Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ni Wakati Wa Vilabu Kula Matunda Ya Timu Za Vijana
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Ni Wakati Wa Vilabu Kula Matunda Ya Timu Za Vijana

    Cosmasy ChogaBy Cosmasy ChogaAugust 16, 2024Updated:August 17, 20241 Comment3 Mins Read922 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Vilabu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Tukiwa shule tulifundishwa nidhamu,nidhamu hiyo ilijumlisha na kuomba ruhusa maalum kwa mwalimu wa darasa endapo una tatizo lolote ambalo linakutaka wewe uende nyumbani,kama mwalimu wa darasa hayupo basi ruhusa hiyo ataifikisha viongozi wa darasa. Yeye ndie mtu wa pili baada ya mwalimu wa darasa,taarifa zote za mahudhurio ya mwanafunzi hutoka kwake kwenda kwa mwalimu wa darasa.

    Endapo utapata tatizo ukiwa nyumbani mzazi wako atalazimika kwenda shuleni kukuombe ruhusa kwa mwalimu wako. Misingi ilizingatiwa,ilikuwa ni utaratibu tu ambao lazima ufatwe kwani bila hivyo shule ingekuwa kijiwe cha bangi ukiamua uende au usiende,ingekuwa kama kilabu cha pombe uamue kwenda kunywa au usiende.

    Kama hutafanya hivyo basi utakapoenda shuleni utaadhibiwa tu hata kama ilikuwa unaumwa,mwalimu bado atakaumbia nakuadhibu kwa kosa la kutoomba ruhusa kwangu au kwa viongozi wa darasa (Monitor s). Walikuwa sahihi walimu,sijui utaratibu wa sasa kwa sababu hapa mjini ambapo mimi sikusoma naona wanafunzi hata shule wanaenda muda wapendao.

    Uwezo wa soka hautafutwi Google,uwezo wa soka hauazii miaka 20,mbinu za utoto wa kutumia mipira ya tambala ndio kipaji huibukia hapo. Hili ni suala ambalo kila mdau wa soka anapaswa kulitambua na kuelewa ipasavyo.

    Soka ni idara kubwa unapomtazama under seven wa kijijini unaweza ukacheka akifuma mpira kwa kutumia mifuko na matambala lakini ndipo akili ya kuupenda mchezo inanzia hapo.Unaweza ukajiuliza huyu mtoto anashindwa kusoma anacheza na milaironi hii baada ya dakika kadhaa utaona kaingia kucheza peku tena kwa furaha sana.

    Aah!,nimewaza tu yule mtoto anayehangaika kufuma mpira ili aonyeshe uwezo wake kama angeonyeshwa njia vilabu vyetu vingekuwa wapi kwa sasa katika utawala wa soka la wazawa.

    Kwa miaka mingi sasa vilabu vyetu vimekuwa na vikosi vya timu za vijana ambako pia kwa kiasi fulani wanatumia gharama kuwalea lakini kwa asilimia kubwa tumeona wakikosa kula matunda ya gharama hizo kwa kutotambua umuhimu wao.

    Kuna vijana wengi ambao wanalelewa na vilabu vya Yanga Sc na Simba Sc lakini huishia kuwaacha tu na mwisho wa siku hao ndio wamekuwa wakiwaadhibu pale wanapokutana na ndio wanaonekana kufanya vizuri na vilabu vingine.

    Nimefikiria zaidi na mbali zaidi kama vilabu hivi vyote vya ligi kuu vingeweza kuwathamini wachezaji wa timu za vijana na kuwapandisha wa kutosha kupata uzoefu na wakubwa ni kwa kiasi gani wangekuwa wamepunguza gharama hizo za usajili wa wachezaji wa ndani.

    Kuna ulazima mkubwa sana wa kukwepa adhabu ya vijana hawa kwani wengi wao ndio wanageuka fimbo za kuwachapa pale wanapokutana,kuna ulazima mkubwa wa kuonyesha nidhamu kwa kuwa na maumivu ya gharama wanazotumia kulea hawa vijana,kuna ulazima mkubwa kwa mashabiki kutambua vijana wanaoshinikiza waondolewe ndio wanakuwa fimbo nzuri za kuchapia vilabu vyao.

    Mashabiki wanatakiwa kutambua baada ya muda mfupi tu vijana hao hao wanaotoka kwenye timu zao ndio hao hao wanakuwa wanawanyoshea vidole vya kutaka timu zao ziwasajili na kujikuta wakitumia gharama huku wakijua kabisa wao ndio waliwalea kabla ya kutotambua thamani yao. Naimani kama watalelewa vyema watawasaidia bila tatizo.

    Tukienda mbali zaidi ya hapo sio lazima wawatumie wao lakini inawezekana ikawa biashara nzuri zaidi ya kujipatua uchumi na kuimarisha timu.

    Nidhamu ni pamoja na kuheshimu matumizi yasiyo ya lazima pale panapowezekana.

    SOMA PIA: Heritier Makambo Kitabu Cha Simulizi Walichokataa Wazawa

    CAF CHAMPIONS LEAGUE SIMBA SC cv ya kocha mpya simba yanga vs vital o

    1 Comment

    1. Pingback: Jean Charles Ahoua,Je Simba Imepigwa Kwenye Huu Usajili?

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.