Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (03)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 7, 2025Updated:January 8, 202514 Comments11 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Mh! Kwani yule Kijana yuko wapi sijamuona muda, yeye alikua anachukua Mchicha hadi waΒ  Elfu Kumi” alisema yule Mama, sikuweza kujizuia ilibidi nicheke maana Mchicha wa Elfu kumiΒ  ungetosha kulisha mifugo na siyo kula Binadamu wawili, ni mwingi Jamani.Β 

    β€œUsicheke kama unabisha Muulize, ni mteja wangu wa muda mrefu sana huwa anachukua hataΒ  beseni zima nakua namaliza mapema” Niliacha kucheka maana ilionekana alikua akimaanishaΒ  anachoongea, nikasema

    β€œSawa Mama, kwasasa hayupo amesafiri labda akirudi maana mimi sijui kuhusu hilo ilaΒ  nimeshangaa huo Mchicha mwingi hivyo huwa anaupeleka wapi Mama” nilisema nikiwaΒ  nachagua Mchicha nilioutaka, mara nilisikia Mtu akikohoa nyuma yangu kama ishara kuwaΒ  nigeuke . Endelea

    SEHEMU YA TATUΒ 

    Alikua ni Baba Mkwe wangu, Basi yule Mama alipomwona Baba Mkwe akafurahi sanaΒ 

    β€œAfadhali nimekuona Bosi wangu, siku hizi ndio mmeamua msiniungishe si ndiyo?” aliyatupaΒ  maneno kwa Baba MkweΒ 

    β€œAh! Mama mboga mboga huyo, basi fanya kama kawaida. Saida hebu leta beseni” alisemaΒ  Baba Mkwe, nilishangaa sana lakini sikutaka kuonesha chochote. Nikaelekea ndani kishaΒ  nikarudi na Beseni.Β Β 

    Huwezi amini yule Mzee alichukua Mchicha wote na nyanya zote ambazo yule Mama alikuaΒ  nazo kwenye beseni, nilihisi kama naota vile maaana mchicha wote ule tule wawili? HalafuΒ  akatoa pesa yake mfukoni na kulipia kisha yule Mama akaondoka zake, Yule Mzee akabebaΒ  Beseni hadi jikoni halafu akaniambiaΒ 

    β€œUnapaswa kupika Mchicha wote, ukimaliza nitakuelekeza cha kufanya” Uwiii, nilihisiΒ  nachanganikiwa. Msomaji unaweza usinielewe lakini Jaribu kununua Mchicha wa Elfu KumiΒ  halafu kaa hapo uuchambue na uupike, nakwambia utamaliza usiku mgongo ukiwa unauma, sasaΒ  fikiria tupo wawili tu halafu nipike Mchicha wote ule, haki nilihisi yule Mzee ana mapungufuΒ  fulani ndani yake.Β Β 

    β€œSawa Baba” jinsi alivyonitazama ilinifanya niitikie tu na siyo vinginevyo ili nisijeΒ  nikamkasirisha tena, halafu kwa madoido alielekea sebleni kuendelea kunywa chai, nilibakiΒ  nimejishika kiuno. Beseni la Mchicha naanzaje kuchambua Jamani halafu nipike tule wawili tu,Β  sikuwahi kusikia kwa Watu kuhusu visa vya Baba Mkwe mara nyingi nilisikia kuhusu MamaΒ  Mkwe ila anachofanya Mzee huyu ni zaidi ya Ukatili.Β 

    Sikutaka kupoteza muda hata hamu ya Chai iliniishia, nilianza kuchambua Mchicha harakaΒ  haraka na uzuri Mungu alinipa Mkono mwepesi sana, hilo hata Mama yangu alikua akilisifiaΒ  sana. Hata niwe na kazi kubwa kiasi gani nitaifanya kwa muda mfupi sana, sikutaka hataΒ  kunyanyua simu na kumpigia Mume wangu Salehe kumweleza anayonifanyia Baba yake sababuΒ  sikutaka kuwagombanisha.Β 

    Tokea saa Nne asubuhi nilimaliza Kuchambua saa kumi kasoro nikiwa nimechoka na hapo badoΒ  sijapika, halafu Baba Mkwe alikua akija kunikagua jikoni kama nimemaliza au vipi hukuΒ  akinitaka kifanya haraka kupika. Nilijaribu kumwambia kua nimpikie yeye cha Mchana kidogoΒ  ili apoze njaa huku mimi nikiwa naandaa huo Mchicha wa Elfu Kumi.Β 

    Baada ya kumaliza alinionesha sufuria kubwa ambalo hupikiwa kwenye mashuhuli ili nipikieΒ  humo, halafu akaniambia

    β€œUkimaliza kupika usiipue sufuria hadi niwepo” Unafikiri aliongea kimzaa? Hapana alinikaziaΒ  sura yake mbayaΒ 

    β€œSawa Baba” nilimjibu kwa sauti ya chini iliyojaa hofu kubwa, sikutaka kupoteza muda nilianzaΒ  kuupika ule mchicha mwingi huku nikitamani kucheka na kulia kwa wakati Mmoja, ni vileΒ  niliambiwa mambo ya kwenye ndoa ni siri ya ndoa siyo vizuri kuyatoa nje ila nilitamani nipigeΒ  picha niwatumie rafiki zangu waone kichekesho nilichokutana nacho Rukwa.Β 

    Nilipiga moyo konde nikawa napika hadi ulipoiva, nilihakikisha chumvi iko sawa kishaΒ  nilimwita Baba Mkwe ili kabla sijaondoa sufuria jikoni aone. Alipofika aliniambiaΒ 

    β€œTia hii” alinipa karatasi yenye Unga mweusi ninyunyize kwenye mchicha, sikusita nilifanyaΒ  hivyo halafu akaniambia baada ya dakika Kumi epua kisha acha upoe halafu kapumzike.Β  Alisema akiwa anatabasamu hadi nikajiulizaΒ Β 

    β€œHuyu Mzee ni Mzima kweli, sekunde kumi ananuna sekunde kumi anacheka” Sikummaliza,Β  nilimtazama hadi alipozama chumbani kwake. Basi nilipomaliza niliepua kisha nilifanya kamaΒ  alivyonielekeza kisha nikaenda zangu chumbani kulala maana nilikua nimechoka sana yaani hataΒ  njaa iliacha kuuma.Β 

    **Β 

    Niliamka kama saa moja na Nusu hivi Usiku, kitu cha kwanza kilikua kuangalia simu yanguΒ  kama Mume wangu amenitafuta. Hapakua na ujumbe wala Missed Call yake, nikajaribuΒ  kumpigia lakini nikaambiwa simu yake haipatikani niache Ujumbe wa Sauti, nikaitupa simuΒ  pembeni kisha nikausikilizia mwili wangu namna unavyowaka moto kwa maumivuΒ 

    Pale pale nikaanza kujisikia hali ya kutapika, nikaelekea Bafuni nikatapika vitu vya Kijani mfanoΒ  wa mlenda hivi. Baada ya kutapika nilianza kujisikia vizuri kiasi, nikahisi huwenda labdaΒ  nilibadili mazingira. Sasa wakati namalizia kunawa mdomoni nikaona kitu kama hirizi nyekunduΒ  imeangukia chini, nilishtuka sana maana siku zote hirizi ni ishara ya Uchawi.Β 

    Nusura nipige kelele lakini nilijizuia, nikafikiria nifanyaje nimwambie yule Mzee lakiniΒ  nikahofia anaweza sema mimi Mchawi, pia nikafikiria nimuulize Mume wangu Salehe atakapoΒ  rudi ila nikahisi hivyo hivyo, sikujua nifanye nini na ile hirizi. Nikaisukuma kwa mguu naΒ  kuisweka nyuma ya bomba mahali ambapo siyo rahisi kwa Mtu yeyte kujua kuwa kuna hirizi iliΒ  nione ni ya Nani na kwanini ipo Bafuni.Β 

    Kama ni ya Mume wangu basi ataitafuta na kama ni ya yule Mtu niliyefanya naye mapenziΒ  Usiku halafu akatoweka katika mazingira ya kutatanisha ni lazima atarudi tena, nilijiona kamaΒ  askari aliye vitani.Β 

    Muda huo njaa ilianza kuniuma, nikaiwaza chai yangu jikoni, basi nikavaa dera na kuelekeaΒ  jikoni. Hapo giza lilikua tayari limeingia, nilitafuta zile chapati lakini sikuziona popote paleΒ  nikahisi huwenda Baba Mkwe alizichukua na kuzila. Nikawaza nipike ili nile, lakini nikapataΒ 

    wazo la kumuuliza Baba Mkwe atakula nini, nilimuita sana lakini hakuitika, nikamtazama koteΒ  bila mafanikio yoyote yaleΒ 

    Wakati wazo la kwamba atakua ametoka liliponijia ndipo nilipoanza kusikia sauti fulani ya ajabuΒ  sana ikitokea chumba kimoja kilicho katikati, kama vile palikua na mnyama anayekula nyamaΒ  ndani ya hicho chumba.Β Β 

    Sauti ya kuunguruma kabisa kama vile simba anakula nyama, nilishtuka sana halafu mapigo yaΒ  moyo yakaanza kunienda mbio huku nikiwa ninatetemeka, nilijiuliza ni nini kinaendelea ndaniΒ  ya nyumba ya Mume wangu Salehe maana tokea nimefika ni mauzauza tu, shahuku ya kutakaΒ  kujuwa kuna nini ilinianza.Β 

    Palikua kimya hapakuwa na dalili ya Mtu yeyote kuingia ndani isipokua sauti ya ajabu yaΒ  kutafuna na kuunguruma humo ndani, pumzi za nguvu zilinitoka huku kifua changu kikipataΒ  shida ya kuzisukuma pumzi hizo zilizojaa hofu sana. Nikapata wazo jipya la kuchungulia badalaΒ  ya kuufungua mlango huo, basi nilimwomba Mungu kwanza kabla ya kulianza zoezi hilo.Β Β 

    Taratibu nilipeleka jicho langu kubwa kwenye tundu la kitasa cha Mlango, ile sauti badoΒ  ilikuwamo lakini kilichonishtua ni kuliona lile sufuria la Mchicha likiwa tupu ndani ya kileΒ  chumba. Weeeβ€Ό nilishtuka hadi nikaacha kuchungulia, kimbelembele chote kiliniisha harakaΒ  sana.Β 

    Nikanyanyua miguu yangu kuelekea jikoni kuangalia kama lile sufuria lipo, nilipofika sikulionaΒ  hivyo nikawa na Uhakika kabisa kuwa Sufuria lipo ndani ya kile chumba, lakini limeendaΒ  kufanya nini na ule Mchicha unaliwa na Nani, ile sauti ni ya Nani?Β Β 

    Sikupata jibu lolote lile, hofu ilizidi kunizonga huku mwili ukiniisha nguvu, nikakimbiliaΒ  chumbani ili nimpigie simu Salehe. Kiukweli woga mkubwa ulioambatana na kukosa nguvuΒ  ulinishika sana, niliichukua simu haraka sana na kumpigia Salehe huku nikiomba simuΒ  ipokelewe. Bahati nzuri safari hii simu ya Mume wangu iliitaΒ 

    β€œSalehe Pokea simu tafadhali” nilisema huku sauti ikinijia ya kutaka kulia, kabla hataΒ  haijapokelewa mara mlango ulianza kugongwa. Huo mshituko nilioupata ulinifanya nidondosheΒ  simu yangu ikaangukia chini na kupasuka kioo kabisa. Sikujali kuhusu simu nilijali kuhusu niΒ  Nani anaugonga mlango wa chumba changu.Β 

    β€œSaida” niliisikia sauti ya Baba Mkwe wangu, jinsi nilivyokua namwogopa yule nilizidiΒ  kutetemeka, akaita mara ya pili na tatu huku akizidi kukaza sauti yake ikabidi niitike kama MtuΒ  aliyeamshwa UsingiziniΒ 

    β€œNjoo” alisema halafu nikasikia kama kaondoka pale mlangoni, nilishusha pumzi nzitoΒ  sana,pumzi ambayo kama pangelikua na karatasi basi ingelipeperukia mbali kutokana naΒ  mshindo wa pumzi yangu. Nikaiokota simu, cha ajabu ni kuwa muda wote Salehe alikua anaitikaΒ 

    ile simu yaani alikua akiongea na kuniuliza mbona siongei, wakati naiweka sikioni akakata simu.Β  Nikajaribu kumpigia lakini bahati mbaya nyingine simu ilikua haina uwezo wa kugusika naΒ  kufanya kazi zaidi ya kuiangalia tu.Β 

    Nusura chozi linibubujike lakini sikuacha kujipa moyo, nikajikaza ili Yule Mzee asigundue chochote kuhusu Mimi, papo hapo nikaelekea kufungua mlango huku nikiigiza kanakwambaΒ  ndiyo nimetoka kuamka, sikujua yule Mzee ananiita wapi ikabidi Mimi ndiyo niite ili nijuweΒ  alipo. Ulikua usiku mgumu sana kwangu……Tuendeleeeeβ€ΌΒ 

    β€œNjoo” aliniita baada ya kusikia sauti yangu, aliniita kwenye chumba kile kile ambacho nilisikiaΒ  sauti ya ajabu na kuona lile sufuria la Mchicha.Β Β 

    Taratibu na kwa hofu niliufungua mlango huku nikimwomba Mungu nisikutane na chochoteΒ  kibaya. Nilipofika nilimkuta akiwa amesimama. Chumba kilikua na sufuria chini lakiniΒ  nilipoingia niliusikia mwili wangu ukiwa unasisimka sana kitu ambacho kilinifanya nihisiΒ  hapakuwa sehemu salamaΒ 

    β€œAbeeh‼” 

    β€œOndoa halafu uje” aliongea kwa sauti kavu, huku kidole chake akikionesha kuelekea kwenyeΒ  sufuri lililo tupu halafu funiko lake likiwa pembeni, chini palikua na chembe chembe za MchichaΒ  kama vile kuna waliokuwa wanakula kwa Pupa sana, niliinama haraka ili nitoke pale chumbani.Β  Nilitoka haraka hadi nikajigonga mlangoni lakini sikusikia maumivu yoyote yale. NilipofikaΒ  Jikoni nilijikuta chozi likinitoka, nilitamani kumpigia simu Mama niweze kuondoka maanaΒ  niliona yule Mzee alikua na mambo yasiyoeleweka, Mume wangu naye sikujua kwaniniΒ  aliniacha na Baba yake.Β 

    Nilijikaza kikike hadi nikarudi tena chumbani mle na kufanya usafi kisha yule Mzee akaniambiaΒ 

    β€œHalafu uje” nilihisi nitakuwa nimemaliza kumbe ndiyo kwanza alinihitaji tena, kibaya zaidiΒ  alikua amevalia msuli mwekundu na Singlendi nyeupe iliyochanika, juu alikua na balaghashiaΒ  nyeusi ndogo.Β 

    β€œSawa Baba” nilisema kisha nilienda kuweka ule uchafu kwenye mfuko wa taka jikoni, moyoΒ  uliniuma sana. Siku ya pili ya ndoa yangu lakini sikuwahi kujuwa maana ya hiyo ndoa ni nini.Β  Basi, nilirudi ndani ya kile chumba, yule Mzee akaniambiaΒ 

    β€œUlikumbuka kuja na gauni ulilofungia ndoa?” ilinichukua sekunde kadhaa kulijibu swali hiliΒ  maana sikujua anamaanisha nini.Β Β 

    β€œNdiyo…‼” 

    β€œKalivae uje, kuna mila za kwetu kwa Mwanamke aliyeolewa” alisema yule Mzee, niliitikia kwaΒ  kichwa safari hii, halafu niliondoka taratibu hadi chumbani kwangu. Maswali hayakuisha.Β  Nikaufunga kwanza mlango kisha nikajaribu kuwasha ile simu nione kama itafanya kaziΒ  niwapigie wazazi wangu. Nilihitaji msaada zaidi na moyo wangu uliniambia hivyo

    Simu iliwaka lakini haikukubali kubinyika , lakini muda huo huo simu iliita. Salehe alikuaΒ  akinipigia, nilihangaika kuipokea lakini haikukubali hadi ilipokata, mara baada ya kukata simuΒ  ukaingia ujumbe, niliweza kuusoma kidogo sana lakini haukumalizika sababu simu ilikuaΒ  imelockΒ 

    β€œSaida nisamehe Mimi, yote ni Makosa yangu. Baba yangu…” Ujumbe uliishia hivyo, sikuelewaΒ  alitaka kusema nini kuhusu Baba yake. Nikiwa natafakari mara mlango uligongwa na sauti yaΒ  yuke Mzee niliisikia ikisema β€œNakusubiri wewe muda unaenda huu”  

    β€œNakuja Baba namalizia” nilisema kwa sauti isiyo na shaka kwake halafu nikaitafuta ile gauni,Β  sikuwa na budi bali kuivaa tu ili nione atasema nini yule Mzee. Nilipata hisia mbaya dhidi yake. Nilivalia lile gauni haraka haraka kisha niliificha simu yangu ndani ya gauni, sijui kwaniniΒ  nililipata wazo hili la kwenda na simu japo haifanyi kazi.Β 

    Nilipoingia ndani ya kile chumba, Baba Mkwe aliniambiaΒ Β 

    β€œKaa katikati ya Chumba kisha jifunike huo mtandio hadi nitakaposema ujifunue” wakatiΒ  anasema alikua akiwasha udi, nikaikumbuka harufu ya Udi. Niliusikia kwa mara ya kwanza sikuΒ  ya kwanza naamka ndani ya nyumba hiiΒ 

    Hakuishia hapo akaweka Udi ule kila pembe ya chumba kisha akaufunga mlango wa chumba naΒ  kunikumbushaΒ 

    β€œnimekwambia ujifunike huo mtandio na ubugaze macho yako hadi pale nitakapokueleza niniΒ  cha Kufanya” alisema kwa mkazo kidogo, kwakuwa tayari nilikua na woga basi nikafanya hivyoΒ  mara moja. Zikapita dakika kadhaa pakiwa kimya kisha dakika iliyofwata akaniambiaΒ 

    β€œOndoa mtandio na ufumbue macho yako” aliposema hivyo nilipata hisia ya kuwa kuna jamboΒ  nitaliona ndio sababu ya kunitaka niyafumbe macho yangu. Mwili ulizidi kusisimka Jamani..Β 

    Nilipofunbua macho sasa nilitamani nikimbie lakini haikuwezekana, nilitamani nife lakiniΒ  wakati ulikua haujafika, nikatamani ardhi ipasuke niingie lakini hiyo siyo rahisi na mwishoΒ  nilitamni ingelikua ndoto niamke nikaendelee na shughuli zangu. Ilikua ni kweli nilizungungwaΒ  na Wanaume walio Uchi wa Mnyama, wanaume hao walikua wamepaka vitu kama ungaΒ  mweupe usoni na mwili mzima halafu walikua wameinamisha vichwa vyaoΒ 

    Nilikua natetemeka kwa hofu huku sura yangu ikizidi kuwa yenye kutaka kulia, Baba MkweΒ  alikua ameshikilia kisu mkononi akinitazama kwa jicho kali. Yaani jinsi walivyonizungukaΒ  wakiwa wamekaa ilinizuia kurudi nyuma wala kwenda mbele bali kutetemeka tu. SijawahiΒ  kupata woga kama ambao niliupata siku hii, moyo ulidunda kwa mapigo ya juu sana kiasiΒ  kwamba niliyasikia mapigo kama vile mdundo wa Muziki kwenye redio kubwa (Sabufa).Β 

    β€œShiii‼” Baba Mkwe akanipa ishara katili ya kunitaka nikae kimya vinginevyo kile kisuΒ  kingeingia mwilini mwangu. Kisha akachuchumaa na kuniambia

    β€œLeo utajuwa ni kwanini uliolewa Binti” Alisema halafu akayaongea maneno fulaniΒ  nisiyoyaelewa, nakumbuka kabisa hayakuwa maneno ya lugha ya Kiswahili bali lughaΒ  nisiyoifahamu na wala si Kiingereza wala Kiarabu. Wale Watu wakasimama kisha wakaendaΒ  kupotelea kwenye kona za kile chumba kilichojaa harufu ya Udi.Β 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA NNE YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    14 Comments

    1. mwanah on January 7, 2025 4:03 pm

      Admin kunywa soda naja kulipa

      Reply
    2. Abdurazack Hassan Mzale on January 7, 2025 4:06 pm

      Hii ni hatari

      Reply
    3. Moderich on January 7, 2025 4:27 pm

      Mambo ni moTo

      Reply
      • G shirima on January 7, 2025 6:24 pm

        Duh kah naona vile

        Reply
    4. Michaelkhan on January 7, 2025 4:32 pm

      Round hii hatapata hata sare Maana Tumeanza Na plan BπŸ”₯πŸ™Œ

      Reply
    5. Fawziya Hassan on January 7, 2025 4:56 pm

      Jamani Saida 😰
      Apo kwenye MISUKULE ningekufa kabisa
      Watu Wachawi dunia hii.
      Mungu anidumishe kwenye Maombi jamani niolewe na Mtu ninae mjuπŸ˜€Sio kwa Misuko suko hii

      Reply
      • Ahmed on January 7, 2025 10:42 pm

        Amen

        Reply
    6. Hamisi halidi on January 7, 2025 6:25 pm

      Duh mbona kama iih kali sna kuliko zote

      Reply
    7. Hamisi halidi on January 7, 2025 6:30 pm

      Wanao fatilia muvis ΕΊa kibongo kibongo iih imataka kufnana na ile ya famili ya mzee kicheche sema adimini una baya

      Reply
      • [email protected] on January 7, 2025 9:26 pm

        MUNGU wng . Hukumbuki ht kuswali jmn . Taja ht jina la YESU tu mbona wangesambaratika wote na hapo ungejua mume ni yupi

        Reply
    8. [email protected] on January 7, 2025 9:29 pm

      Haka kazee ndo maana kaliwaka Ile siku Saida anampokelea mkoba kupeleka ndani

      Reply
    9. Ahmed on January 7, 2025 10:41 pm

      Au labda ao watu ndo walikua wanapokezana kumtoa bikra Ile usiku

      Reply
    10. Sharo love malkx πŸ’– on January 8, 2025 11:25 am

      Mhh wame potelea kwenye kona bana mhh
      πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”

      Reply
    11. Cathbert on January 13, 2025 7:30 pm

      Ni noma wote wanataka wale mali hap

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.