Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Tatu (03)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Tatu (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 14, 2024Updated:September 18, 202410 Comments11 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “James!! tumepima DNA na majibu unayajua kua Patra ni MtotoΒ  wako, kwanini damu yako unaiacha iteseke kisa ulemavu?”Β  alisema Matilda, alipigwa kofi hadi waliokua karibuΒ  walishtukaΒ 

    “Wewe Mshenzi sitaki urudie hiyo kauli, nakwambia nitakufanyaΒ  kitu kibaya endapo utaendelea kusema kua yule kiwete ni MtotoΒ  wangu, Mtoto halali kwangu atazaliwa kwa Neema na siyoΒ  vinginevyo, kwanini unapenda kuniharibia siku Mjinga wewe?”Β  alifoka James, japo alikua kijana mtanashati lakini alikua naΒ  hasira sana.Β 

    Matilda alikasirika, sababu alipigwa mbele za Watu, MamaΒ  Naomi alikua akiona pia japo alikua kwa mbali kidogo lakiniΒ  ilikua ni aibu kubwa, alikimbilia Hospitalini. James nayeΒ  aliondoka huku akiacha minong’ono kwa kilichotokea hapo,Β  aliondoa gari haraka sana.Β  EndeleaΒ 

    SEHEMU YA TATU

    Mama Naomi akamkimbilia Matilda kujua kwanini James alifikiaΒ  uamuzi wa kumpiga, hakuna alichokizungumza Matilda sababuΒ  bado alikua akilia kutokana na kilichotokea, MwanaumeΒ  aliyesababisha akatoroka kwao, akawapa Mawazo wazazi wakeΒ  aliishia kumpiga na siyo kujali hali ya Mtoto kisa tu ulemavuΒ 

    “Matilda usilie hebu nieleze kimetokea nini hadi akakupiga?”Β  aliuliza Mama NaomiΒ 

    “Niache Mama Naomi, ilipofikia nimechoka na mateso ya hiiΒ  Dunia ni bora hata nife tu” Alisema kwa hasira Sana MatildaΒ  huku akilia kwa uchungu sana.

    “Huo ni uamuzi wa kijinga sana Matilda, ukifa Patra atazidiΒ  kuteseka, angalia jinsi anavyoteseka sasa hivi je ukifaΒ  itakuwaje?”Β 

    “Sasa nitakaa nikimwangalia Binti yangu akifa mbele ya machoΒ  yangu alafu Baba yake akiwa na uwezo wa kumsaidia lakiniΒ  hafanyi hivyo, ni bora kufa kuliko kumwangalia Patra akifa”Β  Alisema Matilda.Β 

    “Nakuomba Matilda kwasasa turudi nyumbani tutafakari jinsi yaΒ  kuipata pesa ya Matibabu, hebu nyanyuka” Mama NaomiΒ  alimnyanyua Matilda kisha aliondoka naye.Β 

    ********Β 

    “Mimi nina wao wazo Matilda, kwanini usiende kanisani kwenuΒ  ukaomba Msaada kwa waumini wakakusaidia?” alisema Mama Naomi,Β  yalipita Masaa matatu baada ya kurejea nyumbaniΒ 

    “Wataweza nisaidia kweli?”Β 

    “Ndiyo nina imani kubwa watakusaidia sababu wewe ni MuuminiΒ  mwenzao”Β 

    Ushauri wa Mama Naomi aliufanyia kazi, jioni ilipoingiaΒ  alienda kanisani, wengi walimshangaa maana baada yaΒ  kujifungua hakuonekana tena kanisani, aliofahamiana naoΒ  walikua wakimuuliza jinsia ya Mtoto, Maswali ya kuhusu MtotoΒ  yalizidi kumfanya Matilda ajisikie vibaya sana.Β 

    “Mbona unalia?” aliuliza Mchungaji mara baada ya MatildaΒ  kufika ofisini kwa mchungaji wa kanisaΒ 

    “Mchungaji Mtoto wangu” Alisema Matilda, Mchungaji alishtukaΒ  akamuulizaΒ 

    “Mtoto wako amefanyaje?”Β 

    “Mchungaji Mtoto wangu Mimi” Sauti ya kilio ya MatildaΒ  ilisikikika na kumfanya Mchungaji aingiwe na maswali mengiΒ  kichwaniΒ 

    “Matilda Mtoto wako amefanya nini, hebu punguza kuliaΒ  uniambie” Alisema Mchungaji kwa sauti iliyojaa upole wa HaliΒ  ya juu sana, kwikwi ilimshika sana Matilda kila alipotakaΒ  kusema alijikuta akishindwa, kilio kilimuandama katika kilaΒ  neno alilohitaji kuzungumza, Mtandio wake aliutumia kufutaΒ  chozi lililomiminika kwa wingi, moyo wake ulijawa na simanziΒ  ya hali ya juu sana.Β 

    “Matilda tambua unanichanganya sana Mimi, sielewi hata niniΒ  unataka kuzungumza. Nakuomba acha kulia sababu ukilia MimiΒ  siwezi kujua kilichokusibu” Alisema tena Mchungaji wakati huoΒ  Matilda akiwa ameegemea Meza akiwa analia, hata MchungajiΒ  alilengwa na Mchozi kwa jinsi ambavyo Matilda alikua akiliaΒ  kwa uchungu, dakika tano zilikatika Matilda akishindwa kusemaΒ  chochoteΒ 

    “Unasikia Matilda, kua na imani hakuna kinachomshinda MunguΒ  aliye hai, nijuze Mimi ili tujue tunakusaidiaΒ Β 

    vipi….Unasikia….” Mchungaji alirudia kumbembelezaΒ  Matilda, angalau kilio kilianza kupunguaΒ 

    “Na hapo shavuni umekumbwa na nini?” Aliuliza Mchungaji,Β  shavuni Matilda alikua na alama ya kofi alilopigwa na JamesΒ  kule Hospitalini.Β 

    “Mchungaji napitia wakati Mgumu sana katika Maisha yangu,Β  Mtoto wangu yupo Hospitalini..” Matilda alijikaza akazungumzaΒ 

    “Ulipotea kanisani kila Mtu akawa anajiuliza upo wapiΒ  Matilda, kumbe ulijifungua….Enhee nini kinamsumbua MtotoΒ  wako?” Aliuliza Mchungaji ambaye alionekana kua na umriΒ  mkubwa, ngozi nyeusi na mvi iliyokolea vizuri kichwani, akiwaΒ  amevalia mavazi ya kanisa na msalaba mkononi.Β 

    “Mtoto wangu ni Mlemavu, anasumbuliwa na Mapafu, anahitajikaΒ  kufanyiwa upasuaji na kibaya zaidi Baba yake Amemkana”Β  Alisema Matilda, kilio kilianza upya baada ya kumalizaΒ  kumuelewesha Mchungaji ambaye alishikwa na butwaa, MatildaΒ  alikua Muumini wa kabisa hilo sababu hata kwao alikotokaΒ  alikua Binti wa kanisa hivyo alivyofika Dar alijiunga naΒ  kanisa pia.Β 

    “Yesu kristo! pole Binti yangu Matilda, hakuna linalomshindaΒ  Mungu wetu aliye hai, yeye halali kwa ajili yetu, Mtoto yupoΒ  Hospitali gani?”Β 

    “JM Hospital, inahitajika Milioni nane aweze kufanyiwaΒ  upasuaji, hapa nilipo sina hata senti tano na kadiri sikuΒ  zinavyozidi kwenda tumaini la Binti yangu kua hai linazidiΒ  kupotea” Alisema Matilda akizidi kulia kaa uchungu sana.Β 

    “Twende kwanza Hospitali kwa ajili ya maombi, baada ya hapoΒ  kanisa litaangalia utaratibu wa kukusaidia” Alisema MchungajiΒ  akiwa ameshasimama,

    “Asante Mchungaji George” Alisema Matilda, waliondoka hapoΒ  kanisani kuelekea Magomeni Mapipa ilipo Hospitali ya JM,Β  waliondoka kwa gari maalum ya kanisa, Wakiwa barabaraniΒ  Mchungaji alimwambia MatildaΒ 

    “Hili jambo litaisha kwa namna nzuri Matilda, kua na imaniΒ  thabiti usitetereke. Kupitia Mtihani huu shetani anawezaΒ  akajipenyeza na kukuingiza kubaya zaidi endapoΒ  hautojiimarisha kiimani” Matilda aliitikia kwa kichwa kishaΒ  alijishika tama.Β 

    ********Β 

    “Una uhakika?” lilikua ni swali aliloulizwa Neema, alikuaΒ  kituo cha polisi.Β 

    “Ndiyo sababu yeye ndiye anayeishi pale” alisema Neema kwaΒ  kujiamini kisha akatoa kitita kidogo cha pesa kwa siri sana,Β  Polisi akatabasamu sababu ilikua ni ishara kua alichokuaΒ  akikizungumza Neema kilihitaji kutengenezwa zaidi ili kiweΒ  kikubwa.Β 

    “Jina lako?” Aliuliza Polisi akiwa anaandika jalada la kesi “Neema Ngushi, Miaka 32”Β 

    “Mshtakiwa?”Β 

    “Matilda John, Miaka 28” Alisema NeemaΒ 

    “Vitu vilivyopotea vina thamani gani?”Β 

    “Milioni 16” Alisema tena NeemaΒ 

    Baada ya kumaliza kuandika maelezo marefu aliyoyatoa, alipewaΒ  RB ya kumkamata Matilda, alichofanya Neema ni kwendaΒ  kumfungulia kesi ya upotevu wa vitu kwenye nyumba anayoishiΒ  Matilda, hakutaka kuendelea kumwona Matilda katika MaishaΒ  yake, pembeni alikua amesimama Mwanaume mmoja ambaye kaziΒ  yake ilikua ni kutingisha kichwa tu.Β 

    Alipohakikisha amemfungulia kesi, walitoka na Mwanaume huyoΒ  wakaingia kwenye gari, wakaondoka kituo cha polisi.Β 

    “Unajua huyu Mwanamke anaweza kua kikwazo kikubwa sababuΒ  James alikiri kua Mtoto ni wake lakini anaona aibu kuleaΒ  Mtoto ambaye ni kiwete, sasa hofu yangu ni kwamba akili yaΒ  Matilda ikifunguka alalfu akaenda kudai haki, huwenda JamesΒ  akajirudi kwake sababu atatakiwa kumtunza Mtoto kwa lazima naΒ  pengine akachukuliwa hatua za kisheria alafu MimiΒ  nikahangaika” Alisema Neema akiwa anaendesha gariΒ 

    “Hapo usiwe na huruma hakikisha unamsotesha hadi akili imkaeΒ  sawa, James akijua itakuaje?”Β 

    “Hata akijua hawezi kufanya chochote sababu nimeshamwambiaΒ  kua nataka nitengeneze mchezo ili Matilda akubali kurudi kwaoΒ  Njombe” Alisema NeemaΒ 

    “Bingoo!!! Sasa tunaenda wapi?”Β 

    “Naenda kukuacha kwako Sadam alafu Mimi nirudi nyumbani,Β  kesho tunamkamata Matilda, naamini kitisho hiki kitamfanyaΒ  akubali kurudi kwao”Β 

    “Umetisha sana hakika wewe ni jembe la kujivunia Neema”Β  Alisema Mwanaume huyo kisha akaweka Mkono wake kwenye paja laΒ  Neema ambaye alikua na Ujauzito wa Miezi mitatu tu.Β 

    *****Β 

    Saa 12 Jioni, Gari ya kanisa ilikua ikiingia kwenye geti laΒ  Hospitali ya JM Magomeni Mapipa, Matilda alikua amelia sanaΒ  hadi macho yalimvimba, wakashuka na kuelekea Nje ya chumbaΒ  ambacho Patra alikua amelazwa, Macho ya Mchungaji na Macho yaΒ  Matilda yaligongana na macho ya Daktari ambaye alikua akitokaΒ  ndani ya Chumba hicho.Β 

    “Dokta samahani hali ya Mwanangu inaendeleaje?” aliulizaΒ  Matilda kwa presha.Β 

    “Matilda Mtoto anaendelea vizuri kwasasa, aliamka kishaΒ  akalala hadi sasa hivi”Β 

    “Tunaweza kumwona?”Β 

    “Ndiyo lakini hampaswi kumsumbua” Alisema Dokta akiwaΒ  anaondokaΒ 

    “Asante Dokta, Mchungaji twende” Alisema Matilda kishaΒ  alifungua mlango wa chumba hichoΒ 

    “Mwanangu!!” Alisema Matilda baada ya kumwona Binti yakeΒ  akiwa anapumulia Mashine, Roho ilimuuma sana.

    “Oooh Jesus” Alisema Mchungaji, Chozi likaanza kumbubujikaΒ  tena Matilda, alikua Mtu wa kulia kila dakika kwa namnaΒ  ambavyo hali ya Binti yake ilikua, Mchungaji akamwambiaΒ  MatildaΒ 

    “Kulia hakusaidii chochote, ngoja tufanye kwanza Maombi iliΒ  tumkabidhi Mtoto huyu na hali yake mbele za Mungu” AlisemaΒ  Mchungaji GeorgeΒ 

    Alianza kufanya Maombezi kwa Mtoto Patra, aliomba kwa imaniΒ  kubwa sana, Matilda naye alizama kwenye Maombi akisaidiana naΒ  Mchungaji huyo, maombi yalifanyika kwa sauti ya chini sanaΒ  ili wasimsumbue Mtoto kama ambavyo Daktari alikua amewaambia.Β  Zilitumika dakika arobaini na tano hadi kumaliza kumwombeaΒ  Patra, Jasho lilikua likimvuja Mchungaji huyo ambaye kilaΒ  alivyomwangalia Patra alijiskia vibaya sana kwa jinsi hli yaΒ  Mtoto huyo ilivyokua.Β 

    “Mungu amepokea Maombi Matilda, anaenda kutenda kwa ajiliΒ  yako na Mtoto, atafungua minyororo ya mateso kwa Mtoto huyu,Β  amini kua amekwisha kombolewa” Ilikua ni kauli ya kutia moyoΒ  ya Mchungaji huyo ambaye alikua amemshika bega Matilda, maraΒ  aliingia Daktari akawaambia Muda umeisha.Β 

    “Baby leo nimefanya kitu ambacho kitakuondolea hasira sana”Β  Alisema Neema akiwa anakula embe bichi, alikua akimwambiaΒ  James wakiwa chumbani Usiku.Β 

    “Jambo gani hilo?”Β 

    “Ni kuhusu Matilda”Β 

    “Sitaki hata kumsikia huyo Mwanamke Neema, katika MaishaΒ  yangu sijawahi pata ona Mwanamke King’ang’anizi kama Matilda”Β  Alisema kwa hasira James, alionesha wazi hataki kusikiaΒ  kuhusu Matilda ambaye alitoka kumpiga Kule Hospitalini.Β 

    “Usikasirike sababu hili jambo litaenda kumfanya aondoke hapaΒ  Dar bila kupenda Bby”Β 

    “Nakusikiliza”Β 

    “Hii hapa ni RB ya kumkamata kwa kosa la wizi wa vitu kwenyeΒ  ile nyumba, naamini akilala polisi siku moja akili itamkaaΒ  sawa” Alisema Neema kisha alimpatia Karatasi kutoka polisi,Β  James akaisoma kwanza kabla ya kusema Chochote, kishaΒ  akamtazama Neema

    “Umemfungulia kesi?”Β 

    “Ndiyo!! lengo langu apate kitisho kitakachomfanya aiyone DarΒ  chungu, nimefanya hivyo sababu sitaki kumwona Baba MtotoΒ  wangu mtarajiwa anakosa raha” Alisema Neema, JamesΒ  alitabasamu sababu aliitwa Baba Mtoto, alihitaji sana MtotoΒ 

    “Mbinu yako ni bora sana Neema, naamini kwenye hiliΒ  hachomoki, ataondoka hapa Dar atake asitake, tena kwa kuondoaΒ  kero nitampatia na pesa ya kuanzia Maisha huko aendapo”Β  Alisema James kwa furahaΒ 

    “Umeona jinsi gani nakupenda, nakuhitaji na pia nakuthamini,Β  furaha yako ndiyo furaha yangu Mpenzi” Alisema NeemaΒ  akiendelea kula embe kwa chumvi.Β 

    Neema alishajua udhaifu wa James, wala hakutumia nguvu nyingiΒ  kumfanya James afurahi, ni kumweleza tu kuhusu ujauzito,Β  alichotaka alipewa bila hata kulazimisha.Β 

    Siku iliyofuata, Neema alienda kituo cha polisi akaonana naΒ  yule polisi ambaye aliandika jarada la kesi ya Matilda,Β  akaomba askari kwa ajili ya kwenda kumkamata Matilda, akapewaΒ  askari polisi wawili akaenda nao moja kwa moja JM Hospital.Β 

    Muda huo Matilda alikua kanisani, zoezi la kukusanya pesa kwaΒ  ajili ya kuratibu matibabu ya Patra lilikua likiendeleaΒ  kanisani hapo chini ya uangalizi wa karibu wa MchungajiΒ  George ambayo alimwambia Matilda kua atasimama naye bega kwaΒ  bega hadi Patra apone, Mama Naomi alikua miongoni mwa WatuΒ  waliofika kanisani hapo baada ya kupewa taarifa na MatildaΒ  kua litaendeshwa zoezi la Uchangiaji wa matibabu ya Patra.Β 

    Chozi halikuacha kutoka kwenye macho ya Matilda baada yaΒ  kuona uchangwaji wa pesa hiyo, muitikio ulikua mkubwa sanaΒ  kiasi cha kumtia moyo hata Mchungaji wa kanisa hilo ambaye niΒ  Mchungaji George. Nyimbo za kusifu zilikua zikiimbwa, kilaΒ  mwenye kua nacho alitoa kidogo alicho nacho kwa moyo woteΒ  bila kujaliΒ 

    Waumini waliungana kwa pamoja ili kurejesha furaha ya MatildaΒ  ambaye alikua haamini macho yake jinsi kapu lilivyokuaΒ  linajaa noti. Mikono ya Matilda ilikua kwenye mdomo wake hukuΒ  chozi likiendelea kuvuja, tabasamu pana lilionekana kwenyeΒ  sura ya Mama Naomi ambaye alitoa wazo la Matilda kurejeaΒ  kanisani. Mchungaji George alimtia moyo sana Matilda katikaΒ  kila hatua ambayo walikuwepo, baadaye Mchungaji alikabidhiwaΒ  kapu lenye fedha hizo.

    Watu maalum wa kuzihesabu walianza kazi hiyo huku MchungajiΒ  George akitoa neno kanisani hapoΒ 

    “Hakika leo Bwana ameinuliwa, kwa moyo huu uliooneshwa hakikaΒ  roho mtakatifu yupo ndani yetu, kusimama na Mwenye matatizoΒ  kunaongeza Baraka, hamjui ni kiasi gani Mungu anaendaΒ  kuongeza kilichopungua kwenu. Mungu awabariki sana kwa jinaΒ  la yesu” Alisema Mchungaji huku kanisa likiitika haswa kwaΒ  kusemaΒ 

    “Aaameen” Matilda alizidi kulia kwa uchungu sana,Β  kilichomliza siyo tu kuumwa kwa Binti yake bali ni maishaΒ  anayopitia baada ya kuitwa Mama, jinsi watu bakiΒ  wanavyosimama na yeye wakati Mwanaume aliyemfanya akatorokaΒ  kwao hajigusi kwa lolote lile, alipiga magoti na kusemaΒ 

    “Asante Yesu” Mikono yake ikiwa juu, Mchungaji akaja naΒ  kumwinuaΒ 

    “Matilda, kanisa linakuhitaji useme neno” Mchungaji GeorgeΒ  alimsogeza Matilda hadi Madhabauni, akampa kipaza sauti.Β  Aseme nini? ndicho ambacho Matilda alikua akiwaza, umatiΒ  ulikua mwingi hapo kanisani, macho yote yakawa kwa MatildaΒ  Msichana wa miaka 28Β 

    Alikua akitetemeka kwa kila alichofikiria kukisema, alikuaΒ  kama amepigwa shoti vile, alimtazama Mama Naomi ambaye alimpaΒ  ishara ya kumtia moyo kua aseme chochote hapo kanisaniΒ 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NNE Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    10 Comments

    1. Nelca on September 14, 2024 8:06 pm

      Daaaah jmn
      Kama naangalia tamthia vileee😭😭

      Reply
    2. Halinga1 on September 14, 2024 8:06 pm

      Wakati wa Mungu ukifika Kila lililoshindikana litafanyika kwani hakuna jambo gumu kwake

      Reply
    3. Asia ally on September 14, 2024 9:43 pm

      Mungu hakosei kwakweli

      Reply
    4. Farnoush on September 14, 2024 10:27 pm

      Mambo Yazidi kuwa motooo

      Reply
      • Ryan Bwesigye on September 15, 2024 3:47 pm

        God’s ears are not deaf that he cannot hear your 😭 cry ..

        Reply
    5. G shirima on September 15, 2024 8:25 pm

      Kuna funzo apa

      Reply
    6. Amayner on September 15, 2024 8:45 pm

      Mamb ni moto

      Reply
    7. B on September 17, 2024 1:50 pm

      Am I crying too 😭

      Reply
    8. Abraham on September 18, 2024 10:23 am

      Daah pole san kam wap

      Reply
    9. πŸ“Ÿ Email; Operation 1,423307 bitcoin. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=a73c2adc95104ac3006196a7934c8646& πŸ“Ÿ on May 25, 2025 6:20 am

      ge6l84

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.