Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (07)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 12, 2025Updated:January 13, 202518 Comments15 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Jua lilianza kuzama, nilikua tayari nimemaliza kupika na kuweka chakula kwenye hot-pot.ย  Nilikua na msongo wa mawazo, kichwa nacho kilikua kinaniuma sana kwa sababu ya vileย  vidonda. Nilipoisikia adhana sikujishughulisha nayo nikiamini Mungu ameniacha peke yanguย  niteseke.ย 

    Muda huo huo nikasikia mlango ukifunguliwa, mara moja nikakimbilia Uwani na kumuonaย  Mzee Mwinyimkuu akiwa ameongozana na Kaka Hamidu, moyo ulianza kwenda mbio, nilikuaย  nimejibanza mlangoni nikiwaangalia wakiwa wanaongea, halafu Kaka Hamidu akawaย  anamsaidia Mzee Mwinyimkuu kuufunga mlango wa Uwani tena kwa funguo halafu funguoย  akampa Mzee Mwinyimkuu. Endelea

    SEHEMU YA SABA

    Walionekana kupiga stori za hapa na pale kana kwamba walijuana muda mrefu, nilijua hii ilikuaย  ni tabia yake Kaka Hamidu kupenda kuongea sana na Watu tofauti tofauti pasipo kujua kuaย  aliyekua anaongea naye alikua katili sana na laiti angelijua hata asingelikanyaga mguu wakeย  ndani ya hii nyumba. Taratibu nilirudi ndani nikaingia chumbani, nikafunga mlango huku choziย  likinibubujikaย ย 

    Hapakuchukua muda mrefu mlango uligongwa, halafu uligongwa taratibu sana na hapo hapoย  sauti ya Mzee Mwinyimkuu ikasikika ikiniitaย 

    โ€œMkweโ€ yaani nilizidi kukereka lakini kwa kuhofia uhai wa Kaka Hamidu ikanilazimu kuitikiaย  japo kwa shingo upandeย 

    โ€œAbee Babaโ€ nilinyanyuka na kwenda kufungua mlango, ghafla akanisukumiza hadi ndani kishaย  akaufunga mlango na kunishika shingoniย 

    โ€œNilikuonya lakini unaonekana hutaki kusikia si ndiyo, sasa kwa taarifa yako hakunaย  utakachofanya nisikijue. Ulichojaribu kukifanya leo sokoni kinaweza kukugharimu, subiri Kakaย  yako aondoke nitakuonesha rangi yangu halisi na yule Mtu wako anakufuatilia sasa nayeย  arobaini yake imefikaโ€ alisema kisha akanitupa pembeni, kwakuwa nilikua mwembamba ikawaย  rahisi sana kwake kunisukuma, nikawa nakohoa ila nikawa nimejua kua nilichokusudia kwa yuleย  Mwanaume kule Buchani kilifanya kazi ila sasa nikawa naogopa sababu ni lazima atadhurika tu.ย 

    โ€œJiandae uje uonane na Kaka yako, kumbuka nilichokwambia ukifanye la sivyo naye ataishiaย  humuโ€ alisema kwa sauti yenye mikwaruzo huku akimalizia na ishara ya kuweka mkonoย 

    shingoni kuwa atamuuwa. Lugha ya chozi ndiyo Lugha pekee ambayo nilikua naizungumza kilaย  wakati, umri wangu na yote ninayoyapitia vilinizidi kabisaย 

    Ili kumlinda Kaka Hamidu nililazimika kuigiza kuwa kila kitu kipo sawa, nilifunga vizuriย  kitambaa mguu ambao ulikatwa kidole kisha nikavalia na soksi, Nikanawa usoni ili kujipaย  utulivu wa sura yangu iliyochoka mateso na manyanyaso ya Mzee Mwinyimkuu. Nilisimamaย  mbele ya kioo huku kwa mbali nikisikia namna ambavyo Mzee Mwinyimkuu na Kaka Hamiduย  walivyokuwa wakichekeshanaย 

    Nilipohakikisha nimejiweka vizuri, nilitoka chumbani nikaenda sebleni ambapo Kaka Hamiduย  alikuwepo, niliizima hisia ya majonzi nikaingia sebleni, Kaka Hamidu alifurahi sana sababuย  hakuwahi kuhudhuria harusi yangu na pia ilipita kitambo pasipo kuonana, nilimkaribisha kwaย  furaha ya kuigiza na kumtaka ajisikie yupo nyumbani kisha nilimuacha na kwenda kumuandaliaย  chakula.ย 

    Niliporudi nilimpa chakula akaanza kula huku akinisifia kuwa mapishi yangu hayajabadilika,ย  yeye alionekana kuwa na amani na furaha ya kweli sababu hakuna alichokuwa anakifahamu hadiย  muda huo, isipokua mimi niliyejiona nilikua ndani ya shimo refu lililoenea giza zito nisione paย  kutokea, tabasamu lilitanda kote usoni pangu ili tu kumlinda Kaka Hamidu, na jinsi mudaย  ulivyokuwa umeenda niliogopa sana kama atalala ndani ya nyumba hii ya Kutisha, nilitamaniย  aondoke baada ya kumaliza kula tu.ย 

    Mzee Mwinyimkuu alikua ameketi anasikiliza maongezi yetu, akawa ananikumbusha stori zaย  zamani na kumwambia Mzee Mwinyimkuu kuwa nilipokua mdogo nilikua na tabia ya kulialia,ย  kwake alichukulia kama ni sehemu ya mazungumzo mazuri lakini kwangu niliona anapotezaย  muda badala ya kula akamaliza mapema aondoke, baadaye akaniuliza kama naweza kupokeaย  simu kutoka kwakeย 

    Huwezi amini alininunulia simu ndogo ili nisikae bila simu kwa wakati ambao nilimwambiaย  Mama kuwa namsubiria Mume wangu Salehe akirudi aninunulie simu mpya. Niliitaka sana ileย  simu lakini jicho alilonikata Mzee Mwinyimkuu nikajikuta nikimwambiaย 

    โ€œAsante Kaka, muda siyo mrefu Salehe atarudi atanunua simu ni wajibu wake. Hiyo kampe Wifiย  yanguโ€ nilisema kanakwamba nilikua kwenye utani lakini moyoni nilitamani angenipa kisiri ileย  simu ila sasa alikua hajui kuwa napitia mateso makali sana na vitisho vya kila aina. Mzeeย  Mwinyimkuu akajikoholesha, jasiri haachi asili yake nikashtuka lakini nikajishtukia na kurudiย  kwenye hali ya kawaidaย 

    โ€œSaida, Muandalie mgeni sehemu ya kulala. Apumzike akimaliza kula maana anaonekanaย  amechokaโ€ alisema Mzee Mwinyimkuu, nilishtuka sana sikutaka Kaka Hamidu asikie vitimbiย  vya Usiku vya hii nyumba, nikaitikia kwa wasiwasi sanaย 

    โ€œNjoo Mamaโ€ akasema Mzee Mwinyimkuu, mbele ya Mtu mwingine hujionesha ni Mtu mzuriย  lakini tukiwa wawili ananitendea unyama na ukatili wa kutisha sana. Nilitabasamu nikiwaย 

    namtazama Kaka Hamidu ambaye naye alikua akitabasamu huku akinitazama, ndani ya moyoย  wake aliiamini hii picha ya nje kuwa nina amani na furaha lakini niliamini kama atalala hapaย  basi ataiona picha ya ndani ya Maisha yangu kitu ambacho kitahatarisha Maisha yake.ย 

    Niliongozana na Mzee Mwinyimkuu hadi kwenye korido, akairudisha ile sura yake ya Mbuziย  ambayo niliizoea japo inatisha, kwa sauti ya chini nzito akaniambiaย 

    โ€œChumba cha mwisho kushoto, muandalie mazingira ya kulala.โ€ Alisema, sijui kwanini alisistiza Kaka Hamidu alale wakati alikuja bila begi lolote lile akionekana amekuja Mara moja tu, lichaย  ya yote sikutaka alale pale ila sikujua nawezaje kumshawishi aondoke.ย 

    โ€œSawaโ€ hakunipa onyo lolote lile baada ya kuitikia aliondoka na kurejea sebleni, nilienda mojaย  kwa moja kwenye chumba nilichoelekezwa ambacho Kaka Hamidu atalala. Sikuwahiย  kukifungua kile chumba wala kukisogelea, ilikua ndiyo mara ya kwanza nakifunguaย 

    Nilipoingia ndani nilianza kuona vitu vilivyoniacha mdomo wazi, huyu Mzee alitaka makusudiย  nione pia. Palijengwa kitu kama kaburi katikati ya kile chumba, halafu palikua na mifupa mingiย  sana ya Binadamu, mafuvu ukutani, halafu nikasikia sauti ya kutisha ikisemaย 

    โ€œHiki ni Chumba cha Hamiduโ€ sauti hiyo ilinipa kiwewe nikajikuta nikipiga yowe nikakimbiaย  kuelekea sebleni, Kaka Hamidu akawa Mtu wa kwanza kunidaka na kuniuliza kuna nini. Hapoย  akili ikanikaa sawa kuwa sikupaswa kupiga kelele namna ile, nikajitahidi kujikaza lakini tayariย ย 

    nilikua nimezua taharuki halafu cha ajabu Mzee Mwinyimkuu alikua akitabasamu tu kituย  ambacho kilizidi kunipa maswali yasiyo na majibu.ย 

    โ€œEti Babu huyu ana nini?โ€ akauliza Kaka Hamidu akiwa amenishika bega huku macho yakeย  akiyapeleka kwa Mwinyimkuu aliyeketi bila hata kujitingishaย 

    โ€œSaida Bwana, sasa nini kinakufanya unamshtua Kaka yako, hadi leo hujaizoea hii nyumba tu?โ€ย  Aliniuliza Mzee Mwinyimkuu lakini swali lake lilijaa dhihaka sana kitu ambacho sikukipendaย  kabisa wakati alijuwa alichokua amekifanya. Bumbuwazi niliyonayo ilinifanya nishindwe kujibuย  swali lolote lileย 

    โ€œHamidu hebu twende ukaone kilichomshitua huyuโ€ akasema Mzee Mwinyimkuu, Moyoย  ulifanya kama unataka kusimama hivi kwa namna nilivyoshituka, nikajiuliza kama Kaka Hamiduย  ataenda kule atakiona kile chumba cha kutisha chenye kaburi ndani na hapo kizaa zaa kitaanzaย  kwake, nikajitahidi nimzuie nikamwitaย 

    โ€œKaka Hamiduโ€ฆโ€ alikua tayari ameongozana na Mzee Mwinyimkuu, walikuwa wameshafikaย  kwenye korido wakiwa wamebakisha hatua chache sana kukifikia kile chumba cha kutisha,ย  macho yalinitoka nikiwaangalia walivyokuwa wakienda kisha walisimama mlangoniย  wakatazamana kwa mshangaoย 

    Halafu Kaka Hamidu akaangua kicheko huku akigeuka na kunitazama nikiwa nimesimamaย  mlango wa kuingilia sebleni, alicheka kama Mtu aliyepandwa na wendawazimu, hapo hapoย 

    nikaisikia simu yake ikiita maana aliiacha kwenye kochi, nikatamani kurudi niipokee ili nitoeย  taarifa kusudi akipotea kila Mtu ajue pa kuanzia lakini sikupata hata hiyo nguvu mara akaniitaย 

    โ€œSaida hebu njooโ€ aliniita Kaka Hamidu, alikua tayari ameacha kucheka. Akaniita tena kwaย  kunisitiza kuwa niende, nikajikuta bila kujiuliza mara mbili naanza kupiga hatua kama Mgonjwa,ย  kumbuka hapo nna maumivu ya Uchi wangu pia kidole kilichokatwa halafu nilishakata tamaaย ย 

    Nilisogea taratibu huku nahesabu hatua zangu kama mwendawazimu, nilijua naenda kuona niniย  sababu nilichokiona mwanzo ni kile kile. Nilipofika nilishangaa sana, Jamani eti kile chumbaย  chenye kaburi na mafuvu na mifupa ya Binadamu kilikua hakina chochote zaidi ya kitanda kizuriย  kilochotandikwa shuka safi sana na zaidi kilikua kinanukia ila chini palikua na paka aliyetuliaย  zake.ย 

    Kaka Hamidu akanishika bega akaniulizaย 

    โ€œNi lini utaacha kuogopa paka Mdogo wangu? Wewe ni Mtu mzima sasa pia ni Mke na huwendaย  ukawa Mama baadaye, unaogopa Paka kweli?โ€ aliniuliza, haikuwa siri ni kweli nilikua naogopaย  paka lakini nilichokiona mwanzo wala hakuwa paka, sasa nikajiuliza ni mawazo yangu tu auย  nilichokuwa nimekiona kilikua halisi na hiki tunachokiona ni kiini macho tu.ย 

    Nilihema mfululizo kama vile moyo ulishusha pumzi na kuamua kurejea kwenye mapigo yaย  kawaida, basi nilikaa kimya sikusema chochote kile.ย 

    โ€œUtalala hapa, si ulisema kesho asubuhi unarudi Mbeya?โ€ aliuliza Mzee Mwinyimkuuย 

    โ€œEeeh asubuhi narudi ili nijiandae halafu kesho kutwa niende Darโ€ alijibu Kaka Hamidu,ย  akanishika mkono tukarudi sebleni nikiwa kimya. Nilimhurumia sana Kaka Hamidu maanaย  nilianza kuwa na wasiwasi kuwa Mzee Mwinyimkuu kuna mpango fulani ameupanga dhidiย  yake. Muda huo huo Mzee Mwinyimkuu akapokea simu halafu akatuacha pale akaelekea njeย  kuzungumza ikionekana kama kuna Mtu aliyemtarajia alikua amefika nje.ย 

    Nilipanga kumshawishi Kaka Hamidu asilale ndani ya ile nyumba lakini sikujua naanzia wapiย  Mimi. Nikiwa natafakari Kaka Hamidu akaniulizaย 

    โ€œHuonekani kuwa sawa Saida, kuna tatizo gani hapa?โ€ aliuliza kama Mtu aliyeanza kuoneshaย  wasiwasi wa ghafla japo muda wote huo alikua akionesha kutokuwa na wasiwasi kabisa.ย  Kwakuwa alionesha kuwa na wasiwasi nikaona ni bora nimueleze ili aokoe uhai wake sababuย  uhai wa Wazazi wangu ulikua mikononi mwangu.ย 

    Nilisogea na kupiga magoti mbele yake nikashika na miguu yake huku chozi likinibubujika.ย 

    โ€œKaka Hamidu, usilale ndani ya hii nyumba na kama utafanya hivyo basi kifo chako kitakuwaย  karibu zaidi na weweโ€ nilimwambia chozi likizidi kunibubujika, hata sauti iliyonitokaย  iliambatana na kilio kisicho na sauti Kubwaย 

    โ€œUnamaanisha nini?โ€ย 

    Nikavua soksi na kmwonesha Kaka Hamidu nilivyokatwa kidole ili ayaamini kwa harakaย  maneno nitakayo mwambia, alishtuka sana.ย 

    โ€œHuyu Mzee siyo Mtu mzuri Kaka yangu, okoa Maisha yako bado una muda wa kufanya hivyo.ย  Hii nyumba imejaa uchawi na mateso makali, hata kile chumba unachoambiwa ulale ni chumbaย  chenye kaburi ndiyo maana nilishtuka. Ondoka bado una mudaโ€ Nilimueleza Kaka Hamidu,ย  haikuhitaji elimu ya chuo kikuu kujua kua Kaka Hamidu alikua ameshanielewa.ย 

    Akajawa na taharuki na hasira sababu alikua ananipenda sana na isitoshe hakuna nduguย  anayeweza kumuacha ndugu yake kwenye shida kiasi kile.ย ย 

    โ€œSaida siwezi kukuacha hapa, nitamfundisha adabu huyu Mshenziโ€ akasema Kaka Hamidu,ย  kimwili Kaka Hamidu alikua amejazia jazia hivyo kama utamuweka mizani moja na Mzeeย  Mwinyimkuu basi yeye ndiye atazidi. Akanishika mkono kwa nguvu akasemaย 

    โ€œTunaondoka woteโ€ย ย 

    โ€œKaka nenda wewe tu, mimi niache hapa ili Wazazi wangu wawe salamaโ€ nilisema, sasa Kakaย  Hamidu akaanza kupaza sauti kitu ambacho sikukitaka kabisa. Nilichotaka ni siasa zaidi ili Kakaย  Hamidu aondoke pasipo Mzee Mwinyimkuu kujuwa chochote kile.ย 

    Mara tukasikia mlango ukifungwa tena siyo kufungwa kawaida ni kule kufungwa kwa kufuriย  kabisa halafu ni Mlango wa kuingilia nyumba kubwa, Kaka Hamidu akanipa ishara ya kukaaย  kimya. Alidhamilia kuomdoka na Mimi, nami niliona ni bora niondoke naye kuliko kubaki tenaย  kwa Mzee Mwinyimkuuย ย 

    Akaingia Mzee Mwinyimkuu pale sebleni, alikua amevalia suruali, singlendi na Balaghashiaย  kama kawaida yake, hakututazama kabisa akalisogelea kabati na kuiweka funguo kwenye drooย  kwa mbwembwe sana huku akiwa anapiga zake mluzi.ย 

    Ilikuwa ndiyo nafasi pekee ambayo Kaka Hamidu alikua ameipata, akachukua jagi la kioo lenyeย  maji kisha akasogea taratibu hadi nyuma kwa Mzee Mwinyimkuu, akampiga na lile jagi kisogoniย  kwa nguvu hadi Mzee Mwinyimkuu akagugumia kwa maumivu na damu zikaanza kutokaย  alipopigwa akaanguka chini huku akionekana kutaka kusema jambo lakini alikua akishindwa.ย ย 

    Kaka Hamidu alikua akimuangalia Mzee Mwinyimkuu alivyokua anatapa tapa, kwa sekundeย  kadha tu zilitosha kumnyamazisha akawa ametulia tuli pale chini kama maji ya Mtungi, ikawa niย  nafasi ya dhahabu sana kuondoka ndani ya ile nyumba.ย ย 

    โ€œTwendeโ€ akasema kaka Hamidu akiwa amenishikilia mkono kwa nguvu tukawa tunaelekeaย  mlangoni ili tuondoke. Tulipofika Mlangoni tukapata akili ya ile funguo, ndiyo! Palikua naย  kufuri mlangoni, funguo aliiweka kwenye droo kule sebleni,.ย 

    Hapakuwa na ujanja isipokua Kaka Hamidu kurudi sebleni kuchukua funguo, alipofika Sebleniย  hakumuona tena Mzee Mwinyimkuu pale sakafuni wala sebleni kote, ni kama aliyayuka mithiriย 

    ya Barafu juani. Akaniita, nikakimbilia sebleni nami nikawa shuhuda wa kutoweka kwa Mzeeย  Mwinyimkuu, tulitazama kwa mshangao mkubwa.ย 

    Tusingeweza kurudi nyuma tena, Kaka Hamidu akafungua droo na kuikuta funguo, akaichukuaย  kisha akaniambia tuondoke. Cha kushangaza ambacho kilitufanya tugande kama Barafu niย  kuukuta ule mlango tuliohangaika kuchukua funguo ukiwa wazi kabisa, halafu nje tukisikia sautiย  ya Mtu kama akichakata kuni hivi.ย ย 

    Sote tukawa na hofu sana, Nani ameufungua ule mlango bila kusikila sauti yoyote? Hakunaย  aliyekua na jibu la moja kwa moja, Kaka Hamidu akaona ni bora apige simu ili aombe msaada,ย  alishaona siyo rahisi kuondoka ndani ya ile nyumba ya kutisha, halafu ilikua mishale ya usikuย  mchanga kama saa 3 hivi lakini matukio yaliyotokea na ukimya uliokuwa umetanda na gizaย  ilionesha kama vile ni Usiku mnene.ย 

    Akajipapasa na kukumbuka simu aliiacha Kwenye kochi, kabla hata hajapiga hatua kurudiย  sebleni, pale pale taa zote zikazima. Pakawa giza tupu hata nuru moja isionekane, pakawa kimyaย  kabisa, sikumsikia tena Kaka Hamidu isipokua sauti ya kugugumia ambayo aliitoa kwa nguvu,ย  papo hapo nikasikia kitu kikianguka kama Mzigo โ€˜Puuhโ€™ย 

    โ€œAaaaahโ€ผโ€ niligumia kwa hofu lakini ghafla nikabanwa mdomo wangu halafu sauti ya Mzeeย  Mwinyimkuu ikagonga ngoma za Masikio yangu, nilishtuka sana.ย ย 

    โ€œShiiiiiโ€ผ!โ€ akanitaka nikae kimya. Nilikuwa nahema juu juu, mara papo hapo taa zikawaka.ย  Nilichokiona jamani sitakuja kusahau Maisha yangu yote, nilihisi uchizi, nilihisi wendawazimu.ย  Mwili ulipoa kama nimemwagiwa maji ya Baridi. Kaka Hamidu alikua sakafuni, damu nzitoย  ilikua imetapakaa kila mahali.ย ย 

    Alitenganishwa kichwa na kiwiliwili chake, damu zilikua zinaruka kwenye shingo yake. Hataย  Mzee Mwinyimkuu aliponiachilia sikua na nguvu nilianguka chini nikakalia damu.ย 

    โ€œNilikuonya hukusikiaโ€ akasema Mzee Mwinyimkuu, alisema. Mkononi alikua ameshikilia kisuย  kikubwa chenye damu. Niliishia kudondosha chozi tu, mara akaingia Mwanaume mmoja naย  kuanza kuuvuta mwili wa Kaka Hamidu kuelekea nje, Mze Mwinyimkuu akakichukua kichwaย  cha Kaka Hamidu na kukipeleka kwenye kile chumba alichokua amekiandaa kwa ajili ya kulalaย  Kaka Hamidu.ย 

    Sijui kilichoendelea baada ya hapo nilijikuta nikizidi kuishiwa nguvu, giza zito likatanda nikahisiย  usingizi wa ajabu. Nikapoteza uwezo wa kujitambua.ย 

    **ย 

    โ€œSaida,Mdogo wangu amka Unisaidieโ€ ilikua ni sauti ya Kaka Hamidu, alikua amesimamaย  mbele yangu nikiwa nimekaa kitandani, alikua akivuja damu kila sehemu. Alikua ametisha kiasiย  kwamba niligugumia hadi nikapaza sauti yangu kwa hofu. Hivyo ndivyo nilivyoamka kutokaย  Usingizi wa kifoย 

    Nilikua na maumivu makali sana mguuni, ndoto hii mbaya iliniamsha. Eneo lile lile nililokatwaย  kidole lilikua na maumivu makali sana. Niliusogeza vizuri Mguu wangu na kuangalia kidondaย  kinaendeleaje, nilipoangalia niliona vidole viwili vikiwa vimeondolewa. Yaani jumla ya vidoleย  vitatu vinavyofuatana kuanzia cha mwisho vilikuwa havipo.ย 

    Maumivu yalikua makali, ni bora uyasome kwenye hii hadithi lakini yasikukute, mwili woteย  ulipandisha homa ya ghafla, kichwa kilikua kinauma sana. Safari hii sikuwa na uhakika kamaย  ninaweza hata kutembea, eneo lenyewe nililopatia ufahamu sikulijua kabisa.ย 

    Nilikua sakafuni, chumba kilikua kitupu isipokuwa mimi tu na maumivu yangu. Nilipiga sakafuย  kwa uchovu nikasemaย 

    โ€œKama uliniumba niteseke hadi nife basi nitakufa na kama huu ni mpango wa shetani basiย  hawezi kukuzidi maarifaโ€ nilipomaliza kusema hivi nilijikunyata, Nililia sana. Nilikua tayariย  nimempoteza Kaka Hamidu na sijui walimpeleka wapiย 

    Eneo lile lilikuwa kimya sana tofauti kabisa na nilivyozoea, sikusikia sauti za Pikipiki walaย  mazungumzo yoyote yale. Niliona ni bora nilikague eneo lile, nilichungulia dirishani, nililionaย  Pori la Kubwa, nilishtuka. Nikagundua nilikua nimehamishwa kutoka kwenye nyumba ya Mzeeย  Mwinyimkuu. Nililia sana maana safari hii siwezi kukutana na yeyote yule nikapata msaada,ย  Mzee Mwinyimkuu alishagundua kuwa kama ataniacha huru naweza kutoroka, ilifika hatuaย  nilikua mkali nikajisemeaย 

    โ€œKama kuokoa uhai wangu kutafanya wazazi wangu wafe ni sawa, napaswa kukwepa hayaย  mateso Makali. Mungu atapigana kwa ajili ya Wazazi wanguโ€ hayo ndiyo yalikua maamuziย  yangu.ย 

    Niliveshwa kaniki pekee halafu nilikua na alama fulani kwenye paja langu, ilikua alama ya ajabuย  iliyochorwa kwa moto, palikua na maneno ya ajabu. Huu ndiyo wakati mgumu zaidi kuwahiย  kuupitia katika Maisha yangu yote, haukuwa wakati rahisi kwangu, ulikuwa wakati ambaoย  nilipoteza tumaini la Maisha yangu lakini sikuweza kufanya chochote isipokua kuuguliaย  maumivu na kulia.ย 

    Kilipita kitambo kirefu cha Ukimya, sijui ilikua ni saa ngapi, siku gani au lile eneo ni wapi.ย  Nilichojua ni kuwa bado naendelea kupumua, niliusikia Mlio wa pikipiki. Nikajivuta naย  kuchungulia dirishani, niliiona pikipiki ikiwa imesimama kando kidogo kama mita chache tu hiviย  kisha Mtu mmoja alisogea mbele kuelekea nyumba niliyopoย 

    Kumbuka hapo ni Porini, tokea nimezinduka sikuwahi kumuona yeyote yule isipokua sauti zaย  ndege zilizopita kwenye ngoma za masikio yangu yaliyochoka kusikia sauti za kutisha. Nilikuaย  nimekonda ghafla sana Mimi Saidaย 

    Basi, yule Mtu sikuiona sura yake kwa haraka sababu hata nguvu ya kusimama kwa muda mrefuย  ilianza kuniisha nikajikuta nikianguka chini, maumivu yalikua makubwa halafu nilikua na njaaย 

    sana. Nilisikia tu akifungua mlango ulioonekana kuwa na komeo nyingi, akaingia hadi chumbaย  nilichopoย 

    Yule Mtu nilimkumbuka kwa haraka sana, alikua ni yule Bodaboda aliyenipeleka sokoni siku ileย  ambayo nilikutana na Abuu. Nilikua na wenge zito lakini sikuacha kumtazama kwa makini hadiย  nikamtambua. Alikuwa amebeba chakula kwenye Hot-potย 

    Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.ย 

    โ€œKunywa Majiโ€ alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikuaย  ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuulizaย 

    โ€œMnanimalizia lini nikapumzike?โ€ Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chacheย  nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambiaย 

    โ€œKifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwajeโ€ alisema kisha akanipa maji, sikuwaย  na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe haiย 

    Comments zikiwa nyingi naachia ya NANE leoleo hapa

    Nini Kitaendelea?USIKOSE SEHEMU YA NANE YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xxย 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    18 Comments

    1. Otchou jr on January 12, 2025 4:52 pm

      Simulizi tamu Sana haichoshi na haiishi hamu kuifuatilia.
      Mola mlezi akubariki mwandishi, aturudhuku neema tuzidi kuwa pamoja Hadi tamati.

      Reply
      • Hamisa Joseph on January 12, 2025 6:14 pm

        Leo nitaota haki mwenyew Nina machungu afu nasoma hii story inatishaa

        Reply
      • Lus twaxie on January 12, 2025 6:18 pm

        Jamaniii. Huyo dada akimbieee …

        Reply
    2. Gyakiee on January 12, 2025 4:53 pm

      Mpka machozii ilaa naaminii Mungu atamfanyiaa njiaa

      Reply
    3. Abdul on January 12, 2025 5:01 pm

      Dah inasikitish san ๐Ÿ’”๐Ÿฅบ

      Reply
    4. Egibeth on January 12, 2025 5:20 pm

      Duj umeupiga mwingii sanaa admin

      Reply
    5. Patricia Lizzy on January 12, 2025 5:24 pm

      Duh….

      Reply
    6. Fawziya Hassan on January 12, 2025 6:09 pm

      Simulizi inanitoa machozi jamani ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญya Ajabu sana
      Sijawahi kusoma hadithi mfano wake.
      Maskini Saida.
      Vidole vyake nasikia ganzi jamani
      Kaka Hamidu kaenda jamani
      ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    7. Fawziya Hassan on January 12, 2025 6:13 pm

      Mzee MwinyiMkuu na Salehe wanafaa kuitwa Nguruwe kwa matendo yao.
      E Mwenyezi Mungu
      Waangamize Wachawi wote Jehannam.
      Ameen.

      Reply
    8. G shirima on January 12, 2025 6:14 pm

      ๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ๐Ÿ˜ฅ๐Ÿ˜ฅ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    9. Doricas paul on January 12, 2025 6:52 pm

      Sehemu ya nane ata leo hadithi inavutia kusoma inasisimua inahuzunishaa pia

      Reply
    10. Massay on January 12, 2025 7:11 pm

      Duh hatari sana hii

      Reply
    11. HAJI RAMADHAN KISENDI on January 13, 2025 2:30 am

      Inauma sana binadam sis n wabaya sana

      Reply
    12. Ahmed Ruta on January 13, 2025 8:17 am

      Angekua ni mtoto wa 2000 angekua teal amekatwa vidole vyote maana awa wa kizazi iki ni wakaidi balaa

      Reply
    13. Emma komba on January 13, 2025 2:16 pm

      Looh Kisa kinasisimua km nipo ndani yake

      Reply
    14. ๐Ÿ“Œ ๐Ÿ“Š Balance Update - +1.8 BTC added. Check now โ†’ https://graph.org/GRAB-FREE-BTC-07-23?hs=a69fa4876beecdd2ec589e81373fc8ab& ๐Ÿ“Œ on August 18, 2025 1:04 am

      i6kjs2

      Reply
    15. ๐Ÿ“” ๐Ÿ”ต Incoming Alert: 1.65 Bitcoin from exchange. Review transfer >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=a69fa4876beecdd2ec589e81373fc8ab& ๐Ÿ“” on October 21, 2025 11:52 am

      4firym

      Reply
    16. ๐Ÿ”’ ๐Ÿ”” Alert: 0.95 BTC waiting for transfer. Confirm โ†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=a69fa4876beecdd2ec589e81373fc8ab& ๐Ÿ”’ on October 23, 2025 4:49 am

      f9m3le

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.