona watu haoΒ  si wabaya kwake, akawasimulia kilichotokeaΒ 

    “Pole lakini unaonekana bado una tumaini kwa hayo unayopitia,Β  bado una Muda wa kurekebisha mengi” Akasema Babu huyo,Β  Matilda akaketi vizuriΒ 

    “Unamaanisha nini Babu”Β 

    “Ulipokua umelala nilifanikiwa kuyaona yanayokuzunguka,Β  usishtuke sababu ipo Dunia isiyoonekana, ni Dunia ambayoΒ  mambo huenda haraka mno, huyo Mtoto unayemzungumzia hapa yupoΒ  kwenye usingizi mzito sana, hawezi kuamka kirahisi sababuΒ  nguvu kubwa imetumika kumlaza” Akasema Babu huyo, MatildaΒ  akashtuka sana

    “Usingizi?, kwanza niko wapi hapa nataka kwenda kumwona BintiΒ  yangu”Β 

    “Hapa ni Mkata”Β 

    “Mkata?”Β 

    “Ndiyo, kilomita kadhaa kutoka hapa kuna barabara ambayoΒ  inaelekea huko ulikotoka”Β 

    “Umesema kuhusu Usingizi, sijakuelewa”Β 

    “Namaanisha Mtoto wako amekufa katika Dunia hii lakiniΒ  anaishi kuzimu” Matilda akazidi kushtuka, aliyokua akiambiwaΒ  yalimpa Mshtuko mkubwa sana, chozi likaanza kumtokaΒ 

    “Mtoto wangu amekufa?”Β 

    “Ndiyo lakini usilie sababu bado hajaondoka, mwili umekufaΒ  lakini nafsi inaishi kuzimu, kikubwa unatakiwa kuwahi kablaΒ  hajazikwa”Β 

    Wazee hao wakamwambia mengi sana Matilda, wakampa chupa yaΒ  Maji, wakamwambia kua akifika anyunyize maji kwenye mwili waΒ  Binti yake, ataamka na kua sawa kabisa.Β 

    Haikuishia hapo, wakampa nauli ya kurejea Dar.

    “Mchungaji, naona namtesa Mjukuu wangu, hakuwa na kosa loloteΒ  sitaki aendelee kuteseka zaidi. Kesho Patra azikwe” AkasemaΒ  Mama yake James, alizungumza mbele ya JamesΒ 

    “Asante Mama, najiona nimepoteza thamani kubwa sana katikaΒ  Maisha yangu. Nitamtafuta Matilda kadiri ya uwezo wangu Mama”Β  Akasema James, Siku iliyofuataΒ 

    Taratibu za Mazishi zikafanyika, mwili wa Patra ukawekwaΒ  kwenda sanduku, vilio vilitawala, familia ilizizima, JamesΒ  alilia sana mbele ya sanduku la Patra, alijutia sanaΒ  kumkataa, akatamani hata aamke ili amuombe msamaha BintiΒ  yake, kila aliyefika aliona ni jinsi gani James alikua katikaΒ  hali mbaya sanaΒ 

    Mchungaji George akaongoza maombi ya ibada ya mazishi yaΒ  Patra, hatimaye sanduka la Patra likawa linashuka taratibuΒ  kuelekea chini, ikasikika sauti ikisema

    “Patraaaaaaaa” Ilikua ni sauti iliyotambulika kwenye masikioΒ  ya walio wengi, vilio vilikoma, hakuna aliyeamini, walimwonaΒ  Matilda akiwa ameshikilia chupa aliyopewa kule MsituniΒ 

    “Msimzike Binti yangu bila kumwona” Alisema Matilda,Β  Mchungaji akawaamuru waliokua wakishusha sanduku kulirudishaΒ  juu, Matilda akakimbia hadi kwenye sanduku la Patra, kishaΒ  akageuka na kuwaambiaΒ 

    “Patra hajafa msimzike” Alisema akiwa anatokwa na mchoziΒ 

    Ni kama watu walipigwa Bumbuwazi, hakuna aliyesema chochoteΒ  zaidi ya Mchungaji George ambaye alimuuliza MatildaΒ 

    “Unasema nini Matilda, Mtoto amekaa kwenye jokofu kwa sikuΒ  tatu. Ulikua wapi?” AkaulizaΒ 

    “Mchungaji, moyo wangu unaniambia nimwone kwanza Mtoto ndipoΒ  nieleze kilichotokea, chozi la James lilijikuta likikaukaΒ  lenyewe kutokana na Mshangao ambao alikua nao, minong’onoΒ  ikaanza kusambaa miongoni mwa waliofika Kwenye mazishi.Β 

    Mchungaji akawaambia walifungue sanduku ili Matilda amwoneΒ  Mtoto wake, sanduku likafunguliwa, Matilda akafungua chupa yaΒ  Maji akanyunyiza kwenye sandukuΒ 

    “Unafanya nini?” Akauliza Mchungaji GeorgeΒ 

    “Patra ataamka sasa hivi” Alisema Matilda, Mchungaji akaonaΒ  Matilda amechanganikiwa, akawaamuru wannaume kumshika MatildaΒ  ili Sanduku lifungweΒ 

    “Mchungaji mwanangu ni mzima naomba Msimzike” alisemaΒ  Matilda, ukimya ukatawala kwenye sanduku, alichotegemeaΒ  Matilda kilikua ni sawa na njozi ya mchana, Patra hakuamkaΒ  kama alivyofikiria, akaanza kuona wale wazee walikuaΒ  wamemuongopea, alilia sana huku utaratibu wa kulifungaΒ  Sanduku ukifanyika, Mama Naomi akamwambia MatildaΒ 

    “Mtoto amekufa Matilda hawezi kurudi” Mchungaji akamsogeleaΒ  Matilda akamwambiaΒ 

    “Huu ni mwisho wa Patra lakini siyo mwisho wa Maisha yako,Β  pole kwa msiba”Β 

    Katika hali ambayo kila mmoja alistaajabu, Patra akaamkaΒ  kwenye sanduku na kukaa kitako kitu ambacho si tuΒ kilimfurahisha Matilda bali kilimshtua, tokea amezaliwaΒ  hakuwahi hata kukaa lakini aliamka na kuketi kiisha akaanzaΒ  kushangaa watu. Wasio na moyo wa ujasiri walikimbizanaΒ  Makuburini, wachache wakabakia.Β 

    Muda huo Babu yake Neema alikua amepata ishara mbayaΒ  akamwambia NeemaΒ 

    “Nenda Muhimbili kaokote kile kitu kakitupe jalalani harakaΒ  sana”Β 

    “Babu kwanini unasema hivyo?” Akauliza NeemaΒ 

    “Nenda Neema fanya haraka sana” Akasistiza Babu yake Neema,Β  haraka Neema akakodi Pikipiki ili awahi Muhimbili,Β  haikuchukua muda mrefu, akawa amefika Muhimbili, akakimbiliaΒ  mahali ambapo alitupa kile kitu, kabla hata hajakiokotaΒ  kikawaka na kumwingia machoni, akawa anapiga keleleΒ  akilalamika kua haoni, haraka akasadiwa kupelekwa KwaΒ  Daktari.Β 

    Familia ikawa imekaa, kila mmoja akistaajabu maajabu ya MtuΒ  aliyekufa kurejea tena kwenye Maisha, ukimya ukawa mwingiΒ  sana. Matilda akaanza kuwasimulia kila kitu, siku hiyo ndiyoΒ  ikawa siku ya kumwona Mama yake James, huwezi amini PatraΒ  alikua ni Mtoto mrembo sana, akitabasamu ni James Mtupu,Β  James akaomba Msamaha na kuahidi kua atafunga ndoa na MatildaΒ  na kumlea Mtoto.Β 

    Zikapita siku tatu mambo yakawa shwari, furaha na amaniΒ  ikazidi kutamaraki, kwa shukurani, James akampatia Mama NaomiΒ  ile nyumba aliyokua akiishi Matilda, akampa pesa pia kwaΒ  ajili ya kuanza Biashara. Siku moja akiwa ofisini akapokeaΒ  simu ya Mama Neema, alivyopokea akaambiwa kua Neema amepofukaΒ  macho, James akamwambia kua ataenda kumwona.Β 

    Baada ya kazi akaenda Hospitalini kumwona Neema, Mama NeemaΒ  akiwa analia sana kwa kile kilichomfika Binti yake.Β 

    “Mama huna haja ya kulia, Mimi nimelia sana, Matilda ameliaΒ  sana, Mama yangu amelia sana. Siku zote Mshahara wa dhambi niΒ  umauti Mama”Β 

    “Lakini James, Neema ana Mtoto wako tumboni, hupaswiΒ  kumhukumu moja kwa moja”

    “Namshukuru Mungu sababu amefumbua fumbo zito sana, sikuwahiΒ  kuwa na thamani kwenu hata kwa yale makubwa niliyowafanyia,Β  nilikua mjinga sijui hata nilikwama wapi hadi nikamkataaΒ  Mtoto wangu wa damu” Akasema James kisha akataka kuondokaΒ 

    “James, naomba msaada kama Mama, Neema anatakiwa kwendaΒ  kutibiwa India, sina pesa hiyo Mwanangu, msaidie kwa hilo tu”Β 

    “Siwezi kumsadia adui anayewinda Maisha yangu, alie mbele yaΒ  Mungu wake, amwombe amsamehe” Akasema James kisha akaondoka,Β  Mama Neema akalia sana huku akijilaumu kwa kusema ni ujingaΒ  wake kwani yeye ndiye aliyekua akimshauri vibaya Binti yake,Β  akaona ni bora kufa kuliko kuendelea kumwona Neema akiwaΒ  kipofu, akaondoka Hospitalini na kumwacha Neema akitesekaΒ  kwenye kutanda cha Hospitalini ya Muhimbili.Β 

    MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Β 

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    18 Comments

    1. Lus twaxie on September 20, 2024 4:14 pm

      Adminiiiiiiiii hongera sanaaa πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³πŸ₯³ dah mwisho mzuri ..kesho anza riwaya nyingine

      Reply
      • G shirima on September 20, 2024 7:50 pm

        Kama move kabisa yaani dah nyingine ije mbio basi

        Reply
    2. Daniel on September 20, 2024 4:18 pm

      Kali sana

      Reply
      • Zainabu on September 20, 2024 4:51 pm

        Safi sana mwisho nzur riwaya ilikuwa πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

        Reply
    3. Najma muya on September 20, 2024 4:56 pm

      Daah riwaya nzuri Sana

      Reply
    4. Tyson on September 20, 2024 5:32 pm

      dah story moja nzuri sana

      Reply
    5. Pauline on September 20, 2024 5:40 pm

      Asante Mungu wamepata wanachostahiliπŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    6. Sir yowas on September 20, 2024 5:43 pm

      Mmmmmmm,, mbona imeisha kama inaendelea????????!!?????

      Reply
    7. Cesilia Nkunga on September 20, 2024 5:45 pm

      Big up Admin!
      Riwaya unazotupatia zinatupa fundisho katika maisha halisi yanayotuzunguka.

      Reply
    8. Dickson kikungwe on September 20, 2024 5:47 pm

      Hongera sana mkuu kwa story nzuri sana

      Reply
    9. Zakayo Mngulu on September 20, 2024 7:01 pm

      Dah hatari sanaaaaa

      Reply
    10. G shirima on September 20, 2024 7:52 pm

      Kama move kabisa yaani dah nyingine ije mbio basi

      Reply
    11. Lucas George on September 20, 2024 8:34 pm

      πŸ”₯πŸ”₯ sio powa imeisha kama utani

      Reply
    12. Xavi on September 20, 2024 8:49 pm

      Hongera san kiongozi πŸ‘ŠπŸ‘ŠπŸ‘Š

      Reply
    13. Xavi on September 20, 2024 8:51 pm

      Tujitahid kumtunza admin asivunjike moyo wakutupa madini mazuri kma hya

      Reply
    14. Irene on September 20, 2024 9:27 pm

      😍😍❀️

      Reply
    15. Muharram on September 20, 2024 10:00 pm

      Admini safi kesho anza nyengine

      Reply
    16. Juma on September 23, 2024 9:30 am

      Imeisha vibaya wazaz wake ma patra je

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.