Ilipoishia “Jua lilianza kuzama, nilikua tayari nimemaliza kupika na kuweka chakula kwenye hot-pot.ย Nilikua na msongo wa mawazo, kichwa nacho kilikua kinaniuma sana kwa sababu ya vileย vidonda. Nilipoisikia adhana sikujishughulisha nayo nikiamini Mungu ameniacha peke yanguย niteseke.ย
Muda huo huo nikasikia mlango ukifunguliwa, mara moja nikakimbilia Uwani na kumuonaย Mzee Mwinyimkuu akiwa ameongozana na Kaka Hamidu, moyo ulianza kwenda mbio, nilikuaย nimejibanza mlangoni nikiwaangalia wakiwa wanaongea, halafu Kaka Hamidu akawaย anamsaidia Mzee Mwinyimkuu kuufunga mlango wa Uwani tena kwa funguo halafu funguoย akampa Mzee Mwinyimkuu. Endelea
SEHEMU YA SABA
Walionekana kupiga stori za hapa na pale kana kwamba walijuana muda mrefu, nilijua hii ilikuaย ni tabia yake Kaka Hamidu kupenda kuongea sana na Watu tofauti tofauti pasipo kujua kuaย aliyekua anaongea naye alikua katili sana na laiti angelijua hata asingelikanyaga mguu wakeย ndani ya hii nyumba. Taratibu nilirudi ndani nikaingia chumbani, nikafunga mlango huku choziย likinibubujikaย ย
Hapakuchukua muda mrefu mlango uligongwa, halafu uligongwa taratibu sana na hapo hapoย sauti ya Mzee Mwinyimkuu ikasikika ikiniitaย
โMkweโ yaani nilizidi kukereka lakini kwa kuhofia uhai wa Kaka Hamidu ikanilazimu kuitikiaย japo kwa shingo upandeย
โAbee Babaโ nilinyanyuka na kwenda kufungua mlango, ghafla akanisukumiza hadi ndani kishaย akaufunga mlango na kunishika shingoniย
โNilikuonya lakini unaonekana hutaki kusikia si ndiyo, sasa kwa taarifa yako hakunaย utakachofanya nisikijue. Ulichojaribu kukifanya leo sokoni kinaweza kukugharimu, subiri Kakaย yako aondoke nitakuonesha rangi yangu halisi na yule Mtu wako anakufuatilia sasa nayeย arobaini yake imefikaโ alisema kisha akanitupa pembeni, kwakuwa nilikua mwembamba ikawaย rahisi sana kwake kunisukuma, nikawa nakohoa ila nikawa nimejua kua nilichokusudia kwa yuleย Mwanaume kule Buchani kilifanya kazi ila sasa nikawa naogopa sababu ni lazima atadhurika tu.ย
โJiandae uje uonane na Kaka yako, kumbuka nilichokwambia ukifanye la sivyo naye ataishiaย humuโ alisema kwa sauti yenye mikwaruzo huku akimalizia na ishara ya kuweka mkonoย
shingoni kuwa atamuuwa. Lugha ya chozi ndiyo Lugha pekee ambayo nilikua naizungumza kilaย wakati, umri wangu na yote ninayoyapitia vilinizidi kabisaย
Ili kumlinda Kaka Hamidu nililazimika kuigiza kuwa kila kitu kipo sawa, nilifunga vizuriย kitambaa mguu ambao ulikatwa kidole kisha nikavalia na soksi, Nikanawa usoni ili kujipaย utulivu wa sura yangu iliyochoka mateso na manyanyaso ya Mzee Mwinyimkuu. Nilisimamaย mbele ya kioo huku kwa mbali nikisikia namna ambavyo Mzee Mwinyimkuu na Kaka Hamiduย walivyokuwa wakichekeshanaย
Nilipohakikisha nimejiweka vizuri, nilitoka chumbani nikaenda sebleni ambapo Kaka Hamiduย alikuwepo, niliizima hisia ya majonzi nikaingia sebleni, Kaka Hamidu alifurahi sana sababuย hakuwahi kuhudhuria harusi yangu na pia ilipita kitambo pasipo kuonana, nilimkaribisha kwaย furaha ya kuigiza na kumtaka ajisikie yupo nyumbani kisha nilimuacha na kwenda kumuandaliaย chakula.ย
Niliporudi nilimpa chakula akaanza kula huku akinisifia kuwa mapishi yangu hayajabadilika,ย yeye alionekana kuwa na amani na furaha ya kweli sababu hakuna alichokuwa anakifahamu hadiย muda huo, isipokua mimi niliyejiona nilikua ndani ya shimo refu lililoenea giza zito nisione paย kutokea, tabasamu lilitanda kote usoni pangu ili tu kumlinda Kaka Hamidu, na jinsi mudaย ulivyokuwa umeenda niliogopa sana kama atalala ndani ya nyumba hii ya Kutisha, nilitamaniย aondoke baada ya kumaliza kula tu.ย
Mzee Mwinyimkuu alikua ameketi anasikiliza maongezi yetu, akawa ananikumbusha stori zaย zamani na kumwambia Mzee Mwinyimkuu kuwa nilipokua mdogo nilikua na tabia ya kulialia,ย kwake alichukulia kama ni sehemu ya mazungumzo mazuri lakini kwangu niliona anapotezaย muda badala ya kula akamaliza mapema aondoke, baadaye akaniuliza kama naweza kupokeaย simu kutoka kwakeย
Huwezi amini alininunulia simu ndogo ili nisikae bila simu kwa wakati ambao nilimwambiaย Mama kuwa namsubiria Mume wangu Salehe akirudi aninunulie simu mpya. Niliitaka sana ileย simu lakini jicho alilonikata Mzee Mwinyimkuu nikajikuta nikimwambiaย
โAsante Kaka, muda siyo mrefu Salehe atarudi atanunua simu ni wajibu wake. Hiyo kampe Wifiย yanguโ nilisema kanakwamba nilikua kwenye utani lakini moyoni nilitamani angenipa kisiri ileย simu ila sasa alikua hajui kuwa napitia mateso makali sana na vitisho vya kila aina. Mzeeย Mwinyimkuu akajikoholesha, jasiri haachi asili yake nikashtuka lakini nikajishtukia na kurudiย kwenye hali ya kawaidaย
โSaida, Muandalie mgeni sehemu ya kulala. Apumzike akimaliza kula maana anaonekanaย amechokaโ alisema Mzee Mwinyimkuu, nilishtuka sana sikutaka Kaka Hamidu asikie vitimbiย vya Usiku vya hii nyumba, nikaitikia kwa wasiwasi sanaย
โNjoo Mamaโ akasema Mzee Mwinyimkuu, mbele ya Mtu mwingine hujionesha ni Mtu mzuriย lakini tukiwa wawili ananitendea unyama na ukatili wa kutisha sana. Nilitabasamu nikiwaย
namtazama Kaka Hamidu ambaye naye alikua akitabasamu huku akinitazama, ndani ya moyoย wake aliiamini hii picha ya nje kuwa nina amani na furaha lakini niliamini kama atalala hapaย basi ataiona picha ya ndani ya Maisha yangu kitu ambacho kitahatarisha Maisha yake.ย
Niliongozana na Mzee Mwinyimkuu hadi kwenye korido, akairudisha ile sura yake ya Mbuziย ambayo niliizoea japo inatisha, kwa sauti ya chini nzito akaniambiaย
โChumba cha mwisho kushoto, muandalie mazingira ya kulala.โ Alisema, sijui kwanini alisistiza Kaka Hamidu alale wakati alikuja bila begi lolote lile akionekana amekuja Mara moja tu, lichaย ya yote sikutaka alale pale ila sikujua nawezaje kumshawishi aondoke.ย
โSawaโ hakunipa onyo lolote lile baada ya kuitikia aliondoka na kurejea sebleni, nilienda mojaย kwa moja kwenye chumba nilichoelekezwa ambacho Kaka Hamidu atalala. Sikuwahiย kukifungua kile chumba wala kukisogelea, ilikua ndiyo mara ya kwanza nakifunguaย
Nilipoingia ndani nilianza kuona vitu vilivyoniacha mdomo wazi, huyu Mzee alitaka makusudiย nione pia. Palijengwa kitu kama kaburi katikati ya kile chumba, halafu palikua na mifupa mingiย sana ya Binadamu, mafuvu ukutani, halafu nikasikia sauti ya kutisha ikisemaย
โHiki ni Chumba cha Hamiduโ sauti hiyo ilinipa kiwewe nikajikuta nikipiga yowe nikakimbiaย kuelekea sebleni, Kaka Hamidu akawa Mtu wa kwanza kunidaka na kuniuliza kuna nini. Hapoย akili ikanikaa sawa kuwa sikupaswa kupiga kelele namna ile, nikajitahidi kujikaza lakini tayariย ย
nilikua nimezua taharuki halafu cha ajabu Mzee Mwinyimkuu alikua akitabasamu tu kituย ambacho kilizidi kunipa maswali yasiyo na majibu.ย
โEti Babu huyu ana nini?โ akauliza Kaka Hamidu akiwa amenishika bega huku macho yakeย akiyapeleka kwa Mwinyimkuu aliyeketi bila hata kujitingishaย
โSaida Bwana, sasa nini kinakufanya unamshtua Kaka yako, hadi leo hujaizoea hii nyumba tu?โย Aliniuliza Mzee Mwinyimkuu lakini swali lake lilijaa dhihaka sana kitu ambacho sikukipendaย kabisa wakati alijuwa alichokua amekifanya. Bumbuwazi niliyonayo ilinifanya nishindwe kujibuย swali lolote lileย
โHamidu hebu twende ukaone kilichomshitua huyuโ akasema Mzee Mwinyimkuu, Moyoย ulifanya kama unataka kusimama hivi kwa namna nilivyoshituka, nikajiuliza kama Kaka Hamiduย ataenda kule atakiona kile chumba cha kutisha chenye kaburi ndani na hapo kizaa zaa kitaanzaย kwake, nikajitahidi nimzuie nikamwitaย
โKaka Hamiduโฆโ alikua tayari ameongozana na Mzee Mwinyimkuu, walikuwa wameshafikaย kwenye korido wakiwa wamebakisha hatua chache sana kukifikia kile chumba cha kutisha,ย macho yalinitoka nikiwaangalia walivyokuwa wakienda kisha walisimama mlangoniย wakatazamana kwa mshangaoย
Halafu Kaka Hamidu akaangua kicheko huku akigeuka na kunitazama nikiwa nimesimamaย mlango wa kuingilia sebleni, alicheka kama Mtu aliyepandwa na wendawazimu, hapo hapoย
nikaisikia simu yake ikiita maana aliiacha kwenye kochi, nikatamani kurudi niipokee ili nitoeย taarifa kusudi akipotea kila Mtu ajue pa kuanzia lakini sikupata hata hiyo nguvu mara akaniitaย
โSaida hebu njooโ aliniita Kaka Hamidu, alikua tayari ameacha kucheka. Akaniita tena kwaย kunisitiza kuwa niende, nikajikuta bila kujiuliza mara mbili naanza kupiga hatua kama Mgonjwa,ย kumbuka hapo nna maumivu ya Uchi wangu pia kidole kilichokatwa halafu nilishakata tamaaย ย
Nilisogea taratibu huku nahesabu hatua zangu kama mwendawazimu, nilijua naenda kuona niniย sababu nilichokiona mwanzo ni kile kile. Nilipofika nilishangaa sana, Jamani eti kile chumbaย chenye kaburi na mafuvu na mifupa ya Binadamu kilikua hakina chochote zaidi ya kitanda kizuriย kilochotandikwa shuka safi sana na zaidi kilikua kinanukia ila chini palikua na paka aliyetuliaย zake.ย
Kaka Hamidu akanishika bega akaniulizaย
โNi lini utaacha kuogopa paka Mdogo wangu? Wewe ni Mtu mzima sasa pia ni Mke na huwendaย ukawa Mama baadaye, unaogopa Paka kweli?โ aliniuliza, haikuwa siri ni kweli nilikua naogopaย paka lakini nilichokiona mwanzo wala hakuwa paka, sasa nikajiuliza ni mawazo yangu tu auย nilichokuwa nimekiona kilikua halisi na hiki tunachokiona ni kiini macho tu.ย
Nilihema mfululizo kama vile moyo ulishusha pumzi na kuamua kurejea kwenye mapigo yaย kawaida, basi nilikaa kimya sikusema chochote kile.ย
โUtalala hapa, si ulisema kesho asubuhi unarudi Mbeya?โ aliuliza Mzee Mwinyimkuuย
โEeeh asubuhi narudi ili nijiandae halafu kesho kutwa niende Darโ alijibu Kaka Hamidu,ย akanishika mkono tukarudi sebleni nikiwa kimya. Nilimhurumia sana Kaka Hamidu maanaย nilianza kuwa na wasiwasi kuwa Mzee Mwinyimkuu kuna mpango fulani ameupanga dhidiย yake. Muda huo huo Mzee Mwinyimkuu akapokea simu halafu akatuacha pale akaelekea njeย kuzungumza ikionekana kama kuna Mtu aliyemtarajia alikua amefika nje.ย
Nilipanga kumshawishi Kaka Hamidu asilale ndani ya ile nyumba lakini sikujua naanzia wapiย Mimi. Nikiwa natafakari Kaka Hamidu akaniulizaย
โHuonekani kuwa sawa Saida, kuna tatizo gani hapa?โ aliuliza kama Mtu aliyeanza kuoneshaย wasiwasi wa ghafla japo muda wote huo alikua akionesha kutokuwa na wasiwasi kabisa.ย Kwakuwa alionesha kuwa na wasiwasi nikaona ni bora nimueleze ili aokoe uhai wake sababuย uhai wa Wazazi wangu ulikua mikononi mwangu.ย
Nilisogea na kupiga magoti mbele yake nikashika na miguu yake huku chozi likinibubujika.ย
โKaka Hamidu, usilale ndani ya hii nyumba na kama utafanya hivyo basi kifo chako kitakuwaย karibu zaidi na weweโ nilimwambia chozi likizidi kunibubujika, hata sauti iliyonitokaย iliambatana na kilio kisicho na sauti Kubwaย
โUnamaanisha nini?โย
Nikavua soksi na kmwonesha Kaka Hamidu nilivyokatwa kidole ili ayaamini kwa harakaย maneno nitakayo mwambia, alishtuka sana.ย
โHuyu Mzee siyo Mtu mzuri Kaka yangu, okoa Maisha yako bado una muda wa kufanya hivyo.ย Hii nyumba imejaa uchawi na mateso makali, hata kile chumba unachoambiwa ulale ni chumbaย chenye kaburi ndiyo maana nilishtuka. Ondoka bado una mudaโ Nilimueleza Kaka Hamidu,ย haikuhitaji elimu ya chuo kikuu kujua kua Kaka Hamidu alikua ameshanielewa.ย
Akajawa na taharuki na hasira sababu alikua ananipenda sana na isitoshe hakuna nduguย anayeweza kumuacha ndugu yake kwenye shida kiasi kile.ย ย
โSaida siwezi kukuacha hapa, nitamfundisha adabu huyu Mshenziโ akasema Kaka Hamidu,ย kimwili Kaka Hamidu alikua amejazia jazia hivyo kama utamuweka mizani moja na Mzeeย Mwinyimkuu basi yeye ndiye atazidi. Akanishika mkono kwa nguvu akasemaย
โTunaondoka woteโย ย
โKaka nenda wewe tu, mimi niache hapa ili Wazazi wangu wawe salamaโ nilisema, sasa Kakaย Hamidu akaanza kupaza sauti kitu ambacho sikukitaka kabisa. Nilichotaka ni siasa zaidi ili Kakaย Hamidu aondoke pasipo Mzee Mwinyimkuu kujuwa chochote kile.ย
Mara tukasikia mlango ukifungwa tena siyo kufungwa kawaida ni kule kufungwa kwa kufuriย kabisa halafu ni Mlango wa kuingilia nyumba kubwa, Kaka Hamidu akanipa ishara ya kukaaย kimya. Alidhamilia kuomdoka na Mimi, nami niliona ni bora niondoke naye kuliko kubaki tenaย kwa Mzee Mwinyimkuuย ย
Akaingia Mzee Mwinyimkuu pale sebleni, alikua amevalia suruali, singlendi na Balaghashiaย kama kawaida yake, hakututazama kabisa akalisogelea kabati na kuiweka funguo kwenye drooย kwa mbwembwe sana huku akiwa anapiga zake mluzi.ย
Ilikuwa ndiyo nafasi pekee ambayo Kaka Hamidu alikua ameipata, akachukua jagi la kioo lenyeย maji kisha akasogea taratibu hadi nyuma kwa Mzee Mwinyimkuu, akampiga na lile jagi kisogoniย kwa nguvu hadi Mzee Mwinyimkuu akagugumia kwa maumivu na damu zikaanza kutokaย alipopigwa akaanguka chini huku akionekana kutaka kusema jambo lakini alikua akishindwa.ย ย
Kaka Hamidu alikua akimuangalia Mzee Mwinyimkuu alivyokua anatapa tapa, kwa sekundeย kadha tu zilitosha kumnyamazisha akawa ametulia tuli pale chini kama maji ya Mtungi, ikawa niย nafasi ya dhahabu sana kuondoka ndani ya ile nyumba.ย ย
โTwendeโ akasema kaka Hamidu akiwa amenishikilia mkono kwa nguvu tukawa tunaelekeaย mlangoni ili tuondoke. Tulipofika Mlangoni tukapata akili ya ile funguo, ndiyo! Palikua naย kufuri mlangoni, funguo aliiweka kwenye droo kule sebleni,.ย
Hapakuwa na ujanja isipokua Kaka Hamidu kurudi sebleni kuchukua funguo, alipofika Sebleniย hakumuona tena Mzee Mwinyimkuu pale sakafuni wala sebleni kote, ni kama aliyayuka mithiriย
ya Barafu juani. Akaniita, nikakimbilia sebleni nami nikawa shuhuda wa kutoweka kwa Mzeeย Mwinyimkuu, tulitazama kwa mshangao mkubwa.ย
Tusingeweza kurudi nyuma tena, Kaka Hamidu akafungua droo na kuikuta funguo, akaichukuaย kisha akaniambia tuondoke. Cha kushangaza ambacho kilitufanya tugande kama Barafu niย kuukuta ule mlango tuliohangaika kuchukua funguo ukiwa wazi kabisa, halafu nje tukisikia sautiย ya Mtu kama akichakata kuni hivi.ย ย
Sote tukawa na hofu sana, Nani ameufungua ule mlango bila kusikila sauti yoyote? Hakunaย aliyekua na jibu la moja kwa moja, Kaka Hamidu akaona ni bora apige simu ili aombe msaada,ย alishaona siyo rahisi kuondoka ndani ya ile nyumba ya kutisha, halafu ilikua mishale ya usikuย mchanga kama saa 3 hivi lakini matukio yaliyotokea na ukimya uliokuwa umetanda na gizaย ilionesha kama vile ni Usiku mnene.ย
Akajipapasa na kukumbuka simu aliiacha Kwenye kochi, kabla hata hajapiga hatua kurudiย sebleni, pale pale taa zote zikazima. Pakawa giza tupu hata nuru moja isionekane, pakawa kimyaย kabisa, sikumsikia tena Kaka Hamidu isipokua sauti ya kugugumia ambayo aliitoa kwa nguvu,ย papo hapo nikasikia kitu kikianguka kama Mzigo โPuuhโย
โAaaaahโผโ niligumia kwa hofu lakini ghafla nikabanwa mdomo wangu halafu sauti ya Mzeeย Mwinyimkuu ikagonga ngoma za Masikio yangu, nilishtuka sana.ย ย
โShiiiiiโผ!โ akanitaka nikae kimya. Nilikuwa nahema juu juu, mara papo hapo taa zikawaka.ย Nilichokiona jamani sitakuja kusahau Maisha yangu yote, nilihisi uchizi, nilihisi wendawazimu.ย Mwili ulipoa kama nimemwagiwa maji ya Baridi. Kaka Hamidu alikua sakafuni, damu nzitoย ilikua imetapakaa kila mahali.ย ย
Alitenganishwa kichwa na kiwiliwili chake, damu zilikua zinaruka kwenye shingo yake. Hataย Mzee Mwinyimkuu aliponiachilia sikua na nguvu nilianguka chini nikakalia damu.ย
โNilikuonya hukusikiaโ akasema Mzee Mwinyimkuu, alisema. Mkononi alikua ameshikilia kisuย kikubwa chenye damu. Niliishia kudondosha chozi tu, mara akaingia Mwanaume mmoja naย kuanza kuuvuta mwili wa Kaka Hamidu kuelekea nje, Mze Mwinyimkuu akakichukua kichwaย cha Kaka Hamidu na kukipeleka kwenye kile chumba alichokua amekiandaa kwa ajili ya kulalaย Kaka Hamidu.ย
Sijui kilichoendelea baada ya hapo nilijikuta nikizidi kuishiwa nguvu, giza zito likatanda nikahisiย usingizi wa ajabu. Nikapoteza uwezo wa kujitambua.ย
**ย
โSaida,Mdogo wangu amka Unisaidieโ ilikua ni sauti ya Kaka Hamidu, alikua amesimamaย mbele yangu nikiwa nimekaa kitandani, alikua akivuja damu kila sehemu. Alikua ametisha kiasiย kwamba niligugumia hadi nikapaza sauti yangu kwa hofu. Hivyo ndivyo nilivyoamka kutokaย Usingizi wa kifoย
Nilikua na maumivu makali sana mguuni, ndoto hii mbaya iliniamsha. Eneo lile lile nililokatwaย kidole lilikua na maumivu makali sana. Niliusogeza vizuri Mguu wangu na kuangalia kidondaย kinaendeleaje, nilipoangalia niliona vidole viwili vikiwa vimeondolewa. Yaani jumla ya vidoleย vitatu vinavyofuatana kuanzia cha mwisho vilikuwa havipo.ย
Maumivu yalikua makali, ni bora uyasome kwenye hii hadithi lakini yasikukute, mwili woteย ulipandisha homa ya ghafla, kichwa kilikua kinauma sana. Safari hii sikuwa na uhakika kamaย ninaweza hata kutembea, eneo lenyewe nililopatia ufahamu sikulijua kabisa.ย
Nilikua sakafuni, chumba kilikua kitupu isipokuwa mimi tu na maumivu yangu. Nilipiga sakafuย kwa uchovu nikasemaย
โKama uliniumba niteseke hadi nife basi nitakufa na kama huu ni mpango wa shetani basiย hawezi kukuzidi maarifaโ nilipomaliza kusema hivi nilijikunyata, Nililia sana. Nilikua tayariย nimempoteza Kaka Hamidu na sijui walimpeleka wapiย
Eneo lile lilikuwa kimya sana tofauti kabisa na nilivyozoea, sikusikia sauti za Pikipiki walaย mazungumzo yoyote yale. Niliona ni bora nilikague eneo lile, nilichungulia dirishani, nililionaย Pori la Kubwa, nilishtuka. Nikagundua nilikua nimehamishwa kutoka kwenye nyumba ya Mzeeย Mwinyimkuu. Nililia sana maana safari hii siwezi kukutana na yeyote yule nikapata msaada,ย Mzee Mwinyimkuu alishagundua kuwa kama ataniacha huru naweza kutoroka, ilifika hatuaย nilikua mkali nikajisemeaย
โKama kuokoa uhai wangu kutafanya wazazi wangu wafe ni sawa, napaswa kukwepa hayaย mateso Makali. Mungu atapigana kwa ajili ya Wazazi wanguโ hayo ndiyo yalikua maamuziย yangu.ย
Niliveshwa kaniki pekee halafu nilikua na alama fulani kwenye paja langu, ilikua alama ya ajabuย iliyochorwa kwa moto, palikua na maneno ya ajabu. Huu ndiyo wakati mgumu zaidi kuwahiย kuupitia katika Maisha yangu yote, haukuwa wakati rahisi kwangu, ulikuwa wakati ambaoย nilipoteza tumaini la Maisha yangu lakini sikuweza kufanya chochote isipokua kuuguliaย maumivu na kulia.ย
Kilipita kitambo kirefu cha Ukimya, sijui ilikua ni saa ngapi, siku gani au lile eneo ni wapi.ย Nilichojua ni kuwa bado naendelea kupumua, niliusikia Mlio wa pikipiki. Nikajivuta naย kuchungulia dirishani, niliiona pikipiki ikiwa imesimama kando kidogo kama mita chache tu hiviย kisha Mtu mmoja alisogea mbele kuelekea nyumba niliyopoย
Kumbuka hapo ni Porini, tokea nimezinduka sikuwahi kumuona yeyote yule isipokua sauti zaย ndege zilizopita kwenye ngoma za masikio yangu yaliyochoka kusikia sauti za kutisha. Nilikuaย nimekonda ghafla sana Mimi Saidaย
Basi, yule Mtu sikuiona sura yake kwa haraka sababu hata nguvu ya kusimama kwa muda mrefuย ilianza kuniisha nikajikuta nikianguka chini, maumivu yalikua makubwa halafu nilikua na njaaย
sana. Nilisikia tu akifungua mlango ulioonekana kuwa na komeo nyingi, akaingia hadi chumbaย nilichopoย
Yule Mtu nilimkumbuka kwa haraka sana, alikua ni yule Bodaboda aliyenipeleka sokoni siku ileย ambayo nilikutana na Abuu. Nilikua na wenge zito lakini sikuacha kumtazama kwa makini hadiย nikamtambua. Alikuwa amebeba chakula kwenye Hot-potย
Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.ย
โKunywa Majiโ alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikuaย ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuulizaย
โMnanimalizia lini nikapumzike?โ Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chacheย nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambiaย
โKifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwajeโ alisema kisha akanipa maji, sikuwaย na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe haiย
Comments zikiwa nyingi naachia ya NANE leoleo hapa
Nini Kitaendelea?USIKOSE SEHEMU YA NANE YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย
Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xxย
 
		
 
									 
					
18 Comments
Simulizi tamu Sana haichoshi na haiishi hamu kuifuatilia.
Mola mlezi akubariki mwandishi, aturudhuku neema tuzidi kuwa pamoja Hadi tamati.
Leo nitaota haki mwenyew Nina machungu afu nasoma hii story inatishaa
Jamaniii. Huyo dada akimbieee …
Mpka machozii ilaa naaminii Mungu atamfanyiaa njiaa
Dah inasikitish san ๐๐ฅบ
Duj umeupiga mwingii sanaa admin
Duh….
Simulizi inanitoa machozi jamani ๐ญ๐ญya Ajabu sana
Sijawahi kusoma hadithi mfano wake.
Maskini Saida.
Vidole vyake nasikia ganzi jamani
Kaka Hamidu kaenda jamani
๐ญ๐ญ
Mzee MwinyiMkuu na Salehe wanafaa kuitwa Nguruwe kwa matendo yao.
E Mwenyezi Mungu
Waangamize Wachawi wote Jehannam.
Ameen.
๐ฅบ๐ฅบ๐ฅ๐ฅ๐ญ๐ญ
Sehemu ya nane ata leo hadithi inavutia kusoma inasisimua inahuzunishaa pia
Duh hatari sana hii
Inauma sana binadam sis n wabaya sana
Angekua ni mtoto wa 2000 angekua teal amekatwa vidole vyote maana awa wa kizazi iki ni wakaidi balaa
Looh Kisa kinasisimua km nipo ndani yake
i6kjs2
4firym
f9m3le